Kenya yatamba riadha za wakongwe

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 12. 09. 2024
  • Rais wa shirikisho la riadha ya wakongwe duniani Margit Jungmann ameipongeza Kenya kwa matokeo mazuri kwenye mashindano ya dunia makala ya 25 yaliyokamilika jana nchini Uswizi.
    Kikosi cha Kenya kilimaliza cha 21 duniani kwa medali 26 zikiwemo dhahabu saba, fedha kumi na shaba sita.
    Medali hizo ziliifanya Kenya kuorodheshwa ya pili Afrika nyuma ya Afrika Kusini waliowazidi kwa dhahabu huku nigeria ikiwa ya tatu wakiwa na dhahabu moja pekee. Marekani iliyokuwa imeandikisha wanariadha 600 waliibuka mabingwa wa jumla kwa kukusanya medali 224.

Komentáře •