Wananchi wa Kyela watakiwa kulima kilimo cha kakao kibiashara

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 26. 08. 2024
  • Wananchi wa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya wametakiwa kufanya kilimo biashara katika zao la kakao ili kuinua uchumi wao kutokana na zao hilo kuzidi kupanda bei.
    Ushauri huo umetolewa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe.Exaud Kigahe(Mb) Desemba 18,2023 wakati wa ziara yake ya kuona maendeleo ya zao la biashara la kakao wilayani Kyela.
    Katika ziara hiyo Naibu Waziri huyo amewataka Wizara ya Kilimo kupitia maafisa ugani kutoa elimu kwa wakulima ili kuzalisha kibiashara zaidi kwani zao hilo limekuwa na faida kubwa katika kuinua uchumi wao na Taifa kwa Ujumla.
    Aidha Mhe Kigahe amezielekeza Taasisi za SIDO na TIRDO kufanya utafiti wa namna ya kuzalisha bidhaa ya ziada inayotokana na mbegu ya zao hiyo ikiwemo kuzalisha juisi na pombe ya kisasa.
    Vilevile Mhe.Kigahe amesema kuwa ziara hiyo ina lengo la kuhakikisha Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara inaendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji wa biashara katika kilimo hususani wa zao hilo pamoja na kufurahishwa na mfumo wa stakabadhi ghalani na kupanda kwa bei ya zao la Kakao kutoka Sh 9,800 mpaka Sh10,000.
    Naye Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Josephine Manase amewataka wananchi na wakulima wa zao hilo wilayani hapo kulilimda zao la kakao pamoja na kuacha tabia ya kuuza zao hilo kwa watu wakati badala yake wafike katika minada inayotangazwa ili kuuza zao hilo kwa bei elekezi inayotolewa.
    Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Stakabadhi za Ghala Ndg.Asangye Bangua amewataka wakulima kuhakikisha wanapeleka kakao kwenye maghala lakini pia kuhakikisha tunapeleka kakao yenye ubora kwenye ghala na kwa kufanya hivyo kutaongeza kujihakikishia soko la uhakika la kakao.

Komentáře •