MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"
Vložit
- čas přidán 12. 04. 2018
- MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"
NI wiki ya kitimtim! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutoa wito kwa wanawake waliotelekezewa watoto na wanaume kufika ofisini kwake, Ilala jijini Dar kwa ajili kupatiwa msaada wa kisheria.
Awali, zoezi hilo lililotarajiwa kudumu kwa takriban siku 5 mfululizo, lilianza kuchukua nafasi Jumatatu iliyopita ambapo mamia ya wanawake walijitokeza na kuifanya ofisi ya mkuu wa mkoa kufurika, hadi kufikia hatua ya kuzuia kwa muda safari za magari katika njia ambazo zinakutana katika ofisi hiyo.
Wanawake wasiopungua 480 walijitokeza ambapo kwa mujibu wa Makonda, 47 kati yao waliwataja waheshimiwa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku 14 wakiwa ni viongozi wa dini.
Akizungumza na wanahabari mara baada ya wanawake wengi kujitokeza na kusikilizwa na wanasheria mbalimbali pamoja na watu wa dawati la jinsia, Makonda alitoa wito kwa wanaume ambao wametajwa na wanawake wao waliowatelekeza, wajitokeze wenyewe ili kusikiliza kesi zao. Makonda alienda mbali zaidi kwa kuwataka wanaume ambao nao wametelekezewa watoto au wenye malalamiko mbalimbali dhidi ya wanawake, nao wafike ofisini kwake kwa ajili ya kusaidiwa.
WANAUME NAO WAJITOKEZA
Mara baada ya Makonda kutoa wito huo, Jumanne iliyopita wanaume walijitokeza katika ofisi yake na kutoa malalamiko mbalimbali.
Kuna ambao walidai kukimbiwa na wanawake wao kutokana na kuugua kwa muda mrefu, kuna wengine walilalamikia wake zao kugeuza nyumba kuwa danguro. Kama hiyo haitoshi, kuna mpiga picha maarufu wa Ilala jijini Dar, Vedasto Mdesa ambaye alisema amefika ofisini hapo ili kueleza jinsi alivyokimbiwa na mkewe.
“Mimi na mke wangu tulibahatika kuzaa watoto watatu, wawili wakiwa mapacha, mke wangu niliyezaa naye tulikutana hapa mjini akisoma Chuo Cha Kampala University na tulikuwa tunapendana lakini familia yake ndiyo haikukubali mimi kumuoa mwanamke huyo.
“Nimekuwa nikipata shida sana ya kukutana na mzazi mwenzangu kutokana na uchumi wangu kuwa mdogo kwani mimi ni mpigapicha tu eneo la Buguruni, nimekuwa nikipata vikwazo vingi kutokana na familia yangu kuwa ya kimaskini na mke wangu kutoka katika familia ya kitajiri, kiukweli mke wangu yeye anatoka familia ya kitajiri na ndugu zake wengine wanaishi Urusi na ndiyo hasa wanaosababisha mimi nisiishi na huyo mwanamke lakini bado nampenda na yeye ananipenda, cha msingi namuomba Makonda anisaidie niweze kurudishiwa familia yangu,” alisema paparazi huyo.
WATU WAKESHA
Kuonesha kwamba tatizo hilo ni kubwa, usiku wa kuamkia Jumatano, wapo akinamama ambao walidaiwa kukesha katika ofisi ya Makonda ili kuweza kuwahi foleni asubuhi na mapema.
lnstal GlobalPublishersApp Android: bit.ly/2AAQe1d iOS: apple.co/2Assf4M Subscribe / uwazi FACEBOOK: / globalpublis. .
TWITTER: / globalhabari Visit globalpublishers.co.tz/, Subscribe / uwazi1
kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya… / uwazi1 / uwazi1 / uwazi1 WEBSITE: globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: / globalpublis. . TWITTER: / globalhabari INSTAGRAM: / globalpubli .
Baba umewanyosha Wanaume wanaotelekeza watoto. Mwenyezi Mungu akubariki sana tena sana Makonda Makonda Baba Mwenyezi Mungu Akulipe
Barikiwa sana Makonda.
hongera sana mkuu wamkoa kwa jitihada zako, mh. makonda
Asante makonda piga kaz baba Mungu atakuwezesha
Mungu akubariki ufanikishe ndoto zako
Daaaaa.......wewe ni kiongozi wa namna ya pekee,piga kazi mkuu na Mungu akutetee akupe uzima tele na hekma na nguvu za kuendelea kuchapa kazi.
Asante sana mkuu mungu akubariki sana
Asante makonda
Mungu akubariki kwa hili.
Big up sana makonda.
Makonda Mungu akujarie mafunuo zaidi! Mpaka vidume tuwe makini kutekeleza majukumu yetu!
Yaani wewe unafanya vitu vimekuzidi umri Wako, mungu awe nawe milele nakupenda sana
makonda kweli were nice fundi....
Kaziii nzuriiiiiiii
yaaani Mungu akutunzeer
Yani nakupenda makonda mpaka naumwa mungu akubariki sana
Yes dude! Piga kazi bruh!
We Makonda fanya kazi tu kwani wanaume wamezidi kutelekeza watoto watakaokuwa wanalalamika hajafikwa
mungu akuongezee ujasili wazidi kuuliza unautoa hwezi kktotoresha wanawake Kama vifaranga alaf klea hataki
Hata nakuja nimetelekezwa Mkuu maana hata mama zetu wametufanya tuonekani mayatima
Uyu jamaa mungu amzidishie sana.
kwa kweli makonda chapa kazi maana kwenye jambo zuriii vipangimizi haziishi
Hata Yesu alitukanwa usiwaangalie hao wadhaifu.
😃😃😃😃😃 wambiee haoo Mungu akulinde kaka ata yesu alitukanwa sembuse ww
Yangu macho
Hongera sana kaka nipo oman ningeungana naww maana nimetelekezewa mtoto pia nimefurahi sana kwakulitambua Hilo jukumu Mungu ibariki Tanzania
سلمى سيف
Mungu akubariki Makonda na akuzidishie Afya njema Akulinde na kila baya (IN-SHAA-ALLAH )
سلمى سيف ي سلمي تقوآله
fanya kazi kaka usitazame sura za watu
سلمى سيفnambie dada uko oman sehem gan
Hapo sawa watajielewa
Augustine Mhangazo hivyohvyo mh pongezi kwako
Wewe ni jembe piga kazi usigeuke nyuma utakua jiwe songa mbele
Anaekubeza hana hakili hata kidogo. Mwenyezi Mungu akuzidishie. wewe ni Jembe Kabisa. Rais magufuli Hajakosea kukuchagua. Tena wewe Umeletwa Mwenyezi Mungu Aje kutetea wanyonge. Abalikiwe Rais magufuli kukuchagua uwe mkuu wa mkoa wetu. wewe nijembe tuu.
Wewe ni mti Wa matunda mengi na nimatamu mno , mawe lazima utapigwa , vumilia mungu yupamoja sanaudikate tamaa.
Ali M1966 àà8
Vikao Viki anza machangudoa nao huhamia Dodoma, nao niwabunge? Au ndowahudum wao?
Vumilia na yote wanayo kukashifu kiukweli haifai KWA binadam kwani wao walio zaa na wakawatupa mahodari Sana mungu anaweza kuwanyanya na wakawa hawana hao watoto washenzi Sana tumewachoka kabisa
We miss you! What did he do to be dumped like that.
Watanzania mimi ni mkenya lakini nawaomba baada ya rais Magufuli kumaliza muhula wake naomba uchaguzi ujao muidhinishe huyu makonda awe rais wa tanzania.
Hivi wale walikuwa wanampinga makonda itakuwa wanamichepuka sana....
wanaokumeza kwa jambo hili ni wale wazinzi
Makonda sio karma anabuni mambo haha, la hasha duniani kote Kuna sheria ya haki ya mtoto kulelewa na baba na mama awe hawara mchepuko au wa ndoa. Huko Ktk nchi zingine inaitwa " child support" tena kwa taarifa ni kwamba, kama baba unafanya kazi serikali inakata mkwanja huko huko , wewe unapewa taarifa tu. Good job Makonda , chapa kazi .
Watu wanakazana kuwa wanaume wanatelekeza watoto nao Dada zetu wamezidi kuvuvua
Makonda furahi tuu usijali tupo na wewe Kaka moendwa tunakupenda Sana na utalipwa na mungu unayo huzuni Ila unafuraha Sana moyoni mwako
MUNGU akuwezeshe makonda
Mr makonda endelea kushika msimamo huo kwa ustawi WA taifa letu akina mama wakiwa na furaha nchi yetu itakuwa na amani akina mama wakiwa na hasira hakuna amani ya kweli.
Kweli itaishi milele ukiamua kutenda haki tenda haki katika mambo yote what about rule of law
Wazinzi wanachukia makonda.
huyu jamaa kweli nikiongozi
Viongozi wanatakiwa kuwa kama makonda mbunifu sana, wabuni mbinu mbali mbali kutatua matatizo ya wananchi
Emanuel Mlowe Hakuna kiongozi hapo
Balkiwa baba umetenda jambo jema na mama zetu nao wapumue
wacha waongee huwezi kumzuia binadamu mwenye kinywa
Tuko pamoja MKUU hata Mimi nimetelekezwa na baba ila namuachia mungu
ni aibu kwa wabunge wa ccm kuungana na lowasa
Lakini uzae angalau kamoja kwani unatoa mapovu lakini unaongea kibata kama bata fulani usimtaje sna mungu kwani we mwenyewe u ndumilakuwili
Wabunge wanapoenda kwe bye vikao wengi WAP huchukua wanafunzi Na makahaba Kyle dodoma
fanya kazi kiongozi those are normal challenges
Young Donny Half-Life True
makonda shkamoo
nimekuelewa mzee baba... umetisha ndugu yangu
Wanajidai kuficha Moto wakati moshi unaonekana wapuuzi achana nao
Michepuko cy ishu
Toka inch iundwe hakuna mkuu was mkoa aliyefanya ivoo
Piga kaz kka
Kanuni na taratibu zifuatwe.
Wanao mbeza huyu makonda ni wajinga tuu huwezi mtukana kiongozi kama huyu anae tetea wanyonge wajinga tuu piga kazi baba
Shoga huyu anawatesa wanawake mbulula
Saddy Junior Unamjuaje kama c na ww shoga achakutukana mtu anaesimamia majukumu yake
Penda Sana makona we nikomesha wajinga
boya tu wewe makonda karekebishe kwanza familia yako
Mwazan Gomaa boya mwenywe ndo nyie mnao telekeza watoto bwege weeeee kubali tu yaisheeeee nini kupingaa ukwelii