Dizasta Vina - Hatia VI

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 11. 09. 2024
  • Official lyric video of Dizasta Vina perfoming Hatia VI, Marking a 3rd release Off the album A father figure
    Stream/download Hatia VI
    Mdundo - mdundo.com/son...
    Boomplay - www.boomplay.c...
    Apple Music - / hatia-vi-single
    Audiomack - audiomack.com/...
    Spotify - open.spotify.c...
    Dizasta Vina on socials
    Instagram - / dizastavina
    Twitter - / dizastavina
    Facebook - / dizastavina07
    Lyrics
    Salamu baba mi mwanao
    Naandika waraka kwa maana hutaki vikao
    Nahitaji majibu nikihisi ni haki yangu
    Najisikia vibaya kusikia unaishi na sina ngao
    Nimeshika kalamu haya maandiko
    Yametoka mahala timamu palipo wito
    Sijatumwa na wenzangu hii ni akili yangu mwenyewe
    Waraka huu ni salamu zangu za mwisho
    Nina akili najua mambo yanapokuwa mrama
    Natambua uhalisia nazitambua njama
    Pengine nitachokisema kitazua laana
    Nitaibeba lawama kwa kujifanya najua sana
    Ndugu zangu wanachosema sisawiri
    Mpaka wanahisi nimeanza kuchezwa na akili
    Hata wakitaka kunitenga sibadili
    Ulinitenga jana siogopi kutengwa mara mbili baba
    Majirani wanatamba kukuongelea
    Wakisema sina baba na kazi ya kukusemea
    Na ukweli ni kwamba ni utata sana kukutetea
    Maana shida ilinibana na baba haukutokea je
    Utachukia nikiegemea penye power
    Au utanipa hatia mikono michafu niende nawa
    Nipo mbele yako kamwe siigizi uwepo kama wewe
    Basi jibu kero zangu twende sawa
    Juzi nilikuhonga maua, Jana nikakuhonga na tena
    Subira gani isiyo na heri shaabash
    Nimechoka kuchomwa na jua
    Jionyeshe leo nimechoka barua
    Nimechoka barua
    Barua zako zinahubiri ushindi
    Kutangaza vita wakati mtutu tu haushiki
    Na cha ajabu maadui ni wa kurithi
    Chanzo ni kitendawili nilichokisoma kwenye hadithi
    Njoo ulee wagonjwa ndo' uongee kuhusu upendo
    Tuvae bendera moja ndio uongee kuhusu uzalendo
    Msamehe aliyekufanya uondoke ndo' uendeelee
    Kuhubiri kutubu kuhifadhi na kusamehe
    Jenga daraja baba mahusiano yanavunjika
    Hamna faraja huoni wanao wamekaza ndita
    Jenga imani tena kwa wote waliogadhibika
    Jenga kama ambavyo uliijenga hii nyumba kwa siku sita
    Haukuja tulipopita kwenye
    Miaka 400 ya utumwa njaa maradhi vita giza nene
    Nipe sababu moja vipi nikujali vipi nikupende
    Sababu moja tu kukusikiliza wewe
    Nyumba uliyotupa ina twiga ina ndovu
    Majirani warembo wenye figa na vitovu
    Vinavutia, kuna dhahabu kadhalika
    Zinatutajirisha ila zinafanya tuwe waovu
    Huu uchafu atatetea wakili gani
    Siri ipi na asili zetu hazilingani
    Japo akili mali sio siri asili ghali
    Tunamwagana damu kugombea rasilimali
    Tunaisha kwa wivu wetu
    Tunasita kwa uvivu wetu
    Tunazikwa na mbinu zetu
    Tunapikwa na kinu chetu
    Tunasita kushika insha
    Tunapitwa na wapita njia
    Umoja unavunjika huku
    Tumeshikwa na simu zetu
    Sina tofauti nna watoto kama wewe
    Napata changamoto kama wewe
    Kama soja kwa ajili yao napambana naposhindwa
    Tunateseka pamoja Kwani sina roho ndogo kama wewe
    Asante kwa ulezi dhanifu
    Asante kwa kuniandikia sheria za kishenzi
    Kwenye pegi nadhifu asante kwa kuniacha stendi
    Nikisubiri mapenzi ya ahadi nakesha nikienzi wasifu
    Asante kwakuwa mbali nami
    Kiasi nina shaka kuwa haujui nina hali gani
    Umeacha barua ndefu ambayo sijui kama yako
    Au ya kufoji na bado inahitaji mkalimani
    Ona Napanga mipango ya kijinga
    Ona naghafirika nafanya uliyopinga
    Ona napinda napika chuki wenzangu
    Wenye nyumba ndinga maana mimi ngano tu inanishinda
    Huko mbali umejitenga nashanga
    Haujui kinachosemwa na jamaa
    Haujui usafi ni ndoto, ndoto iliyotengwa na ridhaa
    Haujui ni ngumu sana kuwa mwema ukiwa na njaa
    Haujui kuhusu adha za dunia
    Haujui kero maana maudhi yalipokupata ukakimbia
    Haujui kuhusu kifo na magonjwa haujui kuhusu
    Insha na maandiko haziwezi tibu hivi vidonda
    Ndugu zangu umewajenga kwa vpaji
    Wapo kadhaa umewapa pesa za mitaji
    Wengine warembo wenye vyeo wenye hadhi
    Sisi tusio na hali tulalamike kunyimwa haki
    Imechafuka taswira inaenda slow focus
    Pengine its all bogus
    Pengine I'm mad
    And I'm talking to my own conscious
    Labda haupo ni hadithi tu
    Na kama ulifikia kifo ufalme umefika mwisho
    Haurudi tena so nawaza
    Lini utakuwa mwisho wa uhanithi huu
    Uzazi sio simple but I still care
    Nina watoto shida zipo and I'm still here
    Matatizo yanapokaba kwenye shingo sikimbii
    Napambana mpaka mwisho like a real man
    Sio kosa langu kutokuwa na uhakika upo
    SikujuI sura maana hauna picha Google
    Nipe ishara kuwa unaishi hata nikituma
    bakshishi niwe ninajua kuwa zinafika huko
    Wenye majoho rangi nyeupe na dhahabu
    Wana barua zako za tafsiri za kiarabu
    Wanasema wanakujua kuliko ninavyokujua
    Nikiwatilia shaka wananiita mwanaharamu
    Je ni kweli uliwapa uwakilishi
    Ni ngumu kuwasadiki hasa ukiwadadisi
    Kama wanaongea uhalisi au wanachonga sera
    Sometimes hawafundishi wananiomba hela
    Thibitisha hizi hifadhi si uwongo
    Uliowaacha wana nishani za,,,,
    read full lyrics - genius.com/Diz...

Komentáře • 622

  • @dizastavinafanaccount
    @dizastavinafanaccount Před 8 měsíci +5

    the talent immense

  • @alphoncesamwel6973
    @alphoncesamwel6973 Před 8 měsíci +10

    "Matatizo yavavokaba shingo skimbii
    ....Napambana mpaka mwisho like realMen" ka imekutia hamasa basi like hapa twende sawa na Dizasta Vina as real Men.

  • @DeLaP2908
    @DeLaP2908 Před 8 měsíci +94

    Uumbaji ni mara moja tu. Muumbaji huwa hageuki nyuma. Akishaumba mara moja anaweka vimelea vya usahihi katika mahesabu yake na kuacha utashi na chembe ya usahihi katika viumbe na miimili ya uumbaji na kila kiumbe kujiendesha chenyewe. Muumbaji ndio uumbaji wenyewe, Muumbaji sio mtu, sio baba, sio mama, wala sio mtoto. Muumbaji ni nishati huru, nguvu kubwa uliyopo katika kila kitu. Muumbaji hahusiki na dini wala siasa, hahusiki na mifumo yoyote dhalimu ya kibinadamu. Muumbaji anaona na haoni, Muumbaji yupo na hayupo. Muumbaji ni kila tunachokiona na tusichokiona. uumbaji ni fumbo. Muumbaji hahukumiwi wala hahukumu. So Hakuna hukumu bali kujihukumu wenyewe. Ila kuna hatia. HATIA IS REAL. and the writer is confronting his own consciousness, na mwandishi pia hana hatia. OVER!!

  • @emmanuelpius6387
    @emmanuelpius6387 Před 8 měsíci +10

    Nimesikiliza mara kadhaa nimejifunza mambo mawili, mara ya kwanza nilijua baba anayeongelewa ni baba mzazi ambaye alitelekeza familia yake akiwemo mtoto wake huyu ambaye ameamua kumuweka wazi kuwa hamtaki tena,
    Baadae nimegundua aliyezungumziwa ni Mungu baba ambaye ameumba dunia na akawatelekeza watoto wake wanashambuliwa na matatizo kama umasikini na njaa vinavyopelekeq chuki na maovu, anasema UNAJUA NI NGUMU SANA KUWA MWEMA UKIWA NA NJAA.
    Mungu ameacha wosia ambao haujulikani ni wa Mungu kweli au ni wa kufoji ? hapo anamanisha BIBLIA

    • @Njokaa
      @Njokaa Před 8 měsíci +1

      Rudia tena kusikiliza broo hajamaanisha Mungu

    • @mingajohn6518
      @mingajohn6518 Před 8 měsíci

      ​@@Njokaawe ndo umepotea kabisa rud ukasikilize vzuri,,huyo mwamba kaongea sahihi

  • @dizastavina
    @dizastavina  Před 8 měsíci +220

    Lipia copy yako ya album ya #AFF sasa. Album itatumwa kwa EMAIL, WHATSAPP au TELEGRAM. Tuma 10,000tzs /700ksh kwenda MPESA 0762 158 871 au TIGO PESA 0655 696 811 (jina EDGER MWAIPETA) kisha tuma sms ya muamala wako kwa namba uliyolipia. Usisahau kutuma Email au namba yako ya WhatsApp kwa ajili ya kupokea album. Let's go
    #DZSTVN

  • @davabackup7767
    @davabackup7767 Před 8 měsíci +9

    Kumamake hadi nimeogopa ila sio kwa ubaya bali kwa fact ulizoongea asee ziko on point daah yani kifupi am speechless mwamba sina la kukulaumu pia sina la kumlaumu mungu Dizasta wewe ni zaid ya fire ama moto wa jahannamu 🔥🔥🔥

    • @moudyboe
      @moudyboe Před 8 měsíci

      be careful what you saying next broo 😅😅😅

  • @user-ih6hk5nh7v
    @user-ih6hk5nh7v Před 8 měsíci +5

    Dizasta vina ni next level bongo nzima hakuna huyu jamaa n hatar ni umeme mkubwa

  • @msakatonge.
    @msakatonge. Před 8 měsíci +6

    Napiga magoti chini na kushukuru uwepo wa @dizasta ,sanaa na ujuzi alonao ni safi ni kama nanasi kwa maana ni tamu sana, HESHIMA KWAKO BROTHER kwa maana unatupa tunavyovihitaji na sio tunavyovitaka , Nakiri Kwa kusema Elimu yako ni kubwa zaidi ya masterz levels. I love u so much bro, Napenda sanaa yako ,napenda uwasilishaji wako , napenda ideas zako❤❤❤

  • @freakboy1804
    @freakboy1804 Před 8 měsíci +5

    2 Tim 2:13 SUV
    Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
    Mungu aturehemu sisi viumbe wake tusio stahili hata kulitaja jina lake. Utukufu wako Uishi Milele na Milele Amina

  • @ussiussi3413
    @ussiussi3413 Před 8 měsíci +15

    Good artistic work. Ni ishu ya kugusa existence (uwepo) and inexistence (kutokuwepo) kwa Mungu yaani, imani ya kuamini yupo na yanayofanyika yote ni kwamba kwanini hatuoni reaction yake physically, halafu imani ya kuamini hayupo na yanayofanyika yote ujinga tu wa hii dunia. Ukiwa una akili nzuri utaelewa hapo kwenye uwepo wake amegusa imani hasa ya Kiislamu(wenye majoho meupe na tafsiri za kiarabu) na hapo anapozungumzia inexistence (kutokuwepo kwa Mungu) anazungumzia imani ya wale "Wasioamini Mungu"(ATHEISTS), hapa kawagusa sana Jamaa zetu ambao wengi ndio Matajiri wa dunia(Mabilionea na watu maarufu) walipoegemea na ndipo wimbo ulipobeba maudhui yake makubwa na hoja nyingi alizozizungumza humu ni za hawa ATHEISTS. Skiza vzuri wimbo then, ukielewa ninachokwwmbia like hapa.

    • @Macaveli_tz
      @Macaveli_tz Před 8 měsíci +1

      Sikiliza tena huu wimbo kwa umakini,,, upo nje ya theme Kuna code bado hujazipata vzr ili kuelewa DZST anaongea na nani hasa kwenye huu wimbo

    • @ussiussi3413
      @ussiussi3413 Před 8 měsíci +4

      @@Macaveli_tz Bado hujataka kuelewa Bro, ngoja nikupe mwanga kidogo labda utafungua bongo yako, ni hivi; "HATIA" ni hali ya kushuku au kubaini uwepo wa makosa/ dhambi yaliyotendeka au kutokuwepo, yeye Msanii ame-act kama ni mtoto anayejaribu kuteta au kulalama uwepo wa Baba yake au kutokuwepo kwake wakati yeye (Msanii) yupo physically kwa maana anaonekana na mhitaji wa mambo lakini mahitaji hayo huyapata kwa shida bila uwepo wa kuonekana kwa Baba yake kwa lengo la msaada wa wazi so, ww unadhani ni Baba gani anayezungumzwa!!!??? Hilo moja, lakini pia unapaswa kutambua kuwa, yeye hana uhakika na mafundisho juu ya maisha yake na imani yatokanayo na watoto wenzake(Mitume, Maaskofu, Mapadri, Makasisi, Walimu, Masheikh, watu wa kawaida kwa ujumla waliopita zamanj na wa sasa) hapo alimgusa Yesu kama ni mtoto kwa maana alikimbia baada ya dhiki kwa maana hajarudi hadi sasa na hajui kama amekwenda mazina bila kurudi tena ulimwenguni, tatu ni kwamba yeye Msanii anajaribu kutaja Imani 3 ambazo ni Uislamu kwa maana pale alipotaja waliojivisha majoho meupe na wenye kumtafsiri Mungu kwa lugha ya kiarabu, imani ya pili ya kikrosto pale aliposema Wakivutana kwenye majadiliano na wakati mwengine humuomba hela(sadaka na zaka makanisani) kwa maana kuna usanii, lakini pia imani ya 3 ni hiyo aliyoibeba yeye zaidi kwenye wimbo na kuwekeza mawazo yake mbayo ni imani isiyoamini Mungu (ATHEISM).
      Bro nadhani kichwa chako bado kina akili changa, pull up your socks utaelewa ukiwa muda umeshakupita kitambo.

    • @ommygraphics4355
      @ommygraphics4355 Před 8 měsíci +1

      Fact

    • @rusellcleopas1282
      @rusellcleopas1282 Před 8 měsíci +2

      Umeenda mle mle ninamofikilia mfano hii verse "sio kosa langu kutokuwa na uhakika upo , sikujui sura maana hauna picha google, nipe ishara kuwa unaishi hata nikituma bakishishi niwe najua kuwa zinafika huko" kwa nilivyoelewa anaongelea swala la kutoa sadaki

    • @dizastavinafanaccount
      @dizastavinafanaccount Před 8 měsíci +1

      majoho meupe ma dhahani Catholic..Tafsiri za kiarabu ni Quran

  • @lucasgodfrey6976
    @lucasgodfrey6976 Před 8 měsíci +9

    Fikra zilizoandikwa hapa hazipaswi kuhukumiwa kama utashi wako haujauacha iwe huru. Kwanza ruhusu utashi wako upokee hizi frikra huru alaf usione hvyo vitu unavyoviona vya thaman kila mmoja anaona hivyo. Hii ni kubwa sana inahitaji mtu mwenye moyo huru na akili huru

  • @Njokaa
    @Njokaa Před 8 měsíci +4

    Kabla sijaskiza nacomment kwanza coz najua Vina anajua sana

  • @user-fw9jz6jk3w
    @user-fw9jz6jk3w Před 8 měsíci +3

    I ngoma naisubiri sana mana kila ngoma ya vina lazima iwe kali

  • @dariusmsagha
    @dariusmsagha Před 8 měsíci +8

    The writing is incredible and very relevant to the socio-economic setting of African communities.
    Great love from Kenya.

  • @fredrickwarioba713
    @fredrickwarioba713 Před 8 měsíci +7

    Enyi watoto wa 2070, nawakumbusha kwamba huu wimbo umetoka leo 05/01/2024. Na huyu ndiye msanii wetu pendwa wa hip hop. Toleo la mwisho la viumbe wa aina yake

    • @emmanuellwinga5686
      @emmanuellwinga5686 Před 8 měsíci +2

      😂😂😂😂😂umeiweka kitaalamu kaka utakumbukwa

  • @juliustinala4372
    @juliustinala4372 Před 8 měsíci +7

    Tunapaswa kutambua kua msanii ni kioo cha jamii dizasta alichokifanya humu ni kizuri kabisa maana kunawatu wanawaza hivi....yeye kazungumzia mawazo ya mtu au watu waliokata tamaa na wamejaribu kumkaribia Mungu lkn wanahis bado hawajapata majibu
    Tunapaswa kujua msanii ni mtu huru na ni muwakilishi wa watu,wanayowaza na wanayoyapitia so the guy is presenting peoples feelings
    Imani inachangamoto nyingi sana
    Mm ni mkatoliki na naipenda imani yangu...wakati fulani nilipokua katika huduma moja namuubiria mtu aliniuliza je utajuaje kama Mungu amekusamehe na humuoni!?
    So dizasta ametisha sana humu..MUNGU akubariki edger kwa watu wa imani ya kweli hii ni challenge wala sio kufuru🔥🔥

  • @dizastavinafanaccount
    @dizastavinafanaccount Před 8 měsíci +7

    Dizasta ni msanii, ni kioo. Taswira yake ni reflection ya alichokiona au kusikia kwa watu.
    Hana hatia kuwakilisha mawazo ya watu.

  • @mbarakanassibu5234
    @mbarakanassibu5234 Před 8 měsíci +4

    The black Maradona,hakika hiki ni kiumbe kipo katika dimension ya pekee, Mungu akuweke tuendelee kupata madini kwani kwa sasa tumetumia robo ya akili yako hata nusu hatujafika hii ndo maana ya MSANII NA MWANAFALSAFA. Be blessed Dizasta

  • @sunsetstudioz
    @sunsetstudioz Před 8 měsíci +6

    🔥Hamuongelei baba uliemuacha nyumbani.... Mwana ana kikao na BABA WA MBINGUNI... UTUNZIIIIIII NI NEXT LEVEL. 🔥

  • @mohamedshabani619
    @mohamedshabani619 Před 8 měsíci +7

    I wish dear father angejibu hii diss track kwake ili Dizasta aendelee kusema maana anaonekana bado ana meng ya kumuuliza Baba hasa juu ya Bakshishi anazotuma

    • @Mtumishi2000
      @Mtumishi2000 Před 8 měsíci

      Mungu kashamjibu kabla ya yy kuzaliwa... kamjibu kwa kumpa pumzi aliyotumia kuandika na kuingiza vocal kwenye hii Beat. Binafsi kanichanganya, wengi hawaelewi aliyeongelewa humo "Baba"

  • @LambeDon_
    @LambeDon_ Před 8 měsíci +5

    Kama humpendi dizasta vina nenda Muhimbili kapimwe mkojo + akili nitalipia Gharama za matibabu🎉

  • @arnaldo7319
    @arnaldo7319 Před 8 měsíci +4

    Uyo baba anakuja kama Mungu alafu anakata,yani kiufupi sielewi

  • @aminmohammed4249
    @aminmohammed4249 Před 8 měsíci +7

    Dizasta FANS ..we are in safe HANDS🙌🙌🔥…the kid delivers what we’ve been waitin for

  • @tcm.republic
    @tcm.republic Před 8 měsíci +3

    Siku zote huwa nategea kupata muziki mpya kutoka kwa dizasta vina 🔥💯

  • @emmanuelkiserere3523
    @emmanuelkiserere3523 Před 8 měsíci +4

    Vinaah mwanamuziki genious anaeishi.... Tz kwa sas hv

  • @EjidyJosephu
    @EjidyJosephu Před 8 měsíci +6

    Toleo la mwisho la viumbe wa aina yake na hawatokuwepo tena big up to Dizasta vina (KING VINA)

  • @reaganmakallo6824
    @reaganmakallo6824 Před 7 měsíci +7

    Hii ngomaaa nimeisikiliza zaidi ya mara 24 ndio nimeielewaà..tena nimetafuta eneo ambalo hakuna sauti nitakayosikia zaidi ya sauti ya hii nyimbooo..
    Ukiwa na imani ndogo hii nyimbo inakupoteza
    Na ukijifanya unaiman sana utashindwa kujibu hoja hata moja...
    ....he think more and more
    "Utanihukumu vp na una hubiri masamaha""

  • @morganmwaikusa8194
    @morganmwaikusa8194 Před 8 měsíci +7

    Dizasta vina a living genius. Kumbukumbu zinaonyesha watu kama hawa hawakufikia idadi ya 100 miongoni mwao ni Dizasta vina, leonardo da vinci, michalangelo, socrates na wachache wengine kadhaa… kama sisi ni wanae BABA kwann hajengi daraja tumfikie, alipopata changamoto ya dhambi zetu hima alitoeka asirudi kwann kajificha na anajua mm ni kiumbe dhaifu yeye ndiye alinizaa… hakika nimemtafuta sana lkn kajificha hatak nimuone hivyo nimechoka nae ni dhamu yake kunitafuta maana anajua pakunikuta dear.
    Wachungaji na masheikh wananiomba pesa ya kuwa wanamtumia lkn sina hakika kama hizo bakshishi zinafika huko.. vina GENIUS 😂😂😂

  • @directorerikey3291
    @directorerikey3291 Před 8 měsíci +24

    Wakwanza kukoment daah the long wait is over

  • @carlospaul1032
    @carlospaul1032 Před 8 měsíci +4

    Huyu dizasta ni rafiki yangu sana japo hajui Hilo
    Nakubali sana this story-teller

  • @rick_bey
    @rick_bey Před 8 měsíci +4

    Kaka umemgeukia na mshua kabisaa

  • @tracejeezy8917
    @tracejeezy8917 Před 8 měsíci +3

    Vina anaongea na Mungu .

  • @erastomichael9840
    @erastomichael9840 Před 8 měsíci +3

    Nikiteta hadithi utahisi NGUGI 🔥🔥🔥

  • @raqamzomaica2836
    @raqamzomaica2836 Před 8 měsíci +5

    Mufti mLamba haraM🔞

  • @raphaelchuche6281
    @raphaelchuche6281 Před 8 měsíci +3

    mmmmmh kumuelewa vina inabidi uwe umekula umeshiba na huna stress 🔥

    • @Njokaa
      @Njokaa Před 8 měsíci

      Yaani mm mpaka kichwa kimeanza kuuma bado sielewi , kwani ka zungumzia nini broo!

    • @gagalinodenatrick1652
      @gagalinodenatrick1652 Před 8 měsíci

      ​@@Njokaamjomba nenda kamsikilize zuchu na mond wameachia ngoma mpya kwa huyu maradona utameza sana panado

  • @AzadiSaidi
    @AzadiSaidi Před měsícem +1

    Co malaika we n Mungu w rap!yesu wa hi generation,🎉,

  • @bogertze3129
    @bogertze3129 Před 8 měsíci +4

    the hottest raper @dizasta Vina "nashangaa wenzangu wanakesha wakiimba utukufu Wa dhambi zako"

  • @DismasPhidason-vu6bt
    @DismasPhidason-vu6bt Před 8 měsíci +2

    Kweli Unapika Mawe Yanaiva Maverse... Salamu Baba Mi Mwanao Naandika Waraka Kwa Maana Hutaki Vikao Nahitaji Majibu Nikihisi Ni Haki Yangu Najihisi Vibaya Nikusikia Unahishi Na Sina Nguo... VINA 💪

  • @dinnoboy5803
    @dinnoboy5803 Před 8 měsíci +7

    Hatia namba 6 ni wimbo ambao nimeuelewa vizuri na mkasa ote unamuhusu mungu lakini pia unaweza usimuelewe vizuri kama utatumia vitabu vya kidini kumuelewa sababu dini hujazaliwanayo ni (program) ambayo baada ya kuzaliwa ndio ukaanza kuwekewa taratibu ili ubongo wako uzowee. Lakini pia dini zinaweza zikawa hazijakosea kufundisha ila uelewa wa watu wenyewe ndio tatizo linapoanzia
    mfano: nikisema "mungu yupo" simaanishi ni (object) au ni kiumbe bali ninguvu ambayo ipo kila sehemu, kwakila mtu na kila kiumbe lakini wapumbavu ndio wanamuumba mungu nakusema yupo sehemu anaangalia wanadamu tunavyo teseka😢

  • @EarningsEdge101
    @EarningsEdge101 Před 8 měsíci +3

    Utakuwa muongo ukisema umeielewa hii ngoma kwa kuisikiliza mara moja tu. Its need 🔂🔂🔂

    • @tracejeezy8917
      @tracejeezy8917 Před 8 měsíci +1

      Yaani mara ya kwanza tu bila hata kurudia, nimejua anaongea na Mungu, maybe anatafsiri yake lakini kwangu hiyo ndio theme ya ngoma nilong'amua.

  • @selemanmzee5804
    @selemanmzee5804 Před 8 měsíci +3

    Here we go

  • @tabora_boy
    @tabora_boy Před 8 měsíci +3

    Akili kubwa Sana 🔥🔥🔥

  • @ramadhanichitendile9332
    @ramadhanichitendile9332 Před 8 měsíci +3

    We jamaa una sayari yako 👊

  • @carlpeterthegreat5007
    @carlpeterthegreat5007 Před 8 měsíci +3

    We. Ni nyoko Ngoma Kali

  • @mdcalive
    @mdcalive Před 8 měsíci +3

    Miaka 6 iliyopita kwenye kanisa nikasema this man is hopsin wa bongo and he prove again

  • @BrunohBrunoh
    @BrunohBrunoh Před 8 měsíci +5

    Your The speaking book 📖 🙏 thank you for the free class fam 🙏🙏

  • @shadowmatingo5072
    @shadowmatingo5072 Před 8 měsíci +5

    Viongoz wa dini njoonu mumtetee MUNGU we u huku

  • @SaidiMkinga
    @SaidiMkinga Před 8 měsíci +4

    Uyu mwamba akitoaga ngoma sina muda wa ku loading chapo na download then naunganisha Bluetooth nasikia HIP HOP ASILI 😅😅. Ndomaana ni DIZASTA VINA

  • @user-ru2oz8zj2y
    @user-ru2oz8zj2y Před 8 měsíci +2

    NI NGUMU SANA KUWA MWEMA UKIWA NA NJAA👏👏👏👏🔥🔥🔥🔥🔥🔥🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🙋

  • @AlbetoGwoma
    @AlbetoGwoma Před měsícem +1

    Mungu ni nguvu ya asili

  • @azezizokukufarm825
    @azezizokukufarm825 Před 8 měsíci +5

    Wenye akili kama za DIZASTA, mara nyingi hujenga hoja kwenye kila jambo na ni ngumu kuamini kuhusu MUNGU

  • @boygavana4674
    @boygavana4674 Před 8 měsíci +2

    Kwanza beat kali na limekutana na fundi wakuchora

  • @alextanzania
    @alextanzania Před 8 měsíci +5

    Ringle beats aksante kwa mdundo.

  • @mosesdavid-vm5hk
    @mosesdavid-vm5hk Před 8 měsíci +2

    Kwanza nimechukua maji ya uhai makubwa kabla sijamsikiliza T'TCHA DIZ kisha napitia comments za wanna kisha kila mmmoja unapiga like kwangu kisha tunamsikiliza GENIUS himself✔️

  • @Njokaa
    @Njokaa Před 8 měsíci +5

    Mm nilikosea badala ya kusikiliza wimbo kwanza nikatizama comments na comments ya kwanza kuiona ilisema jamaa anaongea na Mungu na ndo maana nilienda kuiskiza ngoma nilipata taabu sana kuielewa mpaka kichwa kikaanza kuniuma an

  • @paccowilly5672
    @paccowilly5672 Před 8 měsíci +2

    Siri ipi na Siri zetu hazilingani / G.O.A.T shukrani sana 🙌🔥🔥🔥

  • @moudyboe
    @moudyboe Před 8 měsíci +3

    huna baya bkack maradona sijui huwa unawaza nini upatunga tungo tata much respect

  • @Valiant0790
    @Valiant0790 Před 8 měsíci +2

    Vina ndo jina🙌

  • @AlexLihogosa-om3zh
    @AlexLihogosa-om3zh Před 8 měsíci +2

    Kumbe sijachelewa

  • @nawinahke710
    @nawinahke710 Před 8 měsíci +3

    Wa pili

  • @japharysety6890
    @japharysety6890 Před 8 měsíci +4

    Dini nayo ni matrix mbaya sanaa

  • @user-sw4rh6wo1g
    @user-sw4rh6wo1g Před 8 měsíci +2

    Hakuna rapper kama Dizasta apa Bongo case closed 🔥👨‍⚖️🙌

  • @KassimAlly-en3qj
    @KassimAlly-en3qj Před 4 měsíci +4

    Mh vina umesoma shule Gani

  • @zolomwashinga9074
    @zolomwashinga9074 Před 8 měsíci +2

    Uyu ni baba mungu kama sikosei ila umemqambia ukweli yeye anajua pa kukutia

  • @simbaforex
    @simbaforex Před 8 měsíci +1

    Nani ameelewa baba anaye zungumziwa 🔥🔥 Dizasta vina tunzi zimetukuka...✊🏾✊🏾

  • @monixkarim-st4qm
    @monixkarim-st4qm Před 8 měsíci +3

    Sikupingi genius , naenjoy coz kila nikisikiza ngoma zako huwa na madetate uwezo ulio nao wa uwandishi

  • @mzeewakazi2439
    @mzeewakazi2439 Před 8 měsíci +3

    Tiba ya ubongo skuzote💪

  • @user-mb7jh4vh6d
    @user-mb7jh4vh6d Před 8 měsíci +4

    Kama umegundua Baba anayezungumziwa hapa ni MUNGU ngonga like ❤

    • @Macaveli_tz
      @Macaveli_tz Před 8 měsíci

      Sikiliza tena huu wimbo kwa umakini,,, upo nje ya theme Kuna code bado hujazipata vzr ili kuelewa DZST anaongea na nani hasa kwenye huu wimbo

  • @mzee012
    @mzee012 Před 8 měsíci +1

    Kichwa cha uyu jamaa ni hatari aiseee,anawaza mbali sana uyu jamaa ni 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥

  • @johannesjoseph7496
    @johannesjoseph7496 Před 8 měsíci +6

    Ushauri wenye upendo kabisa..naamini vina ni muelewa na hii ni challenge kwetu tunaompenda ila yuko imani tofauti na sisi...tutafte namna ya kujibu hoja zake za msingi...yeye anadai Mungu amejificha, anakwepa majukumu nk..
    Shida ni kwamba elimu kuhusu Mungu aliyonayo inafikia hapo... Shida nyingine anaamini sana ktk yeye mwenyewe(selfbelief) ambavyo ni vzr kujiamini kuliko kiumbe kingne chochote isipokua Muumbaji, ..natamani nipate mda nae tuelekezane unabii, kama ni mwana wa Mungu ataelewa, kama ni mwana wa Lucifer ataendelea na msimamo na inabaki kuombeana tu mwisho mwema.....kwa kifupi uyo anaetamani kuonana nae siku si nyingi kila jicho litamuona, na maswali hayo kama hataruhusu au kutafta majibu yake kwetu tunaojua atajibiwa na yeye mwenyewe..Baba hajajificha wala hajakimbia wala hajatuacha wapweke..Baba ni roho(anaishi ndani ya mioyo ya watoto wake_we feel his presence through holly spirit)).Anachodai D kua yuko mpweke ni sawa maana atheist hawaamini uwepo wake hivyo hayuko nao na amewaacha wafuate akili zao za upotovu...yaani wanafanya karma/jin(mf aladin lamp)-nguvu ya asili kua ndo mungu kumbe hiyo nguvu ya asili nayo imewekwa na Muumbaji(Mungu)....uzuri tupo ndani ya saa moja wa shetani na mawakala zake kutawala kisha Masihi arudi na kuondoa matrix iliyopo na kusimika falme mpya ambamo ndani yake Baba tutamuona kama alivyo katika utukufu wake...Tumepewa ishara za mwisho kabisa kabla ya masihi na Baba kushuka na mji wa yerusalemu hapa duniani....moja ni yule mwana wa kuasi kujidhihirisha na kujiinua ndani ya hekalu la Mungu na pili ni ni watu wote kutiishwa chini ya utawala wa mwana huyo wa kuasi...uzuri sasa ata wenye nuru kiasi wameanza muona na mifumo inazidi imarika adi mataifa ya uku kwetu ambako teknolojia ndo kikwazo kikubwa cha kuyatimiza haya..Nimekuombea rafiki yang D, hunijui ila mi ni mmoja wa fun wako wakubwa mno...imagine kwenye simu yangu sina nyimbo za secular zozote ila zako tu...napenda namna unavyotazama mambo kwa namna tofauti na huo ndo ubunifu unaonivuta kila ukitoa ngoma lazima niitafute,
    Umekua ukimsema sana Mungu nae ni mwingi wa rehema anakujua vzr kuliko sisi tunavyokujua ndo maana maana bado anakuvumilia kama anavyotuvumilia sote...nakuombea uo utaji uliofunga sub conscious yako utoke ndo conscious mind yako itaweza ngamua ukweli kuhusu Baba...kama kweli unataka majibu toka kwa Baba-sikiliza majibu toka kwa ndugu zako-kua na moyo wa kisomi uliotayari kujifunza maarifa mapya na kukubali ulipopungua ila wajuzi wakujazilizie....

    • @reaganmakallo6824
      @reaganmakallo6824 Před 7 měsíci

      Ameuliza ni vipi utanihukumu na unahubiri msamahaa??

    • @mhogomchungu7882
      @mhogomchungu7882 Před 7 měsíci

      Mungu ni conscioussness yenyw it is here and now. Be at the present and sense your being (essence)

    • @johannesjoseph7496
      @johannesjoseph7496 Před 6 měsíci

      ​@@reaganmakallo6824ametoa mda mrefu wa waovu kutubu na kusamehewa makosa yao kabisa--alivumilia maovu yetu ata baada ya kuteswa aliwaombea msamaha, bado anawaita watu watubu ili anapoenda kuishiliza dhambi wasipotee pamoja na waasi..Mungu hafurahii kuangamiza alichoumba

    • @johannesjoseph7496
      @johannesjoseph7496 Před 6 měsíci

      ​@@mhogomchungu7882consciousness(utashi) ni sehemu ya ubongo inayotusaidia kuamua kutenda jema au baya...Mungu katupa hii ili tumpende kwa utashi pasipo kumonitiwa kama robot....ni kwel Mungu ni omnipresent ila haimaaniishi yeye ni sehemu ya uumbaji-yey ndiye aliyeumba na yupo kila sehemu kupitia nguvu ya roho mtakatifu-ulimwengu wote unathibitika kwa nguvu yake

    • @titusjairo6482
      @titusjairo6482 Před měsícem

      Ulipo andika neno lucifer nimejua kitu kuhusu wewe 😂😂 am so sorry

  • @brunoh_bx
    @brunoh_bx Před 8 měsíci +2

    Mwamba huyu hapaaaa🔥🔥👏👏

  • @McBabuAyub-dr1po
    @McBabuAyub-dr1po Před 8 měsíci +2

    Umeiweka hip hop lever za juuu sana

  • @titusjairo6482
    @titusjairo6482 Před měsícem +1

    Watu wengi wamekuwa wakimuomba mungu wakifanikiwa huwa wanamshukuru ila wasipofanikiwa huwa hawamlaumu mungu kwann? Nahisi bwana vina kaamua kuelezea jibu langui😊

  • @Steven3.
    @Steven3. Před 8 měsíci +2

    Ngoma Kali blood uko vizuriii

  • @g_eazmusic1329
    @g_eazmusic1329 Před 8 měsíci +4

    Aujui ningumu sana kuwa mwema ukiwa na njaa 😂😂😂

  • @Deejay_plannet255
    @Deejay_plannet255 Před 8 měsíci +3

    Hiki kisa ni cha kweli na kuna watu wameishi maiaha ambayo mnyama DIZASTA VINA kayoongelea kabisa. Daima utabaki kuwa mwana hip hop bora na storyteller wa muda wote🎉🎉❤❤

  • @hashimmzirai9293
    @hashimmzirai9293 Před 5 měsíci +3

    uweziii kua mwema ukiwa na njaaa

  • @daudmaikomwakapoma213
    @daudmaikomwakapoma213 Před 8 měsíci +3

    Ujumbe kutoka kwetu unaotuwakilisha tunasema kazi umeifanya vyema tumeisikia na tunakushushia baraka tele kutoka Unyakyusani Afrika Tanzania Mbeya. Tunakusihi endelea kuwaeleza ukweli kuwa hizo hisia walizoambiwa ni za kiroho zimefunika furaha yao ya mila na utamaduni wao na kuhubiriwa kukimbia mila zao
    Kaulimbiu
    AJHOBILE MAGUFULI

  • @user-be1kp6sq1g
    @user-be1kp6sq1g Před 8 měsíci +2

    Dizasta ni msanii bora kwa story telling
    Hatia ii, iv na v zitabakia alama kubwa kwake
    wengi tunamfuatilia kwa uandishi wa namna ile
    sababu unaakisi uhalisia wa maisha unasisimua na unaburudisha pia

  • @user-fr3rf6dn7j
    @user-fr3rf6dn7j Před 8 měsíci +2

    Mungu anakupenda atakupenda mpk uamue ww!!! Kama unavyo jiona kuwa Baba bora Mungu n Bora Zaid wala hakuchukiii

  • @Mox-lh6yt
    @Mox-lh6yt Před 8 měsíci +3

    Kaka unajua mpaka unatia huruma 😊

  • @dawhacker2216
    @dawhacker2216 Před 8 měsíci +3

    Commenter wengi mnaniangusha
    Kwenye huu wimbo beba linalo kuhusu km alikuhusu mute tu utakuwa ujaelewa😊 MARADONA MWEUSI👊🇹🇿

  • @victorwilliam9987
    @victorwilliam9987 Před 8 měsíci +3

    kuna mengi sana mekubaliana nayo kuhusu huu wimbo ila kumbuka kuna upande wa pili wa shilingi na hivyo kuna mengi sijakubali kutokana na kua njia yangu au viatu yangu sio viatu vya muandishi na tunatakiwa tujue hajakosea kwasababu hata wewe ungekua kwenye viatu vyake maybe ungewaza na kujiuliza maswali anayoyauliza yeye.. Dizasta ni Giant kwenye hii game ❤

  • @anoldpotentin2446
    @anoldpotentin2446 Před 7 měsíci +3

    Mungu yupo ila shida nikujua jinsi anavyofanya kazi, Mungu ayupo kwajiri ya kumsaidia mtu au kumpendelea mtu, Mungu yupo kwajiri ya kuwatendea haki binadam wote duniani. So ukitaka jambo lolote inatakiwa ulipambanie mwenyewe then ukistahiri ndio unapewa, alafu Shetani sio mtu mbaya kama tunavyoaminishwa kwenye dini, Shetani na Mungu uwa wanapiga story na nimarafiki wazuri tu.

  • @phinaphina3201
    @phinaphina3201 Před 4 měsíci +4

    Sons a genius

  • @user-ju8ud8tx1d
    @user-ju8ud8tx1d Před 8 měsíci +3

    Nime like kabla sijaskiza maana najua hatia ni noma kila siku

  • @victormkello9575
    @victormkello9575 Před 8 měsíci +1

    Mwanzo nilidhani unazungumza na Mungu ila mwishoni nimegundua ni dear father, nafikiri umemkumbusha kila dingi wajibu wake kusimama kama Baba. Akili za ndani sana hizi, kipaji sana D.Vina

  • @vascobruno3936
    @vascobruno3936 Před 8 měsíci +4

    Kaka ulimaliza KANISA
    Hatia V1 umegusa muhusika
    Salute sana

  • @simoncmatanda5135
    @simoncmatanda5135 Před 8 měsíci +2

    Fundi kama fundi hatia namba 5,, n shidaaaa,, hii ni hatia seriz

  • @richardmloha1762
    @richardmloha1762 Před 8 měsíci +2

    Hikii kichwaaa🔥🔥🔥🔥

  • @Sharifufaki
    @Sharifufaki Před 8 měsíci +3

    Nakubali sana dizasta vina sijwahi kupinga ngoma zako❤❤❤❤

  • @Njokaa
    @Njokaa Před 8 měsíci +3

    Yaani hii ngoma usiposikiliza zaiidi ya mara 2 sidhani kama utailewa haraka hajamuongelea Mungu sikilizeni vizuri tena .ukienda kichwa kichwa utatoka kapa au kuelewa tofauti

  • @raphaelmwangosi9295
    @raphaelmwangosi9295 Před 8 měsíci +1

    the verteller mwenyewe dvina never fail❤💪💪💪

  • @khalifasultan2677
    @khalifasultan2677 Před 8 měsíci +3

    NI NGUMU SANA KUWA MWEMA UKIWA NA NJAA🔥🔥✊🏾

  • @marokeyLFM
    @marokeyLFM Před 8 měsíci +3

    Nimechelewa ku coment wahuni wamewai hii 😂 kama una mkubali Dizasta weka moto 🔥

  • @taufiqkweka669
    @taufiqkweka669 Před 8 měsíci +2

    Uwanja ni wako mwenyewe

  • @ivansixbert3602
    @ivansixbert3602 Před 3 měsíci +3

    We love you our bro 🇹🇿🇹🇿🙌🙌

  • @ngotamohamedi1793
    @ngotamohamedi1793 Před 8 měsíci +3

    Akili kubwa

  • @jonasibraysoni1859
    @jonasibraysoni1859 Před 8 měsíci +6

    Uyu jamaa mjanja sana kama akili yako kichwa majia apo ajamzungumzia baba ake kazungumzia mungu😂😂😂😂

  • @FedrickDanielJob
    @FedrickDanielJob Před 8 měsíci +2

    Here we go kaka ❤❤❤❤