AHADI ZA MUNGU - PASTOR SUNBELLA KYANDO

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 26. 08. 2021
  • Kuna eneo ambalo Mungu amekuitia.Na siku zote tambua kuwa hilo eneo tayari kuna ambao wanalikalia tayari.Wakati Mungu amewapa Waisraeli Kanaani,nchi hii haikuwa tupu,kuna ambao walikuwa wanaishi humo tayari.
    Baada ya Musa kutuma wapelelezi kumi na mbili,kumi waliona namna ambavyo hawawezi kuwapiga na kuwafukuza wale wakaao katika nchi ya Kanaani,na wawili tu ndio waliona ushindi katikati ya changamoto.Unapotaka kuingia Mungu alipokuahidia kuwa makini unasikiliza taarifa gani kutoka kwa hao waliokutangulia kufika huko.Kwa kuwa tu wengi wamekwambia hakufai,waliopo hapo tayari wana majina makubwa, haina maana kuwa huwezi kuingia.
    Wanaweza wakawepo lakini Mungu kawaondolea uvuli uliokuwa juu yao.Sio kweli kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.Shikilia Neno na Ahadi Mungu aliyokwambia,Yeye aliyesema ataitimiza.
    #PastorSunbella#

Komentáře • 31