NAVYKENZO! kutoka Banda La Uani Hadi Kumiliki Ghorofa

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 8. 09. 2024
  • NAVY KENZO kutoka Babda La Uani Hadi Kumiliki Ghorofa
    KWA wafuatiliaji wa burudani ni wazi watakuwa wanalikumbuka Kundi la Pah One lililokuwa likiundwa na vichwa hatari kama vile Igwe, Ola, Aika Mariale pamoja na Nahreel.
    Ngoma ya Amatita ndiyo iliyowatoa na kubamba kila kona kutokana na staili yao ya uimbaji na kucheza, baadaye walikuja kutikisa tena na ngoma kadhaa kama vile I Wanna Get Paid pamoja na Ghetto.
    Siku zote kizuri huwa hakidumu! Kundi hili lilikuja kusambaa ambapo Igwe na Ola walibaki kama Pah One huku Aika na Nahreel wakitengeneza kundi lao jipya waliloliita Navy Kenzo.
    Japokuwa Pah One bado wanaendelea na harakati lakini Navy Kenzo limekuwa juu yao kwa muda mrefu wakitamba na vibao kibao kama vile Game, Bajaj, Feel Good na Chelewa. Kwa sasa kila kona gumzo ni ngoma yao mpya ya Katika waliomshirikisha Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ waliyoichia kwenye Mtandao wa CZcams yenye views zaidi ya milioni sita.
    Uzuri wa Navy Kenzo licha ya kuwa ni wapenzi wenye mtoto mmoja, Nahreel ni bonge moja la prodyuza Bongo ambaye anahusika kwenye nyimbo zao ukiwemo wa Katika ambazo huzifanyia katika studio yao ya The Industry. Wawili hawa wamepitia ‘msoto’ wa kuishi pamoja katika mazingira magumu ambapo walikuwa wakiishi kwenye nyumba waliyoigawa studio ndani yake iliopo Mikocheni jijini Dar.
    Kwa sasa wanamiliki mjengo wa ghorofa moja uliopo pembeni ya nyumba waliyokuwa wakiishi zamani wenye thamani ya shilingi milioni 400. Jiunge nao katika mahojiano maalumu kuhusu maisha yao na ya kimuziki;
    #NAVYKENZO
    Watch More Videos here: goo.gl/GvVdZw Watch More Videos here: goo.gl/ae33fL Website: www.globalpublishers.co.tz FaceBook: globalpublishers Instagram:
    globalpublishers Twitter: GlobalHabari Install Global App: ANDROID: goo.gl/QvT6RV Install Global App: iOS: goo.gl/2jDyho USIKUBALI KUPITWA NA HII, BONYEZA LINK www.youtube.co....

Komentáře • 8