SERIKALI IMEAMUA KUWAJENGEA NYUMBA WANANCHI WAKE DODOMA KWA MKOPO

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 10. 06. 2021
  • Baada ya Serikali kutoa mkopo za zaidi ya Bilion 71 kwa Shirika la nyumba la taifa NHC kwa ajili ya kujenga nyumba 1000 katika maeneo ya Chamwino Ikulu na Iyumbu kwa lengo la kupunguza changamoto za makazi kwa wananchi wake kufuatia maamuzi ya Serikali kuhamia Dodoma ambapo lengo ni kuwauzia nyumba hizo wananchi kwa kipato cha chini kwa gharama naafuu.
    leo June 11, 2021 Mkurugenzi mkuu wa Benki ya Azania ambayo ndio itakuwa wadhamini wa mikopo kwa wananchi watakaouziwa nyumba hizo Charles Itembe ametembelea mradi huo ili kujionea ujenzi unavyoendelea huku akiwataka wananchi wa kipato cha chini kujitokeza kwa wingi kuchangamkia nyumba hizo pindi zitakapokamilika.

Komentáře • 137

  • @saidrajabu9589
    @saidrajabu9589 Před 3 lety +17

    Nyumba ya maskini kununua mwisho wa kununua ni mil tano sema mmejijengea wenyewe kipato cha maskini hakifiki milioni 70 tuwekane ukweli

  • @allymapinda8804
    @allymapinda8804 Před 3 lety +9

    Kwa jinsi Bongo ilivyo, hizo nyumba zitauzwa kwa matajiri/watoto wa vigogo na walengwa kuambulia kuangalia tu😳👀

  • @marymfugwa847
    @marymfugwa847 Před 3 lety +8

    Pandeni miti maana Dodoma mungu aliinyima miti.

  • @mklarazaa719
    @mklarazaa719 Před 3 lety +17

    Kuna kipindi zilijengwa mwanza nikauliza bei ni milioni 70 masikini yupo hapo kweli

    • @kennyrogers4734
      @kennyrogers4734 Před 3 lety +1

      Wanazingua hao Milioni.70 kwa mwananchi wa hali ya chini uyo??

  • @mutalemwafaridu5341
    @mutalemwafaridu5341 Před 3 lety

    Thanks for the good work to the nation

  • @kennyrogers4734
    @kennyrogers4734 Před 3 lety +3

    Bei gani mbona maneno meeeeeeeengi mnashindwa kuitaja bei elekezi ya izo nyumba zenyewe?na kwa kipindi gani?

  • @ooafrica3626
    @ooafrica3626 Před 3 lety +5

    Apa inatakiwa miti ipandwe kweli kweli

  • @MrNoNonsenseYes
    @MrNoNonsenseYes Před 3 lety +2

    Concrete jungle in the making, kueni makini sana mimea ni muhimu sana zaidi ya vile munavyofikiria

  • @asiakimolo5616
    @asiakimolo5616 Před 3 lety +5

    Wameshajipanga ,pangu pakavu tutaziona tu kwenye TV

    • @leokamil6284
      @leokamil6284 Před 3 lety +1

      Kama za Kigamboni za wauguzi kama sikosei

  • @rahimaaaaa8699
    @rahimaaaaa8699 Před 3 lety +8

    Jamani wekeni kampuni ipande miti sasa yaani panatisha si kwa ukame

  • @shinipapaya846
    @shinipapaya846 Před 3 lety +1

    Asante sana Raisi wangu mzee baba

  • @kasililamecksatano7302
    @kasililamecksatano7302 Před 3 lety +1

    Safi sana Tz sisi siyo masikini

  • @tusajigwekanemela2864
    @tusajigwekanemela2864 Před 3 lety

    Tunazisubilia yetu machooo

  • @amzamrid3571
    @amzamrid3571 Před 3 lety

    Asante sana

  • @gracielachiloloma2154
    @gracielachiloloma2154 Před 3 lety +2

    Bei gan

  • @highvoltages4169
    @highvoltages4169 Před 3 lety +1

    _"Wananchi wa kipato cha chini kununua hizo nyumba"_
    ULIZA BEI,
    Halafu ndo utajua ni wananchi gani watanunua, wenye uchumi wa hali ya chini au hali ya juu

  • @kiatu
    @kiatu Před 3 lety +4

    Watakopa hao wanaochota pesa zetu huko hazina

  • @ooafrica3626
    @ooafrica3626 Před 3 lety

    Safi sana

  • @ramadhanichalachala549
    @ramadhanichalachala549 Před 3 lety +1

    Siyo kweli hizo nyumba mtauziana wenyewe ila angekuwa JPM nikweli wangekopeshwa masikini

  • @bonyngere3758
    @bonyngere3758 Před 3 lety

    Nakuona kaka mkubwa mkurugenzi mkuu Azania Bank

  • @chingawadunia3621
    @chingawadunia3621 Před 3 lety

    Tunahtji Kaz wakuuu

  • @omaryregga5315
    @omaryregga5315 Před 3 lety +1

    Kiukweri hizo nyumba wanajengewa matajili huku sumbawanga hizo nyumba wanakaa matajili tu

  • @khadijahali4837
    @khadijahali4837 Před 3 lety +2

    Tajeni bei bc tupime km vp bora tujenge wenyw

  • @blackbeauty579
    @blackbeauty579 Před 3 lety +3

    Bei gani tujue mapema

  • @aboubakar4793
    @aboubakar4793 Před 3 lety +1

    Unakopa benk afu ukishindwa kulipa bank inakuwa mali yao wenyewe

  • @AhmedMohamed-so7db
    @AhmedMohamed-so7db Před měsícem

    Bei gan sii mnajua kadirio ama mnatichocha

  • @sponsalfathedj8177
    @sponsalfathedj8177 Před 3 lety +1

    Mvua ikinyesha hapo pako salama?

  • @sijalikifunyo912
    @sijalikifunyo912 Před 3 lety +2

    Miezi mitatu wakati miundombwinu mingi bado!!!!

  • @kabalajunior5441
    @kabalajunior5441 Před 3 lety +4

    Hiyo nchi Ni kavu sanaaa jmn

  • @aishaomari944
    @aishaomari944 Před 3 lety

    Oda plz

  • @aboubakar4793
    @aboubakar4793 Před 3 lety +1

    Tengenezeni nyumba na muuze kwa milion moja hadi mbili na zenye laki 7 ndo tujue mnasaidia wanainch sio hizo

  • @gilbertidi9682
    @gilbertidi9682 Před 3 lety +1

    MAGUFULI MAGUFULI MAGUFULI..................

  • @simonishija8087
    @simonishija8087 Před 3 lety

    Jamaa kafanana na lizy one

  • @ramlazuber6038
    @ramlazuber6038 Před 3 lety

    Watalizwaaaa WATUUU huko ipo siku.

  • @gerkombo6512
    @gerkombo6512 Před 3 lety +1

    Inabidi maji yachimbwe chini, la cvyo hilo ni jangwa.

  • @nipolive..2745
    @nipolive..2745 Před 3 lety

    Mwenye mawasiliano na wahuska. Nitumie namba nipo kigoma nije na mi nikope nyumba

  • @morganrobinson3542
    @morganrobinson3542 Před 3 lety +1

    Swali ni kwamba hao walengwa watazipata kweli! Maana kifuatacho hapo ni vigogo mitoto yao kujimilikisha juu kwa juu.

  • @aganolamotoeliya2027
    @aganolamotoeliya2027 Před 3 lety +2

    Hivi maskini ni yupi? Kama anaweza kununua hizo nyumba atakua maskini kweli?

  • @mrgeorgeisdory5277
    @mrgeorgeisdory5277 Před 3 lety +4

    Magufuli hoyeeeeeeee
    Rest In Peace Mfalme 👑👑👑👑

  • @zuwenaabrahman9913
    @zuwenaabrahman9913 Před 3 lety +2

    mumepoteza pesa hapo mulikuwa mujenge magorofa ya mana ili wakaazi wangepata wengi kuliko Mia tatu mulio taja

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      NENDA MICHENZANI UKAONE PALIVO OZA NA KUNUKA HADI AIBU.

  • @ashamwandu6572
    @ashamwandu6572 Před 3 lety

    Nitanunuwa

  • @frederickmwakatobe4669

    Mimi ni mwananchi maskini napata milioni mbili na nusu kwa mwaka. Ntapateje nafasi ya kununua nyumba hizo?

  • @kiatu
    @kiatu Před 3 lety

    Unakopesha mamilioni halafu ndio kwanza leo unatembelea😟

  • @staralive9260
    @staralive9260 Před 3 lety

    Wanachi wa chini ni kigezo tu lakini kwasababu lengo sio wananchi wa hali ya chini.

  • @awadhrajabu1403
    @awadhrajabu1403 Před 3 lety

    Akuna Nyumba Ya Masikini Apo Maneno Tu Utamkwa

  • @vedastokeya3344
    @vedastokeya3344 Před 3 lety

    Tanzania bhana eti nyumba za watu masikini ukiuliza bei unaambiwa 33M -- 70M Kuna mtu masikini mwenye hiyo hera ongeeni vitu halisia kama tupo tz sio London.

  • @ilynpayne7491
    @ilynpayne7491 Před 3 lety +1

    Bora kununua kiwanja milion 6 kujenga kibanda chumba seble nikae 😅

  • @ilynpayne7491
    @ilynpayne7491 Před 3 lety

    Kwanza kiuhalisia hizo nyumba sio za kimaskini wataenda kuishi wenyewe

  • @chingawadunia3621
    @chingawadunia3621 Před 3 lety

    Tupeni Oda ya Kaz kw madalal wadogo wqkuuu

  • @lucasmhagama8166
    @lucasmhagama8166 Před 3 lety

    Hakuna mtu mwenye kipato cha chini mwenye hiyo hela

  • @marymfugwa847
    @marymfugwa847 Před 3 lety +4

    Hizo nyumba masikini hawazipati.

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      AKIWA NA PESA ATAIPATA.

    • @ambakisyemwakinunu2002
      @ambakisyemwakinunu2002 Před 3 lety

      @@salimsaid7200 kama ni milion 70 ni masikini huyo? Masikini akopeshwe kwa milion 5,6,7 hapo sawa, wewe unavyofikiri zitapatika za Kiasi hicho?

    • @IBENGM
      @IBENGM Před 3 lety

      @@ambakisyemwakinunu2002 Nyumba gani hyo inathamani ya Mil 5? Hyo sio nyumba labda useme banda!

    • @ambakisyemwakinunu2002
      @ambakisyemwakinunu2002 Před 3 lety

      @@IBENGM ndugu yangu hayo ni maisha watu usiyadhihaki kama wewe Unapesa kaa kimya,Hata hiyo unyoiita wewe nyumba waliokizidi kifedha wanakiita kibanda, tuna madaraja hapa duniani kikubwa tuheshimiane

    • @IBENGM
      @IBENGM Před 3 lety

      @@ambakisyemwakinunu2002 Haya bwana isiwe shida sema nia yangu ilikuwa sio kudhihaki bali ni mtizamo tu maana kila mtu anauelewa wake.

  • @williebenmarunda9854
    @williebenmarunda9854 Před 3 lety

    Nyumba zinajengwa barabara za vumbi?

  • @mussaabdiel9797
    @mussaabdiel9797 Před 3 lety

    Ajira babkubwa kwa waliopo huko iyumbu

  • @alhajimbwambo3785
    @alhajimbwambo3785 Před 3 lety

    Bei nishingapi

  • @aboubakar4793
    @aboubakar4793 Před 3 lety

    Hakuna nyumba za wanainchi wenye kipato cha chini hv selikali nayo kumbe ni yakifiki hivi

  • @najmaulaya8819
    @najmaulaya8819 Před 3 lety +1

    Mbona kama jangwani mmmh

  • @Hillary_Daudi_Mrema
    @Hillary_Daudi_Mrema Před 3 lety

    Kujenga nyumba sio tatizo bali nyumba zikikamilika tamaa ya baadhi ya Watendaji wa Ngazi za Juu wanaingiwa na tamaa ya fedha hivyo Rushwa zinakuwepo na kufanya wananchi wenye uhitaji makazi bora kukosa nyumba sababu ya ukiritimba uliopo.
    Azania Benki naomba mtende haki kwa watu wote hasa wastaafu nadhani zingewasaidia sana maana wanapoteza fedha nyingi kupata makazi ya kudumu baada ya kustaafu.

  • @chingawadunia3621
    @chingawadunia3621 Před 3 lety

    Mm nazjua mpk unapoonglea nakupngza San mm Kam machinga San

  • @ambakisyemwakinunu2002

    Hakuna chochote ni danganya toto ni watu kujitengenezea njia za kujinufaisha wao tu, hizo nyumba zitamilikiwa na wenye pesa tu hakuna mtu wa hali ya chini atakaeweza kumiriki nyumba hizo kwani gharama zake hatoweza kuzimudu

  • @antonyvallerian1718
    @antonyvallerian1718 Před 3 lety

    Tukopesha mama

  • @wazirimbwambo672
    @wazirimbwambo672 Před 3 lety +1

    Bei bei

    • @paulnsabi3779
      @paulnsabi3779 Před 3 lety

      Mambo gani muhimu yazingatiwayo kukopa/kununua ni watumishi au wajasiriamali,Bei ya kununua/mkopo,ukubwa wa nyumba muda wa kulipa,je mikoa mingine mradi huu upo,kupanga kero

    • @benethmengele9255
      @benethmengele9255 Před 3 lety

      Bei gan toeni maelekezo ya kutosha

    • @kiehbhzh7044
      @kiehbhzh7044 Před 3 lety

      Hizo nyumba ni za serikal sio maskin

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      @@paulnsabi3779 HIZO HABARI ZOTE NENDA BENKI UTAZIPATA.

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      @@benethmengele9255 HUYO NI MSIMIAJI 2 HIZO HABARI NENDA KITENGO CHA KUNUNUWA WATAKUPA MAELEZO YOTE.

  • @naipendatanzania3248
    @naipendatanzania3248 Před 3 lety +1

    Ulie kuwa kalibu vyumba vingapi izo nyumban na lazima awe mkazi wa dodoma tu au mtanzania yoyote

  • @onesmojustice2348
    @onesmojustice2348 Před 3 lety

    Eti milion 70 kipato cha chini hawa jamaaa hawajielewi

  • @kakamkubwa3210
    @kakamkubwa3210 Před 3 lety

    @Tanzania mmesha tulia hela zetu hakuna masikini atakae pewa hawana uwezo huo mmejijengea nyie wenyewe mtamilikishana kwa kujuana bola mngewapa viwanja tungejua ni kweli ila sio nyumba

  • @salha6596
    @salha6596 Před 3 lety

    Kwa sisi tuliopo nje ya nchi tunapata je uduma?

    • @dostovan5142
      @dostovan5142 Před 3 lety +2

      Uduma gani,rudini kwanza

    • @salha6596
      @salha6596 Před 3 lety

      Naitaji mkopo wa nyumba nitaoataje mkopo huo nipo nje ya tz

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      @@salha6596 PIGA SIMU BENKI.

  • @tanzaboy4824
    @tanzaboy4824 Před 3 lety

    Wanakupanga wanasema kipato cha chini alafu hakuna nyumba ya milion 50

  • @ramadhanimbulu6716
    @ramadhanimbulu6716 Před 3 lety

    Fanyeni kama Kyle Libya alivyofanya Gadafi nyumba kama hizo alijenga watu wakapewa wakae bure kwa watu masikini kama sisi,unawauziaje masikini nyumba?

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      HAPO TUNGEJUWA KAMA SISI SIO MASIKINI........SIO KUBANDIKANA MADENI YA MAISHA.

  • @marcominja8850
    @marcominja8850 Před 3 lety +1

    Mnajinadi kuwa nyumba ni nafuu huku mnaogopa kutaja bei, hakuna cha unafuu hapo na pia vijumba vidogo sana.

    • @salumabdallah6680
      @salumabdallah6680 Před 3 lety

      Jenga yako kubwa sasa maana kila kinachofanywa na serikali awamu ya 6 mnaona hakifai

    • @marcominja8850
      @marcominja8850 Před 3 lety

      @@salumabdallah6680 mnaona na nani?

    • @twilamtumbi5351
      @twilamtumbi5351 Před 3 lety

      @@marcominja8850 kiswahili kigumu. Muulize vizuri

    • @sankofaman4112
      @sankofaman4112 Před 3 lety +1

      @@salumabdallah6680 huu ni mradi wa awamu ya tano. Awamu ya sita haijaanzisha mradi wowote zaidi ya mradi wa mama kubadilisha mishungi na kupiga picha.

    • @kabwelasutiviraka4765
      @kabwelasutiviraka4765 Před 3 lety +1

      Miradi ya awamu ya tano JPM mama hajaanzisha chochote zaidi ya misemo ya kanga taarabu na kubadilisha mishungi na kupuyanga na ndege . Mtamkumbuka JPM angekuwepo hizo nyumba ziko mbali sana

  • @msafiriiddy3135
    @msafiriiddy3135 Před 3 lety +1

    Sio vizuri kupendelea kukaa kwenye makazi ya watu Wenye kipato cha chini kwanza Wizi ,umalaya,wivu, kurogana, mimba za utotoni ni vitu muhimu kwenye makazi ya masikini

    • @ilynpayne7491
      @ilynpayne7491 Před 3 lety

      Kwanza kiuhalisia hizo nyumba sio za kimaskini

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 KWELI UMESAHAU NA UCHAFU WA MAKUSUDI......

    • @salimsaid7200
      @salimsaid7200 Před 3 lety

      @@ilynpayne7491 WABONGO WAMEZOWEYA KUDANGANYWA WAKIAMBIA ZA MASIKINI WANAFURAHI HAJUWI HIYO NI BIASHARA MWENYE PESA ANAUZIWA UTAONA KUNA WATU WANAFURAHIA NA KUSIFIA KAMA WAMEPEWA BURE.

    • @husseinsaid9007
      @husseinsaid9007 Před 3 lety

      Si uwongoo maana nawajuwa mm hlfu mara umepewa jini wa kujitakiA

  • @bjzee1981
    @bjzee1981 Před 3 lety +1

    Hawa walio vaa Makoti kwenye jua hilo jamani

    • @charlesngarapi8434
      @charlesngarapi8434 Před 3 lety +2

      Sasa hvi dodoma baridi

    • @bjzee1981
      @bjzee1981 Před 3 lety +1

      @@charlesngarapi8434 . Hua wana vipindi vya baridi kumbe. Au upepo

    • @edsu3092
      @edsu3092 Před 3 lety +1

      @@bjzee1981 barid tena kali

    • @bjzee1981
      @bjzee1981 Před 3 lety

      @@edsu3092 . Shukran kunifahamisha. Sijawahi kufika Dodoma hua naelewa tu ni sehem ya joto nani pakavu sana

    • @rahimdikungule3737
      @rahimdikungule3737 Před 3 lety

      @@bjzee1981 sahivi sio kama miaka ile ya 2000 kuna baridi hatare