Mume asimulia jinsi mchungaji alivyomuaga, kumlazimisha avae vazi lake la kichungaji

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 8. 09. 2024
  • Mungu ameficha siri kubwa katika kifo. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kimashuku, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Kantate Munis (42) kufariki dunia kwa ajali, saa chake baada ya kumtaka mumewe ambaye pia ni mchungaji, Israel Moshi kuvaa vazi lake la kichungaji kwenda kutoa huduma.
    Mchungaji Munisi pamoja na mzee wake wa Ushirika, Laban Kweka (50), wamefariki dunia jana Jumapili Agosti 4, 2024 baada ya gari walilokuwa wakisafiria wakitokea kwenye uimbaji Usharika wa Gezaulole wilayani Hai, kugongwa na basi la abiria, wakati akikata kona kuingia kwenye usharika huo ambako ndiko anakoishi.
    Akisimulilia namna alivyoagana na mkewe asubuhi, Mchungaji Moshi amesema wakati wanajiandaa kwenda kwenye huduma, mkewe alimweleza hajapendezwa na vazi la huduma alilokuwa amevaa (kanzu), hivyo akamtaka alivue kisha avae vazi lake la huduma.
    Mkuu wa Jimbo la Hai, Dayosisi ya Kaskazini Mchungaji, Biniel Mallyo amesema kanisa limepokea kwa masikitiko makubwa msiba wa mchungaji huyo pamoja na mzee wa kanisa wa usharika huo ambao walifariki dunia papohapo na wengine kujeruhiwa.

Komentáře • 158

  • @glorysungura3180
    @glorysungura3180 Před měsícem +15

    Pole baba MUNGU akupe nguvu, inauma na inasikitisha sana. Usilie, mtumaini MUNGU. Yupo YESU anaetupa faraja, faraja ya mwanadamu inaishia nje ya kaburi. Lakini faraja ya YESU iko milele. Shukuru MUNGU sana, mtumishi amefariki akiwa kwenye huduma. Pole sana. Mshukuru MUNGU kwa yote

  • @sirellyonlinetv8477
    @sirellyonlinetv8477 Před měsícem +11

    Baba Mchungaji Mungu akutie nguvu... Ni wakati mgumu sana... Lakini neema ya Mungu inakutosha. Tunakuombea baba Mungu mwenyewe awe faraja kwako....😭😭

  • @janekamugisha
    @janekamugisha Před měsícem +4

    Kaka yangu Mchg Israel Mungu akushike pole sana hatuna maneno ya kutosha kukufariji neema ya Kristo unayemtumikia akupe nguvu mno mno😢😢😢

  • @StephenKimondo-qw3et
    @StephenKimondo-qw3et Před měsícem +1

    Pole sana Mchg. Israel Moshi. Mungu akutie nguvu. Bwana Yesu akufute machozi yako, na Faraja ya Roho Mtakatifu ikae moyoni mwako.

  • @BM_Smart2-6
    @BM_Smart2-6 Před měsícem +2

    Pole sana baba naiona huzuni yako. Bwana akutie nguvu. Lakini nashauri waandishi wawahoji wafiwa baada ya mazishi. Kumuhoji mfiwa kabla ya mazishi inamuongezea uchungu sana.

  • @janethmmari6968
    @janethmmari6968 Před měsícem +2

    Baba Mchungaji sina lugha ya kusema ,ila namsihi Mungu akupe faraja kutoka kwake na nguvu ya kusitahimili kipindi hiki kigumu unachopitia pole sana.

  • @emmanueltillya2017
    @emmanueltillya2017 Před měsícem +2

    Pole sana Mchungaji Israel Moshi.Mungu awe faraja na kimbilio lako siku zote za maisha yako.

  • @mponjolimwatebela4555
    @mponjolimwatebela4555 Před 22 dny

    Mungu akuwezeshe akupe nguvu na akufaliji

  • @RehemaMsengi-rp5wg
    @RehemaMsengi-rp5wg Před měsícem +2

    Pole sana mtumishi wa Mungu,faraja ya Bwana Yesu iwe nawe ktk kipindi HIKI kigumu.

    • @naomipieter4627
      @naomipieter4627 Před měsícem +1

      Polesan mchungaji kupoteza mwenza ni zaidi ya maumivu inauma sana😢

  • @StephenShayo1
    @StephenShayo1 Před měsícem +2

    Pole sana baba mchungaji...poleni sana washarika! Mungu ni Mungu bado!

  • @nassorowaziri3076
    @nassorowaziri3076 Před měsícem +2

    Pole Sana mkuu na Mungu awabariki Sana IPO siku mutakutana pamoja tena

  • @NeemaNabintu
    @NeemaNabintu Před měsícem +1

    Pole sana baba,MUNGU wa mbinguni akufariji

  • @esturidaruvanda758
    @esturidaruvanda758 Před měsícem +1

    Pole sana mchungaji mungu akufunge mkanda akupe faraja

  • @dorothyndege4555
    @dorothyndege4555 Před 29 dny

    Pole sana Mchungaji. Mungu akupe faraja ya pekee iliyo kuu sana, ambayo sisi wanadamu hatuwezi kuitoa. Tunakuombea🙏

  • @AnithaBiseko
    @AnithaBiseko Před měsícem

    Aisee pole sana Mchungaji. Mungu awape nguvu na kuwa mfariji Mkuu kwa wote walioguswa na misiba hii. Mungu awapumzishe kwa amani

  • @AziziMapunda-vt4nv
    @AziziMapunda-vt4nv Před 28 dny +1

    Imeniuma sana muchungaji ukilia nasisi tunalia😭😭😭😭

  • @neemasiwakwi6528
    @neemasiwakwi6528 Před 21 dnem

    Pole sana baba , Mungu akutie nguvu sana. Mungu awahudumie watoto pia.

  • @LyatuuJudith
    @LyatuuJudith Před 24 dny

    Mungu Akutie nguvu

  • @PhinaEdmund
    @PhinaEdmund Před 25 dny

    Mungu akutie nguvu mtu wa Mungu.. Yesu akupe faraja ya kweli akuvushe

  • @fadhilisecha4268
    @fadhilisecha4268 Před měsícem +1

    POLENI sana wapendwa. Mungu azidi kuwapa faraja KATIKA Magumu haya. Pumzika kwa Amani Mchungaji Kantate. Ni msiba mzito sana kwa kweli.

  • @hawaelymaricca7602
    @hawaelymaricca7602 Před měsícem +2

    Pole sana,.Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu

  • @PhinaEdmund
    @PhinaEdmund Před 25 dny

    Baba mch pole sana kwa msiba mzito Yesu hatakuacha.. Na hatakupungukia

  • @tronline6959
    @tronline6959 Před měsícem +1

    Pole sana baba Mchungaji, Mungu wetu akutie nguvu.

  • @marymushi7923
    @marymushi7923 Před měsícem

    Mungu azidi kukupa faraja baba mchungaji, Mungu awatunze watoto pia! Tunamuombea mama apumzike kwa amani.

  • @dunstankihaa2383
    @dunstankihaa2383 Před 25 dny

    Daaaah!!! Inauma sn, pole sn baba mchungaji Mungu wa mbinguni hatokuacha kamwe... ZABURI 125:1 wamtumainio bwana ni kama mlima sayuni, ambao hautatikisika wakaa milele.

  • @joaskiliba5996
    @joaskiliba5996 Před měsícem

    Daah inaumiza sana Pole mchungaji, kifo hakizoeleki kwakweli imenigusa sana.

  • @jamess.gazigile5916
    @jamess.gazigile5916 Před měsícem

    Pole sana Baba Mchungaji, Mungu awafanyie wewe na watoto moyo mkuu wa kuhimili mapenzi yake maana yeye ndiye hutoa na Kutwaa, Jina lake lihimidiwe, ni jambo gumu sana

  • @robertjuma992
    @robertjuma992 Před měsícem

    Pole Sana baba, Mungu awe faraja kwako na wote waliofikwa na msiba huu.

  • @MafieOnlineTv
    @MafieOnlineTv Před 22 dny

    Daaah mch. Pole sana hakika ni ngumu kuipokea hali hii Mungu akutie tu nguvu😢😢😢😢

  • @margarethpolepole7438
    @margarethpolepole7438 Před 27 dny

    Pole sanaaaa

  • @ziadayasin711
    @ziadayasin711 Před 26 dny

    Innalillah waina lillah rajuuni

  • @happynkya9770
    @happynkya9770 Před měsícem

    Hiii ajali kwa laiyoishuhudia ni zaidi ya maumivu, mungu ailaze mahali pema peponi amina

  • @user-oo1vz3zi1t
    @user-oo1vz3zi1t Před měsícem +1

    Pole Mzazi Allah akusmamie

  • @neemakibona2054
    @neemakibona2054 Před měsícem

    Pole Sana mtumishi. Pole watoto. Mungu awafunge mkanda WA faraja😭😭😭

  • @molenicharles9107
    @molenicharles9107 Před měsícem +1

    M!...kama I Mungu...Mungu...Mungu....Tunakupenda!

  • @jescarwegoshola1754
    @jescarwegoshola1754 Před 29 dny

    Pole Mtumishi wa Mungu,pole sana😭😭😭😭, Mungu awape faraja 🙏🏽

  • @bernadetaemmanuel1824
    @bernadetaemmanuel1824 Před měsícem

    Pole sana Mchungaji Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki

  • @jescamoshi3821
    @jescamoshi3821 Před 29 dny

    😭😭😭😭Daah pole sana Mchungaji. Mungu wa amani akupe nguvu 😢

  • @victoryurima8043
    @victoryurima8043 Před měsícem

    Pole sana Baba Mchungaji Mungu awatie nguvu na kuwa faraja kwenu🙏🏻

  • @yohanatlatlaa4205
    @yohanatlatlaa4205 Před měsícem

    Mungu akupe nguvu kwa wakati huu mgumu kwako mungu amempenda zaidi pole sana sana

  • @connectiondesigner4989

    Pole sana mchungaji moshi,huduma yako ya utumishi ilitukuka sana K.K.K.T sumbawanga mjini 2013,apumzike kwa amani mama mchungaji.

  • @stanleyshoo9602
    @stanleyshoo9602 Před 27 dny

    Poleni sana mungu awape faraja watu wa mungu!

  • @cosmaskapwepwe7203
    @cosmaskapwepwe7203 Před měsícem

    Pole sana mtumishi, mungu akutangulie katika kipindi hiki kigumu,

  • @hellenmwayole8715
    @hellenmwayole8715 Před měsícem

    Amini kuwa upo mlango wa kulishinda Hilo jaribu, Mungu akutie nguvu mtumishi wa Mungu

  • @SINADATITO
    @SINADATITO Před 26 dny

    Pole mchungaji Mungu akupe nguvu

  • @vaikaayagadiel520
    @vaikaayagadiel520 Před měsícem

    Nimekumbuka kifo cha Mch wetu Tumain, poleni sana wanausharika najua mnapopitia maana na sisi tuliumia sana. All in all Mungu atabaki kuwa Mungu tu

  • @WilondjaWitambi
    @WilondjaWitambi Před měsícem

    pole sana mchungaji mungu akutiye nguvu

  • @user-np8ts3dq2y
    @user-np8ts3dq2y Před 26 dny

    Shabiby amekuwa akisababisha sanaaa ajali haswa kila mwaka mwezi wa August.

  • @tupokengwala2027
    @tupokengwala2027 Před měsícem +1

    Poleni sana Mungu awape faraja

  • @ElizaLucas-to1eo
    @ElizaLucas-to1eo Před měsícem

    Pole sana mtumishi wa Mungu. Mungu atakuwa faraja kwako

  • @mwarikimwariki2653
    @mwarikimwariki2653 Před 27 dny

    Poleni sana

  • @ManenoSimkoko-df9yj
    @ManenoSimkoko-df9yj Před 26 dny

    Pole sana mchungaji mungu akutie nguvu

  • @joycemaleo8375
    @joycemaleo8375 Před měsícem

    Pole sana mtumishi wa Mungu ni vigumu sana kupokea

  • @giftnkya
    @giftnkya Před měsícem

    Pole sana mchungaj Mungu awe faraway kuu kwako pamoja na watoto

  • @kingsonkambey1436
    @kingsonkambey1436 Před měsícem

    Mungu anatosha kukufariji mchungaji Pole sana

  • @SaraRaphael-do8zp
    @SaraRaphael-do8zp Před 28 dny

    Pole sana baba mungu akutie nguvu

  • @winermunisi
    @winermunisi Před měsícem

    Pole sana Shemeji yangu. Mungu akupe nguv kipind hichi kigumu

  • @DEBORAHMASANJA-yz3go
    @DEBORAHMASANJA-yz3go Před 29 dny

    Pole sana Mungu baba akutie nguvu sana

  • @SusanNeymar
    @SusanNeymar Před 27 dny

    Pole sana mungu anajuwa sababu

  • @chikujuma18
    @chikujuma18 Před měsícem

    😢😢😢😢 Pole baba pamoja na family yako mwenyezi mungu akutie nguvu

  • @Globalpeace123
    @Globalpeace123 Před měsícem

    Poleni sana familia ndugu na jamaa wote
    Mungu awape faraja

  • @evansasu9717
    @evansasu9717 Před měsícem

    Pole sana,Mungu akutie nguvu

  • @kayulaedwin2587
    @kayulaedwin2587 Před měsícem

    Pole sana baba mchungaji M/MUNGU akutie nguvu

  • @estherboneka1341
    @estherboneka1341 Před 29 dny

    So sad Mungu akutie nguvu

  • @oscanyakunga
    @oscanyakunga Před 26 dny

    Pole sana mtu wa Mungu nawatoto pia

  • @user-ex4hi7fj5c
    @user-ex4hi7fj5c Před měsícem

    Poleni sanaaa jamani mchungaji Ezra Mungu WA faraja awafariji jamani si jambo rahisi ila Mungu wafara awafariji wote ndugu jamaa na marafiki

  • @vaikaayagadiel520
    @vaikaayagadiel520 Před měsícem

    Pole sana Mchungaji, jamani juzi tumepoteza Mchungaji wa Usharika wetu jamani poleni sana Kanisa, Mungu atuimarishe

  • @KapenkwekasaliKasali
    @KapenkwekasaliKasali Před měsícem

    Baba pole naijua hiyo kufiwa na mke usiombe ikutokee sikia kwa mbaliii. Mungu akutie nguvu.

  • @molenicharles9107
    @molenicharles9107 Před měsícem

    M!...Jamani Mungu...Mungu...Eee Munguuu!!...Tunakupenda kwa Yotee!

  • @tumvisiagekonga2142
    @tumvisiagekonga2142 Před měsícem +1

    Mungu akupe faraja

  • @GodluckStahimili
    @GodluckStahimili Před měsícem

    Mungu amuangazie mwanga wamilele mchungaji wangu wako roho

  • @SusanNeymar
    @SusanNeymar Před 27 dny

    Usijali mungu atakubanguza machozi❤

  • @beatriceyustomwakabanje5789

    Pole sana baba mchungaj isee inaumiza Sanaa 😭😭😭

  • @zebedayokatamaduni9676
    @zebedayokatamaduni9676 Před měsícem

    Pole sana kiongozi
    Mungu ni mwema

  • @verynicemonyo8671
    @verynicemonyo8671 Před měsícem

    Pole sana baba mchungaji Mungu ndio mfariji wako

  • @AnnoyedFlowerPot-mr2ps
    @AnnoyedFlowerPot-mr2ps Před měsícem

    Pole mungu akupe wepesi

  • @edwinalexander1170
    @edwinalexander1170 Před měsícem

    Pole sana Mungu akufariji sana.

  • @elibarikmafie7490
    @elibarikmafie7490 Před měsícem

    pole sana baba Mungu akutie nguvu

  • @brantywilson1347
    @brantywilson1347 Před měsícem +3

    Ajali zingine hata hazieleweki...makanisa yote nayajua, kutoka gezaulole kuja kimashuku hakuna mahali dereva anavuka barabara...makanisa yote yako kushoto....kwa mazingira hayo itoshe kusema Mungu amempenda zaidi...pumzika amani mtumishi wa Mungu.

    • @salomewandya7257
      @salomewandya7257 Před měsícem

      😭😭😭😭😭😭

    • @user-cb3vw5fp8y
      @user-cb3vw5fp8y Před 26 dny

      Una uhakika??? Ukitokea boma unatembea upande upi??? Na kanisa la kimashuku liko upande upi??

  • @Stellastella-yi5vu
    @Stellastella-yi5vu Před 26 dny

    Poleni

  • @user-iu6ik4xt5f
    @user-iu6ik4xt5f Před měsícem

    Pole mno mchungaji Mungu akufariji pekeyake

  • @shizamakweta2290
    @shizamakweta2290 Před měsícem

    Pole sana baba mchungaji na familia yote kwa ujimla

  • @florahemmanuel8323
    @florahemmanuel8323 Před měsícem

    Mtetezi wako yu hai
    Hata kuacha Peke yako mtu wa Mungu

  • @user-wy3uc2cd8x
    @user-wy3uc2cd8x Před měsícem

    Mungu akusaidie Baba

  • @GodMigodela
    @GodMigodela Před měsícem

    Pole sana baba Mungu akujalie

  • @user-hz4by6ff5i
    @user-hz4by6ff5i Před měsícem

    Pole sana sana baba Mchungaji

  • @AishamejaAisha
    @AishamejaAisha Před měsícem +1

    Poleni sn

  • @mwalukojohnkongola5471
    @mwalukojohnkongola5471 Před měsícem

    Pole sana mtumishi wa Bwana

  • @mrsdeborahurio
    @mrsdeborahurio Před měsícem

    Poleni Sana ,Mungu awatie nguvu. Ufunuo 21:4!

  • @frenziangella6676
    @frenziangella6676 Před měsícem

    Baba inaumiza Sana lakini naamini Mungu mwaminifu Sana utakaa Sana

  • @user-hn8vd1hr6c
    @user-hn8vd1hr6c Před měsícem

    Pole sana kiongozi!

  • @upendokiwanga9538
    @upendokiwanga9538 Před měsícem

    Pole sana jamani Mungu akufariji mchungaji

  • @robertgeofrey4118
    @robertgeofrey4118 Před měsícem

    Pole Sana Baba Yangu Mchungaji Israel Moshi

  • @tukuswigaikasu5227
    @tukuswigaikasu5227 Před měsícem

    pole sana Mungu awatie nguvu

  • @florarwegerera8025
    @florarwegerera8025 Před měsícem

    😭😭😭 pole sana baba Mungu akutie nguvu

  • @user-zv6mk1jv6s
    @user-zv6mk1jv6s Před měsícem

    Pole sana baba

  • @RobertLuvanda
    @RobertLuvanda Před měsícem

    Sina neno njema lakusema kwako Mtumishi wangu kwani hata Pole Naona kama haitoshi pia Naona kama tarudisha maumivu au machungu pia ukae katika PENDO lake YESU yeye ndiye mfariji wako pekee ndiye atakae ganga moyo wako nakulejesha amani pamoja na familia yako

  • @neemamasimba2981
    @neemamasimba2981 Před měsícem

    Huyu mchungaji namfahamu , poleni sana familia na kanisa kwa ujumla

  • @TabithaObellykasangila

    Poleni sana wapendwa

  • @rehemamwakateba6687
    @rehemamwakateba6687 Před 29 dny

    😢😢😢