MAJALIWA ARUDI NGORONGORO 'YEYOTE ANAYEONA ANAWEZA KUISHI MAHALI PENGINE YUKO HURU'

Sdílet
Vložit
  • čas přidán 25. 08. 2024
  • WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema wakazi wa wilaya ya Ngorongoro, mkoani Arusha wanaotaka kuhama kwa hiari yao wajitokeze na waseme wanataka kwenda wapi.
    “Suala la idadi ya watu ni kubwa. Kumbe huko nyuma kulishakuwa na mapendekezo. Yeyote anayeona anaweza kuishi mahali pengine yuko huru kusema. Kama yuko mtu wa aina hiyo, awe huru kwenda kwa DC (Mkuu wa Wilaya) kajiandikishe na Serikali itakuhudumia vizuri. Hayo ni maamuzi ya mtu binafsi, kusiwe na mtu wa kumshinikiza fulani asifanye maamuzi yake. Kama yuko aachwe afanye maamuzi yake, aseme anataka kwenda wapi na sisi tutamhudumia.”
    Mheshimiwa Majaliwa alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na viongozi na wananchi wa tarafa ya Ngorongoro kwenye kikao cha ndani kilichofanyika makao makuu ya zamani ya NCAA, wilayani Ngorongoro.

Komentáře • 3

  • @Ndu-wa.uroony2
    @Ndu-wa.uroony2 Před 2 lety

    Wamasai nawajua,watasema wanataka kuhamia Serengeti,au Selous

  • @marymfugwa847
    @marymfugwa847 Před 2 lety

    Bora wahame kwa hiyari tu maana baada ya hitimisho watahamishwa kwa vifaru kama kilicho tokea Mtwara bomba la gesi.

  • @rinaldaoman7892
    @rinaldaoman7892 Před 2 lety

    🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😀🤣🤣😀🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 kimyaaaa wako wapi wale waliokuwa wantoa povu hatuhamiiii
    Jitokezeni.muone. etinhamuhami dhubutuuu Tz au hee heeeeee wahame wankunya hovyoo