REV. DR. ELIONA KIMARO: URADIDI-CONSISTENCY I

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 26. 10. 2023
  • IBADA YA MORNING GLORY - THE SCHOOL OF HEALING - 27 OCT 2023.
    KICHWA CHA SOMO : KUENDELEA TOKA NGUVU HATA NGUVU.
    '' FROM STRENGTH TO STRENGTH ''
    NENO KUU: Zaburi 84 : 7
    Huendelea toka nguvu hata nguvu, Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu.
    URADIDI - CONSISTENCY
    Kutoka 2 : 15 - 22
    1 Wafalme 18 : 41 - 45
    Luka 5 : 1 - 11
    Kutoka 2 : 15 - 22
    15 Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.
    16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao.
    17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao.
    18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?
    19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi.
    20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula.
    21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora.
    22 Huyo akamzalia mwana, akamwita jina lake Gershomu, maana alisema, Nimekuwa mgeni katika nchi ya ugeni.
    1 Wafalme 18 : 41 - 45
    41 Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele.
    42 Basi Ahabu akainuka ili ale na kunywa. Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini.
    43 Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu. Naye akanena, Enenda tena mara saba.
    44 Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie.
    45 Ikawa, muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanyesha mvua nyingi. Ahabu akapanda garini, akaenda zake Yezreeli.
    Luka 5 : 1 - 11
    1 Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,
    2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.
    3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.
    4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
    5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
    6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;
    7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama.
    8 Simoni Petro alipoona hayo, alianguka magotini pa Yesu, akisema, Ondoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mtu mwenye dhambi, Bwana.
    9 Maana alishikwa na ushangao, yeye na wote waliokuwa pamoja naye, kwa sababu ya wingi wa samaki walioupata;
    10 na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. Yesu akamwambia Simoni, Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu.
    11 Hata walipokwisha kuviegesha pwani vyombo vyao, wakaacha vyote wakamfuata.
    Mhubiri : Rev.Dr. Eliona Kimaro
    Kwa maoni na ushauri:
    Mch. kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053

Komentáře • 9