Historia Ya Sallam : "Shule Sijawahi Kupenda, Ada Kulikuwa Hamna" | SALAMA NA SALLAM PART 1
Vložit
- čas přidán 8. 09. 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Sallam Sharaff ni lejendari, na hilo liko wazi kwa anayetaka na asiyetaka, kwa umuhimu wake kwenye maisha ya msanii nambari moja kwa sasa ni kama nywele, usipomkuta kichwani basi hata kwapani hatokosekana. Na kwa utashi wangu nadhani kama wana Bongo Flava au wasanii ambao ‘wako tayari kuwekeza’ basi wangemkimbilia kwa kasi ya 4G ilimradi wapate mawazo tu ya jinsi gani wanaweza kufanya ‘meli’ yao ifike na pale panapotokea mrama wajue wimbi gani la kuliepuka na wimbi gani ndo walipandie kwa juu.
Sallam si muongo na hili ninalijua kwasababu ni rafiki yangu, atakavyokuambia ndivyo lilivyo, Sallam anapenda pesa na hilo liko wazi na wala hajifichi nalo ila kubwa zaidi Sallam anapenda MAENDELEO. Ukitaka msielewane naye milele na milele basi onyesha nia au muonyeshe moja kwa moja kama unataka ’kumharibia’ mkate wake. Hakika hatokuacha salama. Atahakikisha unaenda na maji kwasababu mkate wake ndo maisha yake. Tofauti yake na wengi wetu ni kwamba wengi wetu tukijua mtu anataka kukuharibia basi na wewe utajificha au utamuepuka au utamchukia tu, Sallam yeye atakuonyesha waziwazi kama HAKUPENDI.
Muziki anaufahamu vizuri tu na mengine anayang’amua as we go kama binadamu wa kawaida, mapenzi yake kwa mziki huu na kwa kupenda anachokifanya ndo kunamfanya awe THE BEST MANAGER. Maisha na mipango na maendeleo ya msanii nambari moja kwa sasa yalianza kubadilika sana mara baada ya Sallam kuingia kazini, na ilibidi aanze kama International Manager maana kwa upande wa ndani tayari Babu Tale na Said Fella walikua washapatawala. Haikua kesi kwake, ambacho alikifanya ni kuhakikisha Diamond anapata collabo na show nyingi za nje ambazo yeye alikua anaenda naye. Wakati akiwa wanapokua alitumia nafasi hiyo kutengeneza network nyengine. Mipango yake na uwajibikaji na jinsi vitu vilivyokua vinasogea vilimfanya Platnumz ampende zaidi, amshirikishe kwenye mambo mengi zaidi ambayo matunda na malipo yake ndo haya ambayo wanakula leo na kesho na keshokutwa ilhali mimi na wewe tunashuhudia historia inavyozidi kuandikwa.
Kwa Said Fella kupata udiwani nako pia kulimfanya Sallam apate majukumu zaidi ya hata ya ndani sasa maana kipindi kile cha Hayati JPM kazi ilikua inabidi ifanyike na Sheikh Said alipigiwa kura na watu, so mara nyingi ilikua inabidi afanye kazi za kutumikia wananchi wake, na huku nyuma Sallam akawa anaezeka banda lake la kuishi kwenye ufalme wa Diamond Platnumz.
Nakumbuka mwaka 2018, London Town, Diamond alimaliza show zake na Sallam akabaki nyuma, kilichowapeleka kule ilikua ni show ambayo yeye Sallam, my cousin Dulla Meru na moja ya mapromota hodari kutoka Nigeria ambaye anaishi London Ndugu Smed waliiandaa, ilienda poa na naamini ile ilifungua milango mingi sana. Alibaki nyuma kuhakikisha mambi yote yanakwisha freshi na pia kutengeneza network nyengine kwa matumizi ya baadae. Alibaki nyuma na mimi. Tuli enjoy, tuli jifunza na pia yeye aliweza kuweka MIZIZI yake vizuri ili mbuyu huu tunao uona leo usimame.
Mawe mengi mno kapigwa. Maneno mengi sana yamesemwa juu yake, kama binadamu hawezi kuwa amekamilika au kamaliza, ila jitihada zake na kazi ambayo anaifanya inabaki inamzungumza kwa niaba yake. Kama ambavyo yeye anasema, kwanza yeye ni MFANYA BIASHARA, mengine yanakuja baada ya hapo. Diamond anamlipa Sallam kwa asilimia kila mara anapoleta BIASHARA kwenye MEZA YAKE. Faida ni ya WOTE. Sio mmoja ananenepa na mwengine anakonda kama ilivyo kwenye mahusiano mengi ya biashara hapa nyumbani na pengine Afrika na duniani kwa ujumla.
Ukiniuliza mimi nitakuambia, hapa kuna mengi ya kujifunza.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
CZcams Link bit.ly/CZcamsS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
when y see successful people just respect them cause they come from far
Jombaaaa linajuwa kuongea hilii sijuwi ndo anaemfundisha kuongea Diamond da! Hatar
nice interview,tunahitaji pia interview yako na zuchu,we love zuchu so muuuuuch
Kwelii zuchuu interview
Mtu mmoja ambae namkubali sana tanzania ni salam sk yuko realy sana
SJ naomba umcheki this man from Kenya ABDUL MUTAL tukipata interview naye itakuwa bomba sana.
ngoja nirolll kitu changu mie nicheki interview..i😂🔥
Salama My favorite wow I like her a lot
🇰🇪 Salama unapendeza nanipenda sana show zako.
Mwambaaaaa huyu hapaaaa ✌️✌️✌️✌️🦁🤙
Sauti kama diamond kabisaaàa
We've been waiting n waiting salama na ZUCHU
Yeah sijuw ili ishiya wapi
Nakupend sallam😍
Wa Kwanza
Nimejifunza vitu vingi sana kwako Sallam SK
Kama una hamu na kuskia zaidi kuhusu management ya huyu jamaa jipongeze. Likes zangu leo wa kwanza...,😂😂
Watching from South Africa 🇿🇦🇿🇦🇿🇦🇿🇦🇿🇦
salama umri bye bye ,,, nakupenda b kizee nakupenda kikongwe🤣🤣🤣😍
pole kwa kupoteza wazazi Sallam🙏
SALAMA NA SALLAM 🐐
Salama na Diamond platinum please
One dey nataka kuwa kama uyu mwamba...aiseee
Umeitunza Sanaa hii sallama
Much love from Burundi 🇧🇮
Maswali mazuri sana, ni mafupi kuliko majibu.
Ahsante Salama🤸🤸🤸
Nafwatilia sana salama na..... my humble request try have some Kenyans in the show. Thanks
1
Show IPO very smart..
Am TZ 🇹🇿💋❤LOVE ALWAYS SALAMA AND MENDES 🤛🥰🤩💯MTAJUA HAMJUI LIKE ZAO
Salama na diamond...Lin...??
Ni Salama na Salaam!!
how does that make you feel *GOod aah🤣 that's Mendez#DONsallam
Love from mozambique 🇲🇿🇲🇿🇲🇿 salama na salaam
Kaka na dada😎
Don mendezi 🔥
Hii interview kubwa sana
Nice
Nipo kwa mwalimu wangu wa biashara hapa Mr Sallam
Kamati ya roho mbaya 🤣
Salama na DIAMOND PLATINUMZ
Salama unaweza sana kuhoji kwanza una furaha na tabasam zuri✌️
Huyo jamaa aturudishie the JOINT... ana unyama mwingi
Mletee Sheikh Othaman Maalim Vijana tutajifunzaa kupitiaa yeye
mlete P funk please
DON MENDEZ🔥🔥🔥
Double SALA💞💞
Sallama na SallaM
salama na zuchu mbona haipo CZcams
Salama the best 🔥
Kweli ukifanya ukarimu sana mwisho wanakuzoea namazoeya yakizidi inakuwa zarau
Safi sana kumbe huyu jamaaa secure sana
Sauti iko chini Sana
Naomba umwita chid benzi
First time nilijua Sallam ni mtu wa mbele kumbe ni mTz....
😎👍
Ila ni mwarabu
Mluguru bhn
@@zuweinaalhabsya8773 Ila?
Interview Hasheem Thabeet next season.
Mleteni Nikki Mbishii
Diamond platnumz
Anazarahu sana utawa atazikwa na pesa izo hana kubukubu zuri.eti anafanya kazi zake kaulishafu .utajizika ,na uliumwa utakiunguza
Umesemaje wewe?? 👈💁♀️
Acha ujinga wewe tafuta pesa hata mbwa anazikwa!
Pesa Pesa Pesa tutafute
@@UlimeA Kabisa!
Salama always wears BLACK. #shelooksgood
She😂😂😂
@@mwambakizota2874 uhh! Yeah she looks good in black.
Tuwekee salama na zuchu
Yes
Forest Alumnu mwenzangu 😁
Mm pia nlikuwa nakujudge vibaya Don bt nmeekuelea kabisa
Namsubiir Best rapper Stamina hapo, Salama Fanya Yako basi
That how he was......that ....that ninyingi mendez
Salam sk.
Don Mendez as you bro
Mafanikio yana ving
👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿
Apo twenty twelve ss!😄😄
yupo sahihi ni 2012, yani ni kama unaweza kusema twenty twenty
Menenmet diamond platnumz
Salam.. Mzee wa rohom-bi," a.k.a. Rohomfu!"
Sallama na sallam
Richard hananja mlete kwa show tafazali
Neema ...... Siku hiyo Mic zote hapo studio ZITACHEKA
Technically,,,salam huyo
Salama na Diamond Platnumz next session please
Mlete Carry Mastory
Katika ma presenter wenye HQ kubwa ni salama anauliza maswali yamaana sana
IQ not HQ
Sku 1 tuletee sir nature
Salama tunaomba utuletee Niki mbishi
nakubal
NC salama kutuekea m2 waukae p1 sn
Watuuu dunia hiyiii nihatali chid Benz EMAX anafanya mambo yake munajuwa ila hamusemi nyie wote hapo munajuwaa
Mendez kama mendez
🇹🇿
So so so so so so so?? ¿Why so
So
Social media
it's some swaggs, American swagg,
Hvi mbona ya zuchu hukuweka youtube?
Haki nimecheka kwamba mtu mkarimu ambaye Salam sk ktk maisha yake alishawahi kukutana naye ni Ay eti anamfananisha AY na kama Yesu haki nimecheka🤣🤣🤣🙌
Mendez 🙌🙌🙌
El jefe Mendez
Tom boy salama
🇹🇿🇹🇿🇹🇿✌✌
Next time camera man avae headphones ili kudikiliza noise kama izo za salam sk anavyopiga meza
Boss kasema Mimi nani nipinge
Salaama na kipanya itapendeza
Tayari
Sala MBILI
Uongo mwingi sana kwa huyu Mtu
Yuko really hanaga fake but tu ni muongo wa story
Mwite Mwamposa watu wengi sana tutaisikiliza hiyo shoo🤔
Majambo navijambo
Kumbe wakwetu kilosa sallam
Salama na dudu baya naitamani
Itanoga sana
Tunamtaka Wema sepetu
Tuletee Bongo zozo Salama