CASSIAN AMKEMEA PASTA TON KWA KUPOTOSHA MAFUNDISHO POTOFU EV PASCHAL CASSIAN

Sdílet
Vložit

Komentáře • 665

  • @JACKLINEMAHENGE
    @JACKLINEMAHENGE Před dnem +14

    I've never been attentive to pastor Tony preachings but i think he's so much into celebrities world he loves to associate with those kinds, he maybe be have his valid reasons and i pray that the darkness from that side may not overpower the anointing in him if there is any

  • @isdommushi9536
    @isdommushi9536 Před 22 hodinami +2

    Ubarikiwe na Bwana Yesu Mch. Cassian kwa kufanya kazi ya mhubiri wa Injili. Mtumishi wa Mungu hapaswi kuwainua watu wenye roho ya Mpinga Kristo, watungao na kupenda nyimbo zenye uwezo mkubwa wa "mind & spiritual pollution", kuwainua katika madhabahu ya Kristo ni jambo la upotofu. Watoto wamemezwa na nyimbo chafu, vyombo vya habari, vyombo vya usafiri, kila mahali, "mind pollutants are at work", sasa hata kanisani kwa watumishi wa Mungu jamanii?! Hapana. Mambo haya ynapaswa kukemewa kwa neno la hekima.

  • @musachomoitson2350
    @musachomoitson2350 Před 19 hodinami +4

    Mungu akuzidishe paschal, unaifanya kazi yake vizuri na usione uko pekeako ktk kusema kweli, pambana sana na uovu bila kusita maana MUNGU amejisazia wengine wa kuungana na wewe ktk kusema ukweli... Amen

    • @rilekijuma4024
      @rilekijuma4024 Před 8 hodinami

      Kusema ukweli ni kuhubiri injili sio kukosoa watumishi kama humuelewi mtu kaa kimya mnajichumiaga ma laana hivi hivi

  • @dh-bioproducts8205
    @dh-bioproducts8205 Před 2 dny +8

    Hukumu ni ya Bwana. Sisi yetu ni kuitangaza na kuifunua kweli ya Kristo Yesu

  • @user-gj2gc4en3t
    @user-gj2gc4en3t Před 3 dny +23

    Pst ton alijificha nilimutambua mwaka mumoja uliopita kashajichanganya kitambo, but wewe mtumishi mungu Akulinde na tunakuombea na tunakupenda sana sana niko Mombasa kenya

  • @kingsonkambey1436
    @kingsonkambey1436 Před 4 dny +32

    Muonye,mkemee,mkaripie waziwazi bila kuogopa kitu chochote Paulo anamuagiza Timotheo kufanya hivyo Amen!!

    • @ruthmuja7792
      @ruthmuja7792 Před 4 dny

      Amina Amina

    • @RwidhiaRichard
      @RwidhiaRichard Před 4 dny

      MKOMBOZI MITIMINGI HERBAL CLINIC UPONYEKE NAWE UKAFANYIKE SHUHUDA KWA WATU WENGINE TUNA DAWA ZA ASILI ZA TIBA MBALI MBALI ZILIZOTHIBITIKA KUWEZA KUTIBU MAGONJWA MBALI MBALI KAMA VILE :kina dada
      huyo HAPA MITIMINGI TRADITIONALCLINIC
      Anatibu fangasi sungu ukeni na U.T.I sungu
      (2)P. I . D .Maumivu wakati wa tendo la ndoa na halafu mbaya ukeni .
      (3) Mirija ya uzazi uliolegea .
      (4)Maumivu ya tumbo chini
      ya kitovu na changu
      (5)UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
      (6)BAWASIRI AU HEMORRHOIDS )
      BAWASIRI YA NDANI NA NJE
      (7)PRESHA ,SUKARI NGIRI N.K
      (8)LIFE CARE;dawa ya asili yenye uwezo wakuboresha kinga za mwili ni msaada pia kwa wenye virusi vya ukimwi _dawa zote zina kibali cha wizara ya afya kitengo cha tiba mbadala
      WASILIANA NASI KUPATA DAWA piga 0673060366 WhatsApp ♥

    • @jenifferjasper1369
      @jenifferjasper1369 Před 15 hodinami

      Wewe na familia Yako mtakemewa waziwazi mpaka mshangae

  • @andrewmwakabela8686
    @andrewmwakabela8686 Před 4 dny +21

    Kwanza n kosa kubwa sana mbele za mungu kuimba nyimbo za dunia madhabahun haiwezekan kinywa ichoicho kitoe maji masafi na machafu. Enhe mola tusaidie

  • @kelkel4483
    @kelkel4483 Před 4 dny +16

    Kuwataja Hao aliwataja aliwataja katika angle ya kumaanisha kwamba Hao wasanii wanauwezo wa kumrudia na kumtumikia Mungu sema basi tu ni kwamba hawajui,maana yesu alikuja kwa wenye dhambi kwa hiyo na Hao wasanii Wana nafasi ya kubadilika,na pia kama wanaweza kushawishika wakatunga nyimbo ya kumsifu Mungu haitokua na shida yoyote,so wakati wa mungu ni wakati sahihi so anajaribu kuwashawishi wake kundini like kuwin their soul.. so ulitakiwa uanze mwanzo wa kongamano mwanzo mwisho,sasa kama atakua amekosea labda kwa angle za level za kitumishi kwenye vyama vyenu huko..,so shida sio Nani kaimba ila ni nini kimeimbwa,ndio maana rahabu kahaba nae alitumiwa kufanya kazi ya Mungu,so it's possible kwa uelewa wangu mdogo

    • @Samsonnoahndagw
      @Samsonnoahndagw Před 4 dny +2

      Afadhali umekiri kwa uelewa mdogo

    • @user-ll6pj1lg3e
      @user-ll6pj1lg3e Před 3 dny +1

      umenena vyema

    • @sigimwangombola5915
      @sigimwangombola5915 Před dnem

      Bora ungenyamaza tu

    • @gitongaz
      @gitongaz Před dnem

      Mimi hungojea sana mungu anifunulie wahubili wa uongo, tena na wale wa ukweli , kabla ya kutaja mtu, Kisha niedee hizo kondoo hizo simepotea ,Dunia inahitaji unabii wa mungu Ili injili ikubalike bele za mungu

  • @AmyeSanga
    @AmyeSanga Před 4 dny +32

    Kanisa la Sasa tunashindwa kutofautisha mhubiri na inspirational speaker.kisa Kuna kamstari ka Biblia tunadhani ni mhubiri .Hakika Mungu atupe macho ya kuona maana tuna macho ya kutazama tuu huku fahamu zetu zikiwa zimefungamana na kutazama

  • @user-ru6ct4rh3t
    @user-ru6ct4rh3t Před 4 dny +16

    Mtumishi wa Mungu Asante nashukuru. Naomba uniwezeshe kuchanga chochote kwa kazi hii ya mtumishi wako.

  • @user-yz3rl8pd6q
    @user-yz3rl8pd6q Před 2 dny +5

    Barikiwa sana mtumishi,
    Endelea kuwakosoa watumishi wa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Wengi ni matapeli kwa sasa, wamepotosha asili ya Neno la Mungu. Wamekalia mafanikio, sio Neno lakweli la Mungu. Wanaendelea kupoteza utakatifu wa Tanzania katika uso wa Mungu.

  • @Godlovesyou1857
    @Godlovesyou1857 Před 2 dny +6

    Thank you, God, for this Revelation message 🙏🏾 it’s 1:28 am 7/7/2024 watching this beautiful message… Ubarikiwe sana Mtumishi
    🇺🇸

  • @keruboirene
    @keruboirene Před 4 dny +9

    You make me cry 😭 every i listen 👂🏾 your preaching 😭 i hope my kids will never leave my teaching 😢
    Eeh MUNGU saidia watoto wangu.kwa jina la YESU KRISTO naomba 😭🙏🏾🙏🏾🙏🏾Amena

  • @tujajackson8142
    @tujajackson8142 Před 4 dny +33

    Nimegundua mtu kukosa unyenyekevu mbele za Mungu akiwa madhabahuni huwa kuna kujisahau na kwenda nje ya mstari wa kweli aloo.watumishi tujifunze kumentain annoint bila hivyo ni hatari tutaongea ya kwetu.hongera paskali kws hapo nakupongeza

    • @piusbaruhuwundi8987
      @piusbaruhuwundi8987 Před 3 dny

      Hii imewakuta hata manabii wengi. Wapo waliofika sehemu wakajisahau na Mungu akawakataa

    • @AmyeSanga
      @AmyeSanga Před dnem

      @@tujajackson8142 ni kweli Mungu akimutambulisha mtu kwa watu badala ya kumuachia Mungu utukufu anaupokea yeye Mungu anakaa pembeni tunaanza kuona madhaifu yake maana aliyemsitiri anaondoka

  • @ellymtenga8127
    @ellymtenga8127 Před 2 dny +4

    Mungu akubariki sana Paschal unahubiri injili ya kweli be blessed man

  • @laurentraphael5470
    @laurentraphael5470 Před 4 dny +31

    Huyo mpuuzi tangu alipojiunga na ma charlatan kina Ubert angel, kina Bushiri waabudu mashetani ndio amepotezwa kabisa. My Brethren, kanisa limevamiwa na mashetani mbwa mwitu wakali. Pasipo maarifa ya kiroho umekwisha na kuangamia kabisa.

  • @prophetjohnmasso186
    @prophetjohnmasso186 Před 4 dny +15

    Umeongea ktk ukomavu sana kiimani Mungu akutunze akufiche mikononi mwake

  • @user-cw8zn2dn6m
    @user-cw8zn2dn6m Před 4 dny +5

    Ww kweli ni mtumwa wa Mungu. Hakika ww ni nuru. Hakika. Paschal uinuliwe juu Mbinguni. Amen.

  • @user-dq1ss2uq6u
    @user-dq1ss2uq6u Před 4 dny +14

    Asante mtumishi ..ni hatari kuizoea madhabahu

  • @user-tw9td1qy6l
    @user-tw9td1qy6l Před 2 dny +4

    Watching from Kenya,tuweni makini maana hatujui siku wala saa ya kuja kwake Yesu 🙏 tunaweza sema mmoja ni mkweli kuliko mwengine lakini siku moja yaja😂😂 hukumu itamkuta kila mtu..lets be wise 🙏

    • @GraceMuthoni-nz3fh
      @GraceMuthoni-nz3fh Před 2 dny

      Apo umenena

    • @kelvinmbogela4718
      @kelvinmbogela4718 Před dnem

      Kuwa makini haimaanishi kutosema kweli ya Kristo. Acha aseme kilichosahihi kwani yeye hayuko responsible kwako bali kwa anayemtumikia

  • @hopekatemba7861
    @hopekatemba7861 Před 16 hodinami +3

    Yesu aliufia ulimwengu mzima,Tony uzidi kwenda mbele

  • @user-dt5wp5qo4n
    @user-dt5wp5qo4n Před 2 dny +3

    Nabarkiwa kwa mafundisho yako mchungaji pascal,mungu akupe maisha marefu,

  • @ruthhamisi2902
    @ruthhamisi2902 Před 4 dny +21

    Yesu anarudi jamani, tusaidiane, ukiona mwenzako anaenda tofauti na maagizo, na amri za mungu ,tuonyane sisi kwa siku,Mungu baba anatupenda sanaa

  • @ndojes711
    @ndojes711 Před dnem +5

    Kukosoa sawa ila kusifia Aaaaaaaaaaah........ WATU TUMEOKOKA, TUMEACHA POMBE, SIGARA, Hutukuti Kidimbwi, hatukeshi COUNTER, saiv tunakesha LEADER'S CLUB kwa MUNGU hamuon hlo. MAN of GOD fundisha neno, acha kufundisha kupitia mifano ya huduma za watu 😢😢,. Ingia CHEMBA MUOMBEEEE KAM UNAHC ANAKOSEA,. Utakuw hauna tofauti na MAFARISAYO sas

  • @EnockMatembele
    @EnockMatembele Před 3 dny +4

    Mungu akubarik sana mjoli wa Bwana,, akupe nguvu na maono Zaid amen

  • @phillipowwilliam1131
    @phillipowwilliam1131 Před dnem +2

    Acha kuponda watumishi wewe siku ya mwisho ukifika mbinguni hautaulizwa uliwaponda watumishi wangapi utaulizwa, how many souls have you win so sir I respect you go and win souls, achana na watumishi maana haujui wamewekewa reveletion gani

    • @stevenalex9121
      @stevenalex9121 Před dnem

      Wewe revelation ya Paschal unaijua? Je kama hicho anachokifanya ndio revelation yake

  • @princenelsonsinko5237
    @princenelsonsinko5237 Před 4 dny +7

    2Wakoritho 6:4 bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;
    14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
    15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?
    16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
    17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

  • @PeterSimoni-th2re
    @PeterSimoni-th2re Před 18 hodinami

    Kifupitu mtumishii miniko nanyimbo zako zotee napenda sana unachokihubiri kupitia njia ya nyimboo Mungu akubarikii

  • @SuzanneMyles
    @SuzanneMyles Před 17 hodinami +2

    😢😢😢😢God katikati ya ghadhabu kumbuka rehema😢❤

  • @bahatadof5543
    @bahatadof5543 Před 4 dny +13

    Hivi Toni ni mtumishi wa Mungu au inspirational speaker ili baadae awe Mwana siasa

    • @ShawnBeatz
      @ShawnBeatz Před 4 dny +1

      umeona mbali sana! religion sikuizi ni stepping stone tu!

    • @FridayMwassa
      @FridayMwassa Před 4 dny

      Mwanasiasa yukoje na muhibiri yukoje,siasa ni kuleta Maendeleo kwa watu bila kuumiza wengine na kutaza kufanya mabaya hali kadhalika dini ni vivyo hivyo

    • @mshindimpangala731
      @mshindimpangala731 Před 3 dny +4

      Man of God,kama humuelewi mtu anae sema yeye ni mtumishi wa Mungu kwa kukosa mafunuo,nyamaza usiseme vitu huna uhakika.....laana nyingne zinaepukika

    • @SisterDuu
      @SisterDuu Před 3 dny +2

      Uko busy kujadili maisha ya mutu wakati maisha yako mwenyewe ya nakushinda unaacha kushuulikia ndoa yako au watoto wako wewe uko busy kujadili mutu

    • @obbytouchez_pro9430
      @obbytouchez_pro9430 Před 2 dny

      🤗​@@SisterDuu

  • @estermathias8354
    @estermathias8354 Před 4 dny +9

    Paschal YESU akutunze tu.nakwel hatuchangamani.

  • @ruthhamisi2902
    @ruthhamisi2902 Před 4 dny +6

    Mungu anatumia watu wake, kuonya na kurekebishana ili sote tuende mbinguni, hapendi tuanze vizuri na tumalize vibaya anaumia sana mungu baba, sababu anatupenda saaaana kama baba

  • @cydrahope5251
    @cydrahope5251 Před dnem +1

    Wewe unayedhani umesimama angalia ......... I respect anointing ya Kapola God keep you man of God 🙏 hata Yesu alikosolewa sana na mafarisayo 😅

  • @EvarineMdaki
    @EvarineMdaki Před 4 dny +3

    Pastor Casian. Be blessed. Endelea kuihubiri KWELI.

  • @mashande2373
    @mashande2373 Před 6 hodinami

    P T ...nakutambua sana baba keep the real gospel in town lazima utasemwa baba muhimu wako mahusiano yako na MUNGU wako#sisi ni wale tunaosaidiwa na bwana

  • @GloryLubango-tv4hd
    @GloryLubango-tv4hd Před dnem +2

    Hubirini injiri, msikae kukosoana, Nan kasema nn au kafanya nn, tunamuda mchache Yesu yukaribu kuja, na Kama mkristo mwenzako kakosea ungemfata binafsi na sio kutuhubiria sis kumuhusu, unapohubiri ww hubiri kweli ya MUNGU watu wamjue MUNGU na wajue kupambanua kila mmoja Kwa binafsi yake kupitia Roho mtakatifu, mfate umwambie Kwamba ndugu yangu Hapa unakosea

  • @ZakayoKalinga-nq5qy
    @ZakayoKalinga-nq5qy Před dnem +1

    Ubarukiwe na Mungu sanaa MWalimu @Cassian

  • @Franckmulaj-Officiel
    @Franckmulaj-Officiel Před 4 dny +13

    Ni mapepo muchafu inawaongoza awa wantu, brother pascal,ayifayi kumwita ule kijana pasta,asistahili ,kwitiwa pasta.

  • @theonestrenatus954
    @theonestrenatus954 Před 3 dny +4

    Mungu akubariki sana Cassian umenena vyema sana, sasa wahubiri wanaangalia pesa tu

  • @zaralsham3257
    @zaralsham3257 Před dnem +1

    Mungu tutie nguvu safari ya mbinguni ni Ngumu sana Mungu atusaidie tuanze na roho tumalize na roho😢,, niwengi walianza na roho ila sas wamejikuta wanamaliza na mwili😢

  • @jovettedenise2591
    @jovettedenise2591 Před 4 dny +9

    Mungu akupe uvumilivu na mwoyo mugumu manaa hiyi kazi ningumu sana❤️❤️❤️

  • @alexandernyambo7739
    @alexandernyambo7739 Před 4 dny +4

    MUNGU AKUBARIKI BRO CASIAN.... WEWE NI POLISI WA KIROHO. NAKUOMBEA SANA NA NAKUPENDA SANA KWA UKWELI WAKO WA 100%

  • @ev_abediespoir490
    @ev_abediespoir490 Před 4 dny +2

    Ameeeeen!!! Mtumish wa Mungu, lihubirini neno, Onya, karipia na kukemea pia. Natumai Mungu wa mbinguni yupo pamoja na ww

  • @Pendopasilika
    @Pendopasilika Před 4 dny +10

    Amen ameni tena ameni nabarikiwa mno MUNGU wa mbinguni akutunze baba

  • @Loyalnaxhon
    @Loyalnaxhon Před dnem

    Amenii mpendw fanya kazi ya MUNGU Na ss watumw wa mungu tunaomb mungu atup nguv ya kuijua kwel

  • @JenniferAela
    @JenniferAela Před 6 hodinami +1

    MUNGU mbariki Pastor Tony

  • @anordchaula3458
    @anordchaula3458 Před 4 dny +4

    Ubarikiwe mtumishi. naona injili za Paulo zinarudi Mungu wa Mbingu na nchi amrudishe huyo pastor kwenye mstari naona waz anaptea

  • @PastorVitalisSheshe
    @PastorVitalisSheshe Před 4 dny +12

    Pastor tonny haowatu achananao.Kama umeshindwa kuwahubiria injili ya kuwaleta acha

  • @tulimwaipopo-eq3be
    @tulimwaipopo-eq3be Před 3 dny +3

    Baba Mungu akukumbuke hatuwezi kufanya ibada pamoja sio kwelivijana wetu walianza vizuri wanamaliza vibaya

  • @zubedagadson2220
    @zubedagadson2220 Před dnem +1

    MUNGU akutunze mno baba umeongea ukweli kabisa😢💯

  • @dnewztz
    @dnewztz Před dnem +1

    Akiwa mbishi amuulize Godluck Gozbert na ule wimbo wake wa amenyoa Denge.
    Baada ya pale kila akijititutumua hola.
    Mungu sio wa Utani

  • @jonasmanirakizanzinga7882
    @jonasmanirakizanzinga7882 Před 11 hodinami +1

    Wakristu wengi wamejificha katika msemo huu: Hukumu ni ya Bwana. Soma 1Wakorintho 5:12 _Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?
    For what have I to do to judge them also that are without? do not ye judge them that are within?
    Ko kama huu Pasta Tony ni wa ndani tuna ruksa ya kumkanya na kumkemea kwa nguvu zote maana hao wa nje watajuana na Mungu.
    Jonas MANIRAKIZA mwinjilisti kutoka Bujumbura Burundi 🇧🇮

  • @hanagango6922
    @hanagango6922 Před dnem

    Amina mtumish wa mungu 🙏 MUNGU azid kukutia nguvu ya kukemea wanaopotosha neno la mungu

  • @TheOsborns
    @TheOsborns Před 6 hodinami +1

    KUMUELEWA MY SPIRITUAL FATHER PASTOR TONY NEEDS A SPECIAL GRACE NA AKILI😌 ,GO LISTEN TO THE FULL SERMONS!!!!, HIZI CLIPS MNAKATA KAKIPANDE FROM THE SERMON KUTUMIA KUKOSOA NA KUFUNDISHA WATU..KWAN UMEKOSA UJUMBE😂 YANI INASIKITISHA SANA !!!!! US THOSE WHO UNDERSTAND HIM WE ARE GRATEFUL TO GOD TO BE ABLE TO HONOR SUCH GRACE IN OUR LIVES 🙏

  • @user-gr9wc7bc2m
    @user-gr9wc7bc2m Před 4 dny +62

    Hawa vijana wana siri kubwa sana mwanzo alianza vizuri sasa hivi amejifunua enyi mliohama tag eagt holiness klpt rudini haraka mnapotea watoto wetu

    • @geitandelwa299
      @geitandelwa299 Před 4 dny +5

      Sana yaani walidanganya wenginila sasa YESU KAWAUMBUA

    • @FridayMwassa
      @FridayMwassa Před 4 dny +6

      Wapentecost nao siku hizi ni wajanja wajanja tu,wanavaa kama wadunia na vibinti malaya malaya ndiyo viimba choir,

    • @estermathias8354
      @estermathias8354 Před 4 dny +1

      ​@@FridayMwassani kweli kbs.lkn sio wote ila wengi wao mmhhh

    • @jemedalimwakalundwa3520
      @jemedalimwakalundwa3520 Před 4 dny

      Ko eagt irudi kwa tag

    • @user-tt7cu2et1x
      @user-tt7cu2et1x Před 4 dny +3

      Kwan jamn pastor ..kapola kavamiwa na roho chafuuu.. wallah alkua mzurii saana at maandiko...na alkua anasema ukweli..saah ameshakuwa naye Christina shusho dah😢😢😢😢

  • @elizabethjackson2442
    @elizabethjackson2442 Před 4 hodinami

    Namuona mbarikiwa mwakipesile. Barikiwa baba

  • @jelemiamkudiso4660
    @jelemiamkudiso4660 Před 4 dny +2

    Amen barikiwa Sana mtumishi wa Mungu. Ni sahihi kabisaaa Mungu atusaidie sana tupone

  • @linahchrissy7574
    @linahchrissy7574 Před 2 dny +1

    Mungu akubariki sanaa

  • @alicejohn2567
    @alicejohn2567 Před 3 dny +8

    hello handsome😂 kabla hujasema zaidi kuhusu PT naomba pitia shuhuda za siku ya alhamisi😊 ubarikiwe mtumishi

    • @RyanElias1
      @RyanElias1 Před 3 dny +2

      God Bless you my Sister……………. They dont understand what we learn Yet

    • @alicejohn2567
      @alicejohn2567 Před 2 dny

      @@RyanElias1bado hawajajua jmn natamani wapitie mafundisho ya PT mimi yamenibadilisha maisha yangu kwa asilimia zote kabisa maana yeye anafundisha mtu ujielewe na ujue kujiombea na kuweka imani katika kila unalofanya… watu wengi wanapenda mambo ya miujiza ya kuwekewa mikono lakini sisi watu wa mkuyuni tunaamini katika kufunga na kujiombea wenyewe katika kila tunalofanya

    • @neemacassian1869
      @neemacassian1869 Před 9 hodinami +1

      Tunaojua tunajua na haturudi nyuma wacha tuendelee kumtetea Pt wetu kwasababu tunajua vile ametutoa wapi kiimani

    • @japhetstanislaus7956
      @japhetstanislaus7956 Před 6 hodinami

      😂😂😂😂😂😂 sisi wa mkuyuni wala atuna shida wenyewe

    • @japhetstanislaus7956
      @japhetstanislaus7956 Před 6 hodinami

      Mimi najiuliza kama kumrekebisha pt kwanini awake picha ambayo haiendani na somo

  • @SophiaThadei-hx4wd
    @SophiaThadei-hx4wd Před 4 dny +4

    Asante Sana maana me mafundisho anayoyafundisha huaga siyapokeagi vzur roho yangu inakataaga kabisa yani

    • @mslady5824
      @mslady5824 Před 2 dny +1

      😂😂😂Ukiona hivyo ujue hakuna ujumbe uliotumwa kwa ajili yako kupitia yeye.

  • @rebeccabrown5135
    @rebeccabrown5135 Před 6 hodinami

    Tonny ulianza na roho umemaliza na mwili diamond your brother Mungu tusaidie kanisa lako limekia nyumba ya biashara

  • @eliyakabuje9522
    @eliyakabuje9522 Před 17 hodinami

    Ubarikiwe sana mtumishi yaan Asante sana YESU nisaidie 😭😭😭

  • @japhetstanislaus7956
    @japhetstanislaus7956 Před 6 hodinami

    Sisi wa mkuyuni tunaosaidiwa na BWANA tu like hapa

  • @loveandrew9694
    @loveandrew9694 Před 3 dny +3

    Kwani Tony ni pastor!mi namuona kama motivational speaker.....anachohubiri sio Habari za wokovu na kwenda mbinguni....

  • @EstherYoram
    @EstherYoram Před 4 dny +6

    Nia yake iliyojificha inajitokeza taaaaaratibu ,na tabia ya mtu ijifichayo nikama spring ilijibana,kwahiyo kadiri muda ukisogea hujiachia.

    • @user-tt7cu2et1x
      @user-tt7cu2et1x Před 4 dny

      Cha MUNGU kinaonekana tu..at kma kitachelewa vilevile n ibilis kaz yake itaonekna

  • @BEATRICE-ge7ff
    @BEATRICE-ge7ff Před 4 dny +2

    Hii ndiyo injili sasa mbarikiwa sana mtumishi wa mungu

  • @JohnMfundo
    @JohnMfundo Před 4 dny +3

    Mungu akubariki sana mtumishi pascal casian

  • @daudsospeter-zd3iy
    @daudsospeter-zd3iy Před 18 hodinami +3

    Ur need An extra Capacity and revelations kuelewa PT ameitwa kwaajili ya nani na kwaajili ya nini, and by the way Kwa muda Ambao nmemfahamu na kumfatilia, I have no ubishi, The man is Blessed 📌📌
    Wale mnaoanza kumfahamu Leo Acha muendelee kubishana Huku mitandaoni😅

    • @JenniferAela
      @JenniferAela Před 6 hodinami

      Kweli kbs Dav...😂 ngoja inaitaji akili nyingne kumuelewa Pastor Tony kaitwa kwaajir ya watu gan maana sio kila mtu atamuelewa .

  • @peterclaud-fm2ty
    @peterclaud-fm2ty Před dnem +1

    nabarikiwa

  • @Maryc2G
    @Maryc2G Před 4 dny +2

    God continue exposing the bad apples 🍎 to the body of Christ. Too much love of money is root of all evil. God you never fail to me by ashamed my anemias, thank lord for answering my preyer, mtawajua kwa matendo yao.yangu macho, asante kwa kuinua watu kuongea on my behalf. Inua wengine ili jina lako lisije likatukanywa.

    • @Maryc2G
      @Maryc2G Před 4 dny

      God never fail me. Correction on my abave statement 😅😅😂😂😂 yangu macho na maombi👀👀👀👀

  • @EliasGervasMahega
    @EliasGervasMahega Před dnem

    Mungu akutunze nakukutetea katika huduma nuru yakoizidi kung'aa

  • @andrewisaya3382
    @andrewisaya3382 Před 2 dny +3

    Huyo Tona kapola hana adhi ya kuitwa pastor unakosea,huyo ni motivation speaker asi halibu watu kupitia neno la Mungu.

    • @breezy9398
      @breezy9398 Před 14 hodinami

      we em kasafishe kalio ndo uje apa ucoment fala ww

  • @user-zj9op4fb7w
    @user-zj9op4fb7w Před dnem

    Sijui Yesu akirudi itakuaje? maana watu wanaanza vizuri badae wananichanganya vibaya mno...Mungu akulinde Casiani

  • @emanuelnyaki8074
    @emanuelnyaki8074 Před 17 hodinami +1

    Nawewe unajifanya Mungu sasa kwenda huko

  • @joannekesa1835
    @joannekesa1835 Před 4 dny +2

    Amen amen ubarikiwe mtumishi wa MUNGU

  • @samuelpolepoleruhegeza8139

    Huna akili weye mwenye uko unasema wenzako
    Weye njo aujui kweli kabisa
    Mimi napenda mapasta wanaosema kweli siyo wewe unaye kosowa wenzako
    Pasta tony u'are right ▶️▶️👍👍👍👍👍😂

  • @user-ep9by3ui1v
    @user-ep9by3ui1v Před 14 hodinami

    Pôle na kazi kaka 🤝🙏

  • @UswegeRichard
    @UswegeRichard Před 17 hodinami

    aty mzee wa wachaw 😂😂😂 nani mwingine kasikia hili neno😅 gonga like

  • @ukweliwanenokatikahili7526

    Shida Sana , Mtumishi Mungu akutunze

  • @user-ep8ob5ty3e
    @user-ep8ob5ty3e Před 20 hodinami

    Roho ya bwana iko juu yako mtumishi wa Mungu

  • @zyonhopefaith3692
    @zyonhopefaith3692 Před 3 dny +15

    Daah Ila mafundisho ya Pastor tonny.... Huwa nayapenda hunipa ujasili Sana...... Hasa kwenye Biashara Huwa najiamini na kuwa huru....

    • @veeJesus
      @veeJesus Před 3 dny +4

      Naomba nikushauri. Mfuate Pastor Tony usiwaskilize hawa mbweha wanaacha kuhubiri injili wanamuubiri Tony

    • @AnnaJackson-zi3xe
      @AnnaJackson-zi3xe Před 3 dny +3

      @@veeJesusyaniiii seriously mtu anaandaa sermon kumcritisize mwingine🙌🏾🙌🏾🙌🏾did God sent these men to judge other ni huzuni kwanini usiplay nafasi yako , ubiri injiliii eeeeeiiiiiiiiiiiiiii looking at this fyuuuuuu

    • @upendoryobafrancis98
      @upendoryobafrancis98 Před dnem +1

      Naona ameandika pastor Tonny ili apate viewers alafu atangaze kununua vyombo. Maana kwenye ufalme wa Mungu ni kuutangaza ufalme sio kumkandamiza mmoja ili wewe ujiinue Yesu hakufanya hivi.

    • @teklaagustino
      @teklaagustino Před dnem +1

      Alafu muwe mnasikiliza kitu mwanzo mwisho ndio muwe mnalaumu mtu akikosea Kwan Ni vibaya kumkosoa

    • @kelvinmbogela4718
      @kelvinmbogela4718 Před dnem +1

      ​@@veeJesuskuna spiritual understanding ukikosa huwezikujua kipi sahihi na kipi sio. Usiite watumishi mbweha ikiwa kiroho chako hakijakomaa nakushauri tu mpendwa

  • @suzanalucasemanuel7006
    @suzanalucasemanuel7006 Před 15 hodinami

    Mungu atusamehe sana

  • @tajilimtoto5009
    @tajilimtoto5009 Před 2 dny +2

    Nikweli wanamakosq ila ungewaombeq wawe kama wewe au zaidi nasio kuwasema bila kuwaombeq anaeukumu ni mungu tu nao wewe🎉❤

  • @fridberthahaule9489
    @fridberthahaule9489 Před 2 dny

    Hawa akina Natasha, christina shusho, pastor tony, libido ya wachawi na wengineo ndio wachungaji wa dini moja mpya ya dunia nzima nayoitwa chistislam, msishangae,unyakuo umekaribia sana wateule mzidi kujitakasa na wadhambi acha tu wazidi sana kuzitenda

  • @user-gr9wc7bc2m
    @user-gr9wc7bc2m Před 4 dny +4

    Huyu pascal ameletwa na Mungu

  • @debyqueen1
    @debyqueen1 Před dnem

    Mungu afungue macho ya roho jmn Mambo yanatisha.

  • @neemawasha8080
    @neemawasha8080 Před 3 dny

    Mungu akulinze mtumishi Paschal.Mungu alikuleta duniani na kukuacha hai kwa ajili ya nyakati hizi ili Uonyeshe njia bila kupepesa macho.

  • @JohnsonAzaliya
    @JohnsonAzaliya Před dnem

    Ni Kweli Huenda anakosea Lakni Inapaswa Kumuombea Na Kumuonya Wewe Na Yeye Ila sio Kumuonya Ivi public Sio Jambo La Upendo Wa kiMungu Anayotaka Uyo Ni Mtumishi Mwenzio Wa Mungu Then Usihukumu Usije Ukahukumiwa Kikubwa ni KUWAOMBEA Hawa Watumishi Ili Waje Kusimama Kama Wewe 🙏

  • @mahomamahoma775
    @mahomamahoma775 Před 4 dny +9

    Ukipata nafasi piamsikilize Mchungaji Abiudi na Ev Daniel kwa kweli utakuwa kiroho,utumishi wa kwelii ni kukemea dhambi,kuhubiri kuhusu toba na msamaha,Roho Mtakatifu na kumrudia Mungu.

  • @alinependo-bk4jj
    @alinependo-bk4jj Před dnem

    Kweli shetani yupo kazini Mungu tusaidie

  • @mtigandibori7244
    @mtigandibori7244 Před 6 hodinami

    Safi mtumishi zifunguwe fahamu za watanzania tusipende miujiza kuliko kulisoma neno

  • @salima2658
    @salima2658 Před 4 dny +10

    Pasta tonny alianza vizur lakini asa iv kabadilika

    • @priscillahpolepole8427
      @priscillahpolepole8427 Před 4 dny +1

      Baada ya kuja ubert angel naona ndipo alipoangukia na anamwita baba yake wa Imani.

    • @annewanjiru818
      @annewanjiru818 Před 4 dny +2

      True, mimi nilimskiza pastor Tony first time in 2020, na alikuwa mnyenyekevu sana, na alihubiri kwa spirit. But nikajikuta sina hamu tena kuskiza mahubiri kutoka kwake🇰🇪

    • @user-sb7lz9xp4v
      @user-sb7lz9xp4v Před 4 dny

      Ameanzaa kulewa sifa ndio maana

    • @veeJesus
      @veeJesus Před 3 dny

      Acha inafiki ujawahi kumskiliza tony. Watu wa tony hawajawahi kuhama​@@annewanjiru818

    • @BenMudy
      @BenMudy Před 3 dny

      Mbona wengine tunamuelewa na tunafata mafunzo yake mazuri na tunaacha mabaya yake cus hakuna aliyekamilika

  • @user-oc9gb6jv6o
    @user-oc9gb6jv6o Před 3 dny +1

    Ukweli tupu pastor, mungu akubariki.

  • @peter_paulofficialy
    @peter_paulofficialy Před 2 dny +31

    Umejitahidi kuongea, ila nadhani ungekuwa na lengo la kumuonya ungemtafuta inbox na kumueleza haya, mm nadhani unatafuta attention ya watu au kutrend kama yeye, mm nazungumza nikiwa siyo muumini wa Tonny wala muumini wako....cdhani kama umefanya vizuri, jitahidi kuubiri bila kuwasema watu ili Mungu awabadilishe na cyo kumuattack mtumishi yeyote....kama umeliona hili gonga like hapa na itawasaidiq watumishi wengine wahubiri watu wabadilishwe na c kusemana kama kina harmonize na kina diamond na kina kajala

    • @lwimboderick7479
      @lwimboderick7479 Před 2 dny +4

      Hao walio yapokea tayari.. nani atawaambia sio sahihi.
      Casian ana deal na nguvu ya mtandao...kuharibu na Kutengeneza.

    • @jmonlinetv4932
      @jmonlinetv4932 Před 2 dny +3

      Cassian yuko sahihi kwasababu yeye alisema hadharani na watu wengi wamesikia je akimwambia kwa siri hao waliosikia hilo somo la upotovu watajuaje kama hilo somo sio sahihi?, kumsema hadharani inamponya yeye na wote tunaomfuatilia pst Tony ili tujue kapotoka, mi nampenda pst Tony sana ila kuna vitu haendi sawa.

    • @mathiasdioniz5891
      @mathiasdioniz5891 Před 2 dny +2

      Msikilize vizuri mwinjilisti kaka, alafu soma biblia, "ya hadharani yanakemewa hadharani..."

    • @albertfrancis6557
      @albertfrancis6557 Před 2 dny +1

      Wewe mwenyewe umemalizia Kwa kuombea like...Dah! Dhambi inayofanyika hadharani hukemewa hadharani Ndugu yangu!

    • @michaelmagwaza-bc6mk
      @michaelmagwaza-bc6mk Před 2 dny +1

      Amepotosha hadharani akemewe hadharani hii ni Biblia Petro alikemewa hadharani na Yesu tena kwakusema Shetani rudi nyuma.

  • @RamadhaniMusa-jg2cu
    @RamadhaniMusa-jg2cu Před 4 dny +5

    MAHUBIRI YAKIWASHINDA ,MSIHONE HAYA ;HACHENI .
    USIWATUMIKIYE MABWANA WAWILI ENYI WAGALATIYA ,...NANI KAWAROGA.😢😢😢😢😢😂😂😂😂
    AMAKWELI MUNGU ANACHEKA.

  • @katarinaJ
    @katarinaJ Před 4 dny +7

    Watumishi wa baali.....wamejaa kila kona 😢

    • @Bambagatz
      @Bambagatz Před 3 dny

      Aisee sio mchezo, hayo ndo madhara ya kujichanganya na yale mataifa Mungu aliyokataza.

    • @clarissengeni8885
      @clarissengeni8885 Před dnem

      Wamejaa kweli ila Pastor Tony sio mmoja wao.

  • @user-ru6ct4rh3t
    @user-ru6ct4rh3t Před 4 dny +3

    Hakika tunamtaka bwana na nguvu zake.

  • @user-tt7cu2et1x
    @user-tt7cu2et1x Před 4 dny +1

    Ton.anaanza kusifiaa wasanii wa dunia kma nabii mkuu no dev kisongo Arusha wanamsujudia kma mungu wao..na wakiweka nyimbo za Amonais na wengne wengi..wakicheza madhabahuni....n nabii wao

  • @neemamsanga253
    @neemamsanga253 Před 15 hodinami

    😭😭😭 Kwa Sasa hata Mimi simuelewi baadhi ya ma pastor wanapotosha sana watu😭😭😭

  • @siamuchunguzi
    @siamuchunguzi Před dnem

    Naam mtumishi wa Mungu aliye hai