REV. DR. ELIONA KIMARO: KUILINDA IMANI

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 22. 10. 2023
  • IBADA YA JUMAPILI ( IBADA YA KWANZA ) - 20/10/2023*
    UJUMBE WA LEO: KUILINDA IMANI
    2 Timotheo 4 : 7
    Mwanzo 22 : 1 - 19
    2 Timotheo 4 : 7
    7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;
    Mwanzo 22 : 1 - 19
    1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
    2 Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.
    3 Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.
    4 Siku ya tatu Ibrahimu akainua macho yake, akapaona mahali pakali mbali.
    5 Ibrahimu akawaambia vijana wake, Kaeni ninyi hapa pamoja na punda, na mimi na kijana tutakwenda kule, tukaabudu, na kuwarudia tena.
    6 Basi Ibrahimu akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja.
    7 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinena, Babangu! Naye akasema, Mimi hapa, mwanangu. Akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?
    8 Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja.
    9 Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.
    10 Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.
    11 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
    12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.
    13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
    14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,d kama watu wasemavyo hata leo, Katika mlima wa Bwana itapatikana.
    15 Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
    16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
    17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;
    18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.
    19 Basi Ibrahimu akawarudia vijana wake, wakaondoka, wakaenda zao pamoja mpaka Beer-sheba; Ibrahimu akakaa huko Beer-sheba.

    Mhubiri : Rev.Dr. Eliona Kimaro
    Kwa maoni na ushauri:
    Mch. kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053

Komentáře • 7

  • @estherchege9074
    @estherchege9074 Před 9 měsíci +1

    Jamani bona maombi yanakatilizwa ghafla kabla yaishe..tunahitaji maombi in full complete level please..Niko Saudi Arabia mimi ni mkenya na pastor eliona ananisaidia sana nafunguliwa na somo zote na salary anazotutolea.

  • @user-ft3us9sb3p
    @user-ft3us9sb3p Před 9 měsíci

    Amen

  • @alex_vincent
    @alex_vincent Před 9 měsíci

    Hallelujah

  • @user-cy1yy3hj5q
    @user-cy1yy3hj5q Před 9 měsíci

    Msitukatishie Maombi jamn😞

  • @user-qw6ns6ff3z
    @user-qw6ns6ff3z Před 9 měsíci

    Pastar nmenjifuza kitu kwa masomo yako ntailinda imani

  • @furahamtweve4222
    @furahamtweve4222 Před 9 měsíci

    Amen

  • @user-lk8dx1vd6d
    @user-lk8dx1vd6d Před 9 měsíci

    Amen