RAIS DKT MWINYI AZINDUA HOTEL YA NYOTA TANO EMARALD MATEMWE

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 26. 08. 2024
  • RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali
    Mwinyi amewataka wananchi wa Zanzibar kuzitumia vyema fursa za uwekezaji zilizopo kwenye maeneo yao ili kujikwamua na changamoto za maisha.
    Dk. Mwinyi aliyasema hayo, Kijini - Matemwe, Mkoa wa Kaskazini Unguja
    walipofungua hoteli ya nyota tano ya, Emarald Resort and SPA.
    Alisema fursa za uwekezaji haziwanufaishi wageni pekee, bali wazawa wana nafasi kubwa ya kuzitumia na jikwamua na ugumu wa maisha ili kuondokana na mkwamo wa maendeleo kwa kujiongezea kipato na kubadili mfumo wa maisha walionao kupitia fursa hizo.
    Alisema wazawa hunufaika kupitia uzalishaji ikiwemo, uvuvi, kilimo na biashara watakazozizalisha ambazo zitawalenga wageni waliopo kwenye maeneo yao.

Komentáře • 7

  • @SKY-fk3fz
    @SKY-fk3fz Před rokem

    Mashaallah

  • @salyali7807
    @salyali7807 Před rokem

    Ardhi za wanyonge wanafaidika wageni

    • @mansooralaisri5200
      @mansooralaisri5200 Před rokem

      Sally Ali kumbe bado mjinga kiasi hicho.Nchi bila wageni hakuna maendeleo. Hizo ni Mali zisizo Hamishika zitabaki Znz Daima.

    • @salyali7807
      @salyali7807 Před rokem

      Sujui nani mjinga hapa... unapewa unafurahi... uchungu hata kusema

    • @salyali7807
      @salyali7807 Před rokem

      aisri nimekusudia unapewa pipi unafurahi

  • @mansooralaisri5200
    @mansooralaisri5200 Před rokem

    Vijana watapata kazi hapo. Ni jambo la kushukuriwa sana. Mwinyi una Maono makubwa sana. Hawatakusifu Leo ila vizazi vijavyo watakuzungumzia kwa sifa zote. Ziba masikio kanyaga twende. Tutafika tuu.

    • @salyali7807
      @salyali7807 Před rokem

      Umekusudia vijana wa bara.... ndio maana wamemiminika mpaka kisiwa karibu ya kuzama