Salama Na MR BLUE SE6 EP69 KHERI PART 1 SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Vložit
- čas přidán 28. 05. 2023
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kheri Sameer aka Mr Blue aka Lil Sama aka Bayser ni mdogo wangu, mdogo wangu kabisa na uzuri nakumbuka kabisa mara ya kwanza kuonana nae na mpaka alivyokua amevaa. Jezi ya Denver Nuggets, jeans ya light blue na sneakers nyeupeeehh na chain ya Silver, kwenye maskio alikua na hereni za kung’ara zile ambazo zilikua si za kitoboa skio, zilikua zina smaku na nazijua zaidi kwasababu Marehemu cousin brother wangu alikua nazo maana nyumbani ilikua hairuhusiwi kutoboa maskio enzi hizo. Alikua msafi, ana swagg ya kuongea na hata jinsi alivyokua anajibeba. Alikua wa moto sana unaweza kusema hivyo, au niseme hivyo. Kila ‘mtoto’ na kijana alitamani kuwa kama yeye kwa kila kitu, muonekano mpaka hit songs kwenye radio na TV.
Blue alikua na mtu ambaye anamsimamia na huyo hakua mwengine bali G Lover, meneja na Dj ambaye alikua anasimamia kazi zake yeye pamoja na wasanii wengine kama Ally Kiba, Ally Com na Abby Skills kwa kuwataja kwa uchache na wasanii wake hao wote walikua wa moooto sana. Ngoma kali, video mbaya, show nyingi na kwa ‘mhindi’ wanauza sana. Na kuanzia hapo kwa mhindi na kuuza sana ndo ambapo kuliweza kuwapoteza wengi kwasababu wengi walikua wadogo sana na pesa ilikua nyingi. Fitna na utovu wa nidhamu wa kupindukia ulianzia hapo. Wakati naandika hii nilimuwaza Ally Kiba na jinsi ambavyo ameweza ku maintain class flani toka siku ya kwanza tunamskia na mpaka leo regardless ya mengi ambayo yametokea hapo katikati, HAKUWAHI KUPOTEA. Kwa hilo naamini anastahili HESHIMA na recognition ya hali ya juu pengine kuliko tunayompa maana dah, mambo yalikua mengi sana enzi hizo.
Kuna usemi kwamba wakati ni mwalimu mzuri sana na kwa uelewa wangu hakuna ambaye anaweza kuelezea experience kama ilivyo elezewa kwenye usemi huo. Wakati ndo ambao unatufunza na kutuonyesha vitu na watu wengi, ambao tulikua tukiwaamini na wengine kuto kuwaamini, kuwapenda na wengine kuto wapenda, kudhani unajua na ki ukweli hujui, kudhania umezama kwenye dimbwi na mapenzi na huyo alo nae ndo wako wa milele na kumbe si hivyo na hayo yote unayaelewa within kipindi fulani, miaka inavyokwenda ndo na wewe unaelewa na kujifunza mambo kwa uwezo na uelewa wako. Moment za ‘anha’ na ‘wow’ huwa nyingi sana. Wakati ni MWALIMU na majuto huwa ni mjukuu, nadhani utakua umenielewa.
Mr Blue alikua na dunia kwenye miguu yake, ilikua yeye tu aseme anatakaje na anataka ielekee wapi na hivyo ndo ingekua ila haikua hivyo ndo jambo la kusikitisha lakini bahati kubwa ambayo mwenzetu alikua nayo au yuko nayo ni kwamba hayo yote yalitokea mapema sana, wakati yuko mdogo sana kwenye dunia ambayo wengi walikua wakimuangalia na kumpenda sana. Yeye baada ya kuona mapenzi na shangwe hilo basi akadata na akaanza kuwa mgumu kufanya nae kazi, akawa na marafiki tele ambao hakua anawajua kabla hajawa Lil Sama na baadae Mr Blue. Akawa hasikii la muadhini wala mnadi sala. Akajiingiza kwenye uvutaji wa bangi isokua na staha, akaondoka nyumbani na kwenda kuishi kwenye ma ghetto na wana wasokua na ramani. Akawa ana party Jumatatu mpaka Jumatatu. Studio haonekani, kwenye interview hatokei na wale watangazaji ambao walikua wanapiga mgoma zake kwenye Radio akawa hata salaam hawapi. Producer na meneja nao wakagombana nae kwasababu sitofahamu ya pesa kwa mhindi ilishika hatamu.
Mwanzo nilisema Blue ana Kheri sana kama jina lake kwasababu hayo yote yalitokea wakati mdogo sana, dunia ilimfunza nae akafundishika, wakati dunia hiyo ikiwa inamfunza alikua mwanafunzi mzuri sana kwasababu darasa alilolipata wakati kakata ringi ndo ambalo limefanya awe BORA na ajitambue LEO HII.
Kwenye meza yetu ya kigae na kiti chakavu Blue ananielezea hustle zote ambazo alishawahi kuzipitia wakati anakua na huku akiwa anajitafuta na kwa uelewa wangu itasaidia wengi ambao wanaaza au wataanza kuzishika pesa mapema au hata ambao watapata mafanikio huko mbeleni watajua jinsi ya ‘kujibeba’ kutokana na maongezi yetu haya.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
CZcams Link bit.ly/CZcamsSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz - Zábava
Naitizama hii interview mara ya 10 na bado na mpango wa kuitizama tena na tena
NAELEWA KWA NINI ANAANGALIA JUU WAKATI ANAPOMZUNGUMZIA MAMA AKE. NI NJIA PEKEE YA KUZUIA CHOZI LOVE YOU MAMA...🌺💕
Sure sure man, mwanaume akifanya hivyo huwa ndani yake anazuia sana hisia.
salamaa anahoji vyema sana
Yaah maana uchungu na hisia kali ndan yake
Mr blue anajielewa sana na yupo very humble. Kwake tabata ni karibu na nyumbani kwa wazazi wangu
Salama ikiwezekana tuletee Kalapina ikiwezekana
anajitahidi sana kutolia wakati anamuongelea mama ake""Mungu amrehemu
Amen maskin analia kiume
Hapo kwa mama from jela mpaka kuishi mtaani akakupa 500 nahisi kulia kabsa
Mr blue nimtoto wa rafiki Yangu tulimlea mimi na mama yake Halima na mimi naitwa Rahel naishi Sweden kwa sasa
Hongera kwa malezi mama
hongre
Hongerah sana wewe na familia yako kwa utu wenu.
I appreciate Mr Blue not coz of his music but coz he is very honest to himself
12:00 to 12:12 kumenitoa machozi. Ahsante Mungu kwa kuturudisha kwenye mstari kila mara tunapotoka 🙏
Napenda heshima anayo onesha Kwa Salama!! Mwanaume anapoita dadangu na ujazaliwa nae inamaana anakueshimu sana
SURE
Bonge la interview,Byser katulia kwenye maongezi,moja ya interview kali na yenye ubora wa hali ya juu
The way he say... "Yeah Dada yangu".. one of my favorite artist 🥰
Asante
Noo wayyy....🔥🔥🔥🔥🙌🏾
Daah, Naomba niseme ukweli tu leo...Ni hivi leo tu nimemuwaza sana Mr. Blu kwann hapati Mualiko hapa na #Salama?? Daah kama Milunzi yaani Swali langu limepata majibu leoleo❤️🙏🏾
Big up #JahStoneTown💛💛
Hapa kwenye marafiki broo nimekuelewa yan wanapotosha kama mm sinywi sina sikendo za ajab uli wapo marafiki wanipambania niingie huko nawakimbia balaaaa Yan daah na lock nafuta no mtu anakwambia kuolewa nn diri kujiuza marabila pombe ww sio mjanja mm ni mwendo wakuwakimbia tu nikiwa a mama alinipambania sana had kuwa hapa nilipo na mungu kaniona Asante Mungu 💯💕🙏leo nije nimfanye mzaz wangu alie kisa mm hapana 😭💪
Naomba ni like kabla hata sijaisikiliza maana I'm sure 100% it's gonna be a marvelous interview ever
Kwenye interview yoyote Ile ambayo salama hutocheka itakuwa mbaya👍
Naliaa😢kuna neno ameongea ndicho nnachopitia na watoto wangu namuomba Allah subhanah wataala aje kuwa wenye huruma na upendo kwangu waje kunilea. Am happy mr blue kasema kweli we must be humble. Alhamdulilah
🙏
Pole Mungu atakufanyia wepesi
Pole.mungu.atakufanyia.wepesi
Allah akufanyie wepesi🤲
Next Salama na Majani(P.Funk)
Salama fanya mpango utuletee ITD au CHID BENZ. tuwasikie
Very humble May Allah bless him
Even more and his family.
One of the best interviews ❤
Mola awapee maskizano daima kkangu na mkeo in, sha Allah 🤲
Mr Blue anajali sana familia yake,huku kwetu Kinyerezi Mbuyuni kuna duka la viatu basi anakujaga na watoto wake kuwanunulia viatu,ukimkuta sasa anasalimia kila mtu mwenyewe siku hizi kweli hana dharau,havimbi tena😂 peace mwenyewe na fans wake tunaompenda,hapo wife wake yuko kwenye gari, anasubiri wamalize, love his humble self.
🤣
Sally the greatest soul
Wee sema kweli
legends wangu kwenye ubishoo nakupenda.madem😅😅😅
MR BLUE HE IS AMAN
Blue nilikutana nae kwenye show pool bar kenya jamaa nilimuita jina lake halisi akashtuka sana ikabidi anite nyuma ya steji tutulie tutie story mtu safi sana
Pool bar kitambo mwana sikuizi ipo lakni walibadilisha Jina na wanaleta live band wa Congo
@ismaelmatano3571 yap bro wameibadilisha jina yakitambo izo ilikua ndio semu yetu ya kujirusha analipa mtu 1 tunaingia mtu 2 bure tunagandishana zile stump zao
Moja ya interview Bora sana! Mchanganyiko wa hisia za kweli, ukweli wa mambo na umakini katika kuuliza na kujibu maswali! It's one of the best!
Interview nzuri na tamu kuisikia,Mr blue tumecheza nyimbo zako mpaka basi,nimefurahi Salama kutuletea uyu kaka
Tunamtaka chid Benz nahisi itakua best interview
Blue..❤
I wish to see Salama na JB (Jacob Stephen)
HII NI KIU YANGU KUTOKA YAHSTONE TOWN
Tunaisubiriiii
Brue that day alikuwa balaa,hakuna msanii aliyekuwa anavimba kama yeye,akikaa anapinda mgongo😀😀 kwa mikogo
Humble man mashallah
Unajua sana kujishusha, umejaa heshima Keep T up
Apewe maua yake na miti, na bidha zingine za kilimo
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Unaakiri sana broo nakupenda sana broo nimejifunzakitu hapo💕🙏nimecheka ety mibangi🤭😂😂😂😂
msikilize mr blue then nenda kasikilize ngoma yake ya tabasam ndo utamuelewa vzur
Asante Salama kwa kumleta Byser
Lmbaoo Blue interview yako inanifurahisha sana unapozungumzia BHANGI..
😀😀😀 Kwa mwaka huu salama na Blue naipitisha. Alafu dada salama tuletee MPOKI ikikupendazaaa
😅😅😅😅😅nilikua na watu wanguuuuu hahahhaa wa kuwavimbia 🎉🎉🎉🎉😂 🇰🇪🇰🇪🇰🇪
Blue interview zake huwa zinafunzo sna alafu yupo real sna
Jamaa jinsi anavyoongea utafikiri ana PhD 🙌, Babylon byser
Kuongea na PhD wap na wap😂😂😂 jaman
Yani anavutia sana
Nimemkubali blue kuongea ukweli kuhusu bangi,mana alikua ananikodi kama tax drive kutoka tbt mpaka ilala kuvuta bangi tu.miaka ya 2005 - kuendelea.
Lovely soul millionaire ❤❤❤
Back in the days more love from Kenya.....big up bro
Najifunza vitu vingi kutoka kwa brother Bizzy 💓💓💓💓
Salama tafuta msudani mmoja pale muhimbili,hojiana nae tusikie,gonga like kama unaunga mkono
Story ya mama ake imenigusa mno hata kaka Blue almost atoe chozi akati anamuelezea mama ake may her great soul rest in Paradise.
Mr bleu ame kuwa responsable 🙏🏾😍
Leo nimeangalia tena mara ya 37
Oyoo Byser kajikaza kidogo alie... 😢Mzee imenigusa
Kweli asee.. aja tokwa machozi ila una weza kuona moyoni ana lia
@@fongaamike2768 huyu kweli amepitia mengi
Hongera sana blue katika Maisha dharau ni kujisikia ni mbaya sana katika Maisha hongera sana kurudi kwenye mstari Maisha Dunia ndo Elimu ya pili ukitoa Elimu ya darasani
I’m love love blue
Heri sana😂
Sauti kama ya mzee yusufu
thanks for bringing mr Blue..let next be majani p funky
Hapo itakua❤❤❤
Hata mm ningependa kumuona Pfunk
P funk mwamba sa a
Legendary Bayser, nakukubali sana ❤
Umengaa😂😢🎉❤
Salama haujambo unamkumb uka bikati na sabriwake mimi humoud nduguyake sefu mmanga na shoga yako farida mimirafikiyake almlaruhum abdul njegere m/ almukepepon amen na bro musa jabir inrahim kuki abudu ndo nimekuwanao ujana wetuwote sisi ndowenye kiponda bila kumsahau dada yetu halima na boss khamisi wake
Bru bonge lajembee
Thanks Salama for bringing Mr Blue, such an inspiration🫡
Kibenzi cha watuu bless sana mr blue byser ❤
5:18 😂
6:28 mama 💕
6:34 📌 njaa
9:18 mama 💕💕
13:15 📌
18:24 📌📌📌
Star Wangu Wa Muda Wote Babylon Byser Mr Blue, Namkubali Sana Mchizi Ana Kipaji Na Hajui Kulinga Na Hana Dharau Kweli Maisha Ya Kula Ugali Na Kachumbari Yalijitahidi Kumbadilisha, Much Respect Kwake Mzee Wa Kazi
Mwamba kakazia "Mabangi"........
Grew up in his era. Blu and TID, Ferroz and Prof Jay were the bongo flaza guys. They made my days here in Kenya.. good interview.Kindly find Ferroz and interview him.
Fleva not flaza bro
@@yoo_its_yaqub8722 typo bro
Ooooh sorry bro
Blooo Kweli unaujua mziki hongela sana
Nimeipenda sana jamani mungu awajalie ❤❤❤❤
Bizzy kwenye game🔥🔥
Last week niliingia CZcams Kuuliza salama na mr blue ila sikuona kitu nikajiuliza why? Nikakumbuka kuna scandal ya salama kutoka na byser way back a.k.a nyani zee 😂
Mutu wangu ngoma hautuletei ,,hatukusikiii huku congo tena
Blue ni mdogo wangu sana. Nipo kwenye hii fani kabla hajazaliwa. Itoshe kusema he is the GOAT! Toka dakika ya kwanza nausikia wimbo wa BLUE nikajua a star was born! Hajawahi kuniangusha. Yeye na Jay Mo. Hawajawahi kufeli!
H
Nyani zee namkubali since day za Tabasamu ...much love from🇶🇦🇶🇦
Huyu mwamba yupo real sana + mh. FA
Mr blue alianza muziki mdogo sana Hadi kawa mzee baba
Mlete Millard Ayo
Mwamba huyu
LIL Sam A' aka Mr Blue kawainspire wasanii wengi sana upande wa kuchana kwa pozi, kuimba kwa pozi, swaga, mavazi, n.k. he is a Legend
Big up saana Mzee wa Upala
U a humbleman
😂😂😂 eti Daah leo nimeyakanyaga
Blue mtu mkweli sana sanaa
salama vp tozzy
Nachopenda Mrblue Anasema Ukweli Na Mtu Peace Sana Hata Nilpo Kutana Nae Day Wani Na Producer Sulesh Sikutegemea Alivyo Nichangamkia Kama Mi Mtu MKUBWA Vile Tukaenjey Na AkachaMshangoo Kwatu Kama Najuana Nae Before Ana Roho SAFI SI Mtu Wamajivuno Blue MUNGU Amzidishie MAISHA Mareeeeeeeefu Na Furaha Teeeeeele
Jabir, nakuelewa sana! unaset logical questions
Nilivoona tu interview ya Byser NIKACLICK, nasubiri interview ya BELLE 9
Maua yako byser🎉
Legend 🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌
I'm excited to see again Mr blue
Life teach us a lot big up sana byser one of the best interview
Byzy kwenye gamu
Yani leo ume akikisha turikua tume mutamani saanaaa mr blue much love from Bdi
baisa uko sawa
Mr blue utaliza watu sad story na umeonyesha umekuwa very fasta ,but umekuwa baba kaza
Next time mulete mukongwee, Chid Benz,Chumaa
Nice interview asante sana salama
This gonna be the best interview this year.....
TABASAM Mr Blue..mad love from Kenya 🇰🇪
Next Salama na Bishop Eliasaph Mattayo Suleiman
Mapozi naye
Ngwair 😭
Byser ❤️❤️ kontena lenye kutu
Safi sanaa dada salama kwa kumleta mr blue naomba utuletee na mc luvanda if possible...
I love you salama you present the best content
Sapenda sana intarview za salama ,una jua sana dada
Love this interview with Blue, Byser❤️ na nampenda somo yangu Wahida🥰
Interview hii inaenda kubadili maisha yangu kwa kiasi flan