Hadithi ya JOKA na MCHUNGA KONDOO | Hadithi za Kiswahili | katuni za Kiswahili

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 27. 07. 2022
  • HADITHI YA JOKA NA MCHUNGA KONDOO...
    SEHEMU YA NNE…
    MKUZA alifika Hadi nyumbani kwao, Lakini kichwani mwake akiwa ameshaamua kabisa kuachana na fikra juu ya BETINA,maana alijiona kuwa anawaza bure…
    Kwakuwa alikuwa NI mgeni kwenye masuala hayo baba Yake siku moja alimwelezea MKUZA juu ya mahusiano na kupenda….
    Siku zilikwenda BETINA akawapa kazi vijakazi wake wakamtafute MKUZA Hadi wampate kisha waje wamweleze habari za yeye kutafutwa na BETINA,Vijakazi hao walitafut Hulu wakiwa wanauliza kuhusu habari za MKUZA…
    Siku moja wakiwa Porini walikutana na MSUKO peke Yake,vijakazi hao wakamuulizia MKUZA,MSUKO alishangaa Sana habari Hizo,kwani alitambua kuwa hao Walikuwa ni vijakazi wa mtoto wa tajiri wa Kijiji hiko…
    Vijakazi hao wakamwambia MSUKO juu ya habari za MKUZA kutafutwa na BETINA,hakika hapa wivu uliongozeka maradufu kwa MSUKO,kwani Licha ya urafiki wake na MKUZA bado hakupenda kuona MKUZA anapendwa na BETINA…
    Na yote hiyo ni kwasababu ya wivu aliokuwa nao juu ya Rafiki yake,aliona kuwa MKUZA ataenda kuwa mtu Mwenye mafanikio,kwakuwa atakuwa Mume wa mtoto wa tajiri,MSUKO akaendelea kutamani yeye awe ndio MKUZA…
    Roho mbaya Wakati wote haina dawa,MSUKO akaingiwa na roho mbaya kwelikweli kwa Rafiki Yake,Japo MKUZA hakujua juu ya chuki hiyo iliyozaliwa…
    MSUKO akajifanya hamjui kabisa MKUZA akadai wamekutana tu porini kwa kuchunga,Ni wazi alidanganya maana MSUKO Alipajua Hadi nyumbani kwa kina MKUZA…
    MSUKO Akaamua kuwa rasmi Rafiki mnafki kwa Rafiki Yake wa muda wa mrefu…Akawa anapanga mipango ikiwezekana BETINA na watu wake wasije kumuoa kabisa,MKUZA…
    KWELI KUNA WATU NA VIATU,NA MSUKO YEYE ALIKUWA KIATU NA SIO MTU…
    #hadithizakiswahili2022 #swahilifairytales #joka
  • Zábava

Komentáře •