IBADA YA ALHAMIS ( KUPAA) TR 09.05.2024 SOMO:- KATIKA MKONO WA KULIA WA MUNGU

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 8. 05. 2024
  • IBADA YA ALHAMIS ( KUPAA) TR 09.05.2024
    SOMO:- KATIKA MKONO WA KULIA WA MUNGU
    NENO:- 1 Petro 3:22
    [22]Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.
    Luka 24:44-53
    [44]Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.
    [45]Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
    [46]Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
    [47]na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
    [48]Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.
    [49]Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
    [50]Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki.
    [51]Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.
    [52]Wakamwabudu; kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu.
    [53]Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu.
    Mhubili
    Kuhani Harrison Humphrey
    Kuhani Milembe Bakalemwa
    Ibada imefanyika kusanyiko la Kayanga lililopo wilaya ya Karagwe mkoa wa Kagera
    ©09.05.2024

Komentáře •