Salama Na MR BLUE SE6 EP69 KHERI PART 1 SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 28. 05. 2023
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Kheri Sameer aka Mr Blue aka Lil Sama aka Bayser ni mdogo wangu, mdogo wangu kabisa na uzuri nakumbuka kabisa mara ya kwanza kuonana nae na mpaka alivyokua amevaa. Jezi ya Denver Nuggets, jeans ya light blue na sneakers nyeupeeehh na chain ya Silver, kwenye maskio alikua na hereni za kung’ara zile ambazo zilikua si za kitoboa skio, zilikua zina smaku na nazijua zaidi kwasababu Marehemu cousin brother wangu alikua nazo maana nyumbani ilikua hairuhusiwi kutoboa maskio enzi hizo. Alikua msafi, ana swagg ya kuongea na hata jinsi alivyokua anajibeba. Alikua wa moto sana unaweza kusema hivyo, au niseme hivyo. Kila ‘mtoto’ na kijana alitamani kuwa kama yeye kwa kila kitu, muonekano mpaka hit songs kwenye radio na TV.
    Blue alikua na mtu ambaye anamsimamia na huyo hakua mwengine bali G Lover, meneja na Dj ambaye alikua anasimamia kazi zake yeye pamoja na wasanii wengine kama Ally Kiba, Ally Com na Abby Skills kwa kuwataja kwa uchache na wasanii wake hao wote walikua wa moooto sana. Ngoma kali, video mbaya, show nyingi na kwa ‘mhindi’ wanauza sana. Na kuanzia hapo kwa mhindi na kuuza sana ndo ambapo kuliweza kuwapoteza wengi kwasababu wengi walikua wadogo sana na pesa ilikua nyingi. Fitna na utovu wa nidhamu wa kupindukia ulianzia hapo. Wakati naandika hii nilimuwaza Ally Kiba na jinsi ambavyo ameweza ku maintain class flani toka siku ya kwanza tunamskia na mpaka leo regardless ya mengi ambayo yametokea hapo katikati, HAKUWAHI KUPOTEA. Kwa hilo naamini anastahili HESHIMA na recognition ya hali ya juu pengine kuliko tunayompa maana dah, mambo yalikua mengi sana enzi hizo.
    Kuna usemi kwamba wakati ni mwalimu mzuri sana na kwa uelewa wangu hakuna ambaye anaweza kuelezea experience kama ilivyo elezewa kwenye usemi huo. Wakati ndo ambao unatufunza na kutuonyesha vitu na watu wengi, ambao tulikua tukiwaamini na wengine kuto kuwaamini, kuwapenda na wengine kuto wapenda, kudhani unajua na ki ukweli hujui, kudhania umezama kwenye dimbwi na mapenzi na huyo alo nae ndo wako wa milele na kumbe si hivyo na hayo yote unayaelewa within kipindi fulani, miaka inavyokwenda ndo na wewe unaelewa na kujifunza mambo kwa uwezo na uelewa wako. Moment za ‘anha’ na ‘wow’ huwa nyingi sana. Wakati ni MWALIMU na majuto huwa ni mjukuu, nadhani utakua umenielewa.
    Mr Blue alikua na dunia kwenye miguu yake, ilikua yeye tu aseme anatakaje na anataka ielekee wapi na hivyo ndo ingekua ila haikua hivyo ndo jambo la kusikitisha lakini bahati kubwa ambayo mwenzetu alikua nayo au yuko nayo ni kwamba hayo yote yalitokea mapema sana, wakati yuko mdogo sana kwenye dunia ambayo wengi walikua wakimuangalia na kumpenda sana. Yeye baada ya kuona mapenzi na shangwe hilo basi akadata na akaanza kuwa mgumu kufanya nae kazi, akawa na marafiki tele ambao hakua anawajua kabla hajawa Lil Sama na baadae Mr Blue. Akawa hasikii la muadhini wala mnadi sala. Akajiingiza kwenye uvutaji wa bangi isokua na staha, akaondoka nyumbani na kwenda kuishi kwenye ma ghetto na wana wasokua na ramani. Akawa ana party Jumatatu mpaka Jumatatu. Studio haonekani, kwenye interview hatokei na wale watangazaji ambao walikua wanapiga mgoma zake kwenye Radio akawa hata salaam hawapi. Producer na meneja nao wakagombana nae kwasababu sitofahamu ya pesa kwa mhindi ilishika hatamu.
    Mwanzo nilisema Blue ana Kheri sana kama jina lake kwasababu hayo yote yalitokea wakati mdogo sana, dunia ilimfunza nae akafundishika, wakati dunia hiyo ikiwa inamfunza alikua mwanafunzi mzuri sana kwasababu darasa alilolipata wakati kakata ringi ndo ambalo limefanya awe BORA na ajitambue LEO HII.
    Kwenye meza yetu ya kigae na kiti chakavu Blue ananielezea hustle zote ambazo alishawahi kuzipitia wakati anakua na huku akiwa anajitafuta na kwa uelewa wangu itasaidia wengi ambao wanaaza au wataanza kuzishika pesa mapema au hata ambao watapata mafanikio huko mbeleni watajua jinsi ya ‘kujibeba’ kutokana na maongezi yetu haya.
    Tafadhali enjoy.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪CZcams Link bit.ly/CZcamsSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • Zábava

Komentáře • 234

  • @ganjatunikilemile719
    @ganjatunikilemile719 Před 7 měsíci +5

    Naitizama hii interview mara ya 10 na bado na mpango wa kuitizama tena na tena

  • @mchangeboy5928
    @mchangeboy5928 Před rokem +47

    NAELEWA KWA NINI ANAANGALIA JUU WAKATI ANAPOMZUNGUMZIA MAMA AKE. NI NJIA PEKEE YA KUZUIA CHOZI LOVE YOU MAMA...🌺💕

    • @moneythemes
      @moneythemes Před rokem +2

      Sure sure man, mwanaume akifanya hivyo huwa ndani yake anazuia sana hisia.

    • @abisaimuhanji3687
      @abisaimuhanji3687 Před rokem

      salamaa anahoji vyema sana

    • @mchangeboy5928
      @mchangeboy5928 Před rokem +1

      Yaah maana uchungu na hisia kali ndan yake

  • @cdeleo9336
    @cdeleo9336 Před rokem +64

    Mr blue anajielewa sana na yupo very humble. Kwake tabata ni karibu na nyumbani kwa wazazi wangu

  • @blandinamyinga9489
    @blandinamyinga9489 Před rokem +21

    anajitahidi sana kutolia wakati anamuongelea mama ake""Mungu amrehemu

  • @esterdoriye8377
    @esterdoriye8377 Před rokem +14

    Hapo kwa mama from jela mpaka kuishi mtaani akakupa 500 nahisi kulia kabsa

  • @rahelrodin5486
    @rahelrodin5486 Před rokem +14

    Mr blue nimtoto wa rafiki Yangu tulimlea mimi na mama yake Halima na mimi naitwa Rahel naishi Sweden kwa sasa

  • @dostovan5142
    @dostovan5142 Před rokem +38

    I appreciate Mr Blue not coz of his music but coz he is very honest to himself

  • @javanwatson6675
    @javanwatson6675 Před rokem +20

    12:00 to 12:12 kumenitoa machozi. Ahsante Mungu kwa kuturudisha kwenye mstari kila mara tunapotoka 🙏

  • @Heismasai
    @Heismasai Před rokem +26

    Napenda heshima anayo onesha Kwa Salama!! Mwanaume anapoita dadangu na ujazaliwa nae inamaana anakueshimu sana

  • @johariabdalla3319
    @johariabdalla3319 Před rokem +11

    Bonge la interview,Byser katulia kwenye maongezi,moja ya interview kali na yenye ubora wa hali ya juu

  • @pillyjuma3095
    @pillyjuma3095 Před rokem +32

    The way he say... "Yeah Dada yangu".. one of my favorite artist 🥰

  • @CoachHafidh
    @CoachHafidh Před rokem +40

    Noo wayyy....🔥🔥🔥🔥🙌🏾
    Daah, Naomba niseme ukweli tu leo...Ni hivi leo tu nimemuwaza sana Mr. Blu kwann hapati Mualiko hapa na #Salama?? Daah kama Milunzi yaani Swali langu limepata majibu leoleo❤️🙏🏾
    Big up #JahStoneTown💛💛

  • @AsSd-fi1bg
    @AsSd-fi1bg Před rokem +2

    Hapa kwenye marafiki broo nimekuelewa yan wanapotosha kama mm sinywi sina sikendo za ajab uli wapo marafiki wanipambania niingie huko nawakimbia balaaaa Yan daah na lock nafuta no mtu anakwambia kuolewa nn diri kujiuza marabila pombe ww sio mjanja mm ni mwendo wakuwakimbia tu nikiwa a mama alinipambania sana had kuwa hapa nilipo na mungu kaniona Asante Mungu 💯💕🙏leo nije nimfanye mzaz wangu alie kisa mm hapana 😭💪

  • @sophiakassim6784
    @sophiakassim6784 Před rokem +13

    Naomba ni like kabla hata sijaisikiliza maana I'm sure 100% it's gonna be a marvelous interview ever

  • @msafirikilongo7429
    @msafirikilongo7429 Před rokem +10

    Kwenye interview yoyote Ile ambayo salama hutocheka itakuwa mbaya👍

  • @cheka480
    @cheka480 Před rokem +30

    Naliaa😢kuna neno ameongea ndicho nnachopitia na watoto wangu namuomba Allah subhanah wataala aje kuwa wenye huruma na upendo kwangu waje kunilea. Am happy mr blue kasema kweli we must be humble. Alhamdulilah

  • @bellarmeeuma1653
    @bellarmeeuma1653 Před rokem +16

    Next Salama na Majani(P.Funk)

  • @noeljacob9644
    @noeljacob9644 Před rokem +5

    Salama fanya mpango utuletee ITD au CHID BENZ. tuwasikie

  • @salhatmfinanga9467
    @salhatmfinanga9467 Před 5 měsíci +2

    Very humble May Allah bless him
    Even more and his family.
    One of the best interviews ❤

  • @MuniraShughuli-kc7vj
    @MuniraShughuli-kc7vj Před rokem +8

    Mola awapee maskizano daima kkangu na mkeo in, sha Allah 🤲

  • @SallyMinja
    @SallyMinja Před rokem +33

    Mr Blue anajali sana familia yake,huku kwetu Kinyerezi Mbuyuni kuna duka la viatu basi anakujaga na watoto wake kuwanunulia viatu,ukimkuta sasa anasalimia kila mtu mwenyewe siku hizi kweli hana dharau,havimbi tena😂 peace mwenyewe na fans wake tunaompenda,hapo wife wake yuko kwenye gari, anasubiri wamalize, love his humble self.

  • @abiboseleman1649
    @abiboseleman1649 Před rokem +6

    legends wangu kwenye ubishoo nakupenda.madem😅😅😅

  • @MohammedMohammed-uo5sk
    @MohammedMohammed-uo5sk Před rokem +4

    MR BLUE HE IS AMAN

  • @mohamedslh5478
    @mohamedslh5478 Před rokem +7

    Blue nilikutana nae kwenye show pool bar kenya jamaa nilimuita jina lake halisi akashtuka sana ikabidi anite nyuma ya steji tutulie tutie story mtu safi sana

    • @ismaelmatano3571
      @ismaelmatano3571 Před rokem +1

      Pool bar kitambo mwana sikuizi ipo lakni walibadilisha Jina na wanaleta live band wa Congo

    • @mohamedslh5478
      @mohamedslh5478 Před rokem

      @ismaelmatano3571 yap bro wameibadilisha jina yakitambo izo ilikua ndio semu yetu ya kujirusha analipa mtu 1 tunaingia mtu 2 bure tunagandishana zile stump zao

  • @georgeburchard4872
    @georgeburchard4872 Před rokem +7

    Moja ya interview Bora sana! Mchanganyiko wa hisia za kweli, ukweli wa mambo na umakini katika kuuliza na kujibu maswali! It's one of the best!

  • @G.S985
    @G.S985 Před rokem +4

    Interview nzuri na tamu kuisikia,Mr blue tumecheza nyimbo zako mpaka basi,nimefurahi Salama kutuletea uyu kaka

  • @MuhammedAy-tj4yh
    @MuhammedAy-tj4yh Před rokem +2

    Tunamtaka chid Benz nahisi itakua best interview

  • @hassanshame5385
    @hassanshame5385 Před rokem +5

    Blue..❤

  • @asantehyera6746
    @asantehyera6746 Před rokem +6

    I wish to see Salama na JB (Jacob Stephen)
    HII NI KIU YANGU KUTOKA YAHSTONE TOWN

  • @rubberbandman1213
    @rubberbandman1213 Před rokem +5

    Brue that day alikuwa balaa,hakuna msanii aliyekuwa anavimba kama yeye,akikaa anapinda mgongo😀😀 kwa mikogo

  • @chunanachu2529
    @chunanachu2529 Před rokem +7

    Humble man mashallah

  • @mgallason...5686
    @mgallason...5686 Před rokem +3

    Unajua sana kujishusha, umejaa heshima Keep T up

  • @dostovan5142
    @dostovan5142 Před rokem +9

    Apewe maua yake na miti, na bidha zingine za kilimo

  • @AsSd-fi1bg
    @AsSd-fi1bg Před rokem +1

    Unaakiri sana broo nakupenda sana broo nimejifunzakitu hapo💕🙏nimecheka ety mibangi🤭😂😂😂😂

  • @Modoo_255
    @Modoo_255 Před rokem +4

    msikilize mr blue then nenda kasikilize ngoma yake ya tabasam ndo utamuelewa vzur

  • @Curioustraveller254
    @Curioustraveller254 Před rokem +5

    Asante Salama kwa kumleta Byser

  • @misanyamisanya7499
    @misanyamisanya7499 Před rokem +5

    Lmbaoo Blue interview yako inanifurahisha sana unapozungumzia BHANGI..
    😀😀😀 Kwa mwaka huu salama na Blue naipitisha. Alafu dada salama tuletee MPOKI ikikupendazaaa

  • @wahidatwalib4822
    @wahidatwalib4822 Před rokem +4

    😅😅😅😅😅nilikua na watu wanguuuuu hahahhaa wa kuwavimbia 🎉🎉🎉🎉😂 🇰🇪🇰🇪🇰🇪

  • @davidibrahim9138
    @davidibrahim9138 Před rokem +6

    Blue interview zake huwa zinafunzo sna alafu yupo real sna

  • @floranusgwau7122
    @floranusgwau7122 Před rokem +11

    Jamaa jinsi anavyoongea utafikiri ana PhD 🙌, Babylon byser

  • @JanethiRohoma
    @JanethiRohoma Před rokem +2

    Nimemkubali blue kuongea ukweli kuhusu bangi,mana alikua ananikodi kama tax drive kutoka tbt mpaka ilala kuvuta bangi tu.miaka ya 2005 - kuendelea.

  • @user-wq5fx4iu4c
    @user-wq5fx4iu4c Před rokem +4

    Lovely soul millionaire ❤❤❤

  • @boniface3710
    @boniface3710 Před rokem +7

    Back in the days more love from Kenya.....big up bro

  • @nelsonmwaipaja3727
    @nelsonmwaipaja3727 Před rokem +1

    Najifunza vitu vingi kutoka kwa brother Bizzy 💓💓💓💓

  • @mussahancy6591
    @mussahancy6591 Před rokem +1

    Salama tafuta msudani mmoja pale muhimbili,hojiana nae tusikie,gonga like kama unaunga mkono

  • @richardkalanga7216
    @richardkalanga7216 Před rokem +2

    Story ya mama ake imenigusa mno hata kaka Blue almost atoe chozi akati anamuelezea mama ake may her great soul rest in Paradise.

  • @nicolenabintu2509
    @nicolenabintu2509 Před rokem +8

    Mr bleu ame kuwa responsable 🙏🏾😍

  • @mussahancy6591
    @mussahancy6591 Před 3 měsíci +1

    Leo nimeangalia tena mara ya 37

  • @saidsirya6716
    @saidsirya6716 Před rokem +9

    Oyoo Byser kajikaza kidogo alie... 😢Mzee imenigusa

    • @fongaamike2768
      @fongaamike2768 Před rokem +1

      Kweli asee.. aja tokwa machozi ila una weza kuona moyoni ana lia

    • @saidsirya6716
      @saidsirya6716 Před rokem

      @@fongaamike2768 huyu kweli amepitia mengi

  • @maigajohn5828
    @maigajohn5828 Před rokem

    Hongera sana blue katika Maisha dharau ni kujisikia ni mbaya sana katika Maisha hongera sana kurudi kwenye mstari Maisha Dunia ndo Elimu ya pili ukitoa Elimu ya darasani

  • @mr.yahzadochuno7914
    @mr.yahzadochuno7914 Před rokem +3

    I’m love love blue

  • @kekiplus1andonly
    @kekiplus1andonly Před rokem +4

    Heri sana😂

  • @safiahassan6121
    @safiahassan6121 Před rokem +4

    Sauti kama ya mzee yusufu

  • @affleckmusic3709
    @affleckmusic3709 Před rokem +17

    thanks for bringing mr Blue..let next be majani p funky

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Před rokem +6

    Legendary Bayser, nakukubali sana ❤

  • @HumoudSalim-ct1tz
    @HumoudSalim-ct1tz Před 5 měsíci

    Salama haujambo unamkumb uka bikati na sabriwake mimi humoud nduguyake sefu mmanga na shoga yako farida mimirafikiyake almlaruhum abdul njegere m/ almukepepon amen na bro musa jabir inrahim kuki abudu ndo nimekuwanao ujana wetuwote sisi ndowenye kiponda bila kumsahau dada yetu halima na boss khamisi wake

  • @pastoraile7195
    @pastoraile7195 Před rokem +3

    Bru bonge lajembee

  • @drkiti
    @drkiti Před rokem +3

    Thanks Salama for bringing Mr Blue, such an inspiration🫡

  • @rapamafia3365
    @rapamafia3365 Před rokem +1

    Kibenzi cha watuu bless sana mr blue byser ❤

  • @richardcastromzena5136
    @richardcastromzena5136 Před rokem +6

    5:18 😂
    6:28 mama 💕
    6:34 📌 njaa
    9:18 mama 💕💕
    13:15 📌
    18:24 📌📌📌

  • @benjaminsemwenda3152
    @benjaminsemwenda3152 Před rokem +1

    Star Wangu Wa Muda Wote Babylon Byser Mr Blue, Namkubali Sana Mchizi Ana Kipaji Na Hajui Kulinga Na Hana Dharau Kweli Maisha Ya Kula Ugali Na Kachumbari Yalijitahidi Kumbadilisha, Much Respect Kwake Mzee Wa Kazi

  • @ClipsRUs204
    @ClipsRUs204 Před rokem +4

    Mwamba kakazia "Mabangi"........

  • @hobbieh
    @hobbieh Před rokem +12

    Grew up in his era. Blu and TID, Ferroz and Prof Jay were the bongo flaza guys. They made my days here in Kenya.. good interview.Kindly find Ferroz and interview him.

  • @Elia-ty4pl
    @Elia-ty4pl Před 3 měsíci

    Nimeipenda sana jamani mungu awajalie ❤❤❤❤

  • @obafemibuhari3098
    @obafemibuhari3098 Před rokem +7

    Bizzy kwenye game🔥🔥

  • @marcodavid7448
    @marcodavid7448 Před rokem +6

    Last week niliingia CZcams Kuuliza salama na mr blue ila sikuona kitu nikajiuliza why? Nikakumbuka kuna scandal ya salama kutoka na byser way back a.k.a nyani zee 😂

  • @jacquesmulalirya1704
    @jacquesmulalirya1704 Před rokem

    Mutu wangu ngoma hautuletei ,,hatukusikiii huku congo tena

  • @FranklinMtei
    @FranklinMtei Před rokem

    Blue ni mdogo wangu sana. Nipo kwenye hii fani kabla hajazaliwa. Itoshe kusema he is the GOAT! Toka dakika ya kwanza nausikia wimbo wa BLUE nikajua a star was born! Hajawahi kuniangusha. Yeye na Jay Mo. Hawajawahi kufeli!
    H

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 Před rokem +3

    Nyani zee namkubali since day za Tabasamu ...much love from🇶🇦🇶🇦

  • @macknonkibona2401
    @macknonkibona2401 Před rokem +1

    Huyu mwamba yupo real sana + mh. FA

  • @maigajohn5828
    @maigajohn5828 Před rokem

    Mr blue alianza muziki mdogo sana Hadi kawa mzee baba

  • @user-lr4im4vt7y
    @user-lr4im4vt7y Před rokem +5

    Mlete Millard Ayo

  • @didamugya6039
    @didamugya6039 Před rokem

    LIL Sam A' aka Mr Blue kawainspire wasanii wengi sana upande wa kuchana kwa pozi, kuimba kwa pozi, swaga, mavazi, n.k. he is a Legend

  • @vincentmkanda9785
    @vincentmkanda9785 Před rokem +2

    Big up saana Mzee wa Upala
    U a humbleman

  • @saurijafary3581
    @saurijafary3581 Před rokem +1

    😂😂😂 eti Daah leo nimeyakanyaga

  • @neemaedward852
    @neemaedward852 Před 2 měsíci

    Blue mtu mkweli sana sanaa

  • @tariqabdulkarim5892
    @tariqabdulkarim5892 Před rokem +4

    salama vp tozzy

  • @mchinjanyau9055
    @mchinjanyau9055 Před rokem

    Nachopenda Mrblue Anasema Ukweli Na Mtu Peace Sana Hata Nilpo Kutana Nae Day Wani Na Producer Sulesh Sikutegemea Alivyo Nichangamkia Kama Mi Mtu MKUBWA Vile Tukaenjey Na AkachaMshangoo Kwatu Kama Najuana Nae Before Ana Roho SAFI SI Mtu Wamajivuno Blue MUNGU Amzidishie MAISHA Mareeeeeeeefu Na Furaha Teeeeeele

  • @michaelsikapundwa4955
    @michaelsikapundwa4955 Před 7 měsíci

    Jabir, nakuelewa sana! unaset logical questions

  • @sweetcorner-jx6qb
    @sweetcorner-jx6qb Před rokem +8

    Nilivoona tu interview ya Byser NIKACLICK, nasubiri interview ya BELLE 9

  • @kazkaz1943
    @kazkaz1943 Před rokem +2

    Maua yako byser🎉

  • @Paplick9
    @Paplick9 Před rokem +1

    Legend 🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌

  • @mukirerichard5265
    @mukirerichard5265 Před rokem +4

    I'm excited to see again Mr blue

    • @husseinmaganga6947
      @husseinmaganga6947 Před rokem +1

      Life teach us a lot big up sana byser one of the best interview

  • @jaykabyser229
    @jaykabyser229 Před rokem +2

    Byzy kwenye gamu

  • @user-ui4jk6ej8z
    @user-ui4jk6ej8z Před rokem

    Yani leo ume akikisha turikua tume mutamani saanaaa mr blue much love from Bdi

  • @kilamiko8299
    @kilamiko8299 Před rokem +2

    baisa uko sawa

  • @HashimuHashboy-bo2wl
    @HashimuHashboy-bo2wl Před 3 měsíci

    Mr blue utaliza watu sad story na umeonyesha umekuwa very fasta ,but umekuwa baba kaza

  • @lionelgahungu3442
    @lionelgahungu3442 Před rokem +2

    Next time mulete mukongwee, Chid Benz,Chumaa

  • @yousramutwale2463
    @yousramutwale2463 Před rokem +1

    Nice interview asante sana salama

  • @SPK450
    @SPK450 Před rokem +6

    This gonna be the best interview this year.....

  • @yahcanonbenisrael650
    @yahcanonbenisrael650 Před rokem +7

    TABASAM Mr Blue..mad love from Kenya 🇰🇪

  • @thebeststudio8076
    @thebeststudio8076 Před rokem +1

    Next Salama na Bishop Eliasaph Mattayo Suleiman

  • @albertlilechi4906
    @albertlilechi4906 Před rokem +1

    Mapozi naye

  • @diwanikatayankonko2671
    @diwanikatayankonko2671 Před rokem +2

    Ngwair 😭

  • @richardmavoko-nv5mi
    @richardmavoko-nv5mi Před rokem +1

    Byser ❤️❤️ kontena lenye kutu

  • @edinamkubwa2629
    @edinamkubwa2629 Před rokem

    Safi sanaa dada salama kwa kumleta mr blue naomba utuletee na mc luvanda if possible...

  • @shamsally6277
    @shamsally6277 Před rokem +1

    I love you salama you present the best content

  • @ernestpaulo7843
    @ernestpaulo7843 Před rokem +1

    Sapenda sana intarview za salama ,una jua sana dada

  • @wahidasaid6081
    @wahidasaid6081 Před rokem

    Love this interview with Blue, Byser❤️ na nampenda somo yangu Wahida🥰

  • @seifsaidnshuti9812
    @seifsaidnshuti9812 Před rokem

    Interview hii inaenda kubadili maisha yangu kwa kiasi flan