Afisa Mtendaji Mkuu, Mkapa Foundation Azungumzia Mkutano wa Kumbukizi wa Hayati Benjamin Mkapa 2024

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 25. 08. 2024
  • 𝗞𝘂𝗺𝗯𝘂𝗸𝗶𝘇𝗶 𝘆𝗮 𝗛𝗮𝘆𝗮𝘁𝗶 𝗠𝗵𝗲. 𝗕𝗲𝗻𝗷𝗮𝗺𝗶𝗻 𝗠𝗸𝗮𝗽𝗮

    Taasisi ya Benjamin William Mkapa Foundation kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kupitia Wizara ya Afya leo imefanya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ikiwa ni hatua muhimu kuelekea Maadhimisho ya Kumbukizi ya Hayati Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, Rais mstaafu wa awamu ya tatu.
    𝘔𝘢𝘢𝘥𝘩𝘪𝘮𝘪𝘴𝘩𝘰 𝘺𝘢𝘯𝘢𝘵𝘢𝘳𝘢𝘫𝘪𝘸𝘢 𝘬𝘶𝘧𝘢𝘯𝘺𝘪𝘬𝘢 𝘵𝘢𝘳𝘦𝘩𝘦 31 𝘑𝘶𝘭𝘢𝘪, 𝘺𝘢𝘬𝘪𝘵𝘢𝘯𝘨𝘶𝘭𝘪𝘸𝘢 𝘯𝘢 𝘒𝘰𝘯𝘨𝘢𝘮𝘢𝘯𝘰 𝘭𝘢 𝘒𝘪𝘵𝘢𝘪𝘧𝘢 𝘭𝘢 𝘙𝘢𝘴𝘪𝘭𝘪𝘮𝘢𝘭𝘪 𝘸𝘢𝘵𝘶 𝘬𝘢𝘵𝘪𝘬𝘢 𝘚𝘦𝘬𝘵𝘢 𝘺𝘢 𝘈𝘢𝘧𝘺𝘢 2024, 𝘬𝘢𝘵𝘪𝘬𝘢 𝘜𝘬𝘶𝘮𝘣𝘪 𝘸𝘢 𝘒𝘪𝘮𝘢𝘵𝘢𝘪𝘧𝘢 𝘸𝘢 𝘔𝘪𝘬𝘶𝘵𝘢𝘯𝘰 𝘸𝘢 𝘔𝘸𝘭. 𝘑𝘶𝘭𝘪𝘶𝘴 𝘕𝘺𝘦𝘳𝘦𝘳𝘦 (𝘑𝘕𝘐𝘊𝘊), 𝘋𝘢𝘳 𝘌𝘴 𝘚𝘢𝘭𝘢𝘢𝘮.
    🇹🇿Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atakuwa Mgeni Rasmi siku ya kilele, Julai 31, 2024. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kuchagiza Uendelevu wa Ndani kuelekea kwenye Upeo Mpya” ikionesha maono ya Hayati Benjamin Mkapa katika maendeleo ya ndani.
    #MkapaLegacy #HRH #HumanResourceForHealthConference

Komentáře •