Ziara ya Makamo wa Kwanza wa Rais kisiwani Pemba

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 21. 05. 2024
  • Mwenyekiti wa Taifa wa ACT-Wazalendo ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, Jioni ya Leo Jumanne Mei 21, 2024 amepata fursa ya kujumuika na kubadilishana mawazo, pamoja na kuwahutubia Wana-Barza ya Wazee, ya Kichaka, iliyopo Kiwani Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba.
    Awali Mheshimiwa Othman amefika na kutoa Mkono wa Pole kwa Familia za Vijana Watatu (3) Wavuvi, ambao walifariki-dunia hivi karibuni wakati wakiwa katika shughuli zao za uvuvi, huko Mkoani Mtwara Tanzania Bara; Ziara ambayo imeambatana pia na kukagua Nyumba za Wananchi, ambazo ziliathirika kutokana na Kimbunga 'Hidaya' kilichotokea mapema Mwezi huu.
    Viongozi mbali mbali wamejumuika katika Ziara hiyo, wakiwemo Mratibu wa Chama kisiwani Pemba, Wenyeviti wa Mikoa ya kichama ya Mkoani na Wete, Mhe. Said Ali Mbarouk, Ndugu Mohamed Abdallah Bakar, na Ndg. Juma Khamis Ali.
    Mheshimiwa Othman yupo kisiwani Pemba kwa Ziara Maalum ya Siku Mbili, inayohusisha Shughuli za Siasa na Serikali.
    Kitengo cha Habari
    Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
    Mei 21, 2024.

Komentáře •