DKT. BITEKO ALIVYOCHAMBUA MAAJABU YA TUMBO LA MWANANMKE

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 8. 03. 2024
  • Leo Jumamosi Machi 9, Makamu wa Rais Dkt. Phillip Isidori Mpango ameshiriki Kongamano la wanawake kuhusu nishati safi ya kupikia lililofanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa pia na naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko katika ukumbi wa mikutano wa JAKAYA KIKWETE
    Fuatana nasi hapa kushuhudia namna Dkt. Biteko alivyoelezea maajabu ya mwanamke
    " kwenye ajenda hii batani ya kuleta mabadiliko ya nishati safi ya kupikia hapa Nchini ni mwanamke mwenyewe wa Tanzania ,
    huyu akiweza kuibeba ajenda ,akaichukua kama ajenda yake watu wengine watafuata ,Mungu amempa uwezo wa pekee ,
    uwezo wa kibaiolojia lakini na upana wa ubongo wao amemuumba kwa namna ya ajabu sana ,tena ya kupendeza amempa tumbo
    si tu linatumika kwenye mmeng'enyo wa chakula bali limebeba uhai wa binadamu ndani yake , Mungu amempa uwezo mwanamke wakufanya zaidi ya moja
    kwa wakati mmoja tofauti sana na mwanaume ,Mungu amempa uwezo mwanamke wa kusema kidogo na kutenda zaidi ,
    Mungu ammpa uwezo mwanamke wakuwa sababu ya furaha kwa viumbe wengine duniani ,kwakweli kama unamwanamke aliyewezeshwa anayejali nishati safi ya kupikia
    hutatumia muda mingi kuzungumzia nishati safi ya kupikia bali mwanamke ataisukuma ajenda hii"

Komentáře •