Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 12. 09. 2024
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
    Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
    Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
    Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
    Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪CZcams Link bit.ly/CZcamsS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz

Komentáře • 102

  • @peterlujuo1640
    @peterlujuo1640 Před rokem +14

    Ukiitoa show ya ruge kwenye mkasi, hii ndo show bora ya salama, mahojiano yenye contents. Nime enjoy na kujifunza big up y'all

  • @veridianacharles4511
    @veridianacharles4511 Před rokem +5

    Masoudy ni kama muda wake ulikuwa mdogo ilifaa aendelee kutuambia mambo mengi zaidiiii ....... nimejifunza I wish maisha plus irudi tena

  • @msunjigfx8644
    @msunjigfx8644 Před rokem +10

    This is the one of the Greatest Man in the World, pengine hatukumwaga damu back in a days kipindi cha uhuru, ama pengine amani tuliyonayo inatufanya tunarelax na kujisahau but INAWEZEKANA

  • @2116-n
    @2116-n Před rokem +8

    Hilo swali la "Tanzania yako unaiona wapi" majibu yake aiseeee, ni akili ya kiwango Cha juu Sana🙏🙏🙏🙌

  • @philomenamushi5606
    @philomenamushi5606 Před rokem +10

    Hakika nimejifunza vitu vingi na ninazidi kujifunza 🤲🙏salama 🤲🙏masoudy🤲🙏asantee kwa darasa

  • @aloycemwambwiga2318
    @aloycemwambwiga2318 Před rokem +3

    Salama J! Kipindi chako kinaelimisha, kinajenga ujasiri, kinakuza kiimani. Nawe Mungu akuweke kama ulivyomwambia Masoud

  • @mrfashion1687
    @mrfashion1687 Před rokem +5

    Kali sana hii na nilikua naisubiri hongera kwa kutuletea huyu mtu, sasa bado SALAMA NA MILLARD AYO

  • @JohnMadaba-gb1je
    @JohnMadaba-gb1je Před rokem +9

    Salama kama unahitaji kujua uwekezaji was hisa na Hati fungani niambie. Ntakusaidia elimu for free. I am your fan

  • @frankphiri2666
    @frankphiri2666 Před rokem +4

    This guy is one of a kind my best quote "mnanunua hela mnapata wapi" kama nyie ni consumers na si producers

  • @jerrymwakapemba5644
    @jerrymwakapemba5644 Před rokem +2

    Nakupenda sana Masoud, huwa sichoki kukusiliza. MUNGU azidi kukutunza, una vitu vingi sana kwa ajili ya kuisadia jamii yetu (nchi yetu). Salama, nakupenda pia, kipindi chako kina mambo mengi sana ya muhimu kwetu. Big up you all!

  • @STEPHENJUSTINE-ty4nh
    @STEPHENJUSTINE-ty4nh Před rokem +9

    Mtu muhimu sana kwenye taifa letu na maisha ya WaTanzania ...💯🔥

  • @Bob-kz2ql
    @Bob-kz2ql Před rokem +2

    Strong heart Boss Kipanya, hiyo mentality wachache sana wanazo hasa wababa so tumejifunza mamb mengi sana hapo hasa sisi wanaume…be blessed Salama zaidi tupe watu makini sio wale channel za udaku na kutafuta umbea😂😂

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Před rokem +5

    Mungu akupe umri mrefu na Afya NJEMA Masoud Wetu 🙏

  • @businesstanzania
    @businesstanzania Před rokem +3

    Masoud Amezaliwa Zama Ambazo Sio Zake,
    Atusamehe Bure,
    Tukitaka Kumuelewa Tumpe Nchi.

  • @Curioustraveller254
    @Curioustraveller254 Před rokem +2

    Watu wasikujue saana...Familiarity breeds contempt Masoud nailed that

  • @mwengmfaume5301
    @mwengmfaume5301 Před rokem +1

    Nilikuwa nampenda malkom tangu akiwa mdogo japo nilikuja kumuona akiwa amekuwa kuwa,nakumbuka nilikuwa ndo kabinti niliuwa sipitwi na kipindi cha wàtoto chuchuchu , kaka masood na malkom,marehem Amina chifupa na rahmani,,yaani nino, na kaka bonda yey hakuwa na mototo walikuwa wakimcheka kimatani,,aisee

  • @mwandamboevans-wj8kp
    @mwandamboevans-wj8kp Před rokem +2

    Shukran sana Kwa hichi Sister Salama,mbalikiwe sana na muishi sana

  • @kamuchidyblez2136
    @kamuchidyblez2136 Před rokem +1

    God bless you masoud wewe ni genius sana aise naamn watu walio karibu na wewe kuna vitu vingi sana wanavipata kutoka kwako ,pia nikupongeze sana salamaa uko smart kwenye kazi yako #greatinterview

  • @salamisindimwo303
    @salamisindimwo303 Před rokem +1

    Kipindi kizuri...shukran kwa Mtangazaji,shukran kwa mgeni Ustadh Msoud...tumenufaika na kufaidika piya kupitiya mazungumzo yenu...

  • @lukullikiwamba6494
    @lukullikiwamba6494 Před rokem

    Masud kipanya ni Kati ya watu wenye fikra nyingi sana katika nchi ya Tanzania na bara lake sema sisi watu weusi tumeloga na aliyetuloga kafa, watu Kama yeye uwa tunawachukulia kawaida sana …… mungu ampe maisha marefu kaka yetu kwani bado ana mambo mengi sana kutujuza toka kwenye kichwa chake, Salama sina mengi ya kusema juu yako , you one of the best interview ever live in our generation, was good talk I love it

  • @mfaumejuma2375
    @mfaumejuma2375 Před rokem +5

    What an Interview.....Absolutely Sensational!

  • @rm9756
    @rm9756 Před rokem +4

    Plz Salama tuna muitaji tena japo 2hrs tu maana Ana vingi vya kutufunza
    From Kansas in USA 🤜🏿🤛🏿

  • @petermadokola7625
    @petermadokola7625 Před rokem

    Masoud I'm 55years, I studied mechanical engineering, based to motor vehicle, for over 30year, you inspires me big time, man you have great mind weather we want it or not but the truth stand still,
    Is there any chance we can meet, I would say we are some way alike, I'm a practically man ,you won't regret lay the table with me,

  • @glorykileo8601
    @glorykileo8601 Před rokem +2

    Vp ile show ya maisha plus bonge moja la show itufunza mambo mengi sana kama vijana tunaihitaji tafafhali

  • @giftwieland6322
    @giftwieland6322 Před rokem +5

    There is very thin line between love and hate🔥

  • @hellenmroso6786
    @hellenmroso6786 Před rokem +5

    Hiii show imekuwa fupi sana. "Tafuta taarifa upate maarifa"

  • @abdulhakimmwango9370
    @abdulhakimmwango9370 Před rokem +1

    Kuna content mmezikata na zilikuwa zinaumuhimu mno sanjari na Hilo bado show ni Kali mashaallah

  • @alifocusmsham7623
    @alifocusmsham7623 Před rokem +3

    Huwa sikuzote simalizi kiu yangu ya kumsikiliza Masoud, nimeangalia interview zake nyingi sana lakini bado nataka zaidi na zidi.

  • @priscajonas7805
    @priscajonas7805 Před rokem +2

    Daaaaah nimejifunza kitu kikubwa Sana thank brother 🙏

  • @egbertpesha4082
    @egbertpesha4082 Před rokem +2

    Great interview. Thought-provoking. Masoud has a big mind.

  • @faridaissa909
    @faridaissa909 Před rokem +2

    This is the best asante sana salama 🙏

  • @josegisbert4351
    @josegisbert4351 Před rokem +3

    Naomba umuhoji Masoud kila siku...

  • @mwajabumalekela5563
    @mwajabumalekela5563 Před rokem

    Duuuuhhh!! Nimejifunza kitu kikubwa saaana, hongera sana cis Salama na big up kaka Masoud, Mungu aendelee kukuweka na kile kilichopo ndani kiendelee kumea

  • @maridadi_2g
    @maridadi_2g Před rokem +1

    Men 🎉 Big up to Masoud I like your critical thoughts. Asante salama

  • @emerensianamaganza8322
    @emerensianamaganza8322 Před rokem +2

    Hawa ndo watu wa kuwekwa serikalini walete elimu na mabadiliko katika jamii, siyo tuu watu watuuu

  • @allenmanzi9869
    @allenmanzi9869 Před 11 měsíci

    Safi sana Masoud.
    Hapo kwenye Business Plan. Ni Ukweli Mchungu. very true.

  • @aminanamoyo83
    @aminanamoyo83 Před rokem +2

    ❤ masoud, thanks Salama but please mrudishe tena tafadhali 🙏🇹🇿🇨🇭

    • @georgemuigai7427
      @georgemuigai7427 Před rokem

      Hakika nimejifunza kitu kwa brother masoud,Mimi nataka kitabu nitakipata wapi?

  • @fredgrapher9838
    @fredgrapher9838 Před rokem

    Masoud, my faviurite presenter…since Chuchuchu ya Clouds fm, power breakfast…you are genius

  • @abdulhamis9825
    @abdulhamis9825 Před rokem

    Rais Anateua Watu Kushika Nyadhifa MbaliMbali Katika Serikal Na Maeneo Ya Nchi Lkn Iman Yngu Mpka Leo Bado Hajajua Ww Utashka Nafas Gani Ww Ni GENIUS

  • @emanuelsolomoni7003
    @emanuelsolomoni7003 Před rokem +4

    Let me challenge Masoud, Dubai leo ina mafuta na utalii hela wanapata huko as Nation, Urussi ina Gas na Mafuta inapata fedha hapo, sisi tuna Gas, Madini, Utalii how we optimise these resources ziwe na tija kwa Taifa huoni kuna sehemu hatuko sawa, our Gvt needs to be Rich enough tukifika hapo itakuwa simple wao kufacilitate hizo manufacturing ma exports na kuleta Technology mpya, Serikali kama hela ya budget yake ni mpaka itafutane hatufiki, hiyo china, Marekani, Urussi, hata urabuni serikali zao zina hela nyingi sana kwakuwa ni wakali na wamesimamia ukweli kwenye resources zao!!

    • @abdallahmakombo3866
      @abdallahmakombo3866 Před rokem

      Shida kuu Kwa nchi zetu ni ,
      Elimu na ufahamu,
      Tumekosa elimu na ufahamu Kwa viongozi,mtu mmoja mmoja na jamii zetu,
      Hizo nchi uzitajazo Zina technology, knowledge,
      Ufahamu huo huwapa ,
      Mawazo, ambayo huwatafuta watu sahihi Kisha hao watu huwapa mtaji / capital ambayo huleta kutatua changamoto za kidunia Kisha hupata zawadi( fedha nyingi/ THAMANI zaidi.
      Kwa hiyo Kuna haja kubwa ya kuwekeza kwenye wazo ( maarifa)Kisha technology ( mifumo ya uzalishaji Mali kisasa ,na ndipo tufike mbali ,HUKU TUKIJUA UJASUSI WA KIUCHUMI KIMATAIFA .
      Bado sana

  • @UgandanAllstarTales
    @UgandanAllstarTales Před rokem +2

    SHIRT LAKE KALI SANA

  • @dianerditto
    @dianerditto Před rokem +1

    Hili ni darasa huru nimechukua point za kutosha sana leo, ahsante.

  • @gtunewaves2867
    @gtunewaves2867 Před 4 měsíci

    masoud anaongea vizuri na kwa ufasaha sana

  • @barengayabomiriam
    @barengayabomiriam Před rokem +1

    Yaani baba Malcolm iko kama Mimi simtu wamarafiki.naninapenda saaaana kuka pekeangu kwa sababu Mimi nafkiria saaaaaaaana

  • @petermadokola7625
    @petermadokola7625 Před rokem

    I have worked for 30 years I did different kind of innovation, at the meantime I'm thinking of working with sustainable agriculture based to irritation, your a philosopher,

  • @brownngullo4051
    @brownngullo4051 Před rokem +1

    Masoud akili nyingi sana.. very inspired

  • @heriethalexander5145
    @heriethalexander5145 Před rokem

    This is hands down the best interview I have listened to tangu hii show ianze

  • @ayubustanley9069
    @ayubustanley9069 Před rokem

    NAWAKUBALI SANA.NBRO.masoud Kipanya nakukubali sana

  • @raheemkareem8055
    @raheemkareem8055 Před rokem +1

    Super genius🔥

  • @rehemarwanda6039
    @rehemarwanda6039 Před rokem

    I love Masoud Kipanya huyu jamaa ana akili nyingi sana

  • @martinmhando8351
    @martinmhando8351 Před rokem +2

    Genius Masoud.

  • @bakarishaha7331
    @bakarishaha7331 Před rokem

    hua namuelewa sana huyu jamaa. (kipanya) ni moja ya hazina , well done , please tuletee kaimu shehe wa mkoa DSM.

  • @GAVANA-ut2ek
    @GAVANA-ut2ek Před rokem

    Masoud amebarikiwa IQ kubwa..! Best Interview 🙏

  • @glorykileo8601
    @glorykileo8601 Před rokem +2

    Nimependa hapo kwa rafiki

  • @2116-n
    @2116-n Před rokem +1

    12:10,🤣🤣🤣🤣🙌🙌🙌, magari siyo matikiti au siyooo😂😂

  • @AmonAmon-bn6vn
    @AmonAmon-bn6vn Před rokem

    Akili hzi za masoud Hawa ndio ilitakiwa wawepo bungeni,bahati mbaya wapo Africa.

  • @mhangwacastory8765
    @mhangwacastory8765 Před rokem

    Ruge Mutahaba, Masoud kipanya ,Massanja,Zembela, Roma mkatoli ,Nauka nafikiri Hawa jamaa Tanzania inabidi iwatumie sana!

  • @dullywa9973
    @dullywa9973 Před rokem +1

    only content in this mahojiano 🎉

  • @yohanacosmasmachalila9016

    Big up brother Masoud na dada yetu Salama

  • @charlesmasesa89
    @charlesmasesa89 Před rokem

    Masud nakukubali na kunakitu chakujifunza toka kwako

  • @mucci_AI
    @mucci_AI Před rokem +1

    Duuh bonge la interview

  • @ishakafaki3501
    @ishakafaki3501 Před rokem

    Salma na ston town show naomba mniruhusu nitukane ili kiongozii wetu ajee hapa kumsikiliza huyu Kaka 😢😭😭😭

  • @katikatisafaris
    @katikatisafaris Před rokem

    Big brother is not a show to impact an African community, nothing in there.
    May Allah make it easy for Kipanya to continue with MaishaPlus

  • @jacksonndabhisiye4848
    @jacksonndabhisiye4848 Před rokem +2

    kitabu chake kinaitwaje na kinapatikana wapi

  • @Muuaah
    @Muuaah Před rokem +1

    Voice over artist

  • @naziakijangwa983
    @naziakijangwa983 Před rokem +1

    Makini broo❤❤

  • @raimajimoto1122
    @raimajimoto1122 Před rokem +1

    Nakukubali kaka

  • @Mfundo272
    @Mfundo272 Před rokem

    Ningefurahi sana Kama nitapata namba ya Kipanya, from Germany

  • @pauldmajo6827
    @pauldmajo6827 Před rokem +1

    On Podcast is 2 good hours, this is summarized.

  • @maximillianmasangya4784

    Nimejifunza shukran sana kwenu

  • @nevilekileo8262
    @nevilekileo8262 Před rokem

    Nasubiria salama na Roma mkatoliki, salama na Kala Jeremiah

  • @mungonyamilambo1157
    @mungonyamilambo1157 Před rokem +1

    Bonge la interview 👏👏👏

  • @richardmweusi6261
    @richardmweusi6261 Před rokem

    Asaalaam Alleykum naomba utuletee na ezden jumanne!

  • @MwanaidChomba-wx7ty
    @MwanaidChomba-wx7ty Před rokem +1

    Maisha plus ingerudi Tena

  • @lowkeybongo
    @lowkeybongo Před rokem

    Masoud mtu special

  • @Emiliana97
    @Emiliana97 Před rokem

    Big brains maahn🙏

  • @mmn7480
    @mmn7480 Před rokem

    Mi napenda tu slama tabasam lake

  • @abdallahmakombo3866
    @abdallahmakombo3866 Před rokem

    Hakika,
    SISI WA TANZANIA NI WACHUUZI KABISA.
    BIDHAA ILIOTENGENEZWA NA MWINGINE HALAFU UNANUNUA ILI KUUZA KWA FAIDA

  • @fundiseremalamohammedmdoe3711

    Masoud kipanya atafutwe tena, bado hajakata kiu yetu kama watazamaji

  • @dnewztz
    @dnewztz Před rokem

    12:13 utemgenezaji wa magari sio kilimo cha matikiti😉😉

  • @manstiko5890
    @manstiko5890 Před rokem +2

    Usimruhusu mtu akakujua kuna siku atakutumia vibaya sana kukujua kwako

  • @News6Tz
    @News6Tz Před rokem

    Natamani sana kama utakuwa unaleta watu wahivi wengi kuliko ambao hawana uwezo mkubwa wa kuzungumza vitu sensitive kama hawa mkifanya hivi wallah mtafika mbali hata vipindi vyenu kuwa namba 1 tanzania kuliko channel nyingi za hovyo cause hapa kuna vitu vingi vya kujifunza

  • @mcrramon4649
    @mcrramon4649 Před rokem

    Moja kati ya watu ambao wanafanya nijivunie kua Mtanzania

  • @araphatywanyamale6475
    @araphatywanyamale6475 Před rokem +1

    Why wasimpee aat uongoziii uyu jamaaaa ... mee naaminii iii Dhahabu kwa watanzaniaa aseee

  • @ramadhanijuma9655
    @ramadhanijuma9655 Před rokem +1

    Wakwanza

  • @dengahmediatz1230
    @dengahmediatz1230 Před rokem

    Jmn mahojiano mbn mafupi

  • @jobbyandrew4313
    @jobbyandrew4313 Před rokem

    wa pili

  • @reinatave780
    @reinatave780 Před rokem

    I wish Maisha plus Ingerud tena ngoja tuendelee kuomba dua

  • @mwanaidimohamed9200
    @mwanaidimohamed9200 Před rokem +1

    Watatu

  • @erickmorro8852
    @erickmorro8852 Před rokem +3

    Startup is hassling 🛺💪🏿, asante sana KP