NI UHERI BORA KU MWAMINI BWANA (Lyrics) By Bro Rodrigue Banze

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 23. 08. 2021
  • Nyimbo za Wokovu
    223. NI UHERI BORA KUMWAMINI BWANA
    1. Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu kwa wakati
    wa ujana wetu, kabla hatujazionja dhambi na
    mashaka zinazoharibu roho zetu.
    Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu, na kumfuata kila siku. Na ujana wetu ukitukimbia tena, shangwe ya wokovu itabaki.
    2. Ni uheri bora kumtii Bwana Yesu kwa wakati wa
    ujana wetu. Hivyo tutakuwa na dhamiri safi, njema
    kwa maisha yetu yote pia.
    3. Ni uheri bora kumtumikia Yesu kwa wakati wa ujana
    wetu. Bwana Yesu akumbuka kila tendo dogo,
    atalipa kwa neema yake.
    4. Ni uheri bora kumngoja Bwana Yesu kwa wakati wa
    ujana wetu. Atatuchukua kwake kwa furaha kubwa,
    tutakuwa naye siku zote.
  • Hudba

Komentáře • 18