RAIS DKT. MAGUFULI ATOA MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU BEI YA KOROSHO NCHINI 2018

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 27. 10. 2018
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 28 Oktoba, 2018 amekutana na wanunuzi wa zao la korosho na kutoa msimamo wa Serikali kuhusu bei ya zao la korosho kufuatia kuwepo kwa mvutano wa bei ya zao hilo kati ya wanunuzi na wakulima.
    Mhe. Rais Magufuli amekutana na wanunuzi hao katika mkutano wa majadiliano uliokuwa ukiendelea kati ya wanunuzi wa korosho na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
    Katika msimamo huo Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inaungana na msimamo wa wakulima kukataa bei zilizotolewa na wanunuzi katika mnada uliofanyika hivi karibuni ambapo kampuni za ununuzi wa korosho zilitangaza kununua korosho kwa bei ya kati ya shilingi 2,717/= na shilingi 1,900/= kwa kilo ikiwa imeshuka kutoka zaidi ya shilingi 3,600 ya msimu uliopita.
    Mhe. Rais Magufuli amesema endapo wanunuzi hao hawatakuwa tayari kununua korosho kwa bei isiyopungua shilingi 3,000/= kwa kilo, Serikali ipo tayari kununua korosho kwa bei yenye maslahi kwa wakulima na kutafuta masoko yenye bei nzuri.
    “Kama hamtanunua korosho kwa bei yenye maslahi kwa wakulima, Serikali itanunua korosho kwa bei nzuri kwa wakulima na tutaihifadhi, nipo tayari hata kutumia majeshi yetu kununua korosho na tutatafuta masoko ya uhakika ili tuuze kwa bei nzuri” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
    Wakizungumza katika mkutano huo, wanunuzi wa korosho wamekubali kununua korosho kwa bei isiyopungua shilingi 3,000 kama ilivyoelekezwa na Serikali na wameomba baadhi ya tozo zinazosababisha kupungua kwa bei ya zoa hilo kwa mkulima ziondolewe pamoja na kuruhusiwa kusafirisha korosho kupitia bandari ya Dar es Salaam ambako wanaweza kupata meli zinazotoza gharama nafuu za usafirishaji wa korosho kwenda kwenye masoko ya nje ya nchi.
    Mhe. Rais Magufuli amekubali kuondolewa kwa utozaji ushuru wa mara ya pili wa ushuru wa halmashauri uliokuwa ukifanywa baada ya korosho kufikishwa Mtwara, kupunguza ushuru wa Bodi ya Korosho kutoka shilingi 17/- hadi shilingi 10/- kwa kilo na ameruhusu wafanyabiashara kununua magunia yao wenyewe kwa ajili ya korosho badala ya kuuziwa na vyama vya ushirika kwa bei kubwa.
    Kuhusu bandari ya kusafirishia korosho Mhe. Rais Magufuli amekubaliana na maombi ya wanunuzi kutaka kusafirisha korosho kwa kutumia bandari ya Dar es Salaam ambapo kilo moja inasafirishwa kwa shilingi 47/- kwa kutumia meli ambazo zimeleta mizigo mingine ikilinganishwa na bandari ya Mtwara ambako kilo moja inasafirishwa kwa shilingi 203/- kwa kutumia meli zinazokodiwa kwa ajili ya kubeba korosho tu.
    “Bandari ya Mtwara na bandari ya Dar es Salaam zote ni bandari za Serikali, mimi sina tatizo na kusafirisha korosho kupitia bandari ya Dar es Salaam lakini na nyinyi muwe tayari kutozidisha uzito kwenye magari mnaposafirisha kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, kutotorosha korosho na pia kutimiza masharti ya usafirishaji” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
    Ameagiza Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuweka utaratibu mzuri utakaowezesha usafirishaji wa korosho hizo kupitia bandari ya Dar es Salaam kama ambavyo wanunuzi hao wameomba.
    Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka wanunuzi hao kuwekeza viwanda vya kubangua korosho ama kuwahamisisha washirika wao kuja kuwekeza katika viwanda hivyo na kwamba Serikali itaunga mkono juhudi hizo ikiwa ni pamoja na kuweka vivutio vya kikodi.

Komentáře • 123

  • @mohamedkassimu8789
    @mohamedkassimu8789 Před 5 lety +10

    Mh.Rais,simamia maslahi ya wanyonge, hata mimi niliamini lazima utaliingilia Kati TU, wewe ni Rais wa mfano duniani sio tu Tanzania .mungu akulinde Sana na akupe maisha marefu.amin.

  • @lameckbalekele2901
    @lameckbalekele2901 Před 5 lety +24

    Rais 2020 usihangaike kuzunguka tena kupigakampeni tunakupakula mpaka washangae

  • @wasshaincmwanza4374
    @wasshaincmwanza4374 Před 5 lety +11

    This man is a true and patriotic leader and above all he is absolutely genius

  • @kingmayatz9999
    @kingmayatz9999 Před 5 lety +13

    Sikukupigia kula ila hakika unanidai kula yangu 2020 nakpenda huna mpinzan

  • @mohammedjuma6736
    @mohammedjuma6736 Před 5 lety +8

    Raisi wangu, Mungu akulinde na akupe umri mrefu utuongoze miaka mingi, aaaaamin, asante baba

  • @josephsospeter8304
    @josephsospeter8304 Před 5 lety +14

    Hiki kichwa nihatari kinajua mambo mengi sana

  • @yugakiyumbi9909
    @yugakiyumbi9909 Před 5 lety +30

    Mungu atupe nini, this is the best president ever. Endelea kutawala hadi uchoke mwenyewe,hakuna shida,tunahitaji Maendeleo na wewe unatuletea maendeleo na pili ww n mtetezi wa WANYONGE. Nani kama Magufuli ,We love you our President, you're doing what every well minded Tanzanian needs. Rule even 40 years,we still need you.
    Chapa kazi ,HAPA KAZI TU.

  • @mazeramatimo1110
    @mazeramatimo1110 Před 5 lety +4

    Nimeiona hasira yako Mh. Rais ukiona wananchi wako wanataka kuonewa Mungu akubariki. Nikutakie tu heri ya siku ya kuzaliwa Mungu akupe maisha, siku moja nitakuwa kiongozi na nitakuwa na nitaongoza kwa mfano wako na Nyerere,

  • @mwinukafundibombanjombe
    @mwinukafundibombanjombe Před 2 lety +3

    😭Kwenye direcrion ya Mzee Ukilaza unaondoka.

  • @rosenamilia4140
    @rosenamilia4140 Před 5 lety +4

    Mh Rais wetu JPM wewe ndie Rais muwazi,mkweli mchapa kazi, mtetezi wa wanyonge na unaetoa mwelekeo sasa wananchi wako.Mungu akupe maisha marefu Mh JPM. HAPPY BIRTHDAY RAIS WETU.

    • @kingmayatz9999
      @kingmayatz9999 Před 5 lety

      Nilikuwa mpinzani sana ila wewe ni rais unaejielewa sana nakupenda sana

  • @kaizamulinda633
    @kaizamulinda633 Před 5 lety +4

    Ila kumbe kuwa Rais si masihara. Nikisikiliza namna JPM anavyoongea kwa details na uelewa mkubwa wa mambo, najiuliza haya alijifunza lini. Anaongea vitu very technical kwa kweli.

  • @salumkseleman1470
    @salumkseleman1470 Před 5 lety +2

    Baba umenifurahisha sana asante sana mzee baba😂😂😂wanakuletea ujanja hapa wakat zao hili lina kazi c ya kitoto..... Hao wahindi wanajifanya wajanja wakat wao wenyewe ni middlemen pumbavu zao
    Asante magu baba
    Korosho yetu itanunuliwa tu alhamdulilah 👏👏👏👏👏👏👏

  • @acrestv8636
    @acrestv8636 Před 5 lety +5

    Asante sana kwa yote unayoifanyia nchi yetu ..... Kipekee kabisa napenda nkushukuru kwa ujenzi wa barabara ya Mpemba kwenda Ileje unaoendelea .... Asante sana mh rais

    • @derickgambi8627
      @derickgambi8627 Před 5 lety

      Hakika MUNGU alikuleta kwa kusudi maalum ubarikiwe sana

  • @agneomasonda2462
    @agneomasonda2462 Před 5 lety +3

    Mheshimiwa Rais nakuombea mema asante sana Mungu akupe maisha

  • @allymichael7310
    @allymichael7310 Před 5 lety +2

    Sina cha kuongeza muheshimiwa Rais wangu..mwili unasisimka kila ninapokusikiliza , unayawakilisha mawazo yangu. Mungu akulinde na kila wabaya na aina ya ubaya! Pamoja tutaijenga Tanzania.

  • @prospermakundi2787
    @prospermakundi2787 Před 5 lety +2

    Raisi wangu umenifurahisha sana,hakika unafanya kazi ya kutetea wakulima tz.

  • @greensky9607
    @greensky9607 Před 5 lety +4

    Daah! Mheshimiwa Rais sina cha kuongezea, Mungu akubariki sana

  • @acrestv8636
    @acrestv8636 Před 5 lety +3

    Asante rais wetu kwa kuwapigania wakulima ..... Mwenyezi Mungu azidi kukuongoza

    • @talenterick4209
      @talenterick4209 Před 5 lety

      Siku zote haki ikisimama malaghai wengi huumia sana wakati mwingi wanatafuta sehem wakosoe na si kutoa ushirikiano kwa yanayotendeka mh jpm pambana zid ya wanyonge usiwasikilize watakao kukatisha tamaa pambana zaid ya hapa ulipo yupo atakaye kulipa nayeye ni mwenyez mungu si mwanadam Mungu akujalie miaka mingi ili uitetee tanzania na fahari zake

  • @davidandrew9575
    @davidandrew9575 Před 5 lety +5

    Mnaenda kununua au hamuendi

  • @siwonikewilliam8832
    @siwonikewilliam8832 Před 5 lety +5

    Happy birthday Mr.President

  • @samwelmalwa9814
    @samwelmalwa9814 Před 5 lety +3

    Wanaompinga Mh, JPM watapata tabu sana maana utendaji kazi wake umetukuka sana. Hongera sana JPM, juhudi zako tunaziona,tunakuunga mkono na tunakuombea Mungu akubaliki.

  • @angelanather9640
    @angelanather9640 Před 5 lety +2

    Yaani nikimsikia Rais wetu mpendwa John Pombe Magufuli natokwa na machozi kwa furaha. Kweli ni zawadi toka kwa Mungu.

  • @danielmmbaga976
    @danielmmbaga976 Před 5 lety +4

    Hakika huyu ni raisi mtetezi wa wanyonge mungu azidi kukulinda mkuu.

  • @paulchugu9198
    @paulchugu9198 Před 5 lety +3

    Nyerere II in the house.

  • @samiahazali2027
    @samiahazali2027 Před 5 lety +1

    Mweshimiwa rais alipo xema tuzae alikuwa anamanisha angalia nchi zote zilioendelea zina watu wengi xana angalia apo wahindi wengi na angalia kwetu kira sehemu kuna duka la muyindi mweshimiwa anaona mbali xana mungu amuongoze katika majukumu yake 👍👍👍👍

  • @shukurumwangosi1537
    @shukurumwangosi1537 Před 5 lety +10

    Rais wangu nchi yangu.
    Haya tunayoyaandika tunatamani uwe unasoma mwenyewe ha ha ha
    Kiukweli Raisi wangu unawapigania wakulima wanyonge kwa kiwango kikubwa sana
    Tatizo watu wako (watendaji)wanakuangusha.
    Haya mambo sasa ulitakiwa baada ya wewe kulipigia kelele mwaka Jana ilitakiwa sasa upumzike .wanakutesa sana sana.
    Lakin tutafika tuu.
    Good job JPM

  • @susangibai2691
    @susangibai2691 Před 5 lety +5

    Hahahaaaaaa, jkt. Mtabangua korosho kwa mdomo Kweli, chezea jembe we! Hakika Mh. Rais. Unakonga mioyo ya wakulima Mungu akuongoze baba.

  • @milimomashini9432
    @milimomashini9432 Před 5 lety +4

    Nakupata vzur MH.Rais kutoka masharik ya kati kimsing hao wengi madalali huwa wanataka supernormal profit hayo matatzo mengi yako hata kwenye zao la ufuta na mazao mengine ya biashara

  • @yusuphluwali5514
    @yusuphluwali5514 Před 5 lety +7

    Huyu ndie aliekapaswa akabidhiwe nchi km alivyokabidhiwa rais wa China mpk afe

  • @user-pn9ii9iz8f
    @user-pn9ii9iz8f Před 5 lety +2

    The best leader in Africa

  • @iamjoseph795
    @iamjoseph795 Před 11 měsíci +1

    I miss you Mangufuli. Rest in peace ✌️ byou are my hero up to now from Kenya 🇰🇪

  • @siwonikewilliam8832
    @siwonikewilliam8832 Před 5 lety +4

    Happy birthday Mr.president

  • @melickzedeckmunuo190
    @melickzedeckmunuo190 Před 5 lety +1

    Mungu akubariki kwa kuwa mzalendo wa Taifa letu tunakuombea sana wana nchi wamenyonywa sana

  • @paulshamba1746
    @paulshamba1746 Před 5 lety +2

    Mungu akulinde maana wewe ni mtetezi wa kweli

  • @mwamengele
    @mwamengele Před 5 lety +1

    Nimejialika,..! Hehee umetisha mzazi

  • @jenyyusuph4973
    @jenyyusuph4973 Před 5 lety +2

    Kwaajili ya maendeleo yanchi yetu huyu baba alizaliwa mungu ulitupa Bure zawad ya jpm mlinde muongezee muda waungozi siku kwasikuamina

  • @raphaelpaschal7892
    @raphaelpaschal7892 Před 5 lety +3

    mzee hongera sana jitahidi ufike maswa wananchi tunatahabika maji ayatoki wilaya nzima wiki ya tatu sasa fatilia mzee maji ni uhai

  • @isackjuma7973
    @isackjuma7973 Před 5 lety +4

    VIVA magufuli VIVA

  • @japhetmombia
    @japhetmombia Před 5 lety +1

    Mungu akulinde Mh.Rais

  • @makumbele
    @makumbele Před 5 lety +3

    Ukisikia Raisi basi ndio huyu.

  • @jerichoseth4188
    @jerichoseth4188 Před 5 lety +2

    haki ya Mungu ingekuwa ni amri yangu huyu Rais angeendelea angalu hata miaka ishirini maana kumpata kama huyu tena ni mtihani japo nina amini wapo ila kumpata ni shughuli kubwa.

  • @hyeragerald4442
    @hyeragerald4442 Před 5 lety +3

    Nawaza cha kufanya ili kukuongezea muda wa uongozi. Hakuna namna

  • @edwinmalale1513
    @edwinmalale1513 Před 5 lety +3

    ohooo hii ya kubangua kwa mdomo tusiende kichwakichwa asije akaangiza watanzania wote wabangue kwa mdomo

  • @Antibeberu
    @Antibeberu Před 5 lety +3

    Bravo JPM

  • @khadijaabdalla1011
    @khadijaabdalla1011 Před 5 lety +3

    This is my president. ..

  • @allyabbas4793
    @allyabbas4793 Před 5 lety +7

    Rais wa wanyonge

  • @mswadikubushumbilo7170

    mzee umenifurahisha speech yako yale,

  • @salumkseleman1470
    @salumkseleman1470 Před 5 lety +2

    Asante baba jkt na majesh yetu yote hata kwa mdomo👏👏👏👏😂😂😂😂

  • @oscarmisiru9725
    @oscarmisiru9725 Před rokem

    This is the Man of Yes and No, no mbambamba

  • @BennyChristian
    @BennyChristian Před 5 lety +2

    Kweli kabisa wakilaza = kilaza, fukuza tu, hata hii bodi jipu tu, watu wanunue tu hata wauza dagaa wanaweza jalibisha biashara ikiwashinda watavulia samaki

  • @jacksonrwebangira9446
    @jacksonrwebangira9446 Před 5 lety +2

    What a great president!

  • @jamesngundateresia2600
    @jamesngundateresia2600 Před 5 lety +3

    BABA DUNIA ZIMA INAKUTAMANI UJUE UNA MADINI YASIYOISHA ALIKUZAAA ANASTAILI SIFA ZOTE
    DUU HATUWEZI PATA TENA MTU HUYU MIMI NASEMA
    HATA AKIPATIKANA ATAFIA TUU JANGWANI MAANA NCHI WATU KARIBIA WOTE NI WATUMWA WA WA WATU WEUPE TUU

  • @furahamwajeka3708
    @furahamwajeka3708 Před 5 lety

    nakuelewa sana baba magu thanx maana kuongoza ni kazi sana baba piga kaziiii

  • @newtonmunenekaibiria6623
    @newtonmunenekaibiria6623 Před 5 lety +12

    Hakika huyu ni mtetezi Wa wanyonge. Kongole Rais.

  • @mswadikubushumbilo7170
    @mswadikubushumbilo7170 Před 5 lety +1

    mzee tunakukubali,we ni Rais wa wanyonge,asiekubali akafie mbali,

  • @hilalihashimu5693
    @hilalihashimu5693 Před 5 lety +1

    Mr Prisedent anglia uwezekano wa shirika la Tanganyika perkas yale maeneo ni muhimu sana kwani yamesahaulika kwa muda mrefu sana

  • @geraldlazaro4523
    @geraldlazaro4523 Před 10 měsíci

    Yessssssssssssssss assessed tanzaniaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

  • @kareembesta1057
    @kareembesta1057 Před 5 lety +1

    Good Mr president"

  • @sabatojoshwa6684
    @sabatojoshwa6684 Před 5 lety +1

    Hadi Bodyguard ametabasamu!!! Heshima yako mzee Magufuli

  • @musamakuka8319
    @musamakuka8319 Před 5 lety +1

    Ibadilishwe tu katiba ya Tanzania uwendelee mbaka kuzeeka kwako ayupo mwingine wa kuvaa viatu vyako

  • @jilugalamarco9308
    @jilugalamarco9308 Před 5 lety +3

    good president

  • @mwalamimtupa4728
    @mwalamimtupa4728 Před 5 lety +1

    Jpm ever domination...we love u mo

  • @alvangidion9366
    @alvangidion9366 Před 5 lety +3

    Mr president anaijua korosho

  • @samwelhechei8537
    @samwelhechei8537 Před 5 lety +1

    Hongera sana mkuu,

  • @ezekielnjau8830
    @ezekielnjau8830 Před 5 lety +1

    Huyo ndio mh. JPM, my favourite president

  • @tajinehemia3961
    @tajinehemia3961 Před 5 lety

    Mungu Akuzidishie Hekima Na Maarifa Raisi Wetu

  • @alvangidion9366
    @alvangidion9366 Před 5 lety +1

    My President big up

  • @mussambilu229
    @mussambilu229 Před 5 lety +1

    safisana

  • @salimamri9488
    @salimamri9488 Před 5 lety +2

    🔥🔥🔥🔥

  • @athumanomary1438
    @athumanomary1438 Před 5 lety

    Mwenyez MUNGU yupo pamoja nawe raisi wetu

  • @petercosmas4376
    @petercosmas4376 Před 5 lety +4

    Nmeona mzee mmja kama haelewi kabisa,hahaaaa

  • @pascalgwandu1657
    @pascalgwandu1657 Před 5 lety

    mungu akulinde siku zote!

  • @michaelmrosso2106
    @michaelmrosso2106 Před 5 lety +2

    😂😂 hata kwa meno jesh litabenguaa korosho..

  • @athumanomary1438
    @athumanomary1438 Před 5 lety +1

    Ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kuyapa nguvu majeshi yetu yote ewe mwenyez MUNGU mkuu

  • @fbr5113
    @fbr5113 Před 5 lety +1

    Nawapongeza sana Ikuilu mawasiliano pia kwa kuanzisha vyombo vyenu vya habaria na kwenda na wakati kama hivi mana hao waandishi wa TZ wengi tumeshawashtukia washanunuliwa na magaidi wa mabepari, wanakimbilia kutangaza habari za kuvuruga nchi zaidi kuliko habari za kuikomboa nchi. Watu wa hivyo wote wachunguzwe na wanyang'anywe uraia, tunataka watanzania wanaoitetea nchii kama Rr. Magufuli sio kuteketeza nchi na Wananchi.

  • @charlesmakuri792
    @charlesmakuri792 Před 5 lety +1

    Wale wanao jiita wapinza huwa hawakosi kukosoa watatia ujuaji wao et wao ndio wanajua ,upinzani huu ni chuki matusi na lawama ,zito atakosoa tu

  • @jumaulamba25
    @jumaulamba25 Před 5 lety

    Hongera mtetezi wa wanyonge

  • @isayaupson7712
    @isayaupson7712 Před 5 lety +1

    Mheshimiwa tunaomba tuangalie upande wa mbaazi hali ni mbaya kilo mia mbili 200 mkoa wa manyara

  • @mochings8012
    @mochings8012 Před 5 lety +2

    43:50 😅😅

  • @suleimanbakar1271
    @suleimanbakar1271 Před 5 lety

    baada yale kuongelea issue anazunguka kross

  • @yakoboisack9054
    @yakoboisack9054 Před 5 lety

    jamani acheni siasa tunataka ela hadi mwezi wa kumi na mbili hatujapata ela kama hela haipo wapeni wahindi wanunue

  • @shifumponda666
    @shifumponda666 Před rokem

    Kweli ulisema tutakukumbuka kweli nakukumbuka sasa

  • @mbwanaomary7537
    @mbwanaomary7537 Před 5 lety

    Raisi bora wa muda wote

  • @maxmilliankibura1047
    @maxmilliankibura1047 Před 5 lety

    Mbele itabaki kuwa mbele tu speed hainashida nakuunga mkono raisi wangu hata kama tunaspeed ndogo naamini mbele tutafika tu HAPA KAZI TU

  • @Michael-dl1lu
    @Michael-dl1lu Před měsícem

    ❤❤❤❤❤❤❤❤❤🎉🎉🎉🎉🎉

  • @japhetmwamlenga7078
    @japhetmwamlenga7078 Před 5 lety +1

    ndo uzuri wa
    kuchagua rais msomi huwezi kumdanganya.

  • @fraviansweetberty8819
    @fraviansweetberty8819 Před 3 lety

    Leo ih atupo nawewe Jpm pumzika kwa Amani

  • @ramadhanimgaya8287
    @ramadhanimgaya8287 Před 5 lety

    Piga kazi Mr President, Watanzania tupo pamoja nawe

  • @fbr5113
    @fbr5113 Před 5 lety +1

    Tawala miaka yote Magufuli, hadi hao majambazi wa mabepari wakimbie nchi, kwanza wote wale sio Watanzani wanatumwa kuivuruga nchi. Kwa mwendo huu uwezo wa kuiendesha nchi unao hata bila msaada wa wanyonyaji wa nje, sisi hata njaa tutalala mradi ututoe utumwani, kunyonywa Tanzania ibaki kuwa historia, unaonesha njia ambayo wengi walishindwa kwasababu walikwamishwa na kuwaogopa hao wahalifu wa mabepari. Magufuli oyeee

  • @nyakytito4954
    @nyakytito4954 Před 5 lety +1

    nitaasisi maandamano ya kupinga kuondoka madaraka kwa anco magu bado tunakuhitaj

  • @mongliclassic5642
    @mongliclassic5642 Před 5 lety

    Ndomaana 2nakunda Rais. Jpm

  • @singinowelnel4656
    @singinowelnel4656 Před 5 lety

    Pongezi ziende kwa John

  • @dickngimba4333
    @dickngimba4333 Před 4 lety

    Kwanini mzee usiongeze mika 30 mzeee

  • @avax5717
    @avax5717 Před 5 lety

    Natamani nione jinsi jeshi linavyobangua korosho kwa meno.. Lol

  • @salumkseleman1470
    @salumkseleman1470 Před 5 lety +1

    👏👏👏👏😂😂😂😂😂👏👏👏👏

  • @suleimanbakar1271
    @suleimanbakar1271 Před 5 lety

    kigeugeu

  • @najimcompanyltd2096
    @najimcompanyltd2096 Před 5 lety

    kama nikijana alafu huumpend magufuli inabidi ukapimwe akilii

  • @geraldlazaro4523
    @geraldlazaro4523 Před 10 měsíci

    Mangu baba says

  • @stephenshio588
    @stephenshio588 Před 5 lety +1

    Hongera President hili ndo tulikuwa tunalitaka kwa wananchi fukara

  • @athumanomary1438
    @athumanomary1438 Před 5 lety +1

    Ewe mwenyez MUNGU tunazidi kukuomba enderea kumuongoz kumsimamia kumrindi na kuzidi kuimalisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU pia enderea kuwaongoza vyema viyongoz wete wanaomsaidia raisi wetu turiongoza taifa retu