Hoja ya utekaji yaibuka tena bungeni, Spika Tulia, Waziri Mkuu wabanwa kutoa maelezo
Vložit
- čas přidán 13. 09. 2024
- Hoja ya utekaji, mauaji na kupotea kwa watu ikiwemo watoto imeibuka tena bungeni baada ya Mbunge wa Viti Maalumu, Anatropia Theonest kutaka mkakati wa Serikali kukomesha matukio hayo aliyodai baadhi yanahusishwa na vyombo vya dola.
Leo Alhamisi, Agosti 29, 2024, hoja hiyo imeibuka bungeni wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, baada ya Anatropia kusema matukio ya utekaji, mauaji na kupotea kwa watu yanaashiria uvunjifu wa haki za binadamu.
Amesema matukio hayo yamekuwa na sura tofauti tofauti ikiwemo wivu wa mapenzi na ushirikina.
“Lakini na matukio mengine ya kutekwa na kupotea kwa watu yanahusishwa na vyombo vya dola. Nataka kufahamu mkakati wa Serikali kuzuia matendo haya lakini kuondoa taharuki ambayo inajitokeza katika jamii,” amesema.
Hata hivyo, Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson kabla ya kumpa nafasi Majaliwa kulijibu swali hilo, amesema juzi Jumanne Agosti 27, 2024 alisimama Mbunge wa Nkasi Kaskazini (Chadema), Aida Khenani akazungumzia suala hilo.
Amesema mambo hayo yanayohitaji uchunguzi:“Leo asubuhi nimesoma kuna mganga amezika watu sijui 10 na ngapi, sasa huyu mganga ni polisi ambaye watu ameuawa na wamezikwa kwake.”
Amesema mambo hayo yakiwa yanasemwa kwa hisia hivyo inakuwa kama mtu hajali wakati kila mtu anajali na kila binadamu ana haki ya kuishi.
“Lakini tusiweke mazingira kwamba kila anayepotea…si kuna mabasi wanapanda kule chini, akidondoka huko chini si nyumbani wanamtafuta utasema ni chombo cha dola kimemchukua.Sisi lazima tuifanye hii kazi kama viongozi ukichukua mihemko hutoi nafasi kwa Serikali kufanya kazi yake wakati huo huo hutoi nafasi kwa jamii kuendelea kushiriki katika jambo,” amesema.
Amesema wao wote ni viongozi na wangependa wananchi wao wawe salama na kuonya mambo hayo yasichukuliwe jumla jumla.
“Na wewe chukua nafasi ya uongozi, unaweza kutoa ushauri lakini usinyooshe vidole kwa sababu huna hakika. Na wengine wanahama nchi si tunakamata hapa kila siku, na wenyewe huko kwao wanatafutwa watasema chombo cha dola kimewachukua kimewapeleka sijui wapi,” amesema.
Amesema huku kwao wanawatafuta wahamiaji hao waliokamatwa nchini lakini kumbe alipofika hapa Tanzania mazingira yamekuwa magumu na hivyo amekamatwa.
Baada ya maelezo hayo ya Spika Tulia, amempa nafasi Waziri Mkuu Majaliwa kueleza akisema jukumu la kulinda nchi ni wajibu wa Watanzania wote kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama.
“Tunavyo vyombo vya ulinzi na usalama vyenye jukumu la kupokea taarifa mbalimbali zinazoonyesha uvunjifu wa amani popote pale kwenye meza ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. Jukumu lao baada ya kupokea taarifa ni kuhakikisha wanafanya uchunguzi,” amesema.
Majaliwa amesema uchunguzi unapobaini waliotenda makosa, wanawapeleka katika vyombo vya sheria.
Amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kujikita kusimamia misingi ya amani katika nchi yetu na usalama kwa kuhakikisha raia na mali zao zinabaki salama.
Amewahakikishia Watanzania kwamba suala la ulinzi na usalama bado liko mikononi mwao pamoja na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama.
“Jukumu letu ni kuhakikisha tunasaidia vyombo vya ulinzi kwa kutoa taarifa zozote zile ambazo zinaleta tishio la amani ili kuvisaidia vyombo vyetu viweze kuchukua tahadhari na hatua stahiki ili kubaini watu wote wanaotishia kutokuwepo kwa amani katika nchi yetu,” amesema.
Majaliwa amesema lakini pia vyombo vya ulinzi na usalama kuendelea na wajibu wao wa kuhakikisha kila taarifa inayopatikana lazima ifanyiwe uchunguzi na kubaini wale wote wanaohusika na kama wanapatikana wachukuliwe hatua mara moja.
Amemshukuru Spika kwa maelezo yake ya awali ili kuondoa upotoshaji ambao unaweza kuwa unaendelea na kufanya vyombo vyao vishindwe kufanya kazi yake na kuwavunja moyo watu wanaofanya kazi saa 24 kwa ajili ya ulinzi ambao unawafanya wabaki salama.
MaRC na DC tena bungeni
Katika swali jingine, Mbunge Viti Maalumu, Stella Fiyao amesema nchi inaamini katika uongozi wa kisheria na utawala bora ili kujengwa umoja mshikamano na upendo baina ya wananchi na viongozi wao.
Amesema hata hivyo kumekuwa na changamoto kubwa baina ya baadhi ya wateule wa Rais, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kwa kutumia nguvu na mamlaka yao vibaya kukamata viongozi na wananchi na kisha kuwatupa ndani.
“Moja jambo hili limetengeneza chuki kubwa baina ya wananchi na Serikali yao lakini linafifisha jitihada kubwa za mheshimiwa Rais za kuhubiri 4R na mwisho wa siku jambo hili linakuwa halileti mantiki,” amesema.
Ametaka kujua kauli ya Serikali ni ipi katika kukemea jambo hilo ambalo linatengeneza chuki kubwa baina ya Watanzania na Serikali yao.
“Kauli ya Serikali ni ipi kwa hawa viongozi wanaotumia mamlaka yao kutesa na kunyanyasa wananchi,” amehoji.
Akijibu swali hilo, Majaliwa amesema swali hilo ni linafanana na alilolisema jana Jumatano Mbunge wa Mlimba (CCM), Godwin Kunambi ambapo Dk Tulia aliwapa kazi Serikali kulifanyia kazi.
Mungu amlinde Hibrahm TRAOLEEE,,Taa ya Africa,,
Huyu mwanamke tulia ni janga la taifa lazima watanzania tuwe waangalifu na matendo yake ya kubomoa
Uchaguzi huu mbeya hapiti labda agawe jimbo mbeya wanaakili
Yesu Ndiye njia ya kweli na uzima ya kwenda mbinguni hebu MWAMINI Yesu na UOKOKE na ulithi uzima WA MILELE na uende mbinguni.(Yohana14:6, Warumi10:9-10).
Kwahyo na ww Tulia ukaamua ujibu kwa muhemko!? Ila Daaaaa! Inauma sana 😢
Muuliza amefafanua vizuri kwamba matukio ya utekaji yanahusishwa na mambo mengi ikiwa ni pamoja na wivu wa mapenzi, imani za kishirikina na mwishoni amehusisha vyombo vya dola, lkn naona majibu ya spika yamelekezwa kwenye eneo moja tu la vyombo vya dola
Yani ndugu ww mwelevu sana , muulizani katofautisha, ila spearker amna kitu kwa kichwa
Tulia wewe, tuliatu
Mimi nafikiri tulia ndio anamhemko ila muliza naona yupo viziri na apite pale makole ale kilaji nakuja kulipa
Hapo hatuna Spika, na yeye anajibu kwa mhemuko
Upo sahihi ila hii ninjama zakulindana wenyew
Kwanini sikunzote wasitekwe ni sasa. Mnajibu very simple
Mnauwa sana watu nyiyi muogopeni Mungu msijitetee kabisa. Mungu anawaona
Tunaspika mpumbavu sana shenziii kbs.. Na hao wanaopiga meza ni mbwa.
Spika ana mjibia waziri mkuu 😊
Huyu spika ni nyoko sana ila mwisho wa siku naye atakufa tu
La utekaji bungeni n zero, Allah, atusaidie wafe kw Ajali,
Spika anasema watu wasiwe na mihemuko kwenye maisha ya watu
Vyombo vya ulinzi na usalama hivyo vinavyo wateka na kuwaua watu ndo tunavyotakiwa kuendelea kuviamini?
Halafu huyu ndo spika wa mabunge duniani kweli?
Duh! tulia kweli?
Nyie tunawajua sana.
Ipo siku Mungu wetu atashusha kiburi hicho
Mimi ni ccm lakin kuna kiasira kinapanda kufuani mwangu,
Mpak nawish ningekuwa jetriii
😂😂😅😅😢😢 Nacheka ila naumia sana
Kabisa kaka
Yatakugarimu mbeya kwa uchaguzi .sote ni wazazi mungu atajibu tuombe
Kila sekta inakazi yake. Wapo wanaotakiwa wachunguze. Tuache lawama. Wote tumeumia. Siyo wewe tu. Hakuna anayependa haya matukio.
@@MaryMwamwezi-xm3izLikiwa kwenye sekta, serikali haitakiwi kuulizwa?, ila Tulia Mungu anakuona
Turia nimavi kichwani
Mbona huyo spiker anahalalisha watu kufa kwa kutekwa na kuona sawa tu,, hivi dini iko moyoni kwako kweli sio sawa please 😊
Ukristo sio dini
Wasiwasi wangu hapa Kuna kijambo miongoni mwa wanaotuongoza kwa kweli, majibu ya Spika simuelewi.
Spika.anaroho.mbaya.nandio.mana.anajibu
Anavyojisikia.
Uumeona ehh huyu spika hajfikwa na ndiyo maana anajubu atakavyo
Uongozi ni dhamana na busara muhimu sana ,,kiburi sio afya kwa nchi yenye amani utulivu
Naye Spika ana maelezo ya kimhemuko na kuashiria ukiburi fulani hivi! Hivi hawa waliopotea mathalani akina Azori Gwanda, Ben Saanane, akina Soka...walidandia mabasi kule chini kwenye chasis na wakaanguka na kufa na ndo kimekuwa chanzo chao cha kupotea? Au wame-stoaway na wapo katika nchi fulani za ughaibuni? Duuuh! Maelezo ya Spika ni maelezo ya ujumla mno na kimhemko pia! Serkali isifunike kombe mwanaharamu apite katika hoja hii. Uchunguzi wa kina ufanyike na vyombo huru ili kubaini watu halisi walio nyuma ya kupotea kwa watu!
Mungu Anglia ushetan
Yaani hata mganga wa kienyeji ana haki ya kuua au kuteka watu bila kuulizwa na serikali??? Ohh Tanganyika yangu.... Una kila kitu lakini uongozi wetu unatufanya tuishi kwa mashaka makubwa. Mungu unatuona watanganyika usituache na uzao wetu tukaangamia. Kumbuka kazi za mikono yako EE Mungu usiyefichwa na chochote. Unayaona yote yaliyo mioyoni mws viongozi uliowaruhusu waongoze kwa kipindi chote hiki.
Viongozi mtateseka sana kwa marazi kwahaya mungu yupo kwa malipo yenu
Spika kakasirika kisa kuuliza tena kwa msisitizo kuhusu watu kupotea😂😂
Mh Spika ni vema ukatenganisha Bunge na Serikali....Ukweli Bunge lina kazi kubwa kwenye kuisimamia serikali yetu...
Mnakera sana ccm
Mungu yupo anajisikia jibu lako utalikumbuka
Maisha ya watu yanafanyiwa siasa mungu anawaona
Duh mungu isaidie Tanzania tumeisha
Aise mungu atajibu hivi punde
Kimeumana kazi iedelee
Ni wajibu wetu Kila mmoja kuangalia na kujua kwamba tunahaki ya kuilinda nchi yetu Kwa pamoja na umoja
Mbona mbunge kasema wazi ,Haja generalize Mambo
Hatari sana, bungeni hakuna kitu.
Hakun ziro mwanamke anaongea sipo kweli
Inauma sana kwa watanzania wenzetu kutekwa iwe kwa kishirikina au iwe kwa wivu wa mapenzi au iwe utekelezaji wa dola tunachotaka haki kwa watanzania tu serikali ifanye kazi yake na sio idara zingine zisizo julikana
Aisee tumuogope mungu kwa hii hali
L
Madam speaker, YOU SHOULD NOT DEFEND THE GOVERNMENT, acha serikali ijibu… hapo ndipo kunapo kuwa tofauti wa mataifa ya magharib na barani kwetu Afrika!! His excellency Majaliwa, is one of the dude that I always respect tangu nikiwa mdogp na until kesho bado nitazidi kumueshimu tuu. Embu sikilizieni kwa umakini majibu yake. A decent quality one but also reputable leader!!
Kila jambo lina mwesho wake mungu atupe hekima yake mwenyewe
Mungu tu ndie mrizi siyo hao makafiri
Mganga wa kienyeji anaweza kushinda kesi ya kuzika watu 10 kwa majibu haya,yetu macho!!!!.
😭😭😭 MUNGU ikumbuke Tanzania
Amen
ndugu zanguni mungu huyu tulieachiwa na wakoroni nasema tena na tena hawezi kua sehem ya kumaliza matatizo ya Afrika tuamke watu weus ili kuupata mwangaza wetu uliozimwa hapo kitambo sana, vinginevyo juu ya huyu mungu wa kanisa na msikiti mmmmh ah ahhh bado sana
Mh Tulia tuzungumzie watu waliopotea na mpaka leo hawajapatikana... Vyombo vya ulinzi na usalama ni wajibu kulinda uhai wa wananchi na ikitokea mtu/watu wamepotea basi vyombo vihusike katika uchunguzi na taarifa zitolewe... isikae kimya.... ikitokea wahusika wamepatikana basi wakofikishwa mahakamani liwe jambo la wazi ili wananchi wajue serikali inafanya kazi na sio kukaa kimya
Majaliwa tunakuamini sana,vyombo ndivyo vinavyotuhumiwa kwa utekaji
Inabiti tuanze kuwateka na wao...
Mpaka atekwe waziri ndio mtajibu maswali
😂😂😂😁😁😁😁😁
Hivi hilo mbunge linakazi gani maan hawapas sauti kwa matukio Tanzania wapo kula mishahar ya bure 😢😢😢 eti mihimko duuu
Mmmh npo hapa namsubiria ROMA
Tulia ,uwe muunguana ,jiuzulu Mara moja!
Tulia mpendwa tumia vizuri akili yako na kiti chako,mamamama! Umezaa
Hapo sisi wenye D mbil sasa tumeona mwenye mhemko ni tulia, coz hayo aliyoeleza muuliza swali amefafanua vizuri kabisa but akijiwekea limitation ya kufikiria akajibu kwa hisia
Tulia ni ex usalama we taifa she is trained kuua revolution movement in Tanzania
Taarifa mnapewa hamtaki mnasema uchochezi hii ni aibu kwa kiongozi
Waziri majaliwa mara ngap matukio yanatokea na mnayatangaza lakini hatujui mwisho wake, ukweli katika ulinzi na usalama wa mipaka mpo vizuri ila ulinzi wa ndani kwa raia we amna kitu
Amesema mauaji ya aina tofauti
Tulia ume panik unaonyesha hili swala una lijua vizur ila yana muisho 🙏
Kazi kwelikweli
Kwanza hili bunge sasa hivi nalo limekuwa la hovyo sana linaikumbatia serikali kazi ya bunge ni kuikosoa serikali leo bunge ndio limekuwa kichaka cha serikali hovyo sana ila mungu anawaona tu
yan leo w.mkuu anajibu swali zito kwa majibu legelege inasikitisha sana na hii inatoa hisia kuwa anajua kinachoendelea
Kiongozi wa Bunge hakuna kitu hapo .
Poyoyo .
Hovyo wamejichagua hawajachaguliwa ndo maana
Hii serikali ijitadhimini upya bunge hili Ni Kama halina kazi Tena Kama tu hamwooni utekaji Ni mbaya basi
Huyu ni mwanamke na anawatoto akitekewa kijana wake atakumbuka na atajua watu wanaumia kiasi gan
Ivi jamani hiyo mama nikweli anajua swali na nini akijibu na kikubwa watanzania hayupo asie tambua kwenye ubaya na uzuri tusipende kudanganyana
Kiukweli watanzania wa chini tuna changamoto kubwa sana
Sijui kwamba tunajitambua vizur
Hivi Dr. Tulia ana watoto kweli?
Atakuwa tasa huyu
huyu dada bhana, hata mm ambaye sijasoma Shelia naelewa,
Tasa huyo
Yaani kushindwa tu kufikiri, inawezekana kabisa kukawa na viongozi wanahusika kuuwa watu, hata kuwatumia waganga ili kuficha ukweli lakini nyuma yake viongozi wanagusika.Tazameni masuala haya la sivyo damu zitarudi kwenye familia za viongozi wa nchi maana malipo ni hapahapa kizazi hata cha nne.
Spika anaongea kiwepesi tu hana hofu ya mungu,watu kutoweka gafla tu ,kama ndugu yako usingeongea kiwepesi hivyo,tutakusanyika mbele za mungu sikubmoja mungu atukumbuke
Mtatuua kwa kututeka lakini mjue hata nyinyi na familia zenu hamtokaa kwa amani labda mkaishi na familiazenu katika seyari nyingine
Msikatae watu wanauwawawa na serikali. Usijitetee
Huyu spika jamani ni tatizo.
Inakuwaje mbobezi wa sheria kama anavyojinadi hawezi kutafsiri swali lililo "generalized" na lisilo?
Pia aseme anaodai wanatumia "mihemuko" ni mihemuko inayotokana na uwepo wa jambo lipi na kwa manufaa ya kina nani maana melezo yake spika yanaashiria anajua chanzo cha hiyo mihemuko ya wabunge!
Usalama na haki za watu ikiwemo kuishi ni mambo very serious, hatupaswi kuyashughulikia kwa uzembe, milengo ya kulinda vyeo, vyama vyetu au maslahi mengine binafsi!
Ni aibu spika kunyamazisha mjadala au maswali ya aina hii huku ripoti, tena za vyombo vya dola zikisema mtu au vikundi vya watu wanagundulika kupoteza, kuua na/au kuzika watu wengine pasipo wao walio walinzi wetu kujua. Tujiulize, kama watu hadi 10 wameuwa Singida na mtu au kikundi kimoja, je intelijensia ya vyombo vyetu vya usalama inayosemwa kuwa ya hali ya juu inatumika wakati gani, kwa matukio yapi na kwa manufaa ya nani!!?
Unaangamia Tanzania, nakulilia Tanzania...! 😢
Hivi uyu nisipika au ni mtejaji wa mawazo na aki ni zaidi ya tatizo
Tulia tuambia huyu mkuu wa wilaya alikuwa anafanya kazi ya mihemko polini? 😂😂😂
😢
Bogasi spika😊
Hivi Kama hapo bungeni mnasukumwa tu na tulia mna kazi gani ya kuwepo hapo bungeni si abaki tulia mwenyewe tu bunge la mtu mmoja hovyo kabisa
Na ulipoulizwa Hali ya magufuli ulirukaruka hivi hivi kumbe mtu Yuko hoi, watu inabidi wasikuamini, pia swali Moja mmejibu wawili hatujardhika na majibu yenu!!
Nilitegemea kauli inayojitisheleza zaidi yenye kutilia mkazo kuhusu ikomeshaji wa vitendo hivyo kutumia vyombo vya dola ambao ni wataalam waliosomea mambo hayo badala ya kuwatetea na kurudisha kukumu kwa wananchi wote. Polisi ni wataalam wamebobea na wana vifaa maalum vya kazi na wanalipwa mishahara kwa kodi za watanzania ili wawalinde kwa umakini.
Kwanini isitoke kauli Kali ya kurlekeza ili kuondoa taharuki kwa wanyonge wengine na wananchi?
Juzi??? Duh!!
Wanachi hatuna haki sasa......
Hapo spika kamwita Waziri Mkuu ajibu nini wakati maswali yake keshajibu? Wao wana uhakika na usalama wao na watu wao anajibu anavyojisikia aliyeuliza mjinga hicho ni kiburi cha nafsi majibu anayo Mungu
Mambo ya Nosence ya leading group from a sjngle party
Spika acha mambo ya siasa watu wanauliwa na kupotezwa unadai ni mihemuko acha dhalau za hivo ujue wanaouwa ni binadam na wameacha familia zao na wanahaki km binadam km huna point kaa kimya
Kwani we tulia unamatatzo gani afu nyinyi wabunge mnao piga mkofi mnaakili kweli nyinyi
Nikwanini mtuakiuliza swali lamsingi sipika anaingilia kati wakati watu wamepoteza uhai tunakwenda wapi au hii nchi inaongozwa kikekike hatutaki
Huyu tuliya hata simuelewiii😢😢😢
Embu sisi tuseme tumeshindwa ehh MUNGU wa rehema ingilia kati Baba Yangu
Munasiri gani nchi hii viongozi mbona Watton waviongozi hatuwasiki chochote kimewapata
Mbona ccm hawatekwi wala kuuliwa just crazy this country
Hivi unajua ulisemalo au,haya ukimlenga huyo mganga je na hawa walio vyamia basi na mabunduki na mtoa waliye mtaka mpaka kumua na kumtupa hao walinzi wako wapi,hali tukio limetokea kwenye basi,we mama usilinde kiti ulicho kalia fikiria ubinadam kwanza na ndio wamekuweka hapo😮
Msiba usikie2 kwajiran, uskukute jaman Mungu yupo ipo sku
TULIA,OMBA HEKIMA YA NYONGEZA TOKA JUU KWA MWENYEZI MUNGU.POROJO HAZIFAI WAKATI WATU WANAANGAMIA.
Bunge Halifax maamuzi
Kuna mtu akifa wakisema ndugu waje waweke mchanga nitajitokeza na mkokoteni wa mawe niweke ili anakoenda wamuulize huko ulikotoka unaugomvi na watuuu
Hiki ni kipindi Cha uchaguzi,hawa wote walio madarakani ndio hao hao,,kwa hivyo ni ngumu kukubali. Atekwe mtoto wa Mkubwa ndio mtaona
Bunge dhaifu sana, spika kilaza
Huyo mama hayuko sawa
Daah😢😢
hilo ni swali la waziri mkuu au swali la spika
We spika kwahiyo unatetea polisi yani umekuwa mtetezi wa watekaji
Mnaibuaje hoja ambayo spika ashatoa tamko kwamba wanasafiri awatekwi ao waliokutwa wamekufa nikusafiri
Speaker hafai kabisa kwa kauli alizotowa kuwa yeyote atakaye musema vibaya Rais wasimuache bali ashugulikiwe. Huk ni hatari sana ya kuwashsuli watu wachukuwe sheria mikononi mwawo (Mob justice) na huyu ndiye speaker wa watanzania wote. Watanzania seriali hii si salama kwa wananchi wake.
Anaonge kamaatakavyo kwa sababu familia yake ipo salama.
Hanauwakika familia yake aitahingia ktk majanga hayo,
Spika anatoa majibu mepesi na yakupotosha mada kwasababu amesharidhika tumwachie Mungu ila pongezi kwa alieuliza
Tumeumbwa kwa sura na mfano Wa Mungu tambua unapo mtesa mwanadamu unamtesa Mungu tambua ww dada
Inauma sana kwamajibu haya ya kejeri