#TAZAMAl
Vložit
- čas přidán 11. 12. 2022
- Kuanzia sasa serikali itaanza kuzitazama ajira za vyuo vikuu badala ya kuangalia ubora wa ufaulu yaani GPA pekee sasa waajiriwe kwa kupimwa uwezo wao kwa kufanya usaili.
Kuangalia ufaulu pekee wa wanafunzi haitoshi kuboresha elimu badala yake ni muhimu kuongeza vigezo hivyo katika mapitio ya sera na mabadili ya mitaala jambo hilo litatazamwa kwa weledi mkubwa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prof ADOLF MKENDA ameyasema hayo leo tarehe 12 Disemba 2022 mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt PHILIP MPANGO wakati wa mahafali ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania iliyofanyika Kinondoni Jijini Dar es salam.
Amesema wakati serikali inaongeza udahili wa wanafunzi haitakuwa tayari kuona ubora unapungua hivyo serikali inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha ubora wa elimu hususani katika vyuo vikuu unaimarika.
"Zamani ilikuwa rahisi kuwa Profesa ukiandika tu kwenye magazeti unakuwa Profesa lakini kwa sasa vigezo vya kuwa Profesa vimezidi kuwa vigumu kwa sababu tunataka maprofesa wetu wawe sawa na wale wa nchi zingine" Amekaririwa Prof Mkenda
Amesema katika mageuzi ya elimu yanayokuja ambapo wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipo katika mapitio ya sera na mitaala miongoni mwa mambo yatakayofanyiwa kazi itakuwa ni pamoja na kuhakikisha wanaoajiriwa ni wanafunzi wenye sifa zinazotakiwa.
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09 - Zábava
Zinatolewa tuuu GPA mungu atusaidiee
Pia wakati haya Yankee kutekelezwa Mungu awawezeshe kudhibiti mianya ya RUSHWA kwenye wizara yetu ya Elimu.
Kweli aise!!! GPA baadhi ya vyuo sio deal
GPA SIO KIGEZO MAANA UKIFANYA MSAKO VIONGOZI WANAOFANYA VIZURI WANA GPA NDOGO KWA HIYO SIO LAZIMA GPA