Askofu Dkt Msafiri Joseph Mbilu juu ya eneo la SEKOMU

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 11. 09. 2024
  • KKKT yawatoa hofu waumini uuzwaji mali Lushoto KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania -Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), limewatoa hofu waumini kuhusu uuzwaji wa mali za kilichokuwa Chuo Kikuu cha kumbukumbu ya Sebastiani Kolowa SEKOMU, kinachomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
    Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Upendo Media, Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Alex Malasusa na Askofu Dkt. Msafiri Mbilu wa KKKT-DKMs wamesema, Kanisa linaitunza jambo hilo kupitia KKKT-DKMs na kuwataka waumini wa KKKT nchini kote kuwa na utulivu wakati jambo hilo likifanyiwa kazi.
    "Napenda kuwajulisha waumini wote, uongozi wa KKKT-DKMs umekuwa ukifanyia kazi jambo hilo na ni matumaini yangu kuwa jambo hili litapata muafaka na kupewa taarifa rasmi. " alisema Askofu Dkt. Mbilu.
    Viongozi hao wametoa taarifa hiyo kufuatia tangazo la mnada wa eneo la Chuo hicho lililoonekana kwenye vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii na hivyo kuwaomba waumini kutulia.
    "Ni kweli tupo kwenye changamoto lakini jambo hili bado halijawa nje ya uwezo wetu na tunaamini kila kitu kitakwenda vizuri," alisema Askofu Dkt. Mbilu.

Komentáře • 3