MKE WA MARCO WA ZABRON SINGERS AMWAGA MACHOZI, MUME WANGU HAJARUDI

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 12. 09. 2024

Komentáře • 2,5K

  • @irenekhuma
    @irenekhuma Před 19 dny +191

    Mjane hafai kuhojiwa jamani,mpeni nafasi ya kuomboleza.... It's not easy...Pole sana dada

    • @RebeccaBhoke
      @RebeccaBhoke Před 19 dny +13

      Kweli kabisa ndugu yangu
      Wamuache tu maana anamaumivu makubwa sana

    • @eunicendumiofficial9801
      @eunicendumiofficial9801 Před 19 dny +8

      Waambie

    • @MimahMimah-b7k
      @MimahMimah-b7k Před 19 dny +11

      Hawa waandishi ni hovyo yan the same story wanauliza kwa kila mtu yan mtu kafiwa na mume unamhoji iyo nguvu anatoa wapi ebu kuweni na utu ndugu waneshaeleza ilikuaje hamtoshe😢😢ki​@RebeccaBhoke

    • @samouritoure3282
      @samouritoure3282 Před 18 dny +6

      Very true. Angepaswa kuachwa aomboleze kwanza😢

    • @zennahmtoto1867
      @zennahmtoto1867 Před 18 dny +4

      Kweli kabsaa wasihojii mfiwaa jamani maumivu ni makubwa snaa

  • @user-pj9ni2xo7p
    @user-pj9ni2xo7p Před 19 dny +255

    Daah pole Sana dadangu, kwa mtu Ambae amepitia Hali Kama hii yako anajua unachomaanisha , Ila kwa mtu Ambae hajawahi kupitia mapito yako hawezi kukuelewa, binafsi najaribu kuvaa viatu vyako, kiukweli vinanibana mno, pole Sana na mungu atakusimamia vyema, kwani kinachoumiza zaidi ni mazoea ambayo hua tumeyaweka kwa wenza wetu.

    • @edarjoan9002
      @edarjoan9002 Před 19 dny +13

      Mimi nikitoka kazi nikapata wangu amejitia kitanzi 😢last month mpaka saizi Nina machungu nalia Kila siku

    • @israeluronu9958
      @israeluronu9958 Před 19 dny

      ​@@edarjoan9002pole sana jmn Mungu akutie nguvu

    • @saummusa4961
      @saummusa4961 Před 19 dny

      ​@@edarjoan9002oh pole sana

    • @esthersissamo1120
      @esthersissamo1120 Před 19 dny +3

      Pole sana dada maumivu uliyonayo Mungu akupe ujasiri

    • @ashleymohamed6935
      @ashleymohamed6935 Před 19 dny +1

      Pole kipenz mungu akutie nguvu

  • @user-sn6dc9gh8k
    @user-sn6dc9gh8k Před 19 dny +105

    Dada yangu pole sana jmn😭😭tumeumia sote ila ww ndo unamaumivu kutuzidi😭😭Mungu akutie nguvu🤲🙏🏻

    • @user-so3ul4ms6u
      @user-so3ul4ms6u Před 18 dny +3

      Poleni Sana mungu awatie nguvu

    • @user-sn6dc9gh8k
      @user-sn6dc9gh8k Před 18 dny

      @@user-so3ul4ms6u asante 😥😭🙏

    • @everlynekamula4731
      @everlynekamula4731 Před 18 dny +2

      Mungu akutie nguvu dadangu na awafariji familia..

    • @MaryMziray-t3z
      @MaryMziray-t3z Před 12 dny +1

      Pole mamaa😭😭😭😭😭😭tunajua maumivu unayo pitia mungu😭😢😭 akutie nguvu kwenye kipindi hiki kigumu😭😭😭😭🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻😭😭😭

    • @bbclondonulimwenguwasoka6126
      @bbclondonulimwenguwasoka6126 Před 4 dny +1

      Poleni sana , so painful but Mungu atawawekea mkono zaidi zidi kumtumaini sana hakika hatawaacha waja wake.

  • @Doctor_counselor_kids_lover

    Kiatu chako ni kizito saaana... Polee sanaa! Pole dada na familia yako.Mungu akutie Nguvu.

  • @user-hw9um8su3k
    @user-hw9um8su3k Před 17 dny +15

    Kusema za ukweli viatu vyako ni vizito mno,eee Mungu ulie baba wa wajane nakuomba simama na mke wa marco Mungu wa mbinguni mbariki na kumfariji yeye pamoja na watoto wake na ndugu wote amiina

  • @jackiepamba5764
    @jackiepamba5764 Před 19 dny +22

    Mungu akufariji dada wewe Na watoto wako Na pia familia.... Pole Sana twashukuru alijua Mungu . Mambo YA Mungu haina kasoro. Take heart

  • @zahorsuleyman7617
    @zahorsuleyman7617 Před 19 dny +205

    Shenzi kabisa yaani mtu anahali iyo mnashindwa hata kumpa muda kwanza,mnamuhoji tu.Hamjitambui,Yaani huu ni ushenzi wa wazi.Mm binafsi ninalilaani hili kwa nguvu zote.Gonga like kwa mweye kulaani ushenzi huu.

  • @kisinza6077
    @kisinza6077 Před 19 dny +62

    Duuuh! Nimelia Tena Kwa mara nyingine! Mungu awape nguvu sana ni maumivu makubwa sana nakuelewa, poleni sana wapendwa. Marco kamaliza mwendo na kazi zake hapa Duniani amekamilisha. Apumzike Kwa amani. 😭😭🕯️🕯️🕯️🕯️🕯️

  • @MwikaSibahuma-qp3pv
    @MwikaSibahuma-qp3pv Před 6 dny +2

    This is so touching 😢😢,may the Almighty God richly continue councils you mama and the whole family including the zabron singers group.May his soul continue resting in eternity peace ✌️

  • @cathywalwit5437
    @cathywalwit5437 Před 18 dny +8

    Pole sana Mke wa Marco Mungu akupe nguvu imani na tumaini .Bwana Yesu akuongoze akujalie nguvu uweze kuwalea watoto maumivu ni makali sana pokea kwa Imani

  • @mercymburu3498
    @mercymburu3498 Před 19 dny +84

    Woiyee😭Dear God visit this lady and wipe her tears,give her peace and comfort..its very heartbreaking 😭😭😭😭

  • @dorahmushi-we6ts
    @dorahmushi-we6ts Před 19 dny +31

    Pole sana binti, pole mtumishi wa Mungu, maumivu yako ni Mungu pekee anayajua, unajihisi nafsi imegawanyika! Lkn
    Mungu atakutia nguvu na kukufariji.😭😭🙏🙏

  • @salomenjoroge7644
    @salomenjoroge7644 Před 19 dny +16

    Pole sana mum mungu ni mume wa wajane umebaki na yeye jitie nguvu mwache marko apumzike kwa amani

  • @johnbernad3990
    @johnbernad3990 Před 19 dny +15

    Pole sana dada najua viatu vyako ni vikubwa mno hawezi kuvivaa mtu yeyote yule ila tu Yesu awe mfariji wako 😢😭😭😭😭

  • @mijashushu8072
    @mijashushu8072 Před 19 dny +12

    Pole sana sana sana binti yangu kipenzi.
    Poleni familia yote ya Zabron.
    Mungu Baba yetu, awe mfariji wenu.
    Mrs Marco weka maisha yako mikononi mwa Rafiki yetu YESU, huyo ndiye mume wako aliye baki ambaye aliyashinda mauti. Kitambo kidogo tutamwona akija nautukufu juu yamawingu. Kufumba nakufumbua maandiko yanasema walio lala wataamshwa. Utamwona Marco kwa umbo lakutokufa. Jipe moyo mkuu binti yangu kipenzi. Imarisha watoto wako ktk kumjua Mungu. Pambana kishujaa usilie sana. Wewe ndiye uushike usukani ukiongizwa na yeye atakaye kuja, YESU MWOKOZI WETU.
    Nakupenda sana binti yangu kipenzi.

  • @doreengakii7464
    @doreengakii7464 Před 19 dny +13

    Haki Nimelia Sana, Mungu akupe Nguvu Ma'am,😢 la Muhimu Joseph Marco Ayakufa Ni Mwili Amatuaga Yuko Mikononi mwa Babayetu Yesu Kristo, my condolences to the family 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪

  • @hellengodson2803
    @hellengodson2803 Před 19 dny +38

    Bwana Yesu akutie nguvu dada...Mungu akawe faraja yako

  • @deborahmgedzi632
    @deborahmgedzi632 Před 19 dny +40

    Pole I Sana. Ufunuo 21:4 iwafariji. Tunaomba faraja ya Mungu Baba Mwenyezi itawale. Amina

  • @doveadventure
    @doveadventure Před 17 dny +16

    Wakati mwingine mbengo TV muwe mnavaaa viatu vya watu hata kama haziwatoshi
    Mtu Ana machungu makumbwa mnamhoji vipi. Tuwe na utu wakati mwingine.
    Pole sana dada Mungu akutie nguvu

  • @KezaAline-u8b
    @KezaAline-u8b Před 18 dny +9

    Mungu wa mbinguni akawe nanyi dada yetuu maana yeye ni baba wa yatima na hata ni mme wa wajane hata sisi tunaishi ni kwa neema yake pekee 🙏

  • @selynakambili9470
    @selynakambili9470 Před 19 dny +13

    😭😭😭Sina la kusema Mimi nimelia Hadi watoto wamenisaidia kulia aki,pole dadangu 😭😭😭 Mungu akufariji pamoja na watoto kwa jumla,Marco amelala tu, Yesu akirudi hakika tutamuona tena,pata pole zangu kutoka Kenya 🇰🇪🇰🇪

    • @Lamo254
      @Lamo254 Před 19 dny +1

      So sad but kitu inanipa faraja n kwamba haya yoote mlikua mkiomba mungu mpka dakika ya mwisho.
      Jitinyie moyo familia just shukuru kwa yenye yametendeka sababu yy anajua vyema kabsa

    • @user-ki4kh5ub4h
      @user-ki4kh5ub4h Před 19 dny

      MUNGU awe pamoja nanyie kipindi hiki cha majonzi yenu kazi ya MUNGU haina makosa MUNGU awatie nguvu na kuwafuta machozi sifa heshima na utukufu tumrudishie MUNGU anayestahili kuabudiwa milele yote ameni ameni ameni

  • @claraedwardmalingumu3565
    @claraedwardmalingumu3565 Před 19 dny +6

    Yesu wangu ,yaani alijijua eti funga KWa ajili yangu ,omba na watt ucku ,kumbe ndo safari yake alishaanza kiroho ,kimwili haupo nasi ila kiroho upo nasi ,pumzika salama na pole sana dada KWa kumpoteza mume wako,,dada unajua kumpa maneno mazuri mfiwa barikiwa sana

  • @dorahmushi-we6ts
    @dorahmushi-we6ts Před 19 dny +11

    Mama mzazi wa Marco, pole sana mama, Mungu akutie nguvu mpendwa, familia poleni sana, tuendelee kuomba na kushukuru.😭😭🙏🙏

  • @helenarhobi1250
    @helenarhobi1250 Před 18 dny +11

    Pole sana mama. Marco apumzike kwa amani.Amina. Jipe tu moyo!!!

  • @LylahMrombo
    @LylahMrombo Před 18 dny +6

    😭😭😭😭😭😭hyo video iko so emotional pliz mm naomba ifutwe ju mm ileniliza 🫶🫶🫶kwa mke w marehemu n watoto wke aki mamake ndugu marafiki pole kwa msiba much love from 🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪🇰🇪

  • @elizabethmichael6201
    @elizabethmichael6201 Před 19 dny +7

    Pole sana dadangu,,,,Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi amina🙏🙏🙏be strong 💪 my dear sister

  • @sarahmsafiri1062
    @sarahmsafiri1062 Před 19 dny +13

    Pole sana mpendwa wangu dah!! kibinadamu inauma sana sana maumivu yako hayaelezeki ni MUNGU pekee awezae kuponya majeraha yako, MUNGU akutie nguvu

  • @elizabethmakaranga218
    @elizabethmakaranga218 Před 19 dny +16

    Kutukana siyo njia nzuri sanaaa bali kuhujiwa ni jambo la kawaida ,uchngu upo lakini hakuna anaeweza kutoa taarifa kamili zaidi ya mke wake ,rafiki yake wa karibu sanaaa kuliko unavyojua , halafu siyo wa kwanza kufariki na watu kwa kawaida ndivyo inavyokuwa mwenyezi mungu aliweka kila kitu sawa halafu alitujenga ktk kutufariji na kisha kuishi bila mtu huyu tena basi ndivyo hivyo ,kikubwa mwenyezi mungu awafariji tu kila nafsi itaonja mauti ,tuombe wamalize vizuri na ktk kipindi hiki kigumu cha msimba ,

  • @elizabethmureithi5051
    @elizabethmureithi5051 Před 16 dny +3

    Si jameni angekimbiswa hapa tu Nairobi Kenya tuko na madaktari wa moyo ni wengi . Jameni pole sana mama.

  • @ElizaMwandu
    @ElizaMwandu Před 18 dny +3

    Pole sana dada Mungu wa mbinguni akutie nguvu ktk kipindi hiki kigumu ulichonacho.😭😭😭R.IP Marco

  • @pamelamapolu71
    @pamelamapolu71 Před 19 dny +10

    Machozi yananitiririka pole sana mdogo wangu.Bwana Yesu awe mfariji wako ktk kipindi hiki kigumu unachopitia

  • @sophiasomba2837
    @sophiasomba2837 Před 19 dny +11

    Pole sana mdogo wangu, Mwenyezi Mungu akutie nguvu dada. Jikaze mama, baba Mungu tawala, tawala maisha ya mama huyu na watoto wake, ambao wameachwa na Marco. Baba Mungu tunajua hakuna kama wewe, mpe ujasiri mama huyu. Pole sana dada

  • @bwireasteria5604
    @bwireasteria5604 Před 19 dny +5

    Mungu akawe faraja kwako mwanamke mwenzangu. Jipe ujasiri sana ktk kipindi hiki ili uweze kuimalika na kufanyika faraja hata kwa watoto pia. Ni kweli viatu vyako haviwez kumtosha mtu yeyote lkn kuwa naiman kuwa ck moja parapanda itakapolia tutamuona Marco Zabron . Jipe moyo kipenzi

  • @CAROLINENGOGE
    @CAROLINENGOGE Před 16 dny +3

    Pole sana Dada yangu mungu akupenguvu may his grace be upon you.

  • @Janetlulonde
    @Janetlulonde Před 15 dny +2

    My God remember Marcos wife it's going to be a hard journey,but Lord cover her and strengthen her, Jehovah lord he has left behind very young children, i trust in you , You will protect and provide for them . Good lord remember his whole family, personally his departure has hurt me , their songs ministered to me , for now we leave everything to you. May his family never lack. In Jesus name i pray. Amen

  • @LeylaSaria
    @LeylaSaria Před 19 dny +23

    Dah kiukwel mungu akutie nguvu kipnz nimejikuta nalia aisee omba yasikukute

  • @ElizabethJoseph-iq4uj
    @ElizabethJoseph-iq4uj Před 19 dny +10

    Dah inauma sana umeniliza sana dada najua maumivu yake nimeyapitia niliachiwa watoto wadogo sana jipe moyo Mungu akawe mtetezi wako

  • @ShalhaS-wj6qf
    @ShalhaS-wj6qf Před 19 dny +7

    Watangazaji hamna huruma hata kidogo mtu huu bado ana maumivu makali na mnamusumbuwa tu. Mungu amuraze mahali vema nandoa yao ilijuwa ya nachamungu jmn😢😢hii intavyu inaniliza sana

  • @faithchelangat5244
    @faithchelangat5244 Před 2 dny +2

    This is when you tell God your will is hurting me but you can't question it pole sana

  • @user-gh4ym7ji8v
    @user-gh4ym7ji8v Před 17 dny +1

    Mungu akutie nguvu dada na watoto. YEYE tu ndiye anayeweza kutibu maumivu ya moyo mliyonayo familia ya Marco na Zabron.

  • @ritapiusnicolaus7068
    @ritapiusnicolaus7068 Před 19 dny +27

    Inauma sana 😭😭😭😭😭Damu ya YESU ikawaponye mioyo ya hii familia 🙏🙏💔 Apumzike kwa Amani Marco🙏🙏🕯️🕊️

  • @barrehotel-q5t
    @barrehotel-q5t Před 19 dny +6

    Pole sana Mamdogo Mwenyenzi mungu huchukua kilicho chake kwahiyo kilicho baki ni umwoombe tu kwa Mwenyenzimungu ampokee tu na amuweke mahali patakatifu 😢😢😢😢

  • @DorothyPyuza
    @DorothyPyuza Před 19 dny +7

    Oh! Jamani pole mdogo wangu damu ya YESU ikutetee na watoto 😢😢😢p'se msimhoji jamani muacheni kwanza eeh! MUNGU mshike binti huyu Zaburi 125 iwe faraja kwake na familia nzima nasi tulioguswa na msiba huu😢😢😢😢

  • @AshuIddy
    @AshuIddy Před 18 dny +1

    Dada umeniliza sana dah,poleh namuomba mungu akupe nguvu,na tunamuombea kaka etu apumzike kwa amani ,poleh dada angu kazi ya mola Haina makosa 🙏

  • @jumannemwakalinga2586
    @jumannemwakalinga2586 Před 17 dny +1

    Jamani, acheni kumhoji huyu dada. Mnamwongezea majonzi bure.
    Pole sana dada Mungu awe mfariji wako.
    RIP Marco

    • @gloriaamase9764
      @gloriaamase9764 Před 17 dny

      Pia mm sipendi mtu anapo umia kuojiwa very bad😢

  • @Minsirerickjuniorofficial1272

    Mngekuwa watu wema Mngempa huyu Mama Privacy Aomboleze mume wake, Mnamuumiza zaidi, Mngemwacha kabisa bila mahojiano kabisa 😢😢

    • @zainaburuthzainaburuth3376
      @zainaburuthzainaburuth3376 Před 19 dny +1

      Akii 😭😭😭

    • @anneferguson1158
      @anneferguson1158 Před 15 dny

      I agree with you . This was not a good time for an interview. Let her mourn. May God give her strength to continue raising their children.

  • @jamilajamila9682
    @jamilajamila9682 Před 19 dny +23

    I'm Crying 😢 😭 😭 brother wangu pia alikufa kwa same problem hiyo hiyo alipelekwa maskini mpk India pia lakini bila mafanikio wakarudi nyini kwetu na tukaendelea matibabu hospital huku tena.alikuwa kijana umri takriba miaka 28,nimemkumbukia sana alipokuwa mgonjwa na mpk dakika za mwisho tuko nae hospital 😢😢.mola awaweke pahala pema inshallah amin. Dada huyu mola ampe subra kwa maumivu makali anayo makini 😢😢mola ampe faraja ampe wepesi ktk moyo wake yarabi😢😢😢pole sana dada

  • @KSA-hu5he
    @KSA-hu5he Před 19 dny +25

    Poleni sana kazi ya mungu Haina makosa mlipenda ila mungu kampenda zaidi

  • @esthernkurani8300
    @esthernkurani8300 Před 12 dny

    From Kenya pole sana ni uchungu sana Mungu pekee atawafariji, Mungu ni Baba wa yatima na Mume wa wajane, mtegemee Yeye.
    It shall be well

  • @Claris-b7z
    @Claris-b7z Před 18 dny +1

    Nyie waandishi wa habari wakati mwingine kuweni na huruma basi mtu ako kwenye hali hii mnamuhoji hivi kweli jamani,mungu amfariji huyu dada😭

  • @FabianJeremiah-p3t
    @FabianJeremiah-p3t Před 19 dny +17

    Mungu akutie nguvu dada angu na akupe ujasiri uwalee watoto wako wakue jmn

  • @user-ym6ts2tb1i
    @user-ym6ts2tb1i Před 19 dny +6

    Dah pole sana my mungu akutie nguvu dada pole kwakweri unapitia kipindi kigumu sana pole sana kipenzi ni kweri chema akidumu pole my sisi sote njia yeti ni Moja pole kipenzi tizama watoto dajh ingaw ngum lakini atuna jinsi 😭😭😭😭😭😭😭😭 pole

  • @noorischmutisch5321
    @noorischmutisch5321 Před 19 dny +27

    Pole sana dadangu Allah akupe subra na akutie nguvu,sote njia ni hiyo😢,,kazi ya mungu haina makosa yy anajua zaidi,,ni uchungu sana.

  • @user-fi4cg1fo4i
    @user-fi4cg1fo4i Před 18 dny +1

    Huu msiba umenitoa machozi kwakwel pole sana dada mungu akupe faraja kwakwel kiatu chako ni kizito kwakwel

  • @puritykathure9907
    @puritykathure9907 Před 17 dny

    May the grace that supperses all human understanding be upon u mama.n the entire family n Tanzania yooote kwa jumla.frm Kenya we are praying for you.🇰🇪

  • @AnnaKyungai
    @AnnaKyungai Před 19 dny +7

    Bwana Yesu mama huyu anakuhitaji wewe peke Yako sisi tunalia tu hatumsaidii kitu....watoto wake jamani oooh Mungu hakika wewe ni Mungu

  • @GraceIbrahim-i5t
    @GraceIbrahim-i5t Před 19 dny +10

    Jamani ii usimuliwe tu jamani inauma sana umenikumbusha machungu mume wangu aliniaga anasafili jumatano alhamis naletewa maiti kapata ajari pole sana Mungu akutie nguvu

  • @user-mc6um1it1r
    @user-mc6um1it1r Před 19 dny +4

    Pole sana mdogo wangi naomba mungu akutie nguvu kweli inauma sana sikia tyuu kwa mwenzako😢😢😢

  • @user-vn3wz6hd7x
    @user-vn3wz6hd7x Před 17 dny

    Sorrrry mamaaaaa!!!!!!!!!😢 Cant withhold my tears😢😢😢😢😢. It's wellll. The Lord is faithful dear...Mume wa wajane Mungu wa mbinguni hatakuacha katu!!!!

  • @AnnastaciahKaiva
    @AnnastaciahKaiva Před 16 dny

    Pole sana dadagu kwa msiba wa mumeo Marco Joseph.Roho yake ipumzike kwa amani na Mola awajalie amani 🕊️

  • @DEBORAHMASANJA-yz3go
    @DEBORAHMASANJA-yz3go Před 19 dny +6

    Pole sana mwanangu Mungu akutie nguvu sana jipe moyo mkuu

  • @samuelmurugu2710
    @samuelmurugu2710 Před 19 dny +6

    Hakuna kitu kinakuanga na uchungu kama kifo weee poleni sana mungu awape faraja

  • @faithwambui5378
    @faithwambui5378 Před 19 dny +6

    Woooi aki ni chungu 😭😭😭. Binti mdogo hivi na watoto wa changa..Mungu wetu kumbuka Huyu mama🙏🙏

  • @jenikanuth1700
    @jenikanuth1700 Před 17 dny

    Pole Sana Dada angu Mungu akawe Faraja yako Siku Zote Maumivu Unayopitia Ni makali Mnoooo😭😭😭🙌🙌🙌
    Lakin Utayaweza Kwa Jina La Yesu Mungu akawe Mfariji wako Machungu yako yote Mkabidhi Mungu,
    Mungu wetu ni Mwaminifu Hakika Atakutendea Pole Sana Dada kwa Hiki Kipindi Kigumu kwako Inauma Mnoooo😭😭😭🙌🙌🙌🙌 Mungu akutete😭😭😭

  • @schadomaliro1230
    @schadomaliro1230 Před 17 dny +1

    Dah 😭😭😭 hadi manjozi inatiririka jamani Pole sana Mungu akutie nguvu Mama wetu

  • @MariamOmary-uq3rs
    @MariamOmary-uq3rs Před 19 dny +45

    😭😭😭😭nyie waandishi mnadhambi sn ivi mnajua machungu anayo pitia huyo dada kweli au fraha yenu kuona izo maick zenu zinabeba machozi ya watu

    • @Njeriii536
      @Njeriii536 Před 19 dny +2

      Kwani alilazimishwa kuongea?

    • @PelagiaIsdol
      @PelagiaIsdol Před 19 dny

      ​@@Njeriii536tema mate chini wewe

    • @hellenmushi1945
      @hellenmushi1945 Před 19 dny +4

      Yaan wasingemhoji kwa hali hio jaman sio kabisa

    • @MariamOmary-uq3rs
      @MariamOmary-uq3rs Před 19 dny +5

      @@Njeriii536 kama hujui kufiwa tuliza komwe kwani huyo dada alinwita nwandishi nyumbani kwake

    • @lucymburu7082
      @lucymburu7082 Před 19 dny +2

      Very true my sis this is not good time

  • @user-sn6dc9gh8k
    @user-sn6dc9gh8k Před 19 dny +7

    Ataumia sana cku wa2 wakitawanyika hapo akabaki pekeyake yaan unaona maumivu yameanza mwanzo😭😭

    • @HappySamson-hl8tx
      @HappySamson-hl8tx Před 19 dny +1

      Hata hiv anamoyo maana angekuwa mwingine hata kuongea hivi inakuaga haiwezekani

  • @user-li2ux2zn3g
    @user-li2ux2zn3g Před 19 dny +7

    Pole sn dada yg kwa msiba 😭😭😭😭😭😭Mungu akutiye nguvu dada.🇰🇪🇰🇪🇰🇪

  • @DevothaWilbard
    @DevothaWilbard Před 18 dny +1

    Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu na pole sana dada kufiwa kusikie kwingine tu😭😭 Mungu akutie nguvu

  • @tumainingonyanyi
    @tumainingonyanyi Před 18 dny

    pole sana mungu akawe faraja kwako na watoto wako pamoja na familiya yote ya marco mpe nafsi mungu akawe farajakawako siku zote.maisha yako pole sana nimeumia dah kweli tunapita

  • @emes602
    @emes602 Před 19 dny +13

    Dah dah dah dah maskin alijua anawaacha

  • @angelraphael4500
    @angelraphael4500 Před 19 dny +10

    Nataman hata kuwatukana hao waandishi,,,na nngekua boss wao ningewafukuza mnamuhojije mjane ambae hata haelewi akili yake na moyo viko wapi😢😢

  • @carolinewangari6652
    @carolinewangari6652 Před 19 dny +5

    Ooh God,such a young gal and children 😭😭😭🫂🫂🫂hugs mama from Kenya

  • @santydismas3262
    @santydismas3262 Před 16 dny

    Inaumiza sana ,ni huzuni, fikiria mtu wa pembeni roho inauma,unalia unateseka vip kuhusu mkewe na familia yake,inaumiza sana jamani😭😭MUNGU akawe mfariji wa familia na zabron singers wote kwa ujumla,
    Ila nilichokiona kinachonipa matumaini,marco alikua anaamini kwa MUNGU na lipo tumaini kubwa sana,tulie kwa kias kwa maisha ya kawaida ila shujaa hajafa bali kapumzika
    R.I.P shujaa vita umevipiga katika imani,mwendo umeumaliza🧎‍♀️🧎‍♀️🙏🙏

  • @mulwamunyao6237
    @mulwamunyao6237 Před 18 dny

    Waoh...am grateful of the comforting Madam..Mungu awatie na nguvu zaidi...

  • @NeemaNabintu
    @NeemaNabintu Před 19 dny +21

    Jamani,muwe na hutu hâta kidogo.huyo dada was watu kwani kunamuhimu Gani kumuhoji?

    • @CeciliaMutiso2
      @CeciliaMutiso2 Před 19 dny

      Nashangaa

    • @avernegervas5839
      @avernegervas5839 Před 19 dny +1

      Ila ifkie hatua cyo lazima kuhojihoji kwani doctor c alitoa ufafanuzi me wananikera kwakweli,

    • @HappyMnyawami
      @HappyMnyawami Před 19 dny

      Kwakweli wanakwaza

    • @lucylight9341
      @lucylight9341 Před 19 dny +1

      Inaitwa healing therapy ...anapo endelea kunena zaidi kuhusu tukio Hilo anapona kutoka ndani ingawaje ni mazito kweli. It's good to talk infact anafaa akae na WATU wanao mtembelea KWA wakati mwingi ili aongee zaidi apone . Pole sana dada take heart ❤️❤️❤️. Poleni sana kwa all the families and friends en wa Tanzania wote kwa jumla poleni 🙏🙏🙏

    • @NamulindwaBeneth
      @NamulindwaBeneth Před 19 dny

      True it's not good to question her

  • @mpeliibrahim398
    @mpeliibrahim398 Před 19 dny +18

    Nyie waandishi ni wajinga mnawezaje kumhoji mtu akiwa na maumivu

    • @vumiliapaul2659
      @vumiliapaul2659 Před 19 dny

      Waandishi wapuuzi mno wanaona sifa😢😢

    • @janecharo1196
      @janecharo1196 Před 19 dny

      Àki hii sio kweli kwamfàno Fanya kama uko kwako ungeeza jieleza kweli 😢😢😢😢 mbona hivi jaman mnakosa busara kam utu hamna😢😢

    • @SalomeCyprian
      @SalomeCyprian Před 19 dny

      Yaan 😢

    • @MussaKitaluta
      @MussaKitaluta Před 19 dny

      Hata wewe acha ujinga, bila waandishi ungepata wapi haya.

    • @lydiaminyeko1398
      @lydiaminyeko1398 Před 19 dny

      Washenzi saana

  • @ruthmoshi2620
    @ruthmoshi2620 Před 17 dny

    Mungu pekee ndio faraja yako dada,Mungu akupe faraja ya kweli,akuinue akuwezeshe uweze kulea watoto wenu,apumzike kwa amani

  • @NyamateWeja
    @NyamateWeja Před 18 dny

    Pole sana sana mdogo..hatuna namna nyingine wala neno lakuoonya maumivu makali uliyo nayo😭😭😭😭zaidi yakumuomba mungu awefaraja kuu katika kipindi hiki cha maumivu na majonzi ya kumpoteza mume wako mpenzi..mungu akufariji sana sana🙏🙏

  • @MlakitegoPrisca
    @MlakitegoPrisca Před 16 dny

    Pole dada kila nafsi utaona mauti
    Mshukuru Mungu kwa kila jambo Kwake alitoka na amerudi Jina la bwana litukuzwe
    AMINA

  • @preciousism4493
    @preciousism4493 Před 13 dny +1

    Mungu ndiyee mpaji wako na wanao mtegemee yeye ndiye mume sahihi aliyebakiaaa na baba wa wanao 😢😢😢😢

  • @jenniferluka1779
    @jenniferluka1779 Před 17 dny

    Baba Mungu mfariji binti yako na msimaishe imara na kumpa nguvu za kuwatunza watoto wao. Your name be praised Always.

  • @stephenkatunzi8922
    @stephenkatunzi8922 Před 17 dny

    Pole sana kwetu sote tulioguswa,na msiba huu.Mungu akazidi kuwa faraja kwetu sote, hasa mke wa marehemu

  • @LettyogaiAdongo
    @LettyogaiAdongo Před 9 dny

    pole sana dada yangu hii imeniumiza sana nili kuwa nime penda sana nyimbo zake wacha mungu atawale na mungu akufinike na watoto

  • @mohammadomar2872
    @mohammadomar2872 Před 18 dny

    Nimejipata nikitoa machozi.
    Poleni dadangu.
    Weka imani kwa mungu atakulinda na kukufariji pamoja na watoto..

  • @ngehupeter
    @ngehupeter Před 3 dny

    Dah 😭😭😭😭, machozi yamenitoka , inasikitisha na inatia huruma jamaan, kumpoteza mtu ulie zoeana nae ,mhu bas tu , " Binafsi namuomba mwenyz mungu akutie NGUVU na akusimamie ktk kipind iki cha majonzi! Pia awafariji ndugu na jamaa na awape tumaini la kuwa ipo siku mtakutana na Marco na mtafrah nae milele " KAZI ya MUNGU Haina MAKOSA , tumshukuru kwa kila JAMBO" Marco tulimpenda ila MUNGU kampenda ZAIDI!

  • @AdmiringJumpingSpider-jb3xq

    Dah! Polen wafiwa wote hasa familia yake na watoto inauma sana mpk machozi yananitoka for really tumeumia sana kazi ya Mungu 🙏

  • @BrendaPastor-zc4hs
    @BrendaPastor-zc4hs Před 12 dny +1

    Pole sana sana dada mungu akutie nguvu katika jina la yesu

  • @RachaelEddy
    @RachaelEddy Před 12 dny

    Poleni sana. Mungu akushike mkono dada. This is the hardest thing ever. May God give His grace over everything and take care of you.

  • @fradontv7476
    @fradontv7476 Před 19 dny +1

    Msiba ni mtihani unaozidi akili zetu watahiniwa.....hakika bila mungu hatuwez shinda jaribu Hilo tukiwa salama, poleen sana shemeji yetu mungu akushike mkono na kukutia nguvu katika mtihani huo mzito...polen wanafamilia kwa ujumla na ndg Jamaa na marfk cjui mko katika maumivu Gani maana kama sisi watu wa nje tunaumia kiasi hiki je nyie wa ndani😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭..poleni sana na sana Tena sana.....ni Zaid ya maumivu😭😭😭😭😭😭

  • @dianaonesmo6951
    @dianaonesmo6951 Před 18 dny +1

    Pole sanaa kipenzi mungu akutiee nguvu kwenyee kipind iki kigumu,tunakupendaa

  • @nyamisikatama2679
    @nyamisikatama2679 Před 18 dny

    Jamani pole dada pole mnooo ninahisi maumivu japo kwa mbali Mungu akutie nguvu Faraja Mungu wa Mbinguni akukumbatie Maumivu hayo yapoteee kwa Jina la Yesu. Kumbuka dada Kuna tumaini baada ya kifo.

  • @demiliankatabalo2472
    @demiliankatabalo2472 Před 16 dny

    Maumivu unayoyapitia nayajua mpendwa. Viatu vyako nilishawai kuvia. Jipe moyo na ujasili ili uweze kuwalea watoto. Pole sana

  • @deusdedithmanugulilo1980

    Jamii ya Watanzania wanamatatizo makubwa ya kisaikolojia yanayobebwa na tamaduni za kipuuzi. Mwandishi aliyefanya hii interview hongera sana kwa kumfanya Mjane aongee. umepunguza sehemu ya maumivu ndani ya moyo wake kwa kutoa kile anapitia. wote mnaoshutumu waandishi wa habari endeleeni kusalia na uzuzu wenu

  • @JoyceLingtone
    @JoyceLingtone Před 12 dny

    Pole sana dada mungu akutie nguvu yeye ndiye baba wayatima na nimume wawaje

  • @jacksonwahome
    @jacksonwahome Před 19 dny

    Woiyeee hii ni maumivu makali sana mpaka yanatoa mtu machozi bila kujua😭😭😭😭😭😭😭mungu tufaliji na haswa bi marco,may God give him a very sqeet rest 🕊️🕊️🕊️🕯️🕯️🕯️

  • @GetrudaIsaya
    @GetrudaIsaya Před 16 dny

    Pole Sana dada angu najua unayo pitia tumuombee tuu udongo auchagui mtu yoyot wote tutakufa tumuombee bro Marko

  • @deboramsangi360
    @deboramsangi360 Před 18 dny

    Pole kipenzi, Mungu atakufariji jisemee tu kuwa hata kwa haya bado wewe ni Mungu. Pole sana Watoto wako Mungu atawalinda inauma kweli ila ktk yote Mungu anabaki Mungu.

  • @MillicentCarolNyapala
    @MillicentCarolNyapala Před 13 dny

    Pole sana dadangu kwa ukweli yauma sana Tena zaidi lakini kwa hayo yote twa rudisha shukran kwa mwenyezi Mungu na Mungu akutie nguvu

  • @MgayaMayagila
    @MgayaMayagila Před 16 dny

    Pole sana. Dada mungu atakutia nguvu hiyo nikazi ya mungu bwana ametoa bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe