MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 12. 04. 2018
  • MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"
    NI wiki ya kitimtim! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutoa wito kwa wanawake waliotelekezewa watoto na wanaume kufika ofisini kwake, Ilala jijini Dar kwa ajili kupatiwa msaada wa kisheria.
    Awali, zoezi hilo lililotarajiwa kudumu kwa takriban siku 5 mfululizo, lilianza kuchukua nafasi Jumatatu iliyopita ambapo mamia ya wanawake walijitokeza na kuifanya ofisi ya mkuu wa mkoa kufurika, hadi kufikia hatua ya kuzuia kwa muda safari za magari katika njia ambazo zinakutana katika ofisi hiyo.
    Wanawake wasiopungua 480 walijitokeza ambapo kwa mujibu wa Makonda, 47 kati yao waliwataja waheshimiwa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku 14 wakiwa ni viongozi wa dini.
    Akizungumza na wanahabari mara baada ya wanawake wengi kujitokeza na kusikilizwa na wanasheria mbalimbali pamoja na watu wa dawati la jinsia, Makonda alitoa wito kwa wanaume ambao wametajwa na wanawake wao waliowatelekeza, wajitokeze wenyewe ili kusikiliza kesi zao. Makonda alienda mbali zaidi kwa kuwataka wanaume ambao nao wametelekezewa watoto au wenye malalamiko mbalimbali dhidi ya wanawake, nao wafike ofisini kwake kwa ajili ya kusaidiwa.
    WANAUME NAO WAJITOKEZA
    Mara baada ya Makonda kutoa wito huo, Jumanne iliyopita wanaume walijitokeza katika ofisi yake na kutoa malalamiko mbalimbali.
    Kuna ambao walidai kukimbiwa na wanawake wao kutokana na kuugua kwa muda mrefu, kuna wengine walilalamikia wake zao kugeuza nyumba kuwa danguro. Kama hiyo haitoshi, kuna mpiga picha maarufu wa Ilala jijini Dar, Vedasto Mdesa ambaye alisema amefika ofisini hapo ili kueleza jinsi alivyokimbiwa na mkewe.
    “Mimi na mke wangu tulibahatika kuzaa watoto watatu, wawili wakiwa mapacha, mke wangu niliyezaa naye tulikutana hapa mjini akisoma Chuo Cha Kampala University na tulikuwa tunapendana lakini familia yake ndiyo haikukubali mimi kumuoa mwanamke huyo.
    “Nimekuwa nikipata shida sana ya kukutana na mzazi mwenzangu kutokana na uchumi wangu kuwa mdogo kwani mimi ni mpigapicha tu eneo la Buguruni, nimekuwa nikipata vikwazo vingi kutokana na familia yangu kuwa ya kimaskini na mke wangu kutoka katika familia ya kitajiri, kiukweli mke wangu yeye anatoka familia ya kitajiri na ndugu zake wengine wanaishi Urusi na ndiyo hasa wanaosababisha mimi nisiishi na huyo mwanamke lakini bado nampenda na yeye ananipenda, cha msingi namuomba Makonda anisaidie niweze kurudishiwa familia yangu,” alisema paparazi huyo.
    WATU WAKESHA
    Kuonesha kwamba tatizo hilo ni kubwa, usiku wa kuamkia Jumatano, wapo akinamama ambao walidaiwa kukesha katika ofisi ya Makonda ili kuweza kuwahi foleni asubuhi na mapema.
    lnstal GlobalPublishersApp Android: bit.ly/2AAQe1d iOS: apple.co/2Assf4M Subscribe / uwazi FACEBOOK: / globalpublis. .
    TWITTER: / globalhabari Visit globalpublishers.co.tz/, Subscribe / uwazi1
    kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya… / uwazi1 / uwazi1 / uwazi1 WEBSITE: globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: / globalpublis. . TWITTER: / globalhabari INSTAGRAM: / globalpubli .

Komentáře • 74

  • @hamidajuma7804
    @hamidajuma7804 Před 6 lety +2

    Baba umewanyosha Wanaume wanaotelekeza watoto. Mwenyezi Mungu akubariki sana tena sana Makonda Makonda Baba Mwenyezi Mungu Akulipe

  • @leilainnocent6532
    @leilainnocent6532 Před 6 lety +3

    Barikiwa sana Makonda.

  • @emanuelngusa8161
    @emanuelngusa8161 Před 6 lety +2

    hongera sana mkuu wamkoa kwa jitihada zako, mh. makonda

  • @dorahmathias5476
    @dorahmathias5476 Před 6 lety +3

    Asante makonda piga kaz baba Mungu atakuwezesha

  • @navoneiwamgonja9010
    @navoneiwamgonja9010 Před 6 lety +2

    Mungu akubariki ufanikishe ndoto zako

  • @joasalfred4503
    @joasalfred4503 Před 6 lety +5

    Daaaaa.......wewe ni kiongozi wa namna ya pekee,piga kazi mkuu na Mungu akutetee akupe uzima tele na hekma na nguvu za kuendelea kuchapa kazi.

  • @mamyabdalah885
    @mamyabdalah885 Před 6 lety +1

    Asante sana mkuu mungu akubariki sana

  • @henrykulwa6659
    @henrykulwa6659 Před 6 lety +2

    Asante makonda

  • @angelakundi1059
    @angelakundi1059 Před 6 lety

    Mungu akubariki kwa hili.

  • @victorsolomon2140
    @victorsolomon2140 Před 6 lety +2

    Big up sana makonda.

  • @dr.erickjmazyala8905
    @dr.erickjmazyala8905 Před 6 lety +2

    Makonda Mungu akujarie mafunuo zaidi! Mpaka vidume tuwe makini kutekeleza majukumu yetu!

  • @AliM-di8dz
    @AliM-di8dz Před 6 lety +2

    Yaani wewe unafanya vitu vimekuzidi umri Wako, mungu awe nawe milele nakupenda sana

  • @abuuhafsah9630
    @abuuhafsah9630 Před 6 lety +2

    makonda kweli were nice fundi....

  • @fortunatamfinanga287
    @fortunatamfinanga287 Před 6 lety +1

    Kaziii nzuriiiiiiii

  • @dinakidai4118
    @dinakidai4118 Před 6 lety +2

    yaaani Mungu akutunzeer

  • @mamyabdalah885
    @mamyabdalah885 Před 6 lety

    Yani nakupenda makonda mpaka naumwa mungu akubariki sana

  • @wilsonkaseha2034
    @wilsonkaseha2034 Před 6 lety

    Yes dude! Piga kazi bruh!

  • @blandinamwarabu5025
    @blandinamwarabu5025 Před 6 lety +4

    We Makonda fanya kazi tu kwani wanaume wamezidi kutelekeza watoto watakaokuwa wanalalamika hajafikwa

  • @marwaiboroshaisombe6304

    mungu akuongezee ujasili wazidi kuuliza unautoa hwezi kktotoresha wanawake Kama vifaranga alaf klea hataki

    • @danielbugwema6969
      @danielbugwema6969 Před 6 lety

      Hata nakuja nimetelekezwa Mkuu maana hata mama zetu wametufanya tuonekani mayatima

  • @stevenmsaaada.msaada.389

    Uyu jamaa mungu amzidishie sana.

  • @masungakasanda3575
    @masungakasanda3575 Před 6 lety

    kwa kweli makonda chapa kazi maana kwenye jambo zuriii vipangimizi haziishi

  • @leilainnocent6532
    @leilainnocent6532 Před 6 lety +2

    Hata Yesu alitukanwa usiwaangalie hao wadhaifu.

  • @zainabualtz1455
    @zainabualtz1455 Před 6 lety +2

    😃😃😃😃😃 wambiee haoo Mungu akulinde kaka ata yesu alitukanwa sembuse ww

  • @samusonibalazingiza3689

    Yangu macho

  • @user-oh8bn3vg2w
    @user-oh8bn3vg2w Před 6 lety +3

    Hongera sana kaka nipo oman ningeungana naww maana nimetelekezewa mtoto pia nimefurahi sana kwakulitambua Hilo jukumu Mungu ibariki Tanzania

  • @saidsaid9463
    @saidsaid9463 Před 6 lety +2

    Hapo sawa watajielewa

    • @saidsaid9463
      @saidsaid9463 Před 6 lety

      Augustine Mhangazo hivyohvyo mh pongezi kwako

    • @mayungakidoyayi9566
      @mayungakidoyayi9566 Před 6 lety

      Wewe ni jembe piga kazi usigeuke nyuma utakua jiwe songa mbele

  • @hamidajuma7804
    @hamidajuma7804 Před 6 lety +2

    Anaekubeza hana hakili hata kidogo. Mwenyezi Mungu akuzidishie. wewe ni Jembe Kabisa. Rais magufuli Hajakosea kukuchagua. Tena wewe Umeletwa Mwenyezi Mungu Aje kutetea wanyonge. Abalikiwe Rais magufuli kukuchagua uwe mkuu wa mkoa wetu. wewe nijembe tuu.

  • @AliM-di8dz
    @AliM-di8dz Před 6 lety +2

    Wewe ni mti Wa matunda mengi na nimatamu mno , mawe lazima utapigwa , vumilia mungu yupamoja sanaudikate tamaa.

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe6854 Před 6 lety +1

    Vikao Viki anza machangudoa nao huhamia Dodoma, nao niwabunge? Au ndowahudum wao?

  • @MarsUk-cg1gq
    @MarsUk-cg1gq Před 6 lety

    Vumilia na yote wanayo kukashifu kiukweli haifai KWA binadam kwani wao walio zaa na wakawatupa mahodari Sana mungu anaweza kuwanyanya na wakawa hawana hao watoto washenzi Sana tumewachoka kabisa

  • @AdamSaffi211
    @AdamSaffi211 Před rokem

    We miss you! What did he do to be dumped like that.

  • @ibrahimwerejuma4816
    @ibrahimwerejuma4816 Před 6 lety

    Watanzania mimi ni mkenya lakini nawaomba baada ya rais Magufuli kumaliza muhula wake naomba uchaguzi ujao muidhinishe huyu makonda awe rais wa tanzania.

  • @matobholwamanonu5919
    @matobholwamanonu5919 Před 6 lety +2

    Hivi wale walikuwa wanampinga makonda itakuwa wanamichepuka sana....

  • @nzumbimatondo4780
    @nzumbimatondo4780 Před 6 lety +2

    wanaokumeza kwa jambo hili ni wale wazinzi

  • @geoffrieymollel2178
    @geoffrieymollel2178 Před 6 lety

    Makonda sio karma anabuni mambo haha, la hasha duniani kote Kuna sheria ya haki ya mtoto kulelewa na baba na mama awe hawara mchepuko au wa ndoa. Huko Ktk nchi zingine inaitwa " child support" tena kwa taarifa ni kwamba, kama baba unafanya kazi serikali inakata mkwanja huko huko , wewe unapewa taarifa tu. Good job Makonda , chapa kazi .

  • @tedisangaa8886
    @tedisangaa8886 Před 6 lety

    Watu wanakazana kuwa wanaume wanatelekeza watoto nao Dada zetu wamezidi kuvuvua

  • @MarsUk-cg1gq
    @MarsUk-cg1gq Před 6 lety

    Makonda furahi tuu usijali tupo na wewe Kaka moendwa tunakupenda Sana na utalipwa na mungu unayo huzuni Ila unafuraha Sana moyoni mwako

  • @merymrema420
    @merymrema420 Před 6 lety

    MUNGU akuwezeshe makonda

  • @stevenjackson1582
    @stevenjackson1582 Před 6 lety

    Mr makonda endelea kushika msimamo huo kwa ustawi WA taifa letu akina mama wakiwa na furaha nchi yetu itakuwa na amani akina mama wakiwa na hasira hakuna amani ya kweli.

  • @wahazaben7964
    @wahazaben7964 Před 6 lety

    Kweli itaishi milele ukiamua kutenda haki tenda haki katika mambo yote what about rule of law

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe6854 Před 6 lety +3

    Wazinzi wanachukia makonda.

  • @kallahassan4896
    @kallahassan4896 Před 6 lety +2

    huyu jamaa kweli nikiongozi

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe6854 Před 6 lety +4

    Viongozi wanatakiwa kuwa kama makonda mbunifu sana, wabuni mbinu mbali mbali kutatua matatizo ya wananchi

  • @denismgashe5989
    @denismgashe5989 Před 6 lety

    Balkiwa baba umetenda jambo jema na mama zetu nao wapumue

  • @catherinekanyangali4940

    wacha waongee huwezi kumzuia binadamu mwenye kinywa

  • @zulfamnzava6735
    @zulfamnzava6735 Před 6 lety

    Tuko pamoja MKUU hata Mimi nimetelekezwa na baba ila namuachia mungu

  • @utukufueliya5279
    @utukufueliya5279 Před 6 lety

    ni aibu kwa wabunge wa ccm kuungana na lowasa

  • @hassanrwitita2503
    @hassanrwitita2503 Před 6 lety

    Lakini uzae angalau kamoja kwani unatoa mapovu lakini unaongea kibata kama bata fulani usimtaje sna mungu kwani we mwenyewe u ndumilakuwili

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe6854 Před 6 lety +1

    Wabunge wanapoenda kwe bye vikao wengi WAP huchukua wanafunzi Na makahaba Kyle dodoma

  • @youngdonnyhalf-life9175
    @youngdonnyhalf-life9175 Před 6 lety +1

    fanya kazi kiongozi those are normal challenges

    • @Manfilly
      @Manfilly Před 6 lety

      Young Donny Half-Life True

  • @abuuhafsah9630
    @abuuhafsah9630 Před 6 lety

    makonda shkamoo

    • @abuuhafsah9630
      @abuuhafsah9630 Před 6 lety

      nimekuelewa mzee baba... umetisha ndugu yangu

  • @MarsUk-cg1gq
    @MarsUk-cg1gq Před 6 lety

    Wanajidai kuficha Moto wakati moshi unaonekana wapuuzi achana nao

  • @emanuelmlowe6854
    @emanuelmlowe6854 Před 6 lety

    Michepuko cy ishu

  • @philipongenzatv
    @philipongenzatv Před 6 lety

    Toka inch iundwe hakuna mkuu was mkoa aliyefanya ivoo

  • @salmadashlaquimanelaquiman4427

    Piga kaz kka

  • @ceciliajimmy5652
    @ceciliajimmy5652 Před 6 lety

    Kanuni na taratibu zifuatwe.

  • @mamyabdalah885
    @mamyabdalah885 Před 6 lety +1

    Wanao mbeza huyu makonda ni wajinga tuu huwezi mtukana kiongozi kama huyu anae tetea wanyonge wajinga tuu piga kazi baba

  • @kuchiafricancinema
    @kuchiafricancinema Před 6 lety +2

    Shoga huyu anawatesa wanawake mbulula

    • @isackandrew8620
      @isackandrew8620 Před 6 lety

      Saddy Junior Unamjuaje kama c na ww shoga achakutukana mtu anaesimamia majukumu yake

  • @jeftajosiah40
    @jeftajosiah40 Před 6 lety

    Penda Sana makona we nikomesha wajinga

  • @laymapeace4538
    @laymapeace4538 Před 6 lety

    boya tu wewe makonda karekebishe kwanza familia yako

    • @jamyjandro8901
      @jamyjandro8901 Před 6 lety +1

      Mwazan Gomaa boya mwenywe ndo nyie mnao telekeza watoto bwege weeeee kubali tu yaisheeeee nini kupingaa ukwelii