CHALAMILA AWA MBOGO SAKATA LA WAFANYABIASHARA KARIAKOO, ATAKA MAJINA 891 YAFUTWE

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 11. 07. 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Albert Chalamila ameagiza kuondolewa majina 891 ya wafanyabiashara yaliyowekwa kwenye mtandao wa Shirika la Masoko Kariakoo mpaka pale vyombo vya dola vitakapojiridhisha na majina hayo.
    Hatua hiyo inakuja baada ya wafanyabiashara zaidi ya 800 waliokuwepo sokoni hapo kabla ya soko kuungua Julai 2021 kuandamana jana Alhamisi, Julai 11, 2024 kwenda Ofisi za CCM Lumumba kupinga kutorejeshwa.
    Katika orodha hiyo, wafanyabiashara 891 kati ya 1,861 ndio walioelezwa kuwa na vigezo vya kurejea. Uamuzi huo uliwafanya kujitokeza katika viwanja vya Mnazi Moja kuhakikiwa na baada ya kutoridhishwa ndio wakaandamana.
    Chalamila ametoa maagizo hayo leo Ijumaa Julai 12, 2024, alipozungima na uongozi wa Shirika la Masoko Kariakoo katika Ofisi ya Shirika la Masoko Magogoni.

Komentáře • 14

  • @binsherbal6089
    @binsherbal6089 Před 23 dny +5

    Hebu nyoosha maneno, Rais amelipa!!!??? Hapo hapo unasema ni Kodi zetu walalahoi!!!??? Amelipa Rais au tumelipa sisi? Hii kauli inakera sana, Kila kitu Rais kafanya Rais kafanya Rais anatoa wapi pesa? Mbona mambo yakiharibika hamsemi kama Rais kaharibu? Kila kitu ni Uchawa tu siku hizi.

  • @hamidabarraball3162
    @hamidabarraball3162 Před 23 dny +3

    Yaani kila kiongozi akitoa hutuba lazima amtaje rais zaidi ya mara kumi, inatia aibu sana, tunaona nchi za wenzetu raisi hasifiwi kiasi hicho

  • @user-hi8le2vb7z
    @user-hi8le2vb7z Před 23 dny +1

    leo ajastua leo😊

  • @hudhaifamsafiri8731
    @hudhaifamsafiri8731 Před 23 dny +1

    Kwan wakuu wetu hawawezi kufanya kazi bila kumuusisha Raisi

  • @gmdigitostore8550
    @gmdigitostore8550 Před 23 dny

    Hapo safi. Kibano hicho.

  • @maimunaathumani9121
    @maimunaathumani9121 Před 23 dny

    Kweli mkuu wengine pale kariakoo walisishana familia zima sisi twende wapi

  • @GeorgeSikazwe-mm7nn
    @GeorgeSikazwe-mm7nn Před 22 dny

    😂 hii nchi bhn..serikali nd inalipa ww

  • @faustinluambano2958
    @faustinluambano2958 Před 23 dny

    Huyu naye.

  • @mbwanakiting7180
    @mbwanakiting7180 Před 23 dny

    Tuliambiwa pesa katoa maamaa na serikalli sasa shirika limeweka mtaji gani?

  • @evamacha4861
    @evamacha4861 Před 23 dny

    Mkuu wa mkoa nadhani unakumbuka soko la.mbagala zakgiem ulituuza sana kwa kutudanganya kuwa ukiona kuna mafisadi lakini ulitudanganya soko la zakhiem uliweka wafanyabiashara wapya badala ya wale waliopisha soko kujengwa.ulifanya dhambi kubwa sana bado tunalia machozi ya damu na mungu pekee ndio natafuta machozi yetu.

  • @user-tn7ic2ky3i
    @user-tn7ic2ky3i Před 23 dny

    Aneye lipa ni Samiya ao ni serikali acha uchawa

  • @user-xk7vy4gb6g
    @user-xk7vy4gb6g Před 23 dny

    Soko la ccm hilo

  • @hebronmwamwaja7660
    @hebronmwamwaja7660 Před 23 dny

    Siyo ameripa tumeripa acheni ayo mambo ya uchawa tumeripa

    • @edsonnelson4464
      @edsonnelson4464 Před 23 dny

      Amelipa tumelipa au tutalipa tusiharibiane kiswahili