Professor Jay ft Diamond Platnumz - Kipi Sijasikia ( Audio with Lyrics )

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 22. 06. 2014
  • Buy it from iTunes: geo.itunes.apple.com/in/album...
    Niliacha kazi nifanye muziki wakatabiri nitalost, Wengine wakanishawishi tuloge kuondoa mikosi, Nakomaa na muziki ingawa jua la utosi, Naamini wote tunapita na kamwe maiti haijioshi Jina langu lishatumika sana kutajirisha watu, Nyota ndogo alishasema kuna Watu na viatu, Bunduki haiui watu ila watu ndio wanaua watu, Dunia kama jalala tazama kwa Jicho la Tatu,
    Ni saa mbaya watu wanahusda na roho mbaya , Tunawaita watakatifu kumbe ndio mavimpire, Yalisemwa mengi demu wangu alivyotoroka, Ni Fundisho tosha na changamoto kwa Mwanachoka Nimepita Mengi mitihani ya kila Namna,
    Ndio maana mi sishangai wakiniita mbeba Lawama,
    Washkaji wengine fake kwenye deal hawakujui Wanadhani kila jogoo akiwika ni Asubuhi,
    Riziki hamuwezi iziba labda mtaichelewesha tuu,
    Mnakesha mnishushe Mwenyezi ananipaisha,
    Kote mlikobana kidume ndio Natusua,
    Mnanijua,Nakamua, Roho za wanga zinaungua
    PLATINUM!!!
    CHORUS;
    Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilindeee..
    Kwenye hii vita milele Basi nishike mkono nishindeee..
    Unaehukumu ni wewe Mwenyezi Mungu naomba unilindeee..
    Kwenye hii vita milele Mwanachoka daima Nishindeee..
    VERSE 2
    Walishazusha nimekufa, Eti nimepata ajali,
    Washindwe na walegee Mwenyezi niepushie mbali
    Wakasema nina Ukimwi kwa kuwa nilikonda ghafla,
    Wanataka kunizika mzima Kabla sijafa,
    Waliosema nina Ngoma wengine tushawafukia, Wanaoomba nife leo naamini Watatangulia,
    MAMA Pumzika Pema..Daima tunakulilia,
    Na bado wanachonga sana but MAN the KING is here!!
    Daima mtaji wangu ni nguvu zangu mwenyewe, Simwamini mtu kamwe najiamini mi mwenyewe, Hata nikinywa maji wanadai nakunywa pombe, Mi sijali, I KNOCK THEM HARD Mwanalizombe! Bado tu napambana kibarua kisiote nyasi,
    Daima sitawadhuru wale wote walioniasi,
    Nikikaa kimya msidhani Sijasikia,
    Sio Bahati sio Ngekewa ni sauti Iliyobarikiwa HOLLA!!!
    CHORUS;
    Verse 3
    Mungu walaze pema Waliosemwa wakajiua,
    Ingawa wote tunapita naamini Maisha ni hatua, Maneno ya watu Sumu, Yanaponya na Yanaua, Please nipe ujasiri mpaka siku Ukinichukua,
    Wape nguvu wale wote waliokata tamaa, Maneno yanaleta hila na Mzozo kwenye mitaa, Wanahesabu mabaya tuu na mema hawayaoni, Wanakuchekea Machoni, Wanakuroga Moyoni,
    Wanacheka chinichini wakati una Msiba,
    Wa kwanza kukutangaza kwa watu ukiwa na Shida!!
    Wanatamani wapangue kila mola alichopanga, Wanatangaza Amani huku wameficha MAPANGA
    CHORUS;
  • Hudba

Komentáře • 8

  • @moseshandsam1865
    @moseshandsam1865 Před 2 lety

    Best legend the best song of tyms haishi ladha Iseee nipo #qatar and this song it's the best my brother plz mashabiki zako bado twataka utunzi wako wa hali ya juuu best song of all tyms

  • @revocatusmagesa1661
    @revocatusmagesa1661 Před 10 lety +1

    duu profesor eee hii ngoma inanikumbusha zaman saana

  • @saidomary4406
    @saidomary4406 Před 4 lety

    Daaaa hiii ngoma imenigusa maana verse ya kwanza na yapili niyeyapitia na aminipa matumain na nguvu za kupambana nayo

  • @jameskarugu4375
    @jameskarugu4375 Před 4 lety +1

    It's 30th/07/2020 and here am i today💥💥💥

  • @HAMTV77
    @HAMTV77 Před 10 lety

    binge moja la ngoma kk...naomba uitendee haki na video kaaaaliii

  • @MartinTairo
    @MartinTairo Před 10 lety

    Video iko wapi?

  • @revocatusmagesa1661
    @revocatusmagesa1661 Před 10 lety

    duu profesor eee hii ngoma inanikumbusha zaman saana

  • @HAMTV77
    @HAMTV77 Před 10 lety

    binge moja la ngoma kk...naomba uitendee haki na video kaaaaliii