WAZIRI SILAA APIGA MARUFUKU MABANGO YA VIWANJA VINAVYOUZWA | ATOA SIKU SABA YOTE YAONDOLEWE

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 11. 09. 2024
  • Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Silaa amepiga marufuku nchi zima mabango yaliyozagaa mitaani ya Kuuza viwanja maarufu Viwanja vinauzwa na ametoa siku 7 kwa kwa maafisa ardhi nchi nzima kuhakikisha mabango hayo yanaondolewa na agizo lake la makampuni yote yanayouza ardhi kuweka dawati la mauzo ofisi za ardhi za wilaya na mikoa.
    Silaa ametoa maagizo hayo ofisini kwake jijini Dar Es Salaam alipokuwa akisikiliza kero za wananchi waliofika kutafuta haki yao baada ya kuuziwa viwanja na kampuni Digital Auction ltd waliowauzia viwanja hewa kwenye eneo ambalo hawalimiliki katika Manispaa ya Kigamboni na kukusanya Tshs 116,000,000.
    “Huwezi kuuza kiwanja kwa ramani, kiwanja kinauzwa kwa hati, serikali haiwezi kukaa kimya wakati wananchi wanyonge wanateseka na kutapeliwa fedha zao.
    Amewataka wenye makampuni ya ardhi wanaotaka kuuzia viwanja maofisini mwao waombe hati za viwanja wanavyopima.
    Amemtaka kamishna wa ardhi kuharakisha mchakato wa utoaji wa hati kama zao la upimaji wowote wa ardhi.

Komentáře • 26

  • @user-sm7gj4mn5n
    @user-sm7gj4mn5n Před 3 měsíci

    Slaha hongera sana waziri Mungu wa mbinguni na nchi akubariki utendaji wako wa kazi ni mzuri sana Tanzania inahitaji vijana kama wewe

  • @hawaelymaricca7602
    @hawaelymaricca7602 Před 3 měsíci +2

    Silaa yako vizuri sana maana wapo watu wenye roho ngumu kaz Yao ni kudhulumu wanyonge yaani mtu akiwa na pesa na kiwanja kakipenda bas anaingia Aridhi anatoa chochote. Mnyonge anakosa haki

  • @user-xn8jh1yw1h
    @user-xn8jh1yw1h Před 3 měsíci +1

    Nchi yenye Wafanyakazi wenye Uadilifu.. imeendelea. Big up sana Mheshimiwa Silaa.

  • @seleshaban48
    @seleshaban48 Před 3 měsíci +2

    U kweli we ni kiongozi..., nitaongea na mama ulinzi kwako Uwe mara3

  • @abdirizakibrahim1975
    @abdirizakibrahim1975 Před 3 měsíci +1

    MUNGU akulinde kijana wetu Jerry mzalendo wakweli lakin vijana wengine hovyo na wanalipeleka Taifa letu pabaya sana

  • @lawrencegwerino1656
    @lawrencegwerino1656 Před 3 měsíci

    Safi sana waziri hiyo itaondoa matapeli wote wa alithi..

  • @user-kd9dc4li7f
    @user-kd9dc4li7f Před 3 měsíci +1

    Wewe waziri slaa wewe kichwa kama kila waziri angekuwa kama wewe nchi yetu tungekuwa mbali

  • @shariffsagaf2305
    @shariffsagaf2305 Před 3 měsíci +1

    Safi sana

  • @user-gy5en6cy8o
    @user-gy5en6cy8o Před 3 měsíci

    Safi sanaaaa

  • @lailanahd
    @lailanahd Před 3 měsíci

    Vihi ukienda ardhi ukitaka kubadili jina kiwanja fail lazima ulipie ndio litafutwe waziri nakuuliza

  • @joelthomas-mx6gm
    @joelthomas-mx6gm Před 3 měsíci

    Mkuu umenishtua sana ningeend kupigik aiseh. Wauza viwanja ni wengi mno

  • @dayana5513story
    @dayana5513story Před 3 měsíci

    🔥🔥🔥👏👏

  • @thomastemu3332
    @thomastemu3332 Před 3 měsíci

    Jerry slaa hoyee

  • @AbdulmujibAhmed
    @AbdulmujibAhmed Před 3 měsíci +1

    Mhe njo mkuranga kisemvule matapeli wa ardhi kama wote wanshirkiani na wenye viti

  • @maimunaathumani9121
    @maimunaathumani9121 Před 3 měsíci

    Kweli watu wametapeliwa

  • @user-gy5en6cy8o
    @user-gy5en6cy8o Před 3 měsíci

    Nawaona hapo wako buzy na nakalam ila wakitoka hapa job usually 😢

  • @RenaldaZeramula
    @RenaldaZeramula Před 3 měsíci +1

    Tumeshampsta rais 2030 100 kwa 100. Uoewe ulinzi

    • @danielbernad9063
      @danielbernad9063 Před 3 měsíci +1

      Na makonda tusimsahau kaka

    • @ZUWENADELLOW
      @ZUWENADELLOW Před 3 měsíci

      Marais wajao in sha ALLAH,🎉🎉🎉​@@danielbernad9063

  • @MrishoHussein-oz9nr
    @MrishoHussein-oz9nr Před 3 měsíci

    Mh huko bagamoyo ndio dhulma ya ardhi imezidi

  • @user-ib2ew9ec3d
    @user-ib2ew9ec3d Před 3 měsíci

    Natamani Jerry silaa awe rais askofu ngwajima awe makam wa rais

  • @user-df5mj2ft4w
    @user-df5mj2ft4w Před 3 měsíci

    Mabango yamenichosha

  • @godlovemrosso5973
    @godlovemrosso5973 Před 3 měsíci

    Safi sana