RC MTANDA AWAPONGEZA CCM MAGU KWA KUIMARISHA UHAI WA CHAMA

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 12. 06. 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameupongeza Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Magu kwa kuimarisha uhai wa chama hicho kisiasa na kuongeza idadi ya wanachama na akawataka kushikamana zaidi.
    Mhe. Mkuu wa Mkoa akiwa kama Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa ametoa pongezi hizo mapema leo Jumatano Juni 13, 2024 alipotembelea kwenye ofisi za wilaya za Chama hicho na kufanya kikao kifupi na uongozi wa chama.
    Mtanda amesema, Chama hicho ndicho kimeshika hatamu ya kuongoza nchi kupitia uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 hivyo kinastahili uimara kutokana na imani waliyoitoa wananchi hivyo anawapongeza Magu kwa kudumisha hilo.
    Aidha, ametumia wasaa huo kuwataka kumuunga mkono Rais Samia na waendelee kushirikiana baina yao ili kujihakikishia ushindi kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwishoni mwa mwaka huu pamoja na uchaguzi mkuu hapo mwakani.
    Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM, Katibu wa wilaya ndugu Ibrahim Mamba amesema mahusiano yameimarishwa na kwenye matawi yote 110 yanazidi kukua na kuongeza wanachama kuanzia ngazi ya vitongoji jambo linaloashiria uimara wa chama hicho.

Komentáře •