Video není dostupné.
Omlouváme se.
KILIMO CHA MPUNGA IRINGA II
Vložit
- čas přidán 17. 07. 2019
- Mradi wa RICE unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya ni moja ya jitihada za kupunguza changamoto ya upotevu wa mazao baada ya kilimo. Mradi huu unatekelezwa na Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) likishirikiana na serikali, halmashauri ya wilaya ya Iringa na Taasisi ya Maendeleo vijijini na Mijini (RUDI).
Lengo Kuu la mradi ni Kupunguza umaskini vijijini kupitia kuboresha ushindani wa wakulima wadogo wa mpunga katika sehemu ya ukanda wa SAGCOT.
Mradi huu unatekelezwa katika skimu kumi na Mbili (12) za Luganga, Magozi, Mkombozi, Mlenge, Makifu, Mafuruto,Idodi,Tungamalenga,Mlambalasi, Ipwasi Ndorobo na Makuka katika wilaya ya Iringa. Mradi unajenga uwezo wa viongozi wa vikundi vya wakulima ili kuweza kumudu vyema ushirikiano na wadau wengine katika mnyororo wa thamani na hivyo kuongeza uwezo wa kuhimili ushindani, kupunguza upotevu na kukidhi mahitaji ya soko.
nashukuru kwa maarifa mnayotoa ila naomba melekezo ya matumizi ya mbolea ni kiasi gani kwa hekari moja
Nimeipenda Sana ii
Nifunze pitia mtandaoooo
Makala bora zinapatikana hapa kwenu mupo makini
Sijaona mashine yapanda mpunga vzl
Sijaona mashine ya kupandikiza mpunga ambayo unaendesha ukiwa unatembea,nataka nijue vifaa vyake hasa matairi na je ? Yale maboya yake yanasaidia isititie ktk tope,matairi yake yanakuaje,Mimi ninayo lkn tairi zilikuwa na mpira ukaisha ingawa sijaitumia,je unapoitumia ni lazima pale hapana maji au?