EACB NA SEMS APPAREL WAINGIA MAKUBALIANO KUTOA MAFUNZO YA UBUNIFU WA MAVAZI
Vložit
- čas přidán 8. 09. 2024
- #samiasuluhuhassan #biashara #ujasiriamali
Chuo cha East Africa College of Business (EACB) na Kiwanda cha Sems Apparel wameingia makubaliano ya ushirikiano katika kutoa elimu ya ushonaji wa nguo kwa rika mbalimbali hususan Vijana ili kuweza kujiajiri kupitia fani hiyo ya ushonaji.
Elimu hiyo itatolewa katika ngazi ya Certificate (Astashahada), Diploma (Stashahada) Degree (Shahada) kutoka kwa Wakufunzi waliobobea katika fani hiyo ya ushonaji wa nguo na ubunifu wa mavazi.
Vyuo vinavyotoa mafunzo kama hayo, Chuo cha Ufundi (VETA) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wametoa maoni yao kuhusu mafunzo hayo ambayo yatatolewa na EACB na Sems
Aidha, Wadau mbalimbali wanaohusika na ubunifu wa mavazi wametoa maoni yao kuhusu sekta hiyo ya ubunifu wa mavavi na ushonaji wa nguo kuingia kwenye mitaala rasmi ya kielimu.