HOTUBA YA RAIS MAGUFULI BAADA YA KUPOKEA RIPOTI YA UCHUNGUZI WA MADINI YA ALMASI NA TANZANITE

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 6. 09. 2017
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 07 Septemba, 2017 amepokea taarifa za kamati maalum mbili za Wabunge zilizoundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kuchunguza biashara ya madini ya Tanzanite na Almasi hapa nchini.
    Taarifa hizo zimekabidhiwa kwa Mhe. Rais Magufuli na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa Ikulu Jijini Dar es Salaam na tukio hilo limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai, Mawaziri, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa Dini na viongozi wa vyama vya siasa.
    Katika salamu zao Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge iliyochunguza madini ya Tanzanite Mhe. Doto Mashaka Biteko na Mwenyekiti wa Kamati iliyochunguza madini ya Almasi Mhe. Mussa Azzan Zungu wameleeza namna nchi inavyopoteza fedha nyingi kutokana na udanganyifu na wizi katika biashara ya madini hayo na wametoa mapendekezo kadhaa yakiwemo kurekebishwa kwa dosari za kimfumo, usimamizi na kuchukua hatua dhidi ya waliohusika kusababisha Taifa kupoteza fedha hizo.
    Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ameungana na Wabunge wa kamati alizoziunda kumpongeza Mhe. Rais Magufuli kwa dhamira yake ya kuchunguza biashara za madini hapa nchini na ametaka wananchi wamuunge mkono kama ambavyo Wabunge wanafanya.
    Kabla ya kukabidhi taarifa hizo kwa Mhe. Rais, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amezishukuru kamati maalum zilizofanya uchunguzi huo na ametoa wito kwa Watanzania kuwa wazalendo na kujenga umoja na mshikamano katika kutetea rasilimali za Taifa, ili zinufaishe kizazi cha sasa na kijacho.
    Akizungumza baada ya kukabidhiwa taarifa hizo Mhe. Rais Magufuli amempongeza Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai kwa kuunda kamati maalum zilizofanya uchunguzi huo, amewapongeza Wabunge wa kamati hizo kwa kazi waliyoifanya na ameahidi kufanyia kazi mapendekezo waliyoyatoa.
    Mhe. Rais Magufuli amewahakikishia Watanzania kuwa Serikali imedhamiria kuchukua hatua za kutetea rasilimali za Taifa kwa maslahi mapana ya wananchi na amesema inachukua hatua hizi ikiwa ina taarifa zote za udanyanyifu na wizi uliofanyika katika migodi ya madini na maeneo mengine.
    Mhe. Dkt. Magufuli amekabidhi taarifa hizo kwa viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na ameagiza uchunguzi ufanyike ili wote waliohusika kusababisha upotevu mkubwa wa fedha za umma wachukuliwe hatua za kisheria haraka na pia amewaagiza viongozi hao kuweka ulinzi katika maeneo yenye rasilimali za Taifa ikiwemo migodi ya Tanzanite na Almasi.
    Mhe. Rais Magufuli amewataka viongozi na watendaji waliotajwa katika ripoti hizo popote walipo wakiwemo wateule wa Rais wachukue hatua za kiuwajibikaji wakati uchunguzi unaendelea kufanywa.
    “Wale ambao wametajwatajwa katika taarifa hii ambao ni wateule wangu, labda ni Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Katibu Tawala wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi, inawezekana walifanya kazi mahali pengine na sasa wapo mahali pengine lakini wametajwa kwenye taarifa hii, ili vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi vizuri, ni matumaini yangu watalizingatia hili, ni matumaini yangu watakaa pembeni” amesema Mhe. Rais Magufuli.
    Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kuwakutanisha wataalamu na wajumbe wa kamati hizo maalum za Wabunge ili wajadiliane na kuanzisha mchakato wa kurekebisha sheria na mifumo ambayo inatoa mianya ya udanyangifu na wizi wa rasilimali za Taifa.

Komentáře • 102

  • @mahamoudabas8555
    @mahamoudabas8555 Před 5 lety +1

    Hongera sana Mh raisi, pia nakupongeza sana kwa kazi nzuri unayoifanya ya Taifa letu. Hapo Merelani kuna mtu mmoja ana mgodi alisha ua watoto wawili mtaani kwetu, aliwatoa sadaka ili apate Tanzanite kwenye mgodi wake. Na hakuchukuliwa hatua yoyote.

  • @khalidhamka9567
    @khalidhamka9567 Před 3 lety +11

    Waliokuja baada ya kumsikiliza tapel tundu lisuuu tujuane ccm oyeeeeeeeeeeeeee like hapa

  • @richardbagonza2031
    @richardbagonza2031 Před 5 měsíci +1

    i wish you can come back dad rip papa😭😭🌹

  • @katelengumasolwa571
    @katelengumasolwa571 Před 6 lety +4

    Well done my president go ahead

  • @dativashayo7445
    @dativashayo7445 Před 3 lety +2

    Mungu wa miungu akujalie maisha malefu upo vizuli

  • @mahamoudabas8555
    @mahamoudabas8555 Před 5 lety +4

    15 years more for you mr president for guiding our nation.
    GOOD SPEECH 👍💪

  • @wilfredsahila8727
    @wilfredsahila8727 Před 3 lety +1

    Uko vizuri president wetu; keep it up.

  • @titus_maridhia
    @titus_maridhia Před 6 lety +4

    Long live President JPM

    • @aishajami6826
      @aishajami6826 Před 3 lety

      He should have lived even after his retirement. That guy was so clever. There's quality and value in each of his words! RIP and in guidance 🤲🏽

  • @alphoncekagezi4950
    @alphoncekagezi4950 Před 3 lety +2

    Maisha tuliyonayo sio size yetu tumefika hapo kutokana na Nchi kuwekwa rehani na walio saini mikataba ambayo haikuwa na tija kwa Watanania .
    Mungu akubariki sasa tuko ktk uchumi wa kati kabla ya 2030
    Ongereni sana hata kama ujanja utakuwepo ila sio kama siku za nyuma ilikuwa hali mbaya zaidi.

  • @kidjhdf7568
    @kidjhdf7568 Před 3 lety +2

    Magu wallah sijuwi ulikuwa wapi miaka yote hiyo daaa allah akupe umri mrefu uendelee kiwajali watanzania

  • @fahdihasnuu9034
    @fahdihasnuu9034 Před 5 lety +1

    Guuuuuuuud!!!!!!!!!!!!!

  • @crazymuseven717
    @crazymuseven717 Před 7 měsíci

    Best president rip God bless you ❤Lol pole kwa family

  • @isimailimwawa2328
    @isimailimwawa2328 Před 3 lety +3

    Mara 10 uvunje sheria lakin ulinde mali za watanzania

  • @evaemil856
    @evaemil856 Před 3 lety +8

    Kwa swala la kulinda rasilimali za Tanzania, kuokoa madini kweli hapa Magu apewe sifa hapa. Kuweka ukuta kule Merilani ni poa sana. Kuhusu almasi na dhahabu kweli msema kweli ni mpenzi wa Mungu, wazungu wamevusha sana, hata wasomi vijana wa kitanzania waliosemea madini na uchimbaji iliwauma vya kutosha kuona wizi ukifanyika kwani ndege za wazungu hawa zilikuwa zinatua machimboni na kuruka mpaka na mchanga. Yote hayo baba Magu nakupa 100/100. Kwa staili hii ya uchunguzi, basi tuweke wazi waliyempiga Lissu risasi hao walitaka kumuua. Tunaimani viongozi wetu wote wanaogombea uraisi wa vyama mbali mbali na CCM wote wanania ya kuikomboa na kuiendeleza Tanzania. Sasa tusiwauwe na kuwatokomeza wananchi raia wetu wa Tanzania. Watu wasiojulikana wanakivunjia heshima yako, tafadhali watoe wazi. Always vyama vingi huleta maendeleo na tusivivunje. Raha ya mbunge ni kupaza sauti kwa mazuri na mabaya. Hatuwezi wote tukakibaliana na jambo, angalia debate tu za shule vyama vingi ni bora kuliko mfumo wa chama kimoja, au shule za mchanganyiko ni bora zaidi kuliko shule za jinsia moja. Debate hizi huwafanya watoa hoja kusimamia misimamo yao hasa mpaka mishipa inasimama. Again utumwa hatutaki, kuibiwa imetosha, na kuzuia vyama vingi imetosha. Video ya siku ya Lissu kushambuliwa itolewe.

  • @paulmbassa8203
    @paulmbassa8203 Před 2 lety +1

    He loved Silinde

  • @joshuakalinga344
    @joshuakalinga344 Před 3 lety +2

    Ubarikiwe sana Mr President jpm aongoze urais nimzalendo waukweri

  • @makumbele
    @makumbele Před 6 lety +2

    Kama nikuanza upya tuanze✔

  • @willibroadwilliam6798
    @willibroadwilliam6798 Před 2 lety

    Mwezi Mungu ijalie Tanzania ipate rais kama Hayati John Pombe Magufuli

  • @tariqmaduga8051
    @tariqmaduga8051 Před 2 lety +1

    Hii kazi ni ngumu sana hasa kua mzalendo kama JPM..itatuchukua miaka 800 kumpata tena mzalendo kama uyu JPM R.I.P. 🇹🇿MUNGU IBARIKI TZ NA SISI PIA..

  • @piusrweyemamu3900
    @piusrweyemamu3900 Před 2 lety

    Inauma sana, nikiisikiliza hotuba hii.

  • @mimimoop2617
    @mimimoop2617 Před 3 lety +1

    Tutakukumbuka mze baba rip JPM

  • @neemafaustine9815
    @neemafaustine9815 Před 3 lety +4

    RIP Magufuli...daima tutakukumbuka

  • @izrajoseph1406
    @izrajoseph1406 Před 2 lety +1

    R.I.P hero

  • @saymongwaltu9546
    @saymongwaltu9546 Před 3 lety

    Mmmmmh

  • @saxannjo6173
    @saxannjo6173 Před 3 lety +1

    Halla OUR BRIGHT PRESIDENT

  • @emmanuelbonifas3517
    @emmanuelbonifas3517 Před 3 lety +1

    Sjawah kuona chema kikadumu hivi leo magufuri aupo ktk dunia hii umelala chato na utoamka kabisa lala salama baba wengi tunakuombea kwa mungu wetu mwenye huruma akuhurumie upumzike kwa aman

  • @saxannjo6173
    @saxannjo6173 Před 3 lety +1

    ISHI SANA RAIS WETU,

  • @qasammamachinya4448
    @qasammamachinya4448 Před 7 měsíci

    🇹🇿👍

  • @ftheophili_
    @ftheophili_ Před 7 měsíci

    R. I. P JPM

  • @evaemil856
    @evaemil856 Před 3 lety +1

    Nimependa hapo sisi ndiyo wafadhili....i hope kila mtu amekupata hapo...pia hapo nani alituloga sisi? This is true. I used to say tumelogwa na aliyetuloga kafa.

  • @Wallenivo
    @Wallenivo Před 3 lety

    RIP Mzalendo wa kweli

  • @patrickmarwa5024
    @patrickmarwa5024 Před 3 měsíci

    Ukisikiliza hii hotuba ya hayati magu kuna mafunzo ya usalama wa uongozi na umakini kabla ya kupambna na hao matajiri .

  • @ezekielnjau8988
    @ezekielnjau8988 Před 6 lety +3

    President of my dreams

  • @ntegrity277
    @ntegrity277 Před rokem +1

    Kilicho muua Magufuli Ni MADINI!

  • @mremagitero5668
    @mremagitero5668 Před 3 lety

    Mpaka ichezewe ni serikal ni ya chama gan?

    • @wagadiaugustino144
      @wagadiaugustino144 Před 3 lety +1

      Swala s chama gani Bali tunaangalia kwa kipind hiki tunafanya nn,usilete ushabiki kwenye Jambo la kitaifa Kama hili

  • @yegelaabeli6066
    @yegelaabeli6066 Před rokem

    Ukweli mtupu kuwa uzarendo wa huyu baba ulikuwa wakipekee Mungu akusamehe makosa upumzike kwa awam

  • @kingmagufuliforever3144

    Asante magufuli

  • @linalinhwefwe6584
    @linalinhwefwe6584 Před 3 lety +4

    Unalaumu wazungu na ccm ndio mliwapatia vibali, ccm ndio waliokuwa wanakula rushwa ccm ndio hawajawapatia watz uhuru mabeberu walipeana uhuru kitambo.

  • @silverrichard2975
    @silverrichard2975 Před 3 lety

    R.I.P DR MAGUFULI

  • @wagadiaugustino144
    @wagadiaugustino144 Před 3 lety

    Binadamu hasa cc wenye ngoz nyeuc,hatuwez kwenda bila style ya uongoz was huyu jamaaa,mtu anashobokea wazungu wakat wao tukienda kwao wanatubagua sana.sasa haiwezekan

  • @kalonjamabura8119
    @kalonjamabura8119 Před 2 lety +2

    Your death was not natural 😢😢

  • @patrickshabani2776
    @patrickshabani2776 Před 3 lety

    Hutuba mzuri

  • @johnbabo975
    @johnbabo975 Před rokem

    Nani km magu sijaona kiongozi km yeye hata angechaguliwa tena na tena hakuna

  • @jpocherehani3498
    @jpocherehani3498 Před 3 lety

    A lkn mangu bwana mda mwingine ukijaribu kupitia hotuba zake mpka inauma sana lkni haija ujanja bwana

  • @karimkimbugimbugi6106
    @karimkimbugimbugi6106 Před 3 lety

    Kweli Lissu zaidi ya muhongo duuu

  • @joelnassari105
    @joelnassari105 Před 6 lety

    God Bless You My President...Nakuombea Maisha Marefu

  • @augustinomwageni6768
    @augustinomwageni6768 Před rokem

    Jpm

  • @richardtv8339
    @richardtv8339 Před 3 lety

    Hayo maneno cjayasikia me

  • @saranelson3114
    @saranelson3114 Před rokem

    Pumnzika kwa amani baba ye tt

  • @mohamedalaraimi6813
    @mohamedalaraimi6813 Před 3 lety

    Yule askari mpeni fursa akapumzike kidogo

  • @ambanconsultants6892
    @ambanconsultants6892 Před 3 lety +3

    Hii ndiyo hotuba ambayo Lisu anasema akowa njombe inahusiana na kupigwa kwake risasi? Naomba majibu kwa mwenye jibu maana nimeisikiliza Mara ya tatu sasa baada kusikia tuhuma za lisu kuhusu hutuba hii

    • @michaelkaniki4466
      @michaelkaniki4466 Před 3 lety +1

      Lisu anawafanya wasikilizaji matoy. Na anafanya makusudi kucheza mchezo huo was siasa chafu nilimuonea huruma lkn sio kwa maneno anayoyatoa kukashifu kazi ya mzee magu!! Wakati tumeona kabisa. Kweli tunadharaulika Sana jamn wa tz

    • @daudimichael7338
      @daudimichael7338 Před 3 lety

      Ndiyo hii, na mimi nimeiskiliza zaidi ya mara 2 natafuta hiyo kauli ya raisi aliyosema kuna mtu anapiga kelele sana anatetea mabeberu, ni msaliti hastahili kuishi sijaiona. Lisu ni mchochezi, kwa nini asishitakiwe kwa uzushi na uongo dhidi ya rais aliousema njombe?

    • @ukweliunauma4570
      @ukweliunauma4570 Před 3 lety

      Ndio hii sikiliza kuanzia dakika 10 mpka 15 hapo utasikia fumbo alilo piga, na angalia body language yake magu na macho yake, yanaonyesha anapo ongea na spika

    • @davidalphonce8444
      @davidalphonce8444 Před 3 lety

      @@ukweliunauma4570 apo Magu kaongelea kitu kingne kabisaaa.....yaan wala hajaonhelea kuhusu alichokisema lisu....nataman watu waje waitazame wakiwa na akili zao timam kabisaaa ili wajue kuwa wanadanganywa

    • @ambanconsultants6892
      @ambanconsultants6892 Před 3 lety

      @@ukweliunauma4570 hii ndiyo nchi yetu. Hatina nchi nyingine. Mfano alioutoa rais kwenye hizo dakika 10 had I 15 zinahusu MZALENDO aliyejitoa mhanga kwa ajili ya maslahi ya nchi kwa kujifanya adui ili spate taarifa za adui azilete. Siyo habari ya MSALITI anayetoa siri za nchi kwa adui. Msikilze vizuri Lissu kwenye hotuba yake ya Njombe kama hii ndo hotuba anayotuambia inahusika basi nasnza kutia shaka hali ufahamu wake. Au kwa vile anajua hawezi kuupata uraisi na yeye ameshapata uhakika wa hifadhi huko nje badi anataka kusababisha machafuko kwa makududi. Maana ukiangalia comments baadhi ya watu kama wewe mmeshaamini kila kitu anachosema hata bila kutafakari

  • @coolruler6820
    @coolruler6820 Před 3 lety +1

    Inauma ila ndo kazi ya Mungu" Mwamba alitupigania Watanzania jamani,,,lini tungeyajua haya kama Mwamba naye angelikuwa bwana tumbo,,,Rest in Power JPM

  • @ukweliunauma4570
    @ukweliunauma4570 Před 3 lety +2

    Maisha yenyewe temporary ndio upoteze watu, utume watu wasio julikana wakawauwa, sio haki, alafu sasa mnajifanya watu wa dini sasa mnafanya tobacco
    😇🤣

  • @evaemil856
    @evaemil856 Před 3 lety

    Hao wasaliti ni akina nani?

  • @adelaidaruta2930
    @adelaidaruta2930 Před 2 lety

    Baba JPM huko uliko endelea kuliombea Taifa lasirimali zetu manyangau wasiziibe miradi yote uliyoanzisha ikamilike vema nitakukumbuka daima tuombee tupate kiongozi Mzalendo kama wewe

  • @abdulseif4093
    @abdulseif4093 Před 3 lety

    Sura ya ndugu yai inaongea kitu cha hofu na wasiwasi...

  • @kennedyraymond9213
    @kennedyraymond9213 Před 3 lety +1

    Hujui uongozi wewe.

    • @michaelkaniki4466
      @michaelkaniki4466 Před 3 lety +2

      Wewe uliongoza wapi mke wa mabeberu

    • @kennedyraymond9213
      @kennedyraymond9213 Před 3 lety +1

      iyo sio hoja,hatutaki rais dikteta,Tanzania pipoooooozz

    • @michaelkaniki4466
      @michaelkaniki4466 Před 3 lety +2

      @@kennedyraymond9213 unajua maana ya dikteta?? Fikiria. Alfu usome pia vitabu. Maana kusikia sio kazi Bali kuelewa ndio kazi.

    • @kennedyraymond9213
      @kennedyraymond9213 Před 3 lety +1

      Raisi gani ambae hataki kushauriwa,tulishatoka huko zamani enzi za ukoloni.Tumeshachoka kupelekwapelekwa kama kondoo.

    • @michaelkaniki4466
      @michaelkaniki4466 Před 3 lety +1

      Lisu amesoma lkn anatamaa na anauwezo wakuwafanya watu kwamakusudi TU waamini uongo kuliko ukweli ndio maana nikiona mtanzania anakubaliana na maneno ya uongo yakumponda magu nachukiaga mpaka natamani niingie ndani ya ubongo wa huyo mtu nimuonyeshe wapi anadaganyywa na kusudi Ni nini

  • @paulmbassa8203
    @paulmbassa8203 Před 2 lety

    He loved Silinde