Video není dostupné.
Omlouváme se.

OBBY ALPHA_-_NIOKOE - THERAPY MINISTRATION

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 23. 06. 2024
  • #SUBSCRIBE #LUPIMO_MUSIC_THERAPY
    VISIT ALL MUSIC PLATFORMS FOR MUSIC THERAPY,
    Inspirational, Relaxation, Psychological & spiritual Therapy, Prays and worship Ministration.
    SASA NI SAA YA KUWA-AMSHA MASHUJAA, AMKA SHUJAA
    MWL LUPIMO || Psychologist:-
    A FOUNDER OF LUPIMO WORLDWIDE COMPANY
    ZABURI 13:6
    Naam, nimwimbie BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa Ukarimu.
    GOD HAS BEEN USING HIM TO PROVIDE THERAPY THROUGH GOSPLE THERAPY MINISTRATION, AND
    EDUCATE PEOPLE AROUND THE WHOLE WORLD, PEOPLE TO BE OPENED, AND DECIDE
    TO LIVE WITHIN THEIR CALL TO REACH THEIR DESTINY
    NIMEONA NIKUANDIKIE HIKI KISOME MPAKA MWISHO
    NJIA 4 UNAZOWEZA KUZITUMIA KUJUA WITO WA MAISHA YAKO.
    Kila mtu aliyezaliwa na kuja duniani ana kusudi au wito ambao MUNGU amemwitia kuufanya Katika maisha yake. Bahati mbaya sana watu wengi tunaishi maisha yetu yote duniani, bila kujua tumekuja duniani kufanya nini.
    Kama wewe ni mwanadamu umezaliwa na unaishi hadi sasa bila kujali umri wako, unajua au haujui, kitu cha muhimu cha kufahamu ni kuwa unao wito ambao MUNGU kakuitia. Una kusudi la MUNGU ambalo kaliweka ndani yako, ili uliishi na litumike kwa ajili ya watu wengine.
    WITO sio kufanya jambo tuu linalohusiana na dini, Wito ni kufanya jambo ambalo MUNGU lilimsababisha akuumbe ambalo ukilifanya linatatua matatizo ya watu au kuleta mabadiliko kwa watu. Lakini pia, linamfurahisha MUNGU na kumfanya ajisikie kwamba amefanikisha kile alichoruhusu uje nacho duniani.
    Zifuatazo ni dalili au Njia unazoweza kuzitumia kujua WITO au KUSUDI la Maisha yako:-
    ✍️1️⃣ Kitu gani kinakukosesha utulivu au kinakupa usumbufu.
    〰️Ni Kitu gani ndani ya moyo wako kila wakati kinachochukua muda wako mrefu wa kukifikiria, kinachochukua mda wako mrefu kila wakati kukitafakari, Kitu ambacho hata ukitaka kukipuzia unashindwa.
    Inawezekana ukawa umesoma au una kazi unayofanya lakini kuna wakati unakoswa raha nakuona sio sehemu sahihi unayopaswa kuwepo au sio kazi sahihi unayopaswa kuifanya. Yawezekana ukawa unafanya kazi kwa ubora na watu wanakusifia kwa utendaji wako wa kazi, lakini wewe kuna fikra zinakuijia zinazokinyima raha na zinazokuonyesha kuna kitu unachopaswa kukifanya nasio hicho unachokifanya sasa.
    Ikiwa hali hii inakutokea Usipuuzie, ni Ishara inayotoka kwa MUNGU mwenyewe inayokuonyesha wito sahihi wa maisha yako.
    ✍️2️⃣ Isikilize sauti yako ya ndani.
    〰️Sauti yako ya ndani ni Ishara ambayo MUNGU anaweza kuitumia kukuonyesha Wito wa maisha yako, unasikia nini ndani yako? yawezekana watu wa nje wasisikie kilichoko ndani yako lakini lazima wewe unajisikia mwenyewe.
    Ili kusikia sauti yako ya ndani jifunze kujipa mda wa utulivu ukiwa peke yako kwa kutafakari na kuisikiliza sauti yako inasema nini ndani yako.
    Sauti yako ndani yako, inakwambia wewe unataka kufanya nini katika maisha yako? Sauti yako ndani yako inakwambia wewe unataka kuwa nani katika maisha yako? Sauti yako ndani yako inataka uutumiaje mda huu unaoupata na ulioubakiza katika maisha yako?.
    Tafadhali zingatia Sauti yako ya ndani inayokusemesha usiipuuzie, ni sauti inayotoka kwa MUNGU inayokuambia wito wa maisha yako.
    ✍️3️⃣ Angalia vitu au mambo yanayokupa maumivu.
    〰️ Ni njia itakayo kusaidia kujua umepewa wito gani na MUNGU ndani yako, unajua kuna mambo mengi yanatokea katika maisha yako ya kila siku. Mfano kuna mtu anaweza kuwaona mayatima au walemavu wamechoka na wanaomba msaada njiani lakini anawapita tu kama kawaida. Lakini wewe ukiwaona unasikia maumivu na ile picha inabaki akilini mwako ukifika nyumbani unajisikia vibaya, unalia na kujisemea ungekuwa na mapesa ungewasaidia hao watu.
    Aina hii ya maumivu sio yale ya kujijutia ni maumivu ya kujisemea natamani ningekuwa na uwezo wa kufanya jambo fulani, Yawezekana ni maumivu yanayotokana na siasi, Teknolojia, uchumi na kuendelea.Ikiwa unapata aina hii ya maumivu ni ishara ambayo MUNGU kakupatia na kukuonyesha kuwa amekuitia kwa ajili ya jambo fulani.
    Tafadhali usipuuzie maumivu hayo kwa sababu, maumivu hayo unayoyapata wengine hawayapati kwasababu hawajaitwa katika wito wa aina hiyo.
    ✍️4️⃣ Angalia jambo unalolipenda sana.
    〰️ Hapa unaangalia Jambo unalolipenda kulifanya katika maisha yako au jambo linalokupatia furaha. Watu wengi wamejikuta wakifanya kazi sio kwamba wanaipenda, ila wanafanya kazi kwasababu inawaingizia pesa, matokea yake wamekuwa sio wabunifu na hawaleti matokeo chanya katika jamii. kwasababu yakuwa katika eneo ambalo sio wito wao ambao MUNGU kawaitia .
    Nachopenda kukushauri ni kuwa, katika maisha yako kitu unachopaswa kukigundua ni jambo gani au kitu gani unachopenda kukifanya katika maisha yako, na uwe na uhakika kuwa kitu hicho ukikifanya kinakupatia furaha.
    Ikiwa kuna jambo unalolifanya kwa kulifurahia, na unalipenda, bila kujali linakuingizia pesa ua halikuingizii. Ni dalili pia inayokuonyesha kuwa MUNGU amekupatia wito gani.
    Natumaini umejifunza kitu.
    AMUA KUISHI NDANI YA WITO WAKO

Komentáře • 8