MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA AJINYONGA NEWALA

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 9. 06. 2024
  • Mwanafunzi wa darasa la Saba katika shule ya msingi Nachitulo halmashauri ya mji Newala Halima Shaban ,(12) amefariki dunia baada ya kujinyonga akiwa chumbani kwake mtaa wa Nangwala wilayani Newala Mkoani Mtwara
    Akithibitisha kupokea mwili wa mtoto huyo June 2, 2024 mganga mfawidhi hospitali ya mji Newala Dr kideyi Mzelela amesema walipokea mwili wa mtoto huyo majira ya mchana na walipompima walibaini kuwepo kwa alama ya mchubuko wa mfereji shingoni na kuthibitisha kuwa kifo chake kimetokana na ubongo kukosa hewa kutokana na mgandamizo shingoni hivyo mwili wa marehemu umehifadhiwa mochwari kusubiri taratibu za familia
    Baba mlezi wa mtoto huyo Khalifa Halbea Chakupewa amesema siku ya tukio binti yake aliingia chumbani na kutekeleza jambo Hilo baada ya baba huyo kumpa maelekezo ya kutoa vyombo vilivyotumika kulia chakula Huku wao wakidhani amekwenda kulala na kuongeza kuwa wamegundua kifo chake baada ya siku ya pili kugonga mlango wa chumba chake bila mafanikio
    Kwa upande wake mama mzazi wa mtoto huyo amesema mtoto wake alikuwa ni mtu wa hasira za mara kwa mara na kwamba aliwahi kutamka kuhusu kujinyonga wakati wa uhai wake
    Aidha kwa upande wa majirani wa familia hiyo wameeleza namna wanavyomfahamu na tukio Hilo lilivotokea
    Kamanda wa polisi Mkoani Mtwara Issa Suleiman amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa wanaendelea na uchunguzi huku akieleza taarifa za awali zinasema ni kutokana na Mtoto huyo kukemewa.
    Endelea kufuatilia channel yetu kwa taarifa zaidi ,
    Pia usisahau ku - subscribe CZcams channel yetu #mayonlinetv

Komentáře • 3