SOMO LA NDOTO: TAFSIRI YA KUONA UNAFANYA MTIHANI ( johanitha Jeremiah-founder visionary youth org)

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 12. 09. 2023
  • Visionary youth organization Monthly semina
    Lengo la mtihani huwa ni kupima uwelewa WA mtu
    ✓Kumvusha kumtoa hatua Moja kumpeleka hatua nyingine
    ✓Kumtoa hatua ya chini kumpeleka hatua ya juu
    Na aina za mitihani unazofanya huwa zimegawanyika Kwa makundi mawili
    a)kundi la kwanza ni kundi ambalo Ni mitihani inayopima welewa ili ikuvushe hatua Moja kwenda nyingine
    Mfano mtihani WA darasa la Saba unamvuaha mwanafunzi kumpeleka kidato Cha kwanza
    b) Mitihani mingine ni ili kupima maarifa ,katika usaili ili uweze kupata nafasi Fulani/kazi Fulani...
    Ndio maana mtu anaweza kuwa amesona vizuri na ana VYETI lakini asiwe na maarifa ,Wala nguvu ya kutosha kuhusu hiyo kazi anayoomba .....ukifika muda huo WA kumpima ikaonekana Hana maarifa ya kutosha mbali na kuwa na VYETI huyu mtu hawezi kuipata ile nafasi aliyoomba ,itabidi arudi darasani ajifunze zaidi au akajifunze Kwa wengine /njia nyingine ili aongeze ujuzi
    Daniel 1:3-
    ¯¯¯¯¯
    ³ Mfalme akamwambia Ashpenazi, mkuu wa matowashi wake, awalete baadhi ya wana wa Israeli, wa uzao wa kifalme, na wa uzao wa kiungwana;
    ⁴ vijana wasio na mawaa, wazuri wa uso, wajuzi wa hekima, werevu kwa sababu ya maarifa yao, wenye kufahamu elimu, watakaoweza kusimama katika jumba la mfalme; tena alimwambia awafundishe
    TAFSIRI YA NDOTO ZA MTIHANI
    3)Ukiota hukai darasani wakati wengine wako darasani; au hukai kwenye mtihani wakati wengine wanafanya mitihani - ina maana huna utulivu unaotakiwa uwe nao ili uweze kujiandaa vyema kwa hatua iliyo mbele yako
    2)Ukiota unafanya mtihani - ujue: au unapita mahali kimaisha ambapo unapimwa kiwango chako ulichofikia kimaandalizi; au mbele yako kuna kuja kipimo kwa ajili ya kujua ikiwa umefikia kiwango kinachotakiwa kwa wewe kuingizwa hatua nyingine ya maisha
    1) Ukiota unaota unasoma, na ukaona na somo unalosoma, au ukaota unafanya mtihani na ukaona somo la mtihani huo - ina maana unaonyeshwa aina ya, au eneo la - maandalizi unalotakiwa kulifuatilia kimaandalizi
    UNAPOOTA NDOTO YA MTIHANI ZINGATIA MAMBO HAYA ILI UWEZE KUTAFSIRI HIYO NDOTO.
    1)Ulikuwa unafanya mtihani WA ninini,
    Sasa hapa unaweza kutambua hili ijapo sio mara zote kuwa mtihani utakaokumbuka kuwa ndio huo kabisa Kumbuka hata kwenye maisha Kuna mitihani pia....Wakati mwingine unajulishwa juu ya jambo ambalo litakuja kama jaribu kukupima nguvu yako
    2)Ulikuwa na Hali Gani Wakati WA mtihani ,Je ulikuwa unauelewa au ulikuwa haielewi mambo.
    -Hali unayokuwa unaona kwenye ndoto ndiyo Hali ya mtu wako WA ndani
    Ukiona ulikuwa mwenye kujiamini,umejiandaa ,huogopi basi jua ndani Yako una nguvu kuelekea mtihani huo na hata kama ni jaribu Bado utashinda
    Lakini ukijiona kwenye mtihani ni mwenye mashaka ,mara unasahau daftari,mara umechelewa kwenye mtihani ujue wewe hauna MAANDALIZI ya kutosha katika jambo unaloliendea
    3)Ulikuwa wapi Wakati unafanya mtihani,
    -Mazingira unayokuwepo yatakusaidia kujua kuwa aina Yako ya mtihani ni ipi ??? Mfano unaona upo kanisani unaletwa mtihani...? Au upo nyumbani kwenu ulikozaliwa unaletwa mtihani..hii inaonyesha kuwa wewe mtihani unayotakiwa kufanya umeahikamana na masuala ya utumishi,au ya kifamilia pengine wewe ndiwe lango la familia na Kuna mambo unatakiwa kufanya na haujafanya Bado.nk
    4)Mwisho wake ilikuwaje matokeo yake yalikuwaje ??
    -Ukiona kuwa ulikuwa unafanya mtihani na mwisho wake umeweza ,umefauru,umeujibunvizuri bila shida ,au ulkuwa na shida lakini mwisho ukaujibu vizuri uwe na uhakika kwamba eneo ambalo unapimwa kiwango basi kiwango chako kinajitosheleza umefauru,kama ni utumishi ,wito ,nk basi ni ishara nzuri
    -Ukiona mwisho umefeli,umepata vikwazo ,daftari mara limepotea ,mara unaingia kwenye mtihani unasahau...Basi ni dhahiri Mungu anakweleza katika jambo Hilo unalotakiwa kuliendea Bado hauna unuzi WA kutosha Bado haujasimama imara,Bado unahitaji maarifa zaidi ,Bado Kuna upinzani unatakiwa ushughulike nao ili uweze kufaulu.
    MAANA NYINGINE
    ✓UKIOTA UNAFELI MTIHANI NA MAJIBU yake ulikuwa unayajua ila umechelewa
    Ujue kabisa eneo lililokuwamisha ni Muda ,Adui ameshikilia majira Yako,MUDA ..Omba maombi kwaajili ya kukomboa Wakati
    Majira /nyakati ni kati ya SIRAHA Ambazo shetani amezitumia kukwamisha maisha ya Watu,na kuyashikilia
    ✓UKIOTA UMRINGIA KWENYE MTIHANI NA BADO ULIKUWA UNAFANYA ILA MUDA WA KUKUSANYA..UMEFIKA
    Ujue maarifa unayo ila imefungwa katika majira laizma ushughulike kukomboa majira ili uweze kufanya sawa sawa na kile unachotakiwa.
    (Mhubiri 3:1)
    ✓UKIOTA UKO KWENYE MTIHANI NA HUNA UTULIVU UNAANGALIZIA ..
    Ujue kuwa unachotaka kufanya hutaki kufanya ulichopewa wewe kilicho kwenye Kusudi la Mungu Bali unapiga ,hivyo basi unatakiwa ujitathmini ujue ni eneo lipi ambalo unaiga na sio ulichopewa wewe ..na Baada ya hapo umuombe Mungu MAARIFA YA KUSIMAMA NA KILE CHA KWAKO.
    ✓UKIOTA UKO UNAFANYA MTIHANI WA KIWANGO AMBACHO UMEVUKA TAYARI MFANO MTIHANI WA DARASA LA SABA WAKATI UKO CHUO.
    Ujue hatua ,kiwango ulichonachobsasa sicho unachotakiwa kuwa nacho,Kwa kawaida unatakiwa uwe chuo ila rohoni Bado upo nyuma sawa na darasa uliloona

Komentáře • 30

  • @SaraMateru-xb4zf
    @SaraMateru-xb4zf Před 8 dny

    Ubarikiwe sana mtumishi
    Nimejifunza kitu kikubwa sana...

  • @pendocoster4170
    @pendocoster4170 Před 7 měsíci +3

    Daah Asante Sana mtumishi umenifungua Sanaa MUNGU akubariki,,,,,AMEN

  • @yohanakiongo5094
    @yohanakiongo5094 Před měsícem

    Tataz unarudia rudian sana maneno unachelewa kufika kwenye point

  • @ANETHLUSANGIJA
    @ANETHLUSANGIJA Před měsícem

    Asantee saana dada, hii ndoto nafanya mtihani imekua kama sehem ya maisha angu

  • @bonifackayuni9575
    @bonifackayuni9575 Před měsícem

    Mimi aipiti wiki sijaota nipo kuchunga ng'ombe!! Manayakenini namba msada wako mtumishi!!

  • @user-qt6qp2kt3q
    @user-qt6qp2kt3q Před 7 měsíci +5

    Nmeotaaa najisomea kujianda kufanya mtian wa physics na mathematics yan was busy kujisomeaa iliii nikaufanye mitian mim na rafik angu wa second alikuwaga anashika namba moja nilikuwa nadiscus nae physics

  • @RehemaNobert
    @RehemaNobert Před měsícem +1

    Ubarikiwe sana, umenisaidia

  • @HappynessMkuya
    @HappynessMkuya Před měsícem

    Ndoto za aina hyo imekua km sehem ya maisha ila cjawahi kujua tafsri yake nam tyr nshahitim mda mref san masomo yangu

  • @wondersarena
    @wondersarena Před 2 měsíci

    Ubarikiwe sana dada somo lako limefika panaponihusu nitapafanyia kazi

  • @user-rq6lp1kd6h
    @user-rq6lp1kd6h Před 7 měsíci +1

    mimi nimeota tumefanya mtihani wa Geography, kisha mwalimu akaja kuita waliofeli lakini mimi sikuitwa

  • @NekemiaIluganyuma
    @NekemiaIluganyuma Před měsícem

    Barikiwa madame

  • @WELMADONATUS
    @WELMADONATUS Před měsícem

    Ubarikiwe

  • @user-qr5hw3mg1p
    @user-qr5hw3mg1p Před 6 měsíci +2

    Daah..m ht sielwi jnm kwasababu kil mara naota nafany mtihn lkn sik nyingn naota nip maeneo y shule ya msing kweny uwanj wa mpir nafany mtihan nikiwa nimesimama alf mtihan n wa secondar na nip n watu ambao nimesom nao secondar kun marafik zang wawil wakanisaidia maswal mawil..gafl skashtuk..mar nyingn naota nip shul y secondary nilikosomeaga nip darasan nafany mtihan mgum sana mda unaish n maswal mengn sjafany..siku nyingn niliot nip kanisan nafny mthian alf nimefik nimechelew nikaingia kanisan katekesta akanip mtihn ile nafany peni yangu aiandiki kabisaaa nikaazim pen pia aiandik inagoma gom kwahy md umeish sjamaliz kufny n ndot ikaishaaa...na kil nnapoot uwa naot tyuu nafany mtihn sio kwamb najiandaa war nn

    • @user-ye1dt2eb8u
      @user-ye1dt2eb8u Před 2 měsíci

      Watu huwa hawajibu maswali ya watu, aki mi uwa nashindwa kujielewa

  • @MosesSilumbwe-dv1ul
    @MosesSilumbwe-dv1ul Před měsícem

    Amen 🙏🙏

  • @MosesSilumbwe-dv1ul
    @MosesSilumbwe-dv1ul Před měsícem

    Amen🙏🙏

  • @user-hb5mn6zg9q
    @user-hb5mn6zg9q Před měsícem

    Dada nimeota natakiw kufanya mtiani. Lakin. Sikuweza kuufanya. Sababu nilivutadigala. Na mm Nina asili ya pumu mwalimu akaniadhibu Sana adi Nika stuka

  • @anicethkalori-vv4pi
    @anicethkalori-vv4pi Před 2 měsíci

    Mtumishi Mimi ninaitwa aniceth ni mhitimu wa chuo lakn nimekuwa nikiota nafanya mtihani ninafanya vibaya mara nimechelewa nimekuta washamaliza mtihani wakati Mimi nishamaliza sijui maana ya mtumishi naomba unisaidie

  • @AisharNyange
    @AisharNyange Před 27 dny

    Mimi naota Sana lakin mwenzenu na kabidhiwa mtihan nifanye lakin unakuta wenzangu wote wanamaliza lakin Mimi ndonakuwa wamwisho na sijajibu hata swali moja yaani inakuwa sikumbuki chochote naomba nisaidie hilo Lina maana gani Mana Mimi sisomi Sasa na maanisha sio mwanafunzi

  • @Ummy-yv7nc
    @Ummy-yv7nc Před 2 měsíci +1

    Jaman mm ni mama wa watoto 2 Nina maisha yangu lakin hii ndogo ya shule inanisumbua San naota nafanya mtihan wa form 4 tena necta sioti mtihan mwingine ni necta tu na nikiwa nafanya ule mtihan simaliz ule mtihan hata nijitahid vip simaliz nisaidien jaman nifanye nn na ina maana gan asante

  • @BeryniceMaerere-lf6du
    @BeryniceMaerere-lf6du Před měsícem

    Naota watoto wamepewa karatsi ya maswali imeambatanishwa na msimbo wa usahihishaji,

  • @PreciousBuyaga-zi5vn
    @PreciousBuyaga-zi5vn Před 7 měsíci

    Dada mi nimeota nafanya mitiani na nokakusanya kwa asikali keshi baada ya apo askali kanipa ela na akaomba tumpikie chai ya maziwa

  • @ProsperMichael-mj9qe
    @ProsperMichael-mj9qe Před 2 měsíci

    Nisaidie Namba ya simu yako

  • @ANETHLUSANGIJA
    @ANETHLUSANGIJA Před měsícem

    Naomba unisaidie namba ako plz

  • @SaraMateru-xb4zf
    @SaraMateru-xb4zf Před 8 dny

    Mtumishi unapatikana wapi?