IBADA YA ALHAMIS ( KUPAA) TR 09.05.2024 SOMO:- KATIKA MKONO WA KULIA WA MUNGU
Vložit
- čas přidán 8. 05. 2024
- IBADA YA ALHAMIS ( KUPAA) TR 09.05.2024
SOMO:- KATIKA MKONO WA KULIA WA MUNGU
NENO:- 1 Petro 3:22
[22]Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.
Luka 24:44-53
[44]Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.
[45]Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
[46]Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
[47]na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
[48]Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.
[49]Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
[50]Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki.
[51]Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.
[52]Wakamwabudu; kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu.
[53]Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu.
Mhubili
Kuhani Harrison Humphrey
Kuhani Milembe Bakalemwa
Ibada imefanyika kusanyiko la Kayanga lililopo wilaya ya Karagwe mkoa wa Kagera
©09.05.2024