PART 3: AGIZO LA MAGUFULI KWA MFANYABIASHARA MWENYE MGOGORO NA TRA LIMEFIKIA HAPA...

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 11. 04. 2020
  • PART 3: AGIZO LA MAGUFULI KWA MFANYABIASHARA MWENYE MGOGORO NA TRA LIMEFIKIA HAPA...
    GLOBAL TV imefunga safari mpaka eneo la biashara la Kariakoo na kufika dukani kwa mfanyabiashara maarufu eneo hilo anayetambulika zaidi kwa jina la RAMADHAN HAMISSI NTUNZWE, au Babu Rama, ambaye mwaka 2016 aliingia katika mgogoro na mamlaka ya mapato nchini (TRA) ambao ulishatolewa maamuzi na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kwa mara ya kwanza na baadae Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli nae akaingilia kati na kutoa maamuzi ya mwisho kuwa alipwe fidia, lakini agizo hilo Ramadhani amedai halijatelekezwa hadi leo....
    UNA HABARI? WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE ( +255 784 888982)
    ( +255 676 229628)
    Email: globaltvbest@gmail.com
    abbymrisho@gmail.com
    HABARI MPYA DAILY: bit.ly/habarimpya
    HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: bit.ly/mikasa_ya_kusisimua
    GLOBAL RADIO TV: bit.ly/255globalradio
    EXCLUSIVE INTERVIEW: bit.ly/exclusive_interviews
    Subscribe Global TV, Channel itakayokupa Habari na matukio ya kipekee nchini Tanzania Subscribe bit.ly/globaltvonline

Komentáře • 386

  • @faridmnyamike556
    @faridmnyamike556 Před 4 měsíci +8

    Ramadhani Hamisi Ntunzwe, Allahuma Ghifirllahu Warahmahu Waskanhu Filjanna, MwenyeziMungu atakulipa haki yako duniani na kesho akhera Mzee wangu.

  • @rashidabasi7940
    @rashidabasi7940 Před 4 lety +14

    MALIPO YA TRA NI SYSTEM.. WALITAKA WAKUMALIZE USINGEENDA NA JAMAA YAKO

  • @bishopmosesmagadula7572
    @bishopmosesmagadula7572 Před 4 lety +45

    HUYU anawakilisha WATU WENGI wanaoangaishwa na TRA NA kuteswa na maafisa wa TRA.

    • @maijajumbe8957
      @maijajumbe8957 Před 4 lety +1

      Mungu anawaona mjue mpeni haki yake

    • @abhambomihambo6754
      @abhambomihambo6754 Před 4 lety +1

      Hapa ndio namuelewa muheshimiwa rais km kuna kila sababu za kutumbua hata kila siku mpka watu wakae sawa na kuendana na kauli mbiu ya Hapa kazi tuu....yaani hata hawaogopi Executive order na hawasomi saa za nyakati km wakati wa ubabaishaji umekwisha na Magufuli kashatuamsha watanzania wengi,kwa hiyo tumbua huyo ndio walewale,miaka 20 na wako wa wengi wa aina hiyo fukuza wote hao lao moja na ndio chanzo cha sabotage mpka anatumbuliwa kamishna mkuu lazima ufumue mfumo mzima wa watendaji na kuanza upya

    • @aikamosha5644
      @aikamosha5644 Před 4 lety

      Hivi mzee baba uko wp? Naomba nitumbulie hawa watu,wanafanya mzaha kwa hii issue, fanya yako Uncle magu msaidie mnyonge alipwe haki zake,nakuaminia sn Uncle magu.

    • @clausemsemwa297
      @clausemsemwa297 Před 4 lety

      Wanaoangamizwa sema hivyo

    • @dowhatyourepassionateoftra1668
      @dowhatyourepassionateoftra1668 Před 4 lety

      Kuna muda kama 1995 wameshawahi kumtoa baba Yangu Milioni 2 kisa tu ni chuki za watu. Kuna muda Mtumishi amesoma anaumia kuona mfanyabiashara hata hajamaliza la saba anawazidi Hela. Mana wasomi wengi wanajiamini kuwa kusoma ndo watakuwa juu kimaisha Kumbe hawajui kuwa wanajiingiza katika kifungo cha maisha cha mshahara kinawadanganya

  • @sadamramadhan2754
    @sadamramadhan2754 Před 4 lety +8

    Isingekuwa TRA nadhan Watanzania kwa wakati huu tungekua tunaisha vzr kama Dubai, au libia ya Kipindi cha Gadaf.

  • @Ali-nl2du
    @Ali-nl2du Před 4 lety +14

    TRA wafukuzwe kazi wote, halafu iundwe upya na waipe a new name. Hili jina limeshachafuka mno.

  • @AliOmar-bx2oz
    @AliOmar-bx2oz Před 4 lety +17

    Hapo serekali ya magufuli inapofeli lakini vitu vingine poa. Pengine magufuli hajui Kama watu wanakomolewa na kuonewa na TRA.

  • @mkubhimkubhi
    @mkubhimkubhi Před 4 lety +6

    Hii nchi inaonekana ni ya watu wachache. Kwa kusema hivi kuna baadhi ya watu watasema ni kuwa huu ni uchonganishi na uvunjaji amani. Lakini si kweli na ni kawaida kwa baadhi ya watu hawa kusema hivi kwa kuwa hawajui vipi wakibiliane na ukweli. Na kuthibitisha hili kuwa hii nchi ni ya kundi fulani la watu wachache fuatilia sakata hili kwa kumhoji Kamishina je wale watu waliolianzisha sakata hili la kumata mali za mfanya biashara huyu walichukuliwa hatua gani. Na kwa nini hawajafikisha Mahakamani kujibu tuhuma za kuipatia serikali hasara na kutowajibika ipasavyo katika kazi zao. Nyie vyombo vya habari ulizeni maswali ya msingi na sio maswali ya mepesi na ya kipuuzi kama hilo swali ulilllo muuliza kwamba labda walimwona yeye ni mkali sana na ndio maana wakaogopa kuja kuzungumza naye. (Sorry, with that such question, you sound not smart guy)

  • @Mamatonny2065
    @Mamatonny2065 Před 4 lety +4

    Pole sana Baba.
    Mheshimiwa Rais uko wapi?
    Huyo baba anasumbuka kiasi hiki kwanini?...

  • @ashamwandu3781
    @ashamwandu3781 Před 4 lety +6

    Ewe mwenyezi mungu ,mwingi wa huruma.mja wako huyu msaiidie Allah mjuzi hujawahi shindwa.yaani huo niuonevu,Nahilo ni deni mwenyezi mungu awaazibu mnanyanyasa kwa jasho lake.mungu awallani

  • @nahyialetomia9284
    @nahyialetomia9284 Před 4 lety +24

    Huyu ni genius, apewe haki zake

  • @samsonkatigiri2344
    @samsonkatigiri2344 Před 4 lety +13

    Hii kesi ni ya mheshimiwa Rais,tunamuomba aende nae chemba aongee nae kama anavyoongea na wale jamaa wa kukamata ndege zetu,mwite mpatie Bilioni moja au hata milioni mia nane muombe yaishe maana ulishatoa amri kwa hiyo swala liko kwako mkuu.

  • @frankminga9307
    @frankminga9307 Před 4 lety +17

    MAGUFULI MAGUFULI WHERE ARE YOU,KUNA NINI HAPO NINA UHAKIKA HAYA YOTE UMEYASIKIA HEBU MALIZA HILO

    • @festokomba5404
      @festokomba5404 Před 4 lety

      Ndugu Mkuu kagawa madaraka mwacheni watajua tuu

  • @ashaally6993
    @ashaally6993 Před 4 lety +28

    Mashaallah nakupendea akili yako mungu aliokupa kaka...usichoke kupigania haki yako na mungu atakusimamia ....madhalimu hao wanakula moto huku duniani bado akhera wataenda kujibu!!!

  • @saudambinga3832
    @saudambinga3832 Před 4 lety +12

    Pole Sana, inabidi Rais wetu mtetezi wa wanyonge aliingilie tena Jambo hilo

  • @angeljasson4376
    @angeljasson4376 Před 4 lety +6

    Mungu akulinde wana nia mbaya juu yko kwa uwezo wa Mungu watashindwa

  • @davidmadudu8859
    @davidmadudu8859 Před 4 lety +6

    Sasa mfanyabiasha mkubwa kama huyu anafanyiwa hayo yani mpaka rais ashatoa tamko bado haitekelezwi mfano sisi wafanyabiasha wadogo zaid kweli tutatendewa haki dah kweli rais bado anakazi majipu mengi mpaka atachoka kuyaminya

  • @AliOmar-bx2oz
    @AliOmar-bx2oz Před 4 lety +7

    TRA hawataki mtu msafi kama huyu wanataka watu wanaotoa rushwa.

  • @mozasaid3869
    @mozasaid3869 Před 4 lety +3

    Pole sana bwana Ramadhani Ntunzwe ! Haki ya mtu haipotei! Ingawa itachelewa! Hatari sana!! Wanazidi kumletea zengwe kila siku!!

  • @thaubannaftal7265
    @thaubannaftal7265 Před 4 lety +3

    Hii nchi ya ajabu sana rais keshatoa maagizo hayajatekelezwa hata moja na rais yuko kimya.

  • @Jassmin-media-official
    @Jassmin-media-official Před 4 lety +4

    Rais waziri mkuu simumusahidie huyu Baba mbona wanampiga umasiki jamani

  • @greengenerationtv9012
    @greengenerationtv9012 Před 4 lety +4

    Yan TRA wanakela sanaaa tena sana kuna madudu Mengi sanaaa
    Sema baba semaaaa

  • @georgekimboka6218
    @georgekimboka6218 Před 4 lety +3

    Watu wa TRA kuweni makini na hili jambo viongozi wetu wa TRA kuweni makini sana jambo dogo sana hili mnachafua taswira Zuri ya TRA tufunike kombe haraka twende mbele

  • @natashafuture8263
    @natashafuture8263 Před 4 lety +7

    Mzee anaongea kwa uchungu adi roho inaniuma siwamlipe haki yake jamani mbona wanamsumbua sana

  • @BMx-zj3lz
    @BMx-zj3lz Před 4 lety +6

    Wapo watumishi wengine na wakuu wa idara wanatumia nyadhifa zao kunyanyasa wengine, hapo wanamtishia ningekuwa rais nafukuza wote.

  • @angelkileo7851
    @angelkileo7851 Před 4 lety +4

    Mzee kaza uzi mpaka kieleweke wamezoea unyanyasaji aoo

  • @mrdeniskomba2596
    @mrdeniskomba2596 Před 4 lety +1

    Usilolijua ni sawa na usiku wa giza.... Magifuli/Majaliwa nauhakika taarifa wanazo pengine wanalitungia sheria. Usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Tuendelee kuvuta subra. Inauma sana kwa ofisi ya mashetani TRA.

  • @mdroman6547
    @mdroman6547 Před 4 lety +4

    Rasi wetu mpendwa tunaomba msimamia huyu kaka apate haki yake

  • @mafinamaizez2514
    @mafinamaizez2514 Před 4 lety +4

    Mungu atasimama nawe kaka yangu haki ya mtu haipotei

  • @glorymushi7397
    @glorymushi7397 Před 4 lety +4

    Pole kaka Mungu hawezi kukuacha atakupambania tu

  • @bahatimnanka4848
    @bahatimnanka4848 Před 4 lety +2

    Pole sana mzee M/MUNGU abariki kazi ya mikono yako

    • @cyprianokassase8293
      @cyprianokassase8293 Před 4 lety

      Nashangaa sana hadi sasa imekuwa ni comedy. Angalia wasije wakakuua. Jipe moyo nadhani wakubwa wamesikia

  • @mastajabudekula4828
    @mastajabudekula4828 Před 4 lety +10

    Tunzwe baba uwe makini awa watu TRA wanamupango wakukuuwa

    • @devisgosbert1623
      @devisgosbert1623 Před 4 lety

      mtu wa kigoma sio rahisi kumuua mzee watu wazito hawa

  • @Juls7ur
    @Juls7ur Před 4 lety +4

    hii kesi sio kwamba viongozi hawa jui huyu jamaa ana lalamika kwenye vyombo vya habari, bali hawawezi au hawataki kumsaidia. pengine hakuna pesa.

  • @jamalsalim8693
    @jamalsalim8693 Před 4 lety +6

    Ww ni kamanda Ramadhani

  • @trybatinemahenge9358
    @trybatinemahenge9358 Před 4 lety +4

    Rais mwenye dhamana huon

  • @jumaigoti8638
    @jumaigoti8638 Před 4 lety +4

    Sio tra serekali wana jenda kwako kaka shituka.kama tra wanazalau amri ya raised kuna mini?

  • @tangaoldtv1067
    @tangaoldtv1067 Před 4 lety +1

    BABU SEA NA PAPIKOCHA nandio itakuwa kama vile kesi haina kichwa wala miguu gonga like kama unaamini kunafigisu kama mfano wa kesi ya babu seaaaaaa

  • @blesslory7653
    @blesslory7653 Před 4 lety +3

    Hili linamaanisha maagzo yte kwe ziara ya rais hayatekelezwi

  • @mandegoro9322
    @mandegoro9322 Před 4 lety +1

    Mm nakushauri kuwa badala ya waandishi was habari na mivutana na TRA wakati walikunyanyasa hali iliyopelekea mhe.. Rais akaagiza wakurejeshee mzigo wako pamoja na kukufidia, Mwandikie mhe. Rais Magufuli barua ya wazi kuwa bado suala lako bado lina mivutano na linapelekea kuathiri biashara yako na kutishia usalama wa maisha yako na unaomba aingilie kati.

  • @abburakkaan5694
    @abburakkaan5694 Před 4 lety +3

    Tatizo magufuli anawaogopa TRA sifahamu kwa nini!!

  • @alijuma1189
    @alijuma1189 Před 4 lety +2

    Sasa hao t r a wanaona taabu gani kumlipa pesa zake

  • @devothaignatus5911
    @devothaignatus5911 Před 4 lety +3

    pole sana, magufuri lais wawanyonge jmn muokoe uyo baba amepata tabu sana

  • @hakikahoman615
    @hakikahoman615 Před 4 lety +3

    baba waendee kigoma kwanza maana mbona wanatingisha kibirit .awa mbwa

  • @barakamaendeleo5202
    @barakamaendeleo5202 Před 4 lety +3

    Sijaelewa ni kwa nn wnamzungusha hivi huyu mfanyabiashara inaashiria hata alowaweka kwenye hizo nafasi hawamweshimu kabisa maana wamepuuza agizo la rais mkuu tumbua hawa hawafai kabisa

    • @ziadisalim495
      @ziadisalim495 Před 4 lety

      Pole sana mzee hakiyako utaipata endelea kupigania mungu yupamoja nawe

  • @msafiriandrea3523
    @msafiriandrea3523 Před 4 lety +3

    Onesha kuwa sina hatia ee Mungu utetee kisa changu dhidi ya watu wabaya uniokoe na watu waongo na waovo.

  • @doljaston7807
    @doljaston7807 Před 4 lety +2

    Unaweza kununua uchawi kwa sababu TRa

  • @farajibugi9924
    @farajibugi9924 Před 4 lety +4

    Mzee wangu Kama unahitaji haki yako nenda haraka kwa wazuri mkuu au rais ndio ukawaulize hao wakuu kuwa pesa yako utapata au vp lakn hao jamaa huwez pata haki yako watakuuwa mzee

  • @meryshekoloa961
    @meryshekoloa961 Před 4 měsíci

    Yaani kk yangu kila siku nakusihi watakuua selikali ya nchi hii ngumu Sana mimi nimeinua mikono na hata kula yangu anaijua mungu kwakua bado una mtaji achana nao

  • @ahmadkazema1055
    @ahmadkazema1055 Před 4 měsíci

    Pole sana mzee wangu,.kila kitu kina mwanzo na mwisho,haki ya mtu huwa haipotei..pole kwa kupotezewa mda wako,pamoja na adha zote zilizowapata wana familia yako..

  • @amanimyolo1478
    @amanimyolo1478 Před 4 měsíci

    Wote mlioshiriki kumuua ntunzwe Ramadhan mungu hatowaacha Salama

  • @magrethmbawata1269
    @magrethmbawata1269 Před rokem

    Mwambie mungu asimame juu ya hakiyako kama ni mkristo funga siku unazoweza kwamaombi utaona majibu bro.amen

  • @mastajabudekula4828
    @mastajabudekula4828 Před 4 lety +5

    Ili jambo lina onesha wazi kuwa kwamana TRA wote wanafahamu ili tatizo TRA wote niwafisadi

    • @ashamwandu3781
      @ashamwandu3781 Před 4 lety

      Wababaishaji wananataka wampe makashikashi akate tamaa nayeye anaakiri hawamuwezi.mambwa hayo watanzania wa 1990siyo wa Leo wanaakiri na wamesoma.

  • @krispinkomba4606
    @krispinkomba4606 Před 4 lety +3

    TRA acheni upumbavu!!!! Kuna wasomi mmepelekwa huko lkn mnatuharibia wafanyabiashara kwa tamaa ndogondogo za wafanyakazi wa TRA ,,, Sheria ziko wazi aliyeomba rushwa afukuzwe kazi mlipeni huyu pesa zake"**" yaan nngekuwa mm ndo Mzee Magu nawabomoa TRA tokea mkurugenz mkuu mpk wa kufagia hapo makao makuu** yaan mpka jengo mnalotumia

  • @muonambali
    @muonambali Před 4 lety +1

    Hii nchi ina uozo kila mahali. This is a BIG shame. Where is the rule of law!?. Pole sana mzee kwa haya madudu unayopitia.

  • @janethjackson1257
    @janethjackson1257 Před 4 lety +1

    Mh Rais tunaomba uje tena jamani bado haki aijapatikana kwa mtu huyu Tunaomba,sana,sana

  • @peterkailembo4101
    @peterkailembo4101 Před 4 lety +4

    Hii kesi ya huyu jamaa itaondoka na kundi la watu, Rais anawasikilizia wanalimalizaje hili swala wenyewe tuvute subira ya hii episode

  • @mwaminilikane2281
    @mwaminilikane2281 Před 4 lety +2

    Mungu yu upande wako amini nasi wote tunaofuatilia sakata. Inshaalah haki ya mtu haipotei bure.

  • @happynicholaus6474
    @happynicholaus6474 Před 4 lety +8

    RAIS magufuri yupo wapi

  • @hawangeu2465
    @hawangeu2465 Před 4 lety +2

    Ikawa asubuhi ikawa jioni siku ya tatu
    TRA whatch out, this is ridiculous

  • @evancemwaitubi6382
    @evancemwaitubi6382 Před 4 lety +3

    Ukitaka kuonja machungu ya nchi hii fanya km unataka kufanikiwa weee, na ukitaka kuonja matunda yake kuwa masikini mpaka unakufa.

  • @hamisyasinwapi9122
    @hamisyasinwapi9122 Před 4 lety +1

    Nchi za afrika na viongoz wao shenzi sana.ndio maana huwa tunauwana kwasababu ya visasi km hv.

  • @weremamwita9740
    @weremamwita9740 Před 4 lety +2

    Yaani TRA bado kuna uchafu mwingi mno, ilipaswa hata kamishina mkuu awajibike kuingilia hili. hivi hakuana viongozi huko? tokeni tuwatambue nia zenu!

  • @jestinabenedict4620
    @jestinabenedict4620 Před 4 lety +3

    MUNGU YUPO UMESHINDA BABA YANGU

  • @petersume2780
    @petersume2780 Před 4 lety +2

    Hii ni aibu sana kwa TRA

  • @jacobmigera2626
    @jacobmigera2626 Před 4 lety +4

    Dunia Majanga hayato kwisha; hivi tamko la Mh; Magufuli kuhusu huyu ndugu lili kuwa fake; mbona anaendelea kusumbuliwa; Ndugu Kasimu Majariwax2; Mnalijua swala hili ''Please!! Let' this issue come to an end; mpaka auwawe Na watu wasio julikana ndo mtashituka?? We are watching you gays; Haki itendeke

  • @beatricenicholausiwasa7601

    mie najiuliza rais ameshidwa hii kesi

  • @seifmohamedseif9467
    @seifmohamedseif9467 Před 4 lety +3

    Hapo ujue wana unda kesi ili deni life iwe ngoma droo usikie tuna kudai 🤣🤣 wana jua hazipo rekodi za miaka ya nyuma na huwez kua nazo we nenda dodoma kaombe kukutana na waziri mkuu mbona simple tu wakaa kuongea na viombo vya habari tu

  • @justamarydawson6908
    @justamarydawson6908 Před 4 lety +1

    Jamani rais wetu mbona humsaidi huyu mfanyabiashara wevwe ndiye pekee tumaumia tunaomba mumsaidie raisi wetu

  • @evansm8802
    @evansm8802 Před 4 lety +1

    Kwani wanapinga uamuzi wa raisi ,na kwanini raisi yupo kimya au waziri mkuu.

  • @cleofasladislaus2177
    @cleofasladislaus2177 Před 4 lety +2

    Huyu mzee htari sana akili yake inawaza mbali sanaaaaa👉👉👉👉👉👉

  • @erickmbegalo1152
    @erickmbegalo1152 Před 4 lety +15

    Hivi jamani hii hbr kweli rais bado hajaiona? Mbona mzee wawatu mnamsumbua hivo? Bora mwambie moja kwa moja Kama anapata au laa. Kweli kabisa tra mnatutisha mpaka hapo,,, huyo anapesa na anapata shida hivo je mwenzangu na mm tutakimbilia wapi?????????

    • @Aysha-ms3ln
      @Aysha-ms3ln Před 4 lety

      Yani mi nilivyoona part 3 nikadhani magu ndo anazungumza mwisho wa picha

    • @josephjohn2114
      @josephjohn2114 Před 4 lety

      Hii ishu imenifanya nimekosa imani imenitoka. Naamini hii ishu ilishafika juu. Nachosikitika ni kwa nn hakuna tamko la serikali kuwa ntuzwe madai ni ya kweli au si ya kweli ili achague aidha kwenda mahakamani au kukubali matokeo. Sasa kutokana na ukimya huu naamini hakuna mpango a kumlipa huyu bwana wanamzungusha tu. Ntuzwe nenda mahakamani TRA achana nao biashara zako hamishia hata nje maana TRA wako juu ya sheria kwako. Ndio maana pamoja na kuwaanika uovu wao lakini bado wanakutesa na kukufilis. Nakutakia ramadhan njema Mwombe sana MUNGU ikiisha tafuta manasheria peleka TRA mahakamani.

  • @husseinkarim6745
    @husseinkarim6745 Před 4 lety +2

    Nenda mahakamani ndio utapata haki labda. Inaelekea hakuna maelewano tena hata maneno ya Raisi hawakufatilia.

  • @liliansamson674
    @liliansamson674 Před 4 lety +12

    Mafisa oneni aibu, malizeni huu mgogoro wa huyu mzee.

    • @ericjonstz3120
      @ericjonstz3120 Před 4 lety +1

      babu nikushauri kitu,, pamoja na kila unapoitwa nenda na waandishi wa habari pia simu yako danlod app inayorecod mazungumzo yote mnayofanya, kua makini babu

  • @aminamaulidi1788
    @aminamaulidi1788 Před 4 lety +1

    Pole sn Baba yng haki yk utaipata kwa mung lakin malipo hp hp

  • @revmckenzie1503
    @revmckenzie1503 Před 4 lety +3

    Nchi ya Wagaratia wasio kuwa na Akili

  • @greengenerationtv9012
    @greengenerationtv9012 Před 4 lety +2

    TRA kwa huyu jamaa mmechemka atawatia aibu na kuwachafua jitahidini mmalizane nae......!!!

  • @sirajibakari8150
    @sirajibakari8150 Před 4 lety +4

    Magufuli aliwatuma hawa jamaa wa TRI wamfirisi huju mzee ila mungu yupo

  • @wlisonjoston7088
    @wlisonjoston7088 Před 4 lety +9

    Ikiwa mnamtenda huu mti mbichi itakuaje kwa mti mkavu? Ambao ni cc wakina hohe hahe. Tra mwogopeni MUNGU Mungu malipo ni hapa hapa duniani.

  • @lindamorio1111
    @lindamorio1111 Před 4 lety +1

    Tunakuombea Mungu Azidi kukulinda, maana hao wahuni wanaonekana kukufanyia mipango mibaya kila kukicha. Mungu Akuwekee jeshi kubwa la Malaika mahali popote. Hadi wakupe haki yako.
    - Endelea kusema na kutangaza huo uhalifu.
    - Andika notes, kila kitu.
    - Nenda na kinasa sauti ili ukitoka usisahau chochote na kila aliesema ajulikane wazi na njama zao.
    Muheshimiwa Rais, tafadhali msikilize huyu mnyonge.

  • @BonifaceSambo-ze6jh
    @BonifaceSambo-ze6jh Před rokem +1

    Aahaaaa digrii na ma PHD yamefumaniwa na STD VII au darasa saba.

  • @user-tz9ic7jn4j
    @user-tz9ic7jn4j Před 4 lety +2

    Pol sana Baba Mungu yupo

  • @uswegemwakajinga4218
    @uswegemwakajinga4218 Před 4 lety +3

    Mtafute mh Raisi kwa Mara nyingine umjurishe kwamba haujaripwa hela yako had Leo wakati yeye alikwisha kutoa sauti ulipwe hela pole sana mtanzania mwenzetu uliyemzalendo na kwa nchi yako na wenye roho mbaya wakiendelea kukuvunja moyo mungu akusimamie upate haki yako

  • @samirnaty8774
    @samirnaty8774 Před 4 lety +4

    Mungu muekee rehma huyu kaka katika utaftaj wa mali zake

  • @estamelejomah572
    @estamelejomah572 Před 4 lety +5

    Usikate tamaa mpaka kitaeleweka tu

  • @Ali-nl2du
    @Ali-nl2du Před 4 lety +6

    Mhe Rais anapotoa maelekezo awaagize wasaidizi wake wafanye follow up. Awape clear deadlines na a demand periodic updates. Kama si hivyo itakuwa kazi bure.

    • @seifmohamedseif9467
      @seifmohamedseif9467 Před 4 lety

      Huyu ana potea mwenyewe nilimsikia akiongea alijingiza mazungumzo ya pemben na watu wa TRA walipane kimya kimya ila pesa kidogo na akanza nao mjadala sasa mjadala wa nn nao rais kagiza ulipwe mara ana dai wanataka kuumua leo ni rahis kumwona hata waziri mkuu nae anafaham si nenda kamwone umweleze tu kua jamaa sasa wanataka hv na hv amebaki kuongea na viombo vya habari tu

  • @idrisaallysalum9447
    @idrisaallysalum9447 Před 4 lety +1

    Nafikiri SERIKALINI Kuna tatizo kubwa, inakuwaje habari mbaya dhidi ya TRA zinatajwa lakini Serikali IPO kimya tu?....TRA Kuna matatizo mengi makubwa kwanini Serikali kuu IPO kimya tu?

  • @queenhusna5322
    @queenhusna5322 Před 4 lety +1

    Ila kwa sasaivi litaisha tu in shaallah

  • @loner_wolf
    @loner_wolf Před 4 lety +1

    Hii issue ilifika kwa rais kupitia waziri mkuu ...... Je ramadhani umeshindwa hata kumuona waziri mkuu na kumwambia mlipofikia .... ?

  • @wahidashabaz5982
    @wahidashabaz5982 Před 4 lety +6

    Haki ya mtu haipotei asipokulipa dunia atailipa akhera fanya ibada.Allah atakusimamia

    • @sadaoman1667
      @sadaoman1667 Před 3 lety

      Pole babu Rama Mungu yupo pamoja na ww

  • @sebastianbesha44
    @sebastianbesha44 Před 4 lety +4

    Mahojiano yote haya mpaka sasa inafikia part 3 na tuhuma ni TRA kweli mkuu hajalipata? Na agizo katoa yeye? Hapa kuna siri nyuma ya pazia, mzee kua makini baba mtu!

    • @hatibuahmadi7237
      @hatibuahmadi7237 Před 4 lety

      Kweli kabisa hata mimi siamini kama aja ipata taarifa hi

  • @EddazariaMsulwa
    @EddazariaMsulwa Před 4 lety +1

    Mzee ana akili nyingi sana anajua anacho zungumza na kuhoji

  • @thaubannaftal7265
    @thaubannaftal7265 Před 4 lety +1

    Nashangazwa na mambo mawili,LA kwanza ina maana mheshimiwa rais hajaona hizi clip,LA pili kumbe hata maagizo yke yote hajatekelezwa,hili ni jambo la kushangaza hawa maafisa wa TRA hiki kiburi wanakitoa wapi.

  • @bakarymadua7198
    @bakarymadua7198 Před 4 lety +1

    Plz Tanzania a jamani Rais uko wap nchiii inaymbishwaaa na we unaona tunajengajeee hiii nchi jmn Tanzania ye2

  • @maxlattinokiki8105
    @maxlattinokiki8105 Před 4 lety +1

    Hivi Raisi anona hivi interview? Kama ameamuwa kumsaidia huyu jamaa awafukuze TRA wa ngazi za juu wote wamesha ambiwa wamlipe huyu jamaa wanacho ruka ruka ni nini?

  • @mathewleonard8973
    @mathewleonard8973 Před 4 lety +1

    Pole Sana mzee

  • @johnsonlweyemam7944
    @johnsonlweyemam7944 Před 4 měsíci +1

    HII NCHI NI NGUMU SANA ..KUMBE NDO MAANA JPM ALIKUWA ANAWATUMBUA HAPO HAPO WATENDAJ WAZEMBE

  • @juniorrevokatus3717
    @juniorrevokatus3717 Před 4 lety +1

    Pole sana Mungu ata kupambana nia,😫😫😫

  • @smarty1064
    @smarty1064 Před 4 lety +1

    TRA wamekanyaga kaa la moto kwa huyu jamaa, ni facts , facts, facts, facts kwenda mbele

  • @aceotz2579
    @aceotz2579 Před 4 lety +6

    AKILI NYINGI NICE❤❤❤

  • @idrisaallysalum9447
    @idrisaallysalum9447 Před 4 lety +3

    Global Publishers Hamjui taaluma yenu, inatakiwa "ku-balance" story kwa kwenda upande wa pili...

    • @husseinmbago399
      @husseinmbago399 Před 4 lety

      Wamesema wataenda na upande ule hawawezi kutoa zote hapo

    • @pilimwanza8117
      @pilimwanza8117 Před 4 lety

      mbona kuna medi waliwahoji watu wa TRA inabidi uitafute uangalie.

  • @robertempire9542
    @robertempire9542 Před 4 lety +3

    Pambana Kaka uko sahihi