Kaburi Moja La Posta Lagoma Kuhamishika
Vložit
- čas přidán 12. 08. 2023
- katikati mwa jiji la Dar es salaam kuna kaburi moja la ajabu ambalo mpaka sasa watu hawajua kwa uhalisia ni kaburi la nani zaidi ya kuwepo kwa nadharia ni la Sharifu Attas
Kaburi hilo liligoma kuhamishika mara baada ya watu kujaribu kulihamisha maeneo ya posta clock tower na kuzua taharuki kwa mashuhuda wa tukio hilo
kaburi hilo ni miongoni mwa makaburi yenye historia za kipekee nchi tanzania,sababu ya kubeba upekee wa eneo hilo na maajabu ya kugoma huhamishika ndani ya posta clock tower
Wakaazi wa eneo hilo wanasema kaburi hilo lipo hapo zaidi ya miaka 50 iliyopita na kusadiki ni mtu wa maajabu aliyekuwa na kipawa kikubwa - Zábava
Kaburi hilo ni la sayyid Abdul Shakur bin said Al attas huyu ni sharifu nani mwanazuoni mkubwa asili yake ni kutoka hadhramout nchini Yemen Allah swt amrahamu walii huyu pamoja na wanazuoni wote waliotangulia barazakh,
Ulijuaje
Innalillah wainna illah raji'uun, Allah atjaalie mwisho mwema , tuwe watu wema , waumini na wachamungu wema inshaallah
Mwenyezi Mungu akiamua mtu anae mpenda abaki alipo atabaki alipo hakuna wakumuondoa ila Mola akubali asipo kubali Mtakiona cha mtemakuni Allahu AKBAR Muacheni Alie lala hapo alale hapo ndio mola alipo mtaka alale hadi hatima❤❤❤
Mimi mwenyewe nilikua napita sana nilikua sijui mpaka nikaambia na iyo store pia nilipewa na pia nilikua nawaona watoto wa madrasa wakija kudoma Dua
Masha Allah sio kila sehemu au pahala la KUCHEZEA
Au hapo chini kuna madini yamefichwa
LIANDIKWE KWA ANAE JUA.NI NANI HUYO NA UTUKUFU WAKE
mwenye kaburi hili jina lake anaitwa abdulshakir said latas hapo palikuwa na makaburi mengi yalihamishwa hili lilishindikana tuseme tunayoyajua tusiyoyajua tuulize
Nenda pale ukarikodiwe ujulikane ukweli
Yote haifai kuweka utalii wa pesa
Al Atas ni Shariff kutoka Yemen
Haifai kuja kuomba unachotaka.ila ni kumuombea aliefariki tu..yasiabudiwe
Katika Uislam maombi hufanyika kwa njia nne:-
1. Omba kwa Mungu directly.
2. Nenda kwa Mtu unaemdhania ni mwema akuombee. Mitume waliombea watu.
3. Kuomba kwa kutawasuli yaani kuhusisha mazuri uliyofanya au utayoacha
4. Kumuomba Mungu kwa Uchawi, njia hii Mungu yupo karibu zaidi kupokea maombi LAKINI ni HARAM haitakiwi utumie na ataetumia atakuwa mbali na rehema za Mungu. Mungu atuepushie na UCHAWI kufanya na kufanyiwa.
Makarama ya Allah
😂😂😂😂😂❤
Subhanallah
Kuomba makaburi ni shirki
Hawaombi kaburi kwa taarifa yako
@@froma3732
Nilichokusudia wanamuomba huyo aliopo kaburini, hata akiwa nani itabaki kuwa ni shirki
Hao wanaenda kumuombea dua na si vinginevyo
@@rayisadesigns2646
Lkn wanakiwa watumie njia sahihi,
Unatoa salaam n kuwaombea dua waliokaburini kisha unatoka.
Hakuna mambo ya vyetezo.
Cha kujiuliza mbona makaburi mengjne gawafanyi?
Umelishwa na kuaminishwa maneno na wala ujaulizwa na mada sio shirki au la sasa unaingiza maneno ya shirki yanahusu vip, ulewa ni kinazungumzwa. Wacha pumba na likija suali la hukmu ndio utowe sheria.
Hapo kuna mapepo
Acha ujinga wa kanisani, mapepo mavumbi, upuuzi tu lini mtaji tambua
Sijambo. Hamjambo? HILI ni kaburi la Sharifu (Mtu mwenye karama) mwenye asili ya nchi ya Uajemi (Iran). Marehemu huyu amezikwa hapa katika mwaka 1850+ (Karne ya 19). Jina lake ni ABDUL SATAA SALIM AL ATAS.
Ahsante sana kwa mchango wako na tunakutakia utazamaji mwema wa chanel hii
Ulijuaje km hutudanganyi hapo
kutoka yemen nasio iran sagaf ni kutoka yemen
al atas kutoka yemen hadharamut
Hii nimeipenda ndio wakome viherehere vya kuvunja makaburi ya wenzao.
Kuna thehebu la wa Hindi hapo wali uziwa hicho kiwanja na mjanja mmoja aliye kuwa Meya wa Jiji walipo gundua wame pigwa katika kulazimisha kiwe halali waka mzika Imamu wao siku ya Jumapili na huyo Meya ambae sasa hivi ni Marehemu ali huzuria mazishi
Mbona wengine wanasema hapo kazikwa Sharifu Myemen?Sasa cjui tushike lipi?Ila nimeipenda hii wakome kufukua makaburi ya wenzao
Rafaeli acha uongo hapo kazikwa mjukuu wa Mtume Muhammad (S.A.W) aliyekuwa akiitwa Sharif Khatwas ambaye ndiye aliyekuwa mmiliki wa eneo hilo zama hizo lilipokuwa shamba lake ambalo lilikuwa eneo lote hilo la Stesheni mpaka Posta, maeneo ya Posta alipakana mzee Jumbe Tambaza aliyemiliki kuanzia maeneo ya Ikulu ya Magogoni, Upanga mpaka Muhimbili, na ndiyo maana hata eneo hilo lililopo jirani na hospitali ya Muhimbili linaitwa Tambaza kwa sababu ya huyo mmiliki wake, kizazi cha mzee Tambaza kipo mpaka leo na ni miongoni mwa familia zilizojitoa sana ktk kupigania uhuru wa nchi hii wakishirikiana na Mwalimu Nyerere na wazee wengine wa Dar es Salaam, makaburi ya Tambaza na ule msikiti wa Tambaza pale Upanga ni ya kwao hata shule ya Tambaza imeitwa hivyo kwa heshima ya mzee wao. Baadhi ya maeneo ya Sharifu Khatwasi aliyezikwa kwenye hilo kaburi na maeneo ya Magogoni yalinunuliwa na Sultan Sayyid Majid mtawala wa Zanzibar na eneo kubwa la Afrika Mashariki, alinunua eneo hilo akaasisi jiji hili la Dar es Salaam, akajenga Ikulu ya Magogoni ambayo kwa kipindi hicho ilikuwa ni chuo kikuu kabla ya kubadilishwa matumizi na wavamizi wa koloni la wajerumani, majengo mengine aliyojenga ni pamoja na ikulu yake ndogo iliyokuwa Posta, pia alijenga jengo la hopitali ya Ocean Road ambalo kwa kipindi hicho lilitumika kama hosteli ya wanafunzi wa chuo hicho kilichogeuzwa ikulu na wajerumani. Na hilo sio kaburi pekee eneo hilo la mjini bali yapo makaburi mengine ya wakazi wa eneo hilo ambao ndiyo wenye Dar es Salaam yao, makabari hayo yanapatikana ktk baadhi ya fensi za majengo pale Posta, pia baadhi ya walimu waliokuwa wakifundisha ktk chuo cha magogoni ambacho leo kimekuwa ikulu yetu makaburi yao yapo ndani ya maeneo ya ikulu ya Magogoni na hili la kuwepo kwa makabuli ya walimu hao ndani ya eneo la ikulu hata Ridhiwan Kikwete alishawahi kulizungumzia ktk moja ya hadhara, na pia ili kujua Sharif Khatwasi mwenye kaburi hilo na Mzee Jumbe Tambaza ndiyo waliokuwa wamiliki wa maeneo hayo fatilia mahojiano ya Zuhura Yunus na mmoja wa wajukuu wa mzee Tambaza.
Hiyo kaburi ikae hapo hapo vizazi na vizazi Karne na Karne atakae jaribu kuivunja Ataona moto na unafiki wao
@@ismailmshana2828 Kabisa
Allahu-akbar.
Ndani ya ofic ya waziri mkuu magogoni yapo
Kama ni kaburi mbona halioneshi kichwa kimeelekea wapi
Hayo ni miongoni mwa maajabu yake
Kama wewe ni Mwiilasalamu utajuwa kichwa kipo wapi
Ukijua kibra Iko wapi,basi utajua kichwa kilipo
Makaburi ya Kiislam kuchwa huelekezwa kibla..na sio kuwa liwe sawa na majumba ya pale ila ni kibla tu
Hilo Sio Kaburi Nigari