Video není dostupné.
Omlouváme se.

(LOST) FKF BUS NOW FOUND, READY TO SERVE THE CLUBS

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 19. 02. 2024
  • BASI LA FKF NDIO HILI SASA, HATIMAYE
    Rafiki basi la FKF ambalo lilikuwa 'limepotea' kwa muda hatimaye limepatikana. Lilikuwa gereji likifanyiwa ukarabati na sasa tunaweza sema laeza tumika.
    Kuna suala la kukosa vibali lakini Tom Lango (FKF Chairman Malindi Branch) ametuhakikishia laweza rudi barabarani bila shaka yoyote.
    Amethibitisha kuwa laki 170,000 zilizopeanwa na Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi mwaka jana zilitumika zote hapa kwenye ukarabati huu.
    Kuhusu logbook na transfers amejibu kwamba kwa sasa basi hilo bado stakabathi zinasoma jina la Bi Aisha Jumwa Mbunge wa zamani wa Malindi (aliyehusika pakubwa upatikanaji wa basi hili kwa vilabu vya Malindi).
    Hata hivyo mchakato wa kutafuta 'umiliki' wa basi hilo liende kwa FKF Malindi unaendelea.
    Ametaja kwamba klabu yoyote inayohitaji huduma za basi hilo inaweza kumjulisha nao wakalitumia kwa urahisi kabisa. Wekeni mafuta muende mechi.
    Mengi zaidi tegea Tama La Spoti na Lulu Viwanjani ukiwa na Paaaps Mkare kwa maelezo kuhusu basi hili.
    Swali lako ni lipi tena?
    #TamaLaSpoti
    #LuluViwanjani
    #LuluDrive

Komentáře •