Taharuki makaburi 19 yakibomolewa na wasiofahamika Tabora

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 5. 07. 2024
  • Katika hali isiyokuwa ya kawaida watu wasiofahamika wameyavamia na kuyavunja makaburi 19 yaliyopo Mtaa wa Magubiko kata ya Kiloleni Manispaa ya Tabora, huku tabia hiyo ikitajwa kuwa imekuwa ya ikijirudia kwa matukio tofauti yanayofanana na hilo.
    Alexander Ntonge aliyezika ndugu yake hivi karibuni, amesema yeye alipigiwa simu kuwa umetokea uharibifu wa kuvunjwa makaburi na kwamba kaburi la babu yake limebomolewa.
    Peter Kubingwa ni mwenyekiti wa mtaa wa Magubiko kata ya Kiloleni amesema vitendo hivyo ni vya kusikitisha.
    Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amesema: “Nimepata taarifa za makaburi kuvunjwa na watu ambao hawajafahamika, tayari uchunguzi unaendelea ili tuwabaini waliofanya uhalifu huo na kisha hatua kali dhidi yao zichukuliwe.”

Komentáře • 5