Jux: "Show Yangu Ya Kwanza Nilikuwa Na Diamond, Nilipewa Elfu Hamsini" | SALAMA NA JUX PART I

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 4. 09. 2022
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Juma Jux ni mtanashati haswa hicho ndicho cha kwanza na suala la yeye pia kuwa muimbaji mzuri (na anayeendelea kujengeka) kunamfanya pia awe wa kipekee, anajua maana halisi ya kufanya kazi kwa bidii ili uweze kutimiza malengo ambayo wewe unakua umejiwekea. Ana aibu pia sana ila hili unaweza ukalitilia shaka kwasababu ya kazi aliyoamua kuichagua. Kwa nilivyo muelewa mimi yeye aliamua kufanya muziki kwasababu rafiki zake walikua wanafanya muziki na zaidi akiamini yeye ni Rapper kuliko hata kuwa muimbaji.
    Kwa mujibu wake kwenye kundi lao hilo la shule yeye ndo alikua sio mkali na wala hakua na neno juu ya hilo, zaidi yeye alikua anataka ku fit in zaidi. Lakini leo hii yeye ndo mwenye mafaniko zaidi kwenye fani yake kuliko wale walokua ndo wakali wa kazi hizo wakati bado wako shuleni. Jux ananiambia mpaka leo wanaendelea kuwa marafiki na rafiki zake wa shule, zaidi Cyrill Kamikaze ambaye amekua kama ndugu yake. Pia anakumbuka mara ya kwanza wimbo wake ulipoenda redioni bila ya matarajio yake na wakati anaambia B12 ameupenda na angependa akutane nae anasema baridi na uwoga na aibu aliyokua anasikia ni Mungu pekee ndo anajua.
    Uzuri pia Jux ana muonekano mzuri na utanashati wake umekua ukimfanya ajikusanyie mashabiki wengi haswa wanawake na ku inspire vijana wengi watake kupita kwenye nyendo zake ili nao waweze kuja kuwa kama yeye siku moja. Combination yake na Bob Maneke nayo ni kitu ambacho kimemfanya Jux aendelee kuwa pale. Wanafahamiana vizuri na kazi ambayo wamekua wakiifanya pamoja imekua ikijieleza yenyewe.
    Jux anakumbuka utanashati na kujituma kwa Marehemu Baba yake ambaye kwa maelezo yake anasema alikua Baba BORA sana, kwanza hakuwahi hata siku moja kumuona Mzee wake na Mama yake wanagombana na siku zote alikua anahakikisha watoto wake wanaishi na kusoma vizuri, nadhani nia yake ilikua kutaka kuwaona watoto wake wakiwa wasomi labda na kufanya kazi za maana zaidi au kuishi maisha mazuri zaidi kuliko yeye wakati anakua. Jux ana kumbuka Mzee wake kama mtu wa kujituma sana ambaye alijichanga kumfikisha mkewe mjini baada ya kupata kazi, yeye alikua tu fundi wa magari ila baada ya mke wake kupata kazi mjini, alihakikisha anafika na mambo mengine yaende kwa uzuri kama ambavyo alikua akiyataka kwa wanawe.
    Mama yake pia humuambia zaidi siku hizi za karibuni baada ya Jux kuanza kung’ara kwenye muziki na biashara zake, Mama yake anamuambia anamkumbusha mno Marehemu mume wake na anajua fika kama angekua hai basi angekua anajivunia yeye kupita kiasi. Uvaaji wake na utanashati na jinsi ambavyo anajituma hivyo vyote Juma Jux amerithi kutoka kwa Marehemu Mzee wake. Mwenyezi Mungu Aendelee Kumpumzisha kwa Amani.
    Mapenzi yake ya dhati ambayo huyaonyesha kwa watu ambao amekua nao katika mahusiano nae pia kwa kiasi kikubwa amechukua kutoka kwa wazazi wake, jinsi ambavyo Baba yake alivyokua anampenda Mama yake, ni kitu ambacho Juma amekua akikikubali sana. Na yoyote ambaye anakua nae amekua akifanya analoweza ili waendelee kudumu. Mwenzetu amekua na mwalimu mzuri sana.
    Kwa akili ya muziki na biashara nadhani tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa kijana huyu hodari wa ki Tanzania. Hivi karibuni brand yake ya African Boy imetia makubaliano na kampuni moja kutoka China ambayo wamekua wakimuona Juma anafanya biashara hiyo tokea akiwa mwanafunzi na kwa jinsi ambayo amekua akifanya kwa muda mrefu na brand na yeye kama mwanamuziki kuzidi kukua nadhani na wao pia waliona fursa ya kufanya nae ushirikiano ili waweze kumuwezesha zaidi ili waweze kushinda WOTE.
    Yangu matumaini kama ada uta enjoy episode hii na kujifunza zaidi.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪CZcams Link bit.ly/CZcamsSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • Zábava

Komentáře • 81

  • @noelbernard6390
    @noelbernard6390 Před rokem +5

    Salama naomba umlete masoud masoud, yule Mzee ana vitu vikubwa Sana.

  • @ilhamsalum6815
    @ilhamsalum6815 Před rokem +5

    Hiki kipindi kishajaza dayari yng salama, thanks so much najifunz mengi 💞

  • @tantinebettynduwimana380

    Salama umependeza ulipo jistiri mashallah

  • @fredyjuma1121
    @fredyjuma1121 Před rokem +3

    Shangazi Fanya bdozen afike Apo ! 🏌️‍♂️ 🔥🔥🔥

  • @chillahthomas3265
    @chillahthomas3265 Před rokem +16

    Salama is Africa's Ellen Degeneres

  • @liciouscharles3370
    @liciouscharles3370 Před rokem +5

    Cyril kamikaze is a GEM

  • @sweetie6934
    @sweetie6934 Před rokem +7

    Iko wapi interview ya binti Zuhura Othman Soud @ Salama

  • @fralex_1276
    @fralex_1276 Před rokem +1

    Nice sema jux mdomo kapaka sukari itakuwa maan sio kwa kuulamba huko

  • @uzungupoint
    @uzungupoint Před rokem +2

    You're so cute Salama, narudia kuangalia tabasamu lako muda wote najikuta nasmile mwenyewe jamani ♥️😊

  • @sankybadee7894
    @sankybadee7894 Před rokem +2

    Salama my sister umekua bibi now Sasa duh bigup sana

  • @barnabasmafuru6735
    @barnabasmafuru6735 Před rokem +1

    Dada Salama unajuaa sanaa na unanifundisha kufanya jambo kwa ufanisi na ufasaha wahari ya juu maana kufanya tuu haitoshi kila mtu anaeza fanya.

  • @nasmasalimu9508
    @nasmasalimu9508 Před rokem +3

    Wow big up sis love you 😍

  • @emojimakopakopa
    @emojimakopakopa Před měsícem

    Bro nakubali sana

  • @danielafelix9856
    @danielafelix9856 Před rokem +3

    I’ve Never missed an episode 🙈😍

  • @flavianchuwa4370
    @flavianchuwa4370 Před rokem

    Kipindi Bora Sana Asante Salama Allah azidi kukulinda

  • @saidabdulkadirmjahid8255

    Chemistry ya #Manecky and #jux is always 🔥🔥🔥

  • @zejuchaztips353
    @zejuchaztips353 Před rokem +2

    Jux is the best

  • @ramakadege7448
    @ramakadege7448 Před rokem +1

    Big up salama j

  • @edwardmachaku1661
    @edwardmachaku1661 Před rokem +1

    Salama, Congratulations 🎉

  • @salimbazmul5806
    @salimbazmul5806 Před rokem +5

    Big Up Sis Salama....✊Shabiki Sugu Huajawahi nifelisha

  • @lastsimbatv1497
    @lastsimbatv1497 Před rokem +2

    Cjawah miss hta kdg salam nakukubar san mlete mondi

  • @wairimu9113
    @wairimu9113 Před rokem +3

    jux is a fine man,God did take his time on him😍😍

  • @thebeneficialknowledge3399

    Kudos to you and your whole team “Salama” you are indeed amazing at what you do, tunasoma mengi kupitia interviews zako, keep up the good work my Zanzibari sis… love from the UK.

  • @BBrown_vevo
    @BBrown_vevo Před rokem +1

    Big interview

  • @khamisimtame7848
    @khamisimtame7848 Před rokem +1

    🔥🔥

  • @AmCool_
    @AmCool_ Před rokem +2

    Ramba ramba lips sana mzee 🥲🥲🥲

  • @issrahayattv1356
    @issrahayattv1356 Před rokem +2

    Kama we ni fun w hipop tujuane hapa 😆 salama atami hua nasikiliza aren b ila c vile sana bt jux namtambua nimnyamwezi sn, please pitieni kw Chanel yngu pia kuna mazuri

  • @mwajumabinwa604
    @mwajumabinwa604 Před rokem +1

    your mom she is here or she’s alive 😁🥰🥰🥰

  • @richardcastromzena5136
    @richardcastromzena5136 Před rokem +1

    6:13Kujiskia studio mara ya kwanza ni magical
    17:40

  • @nicksonchesco233
    @nicksonchesco233 Před rokem +2

    Hii ndio nilikuwa naisubir

  • @samwelisaid5013
    @samwelisaid5013 Před rokem +1

    👍👍👍

  • @officialaftab8760
    @officialaftab8760 Před rokem +1

    GOOD JOB ...,

  • @papaamayux-paps7883
    @papaamayux-paps7883 Před rokem +1

    mbona hii interview haipo Podcast

  • @daudisaidi2267
    @daudisaidi2267 Před rokem

    🚀🚀

  • @adamjoseph9370
    @adamjoseph9370 Před rokem +1

    #AsohiliAnaLile

  • @leejames1536
    @leejames1536 Před rokem +1

    my mom she's proud of me✋😂...sawa kaka

  • @khadijamisayo7476
    @khadijamisayo7476 Před rokem +1

    mwanamuziki ninae mpenda

  • @MARTIN_M9.
    @MARTIN_M9. Před rokem +2

    hii mbona kama imerudiwa🙄

  • @abdulraufmohammedsalum6806

    Wakishua hawatumii nguvu nyingi kutoka

  • @lizaeli6732
    @lizaeli6732 Před rokem +2

    Jamani mtuletee Vicent Kigosi

  • @deograsiaomary62
    @deograsiaomary62 Před rokem

    Salama mbona interview zako nyingi unavaa nguo nyeusi

  • @salumpagae1757
    @salumpagae1757 Před rokem +2

    Misosi akuna😆😆

  • @gsmartcreation5655
    @gsmartcreation5655 Před rokem +1

    Salama Aliwahi kumsaidia Godzilla Katika kuhakikisha anatumia “La na Ra” kwa usahihi. Hili swala hata kaka yetu Juma linamsumbua. Je, kuna msaada wowote anaweza pata hata akiwa studio? Maana inakuta anaimba vizuri Ila unasikia “Nipo Sarama ….” Msaada please

  • @vincentmchau5903
    @vincentmchau5903 Před rokem +2

    Salama kwann usiwe na watazamaji live ?

  • @ommietrendz7175
    @ommietrendz7175 Před rokem +2

    Jux kutoka google unamiaka 32/33 12 yrs ago ulikuwa 20/21 sio 13/14 bro 😎

  • @mshangaf1726
    @mshangaf1726 Před rokem +1

    kwa hiyo yale majina flani ya vinywaji vya hapo huwa kuna baadhi ya watu huwaambii ???😁😁😁

  • @Soft_Touch7
    @Soft_Touch7 Před rokem +1

    @salama hii interview Na Jux ni ile ile tu mlofanya nae kwny MKASI…badilika kidogo dada no hard feelings

  • @__thereal_unclechibo_7953

    Msanii gn unaitwa juma😂😂😂😂😂

  • @TradersEasyWay
    @TradersEasyWay Před rokem +3

    salama umenichekesha, eti ulishwai kuiba? ili swali limekea la ghafla..hahaha

  • @masungajonath8339
    @masungajonath8339 Před rokem

    AFB

  • @Memphisblue22822
    @Memphisblue22822 Před rokem +2

    Kwamba diamond yup out of reach au?

  • @johannahakim8470
    @johannahakim8470 Před rokem +3

    Sasa iyo midomo inakuwasha bro,ata miye nakupendaga mpaka Na nyimbo zako, Ila sipendagi mukiwaga mu ma Interview mukivala izo ma RAYBAN yani Ama mko bipofu mjikeribishi,acha nikamtizama kipenzi changu DIMPOZ

  • @abdallahkhamis7663
    @abdallahkhamis7663 Před rokem +1

    Show huwa inarushwa chanel gani, siku na muda gani pia tafadhali kwa anayefahamu naomba msaada?

  • @kelvinduper
    @kelvinduper Před rokem +2

    Daradara😤

  • @nasralema749
    @nasralema749 Před rokem

    Ankal katoweka

  • @queenmaa30
    @queenmaa30 Před rokem +3

    My mom she's proud of me....jomon kidhungu....

  • @anwaralimuhammed1481
    @anwaralimuhammed1481 Před rokem

    Tunaitaji aje tena king Kiba

  • @ziyandamhlana8776
    @ziyandamhlana8776 Před rokem +4

    Sorry awant knw sister Salama long time people iknw why you don’t bring your husband to do interview

  • @ziyandamhlana8776
    @ziyandamhlana8776 Před rokem +1

    Onasasa unakuta jama sio tena mtuu wako

    • @omarymhomakilo7215
      @omarymhomakilo7215 Před rokem

      Maisha yanatakiwa kuendelea unatakiwa kuwaheshimu tu hata Kama hampo pamoja

  • @noelbernard6390
    @noelbernard6390 Před rokem

    Salama naomba umlete masoud masoud, yule Mzee ana vitu vikubwa Sana.