WIMBO WA JAMII ZA KENYA the Kiswahili version of SONG OF THE COMMUNITIES OF KENYA

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 9. 05. 2024
  • WIMBO WA JAMII ZA KENYA ni wimbo ambao watoto wa kutoka jamii mbalimbali nchini Kenya wanaimba na kila mtoto anajivunia jamii yake, kule alikotoka, chakula wanachokipenda na pia kuwafunza wenzake jinsi ya kucheza ngoma zao za kitamaduni. Ni wimbo unaowafunza watoto kuhusu jamii mbalimbali nchini Kenya, mambo yanayovutia katika sehemu wanazoishi, vyakula na ngoma za kitamaduni za jamii hizo. Katika wimbo huu tuliteua jamii kumi na moja kutoka kaunti mbalimbali nchini Kenya ili kuwakilisha kila sehemu ya nchi. Wimbo huu unawafunza watoto kujua na kuthamini tamaduni za jamii nyingine na pia kuleta utangamano na umoja wa jamii mbalimbali. Wimbo huu utamsaidia mwalimu kutimiza lengo la kwanza la elimu ambalo ni: Kukuza utaifa na uzalendo na kukuza umoja wa kitaifa. Watu wa Kenya ni wa jamii, rangi na dini tofauti, lakini tofauti hizi hazihitaji kuwagawanya. Ni lazima waweze kuishi na kutangamana kama Wakenya. Unaweza kuutazama wimbo huu kwa lugha ya Kiingereza SONG OF THE COMMUNITIES OF KENYA kwa • SONG OF THE COMMUNITIE...

Komentáře •